Mswada Katiba Mpya: MAONI YA KAMBI YA UPINZANI BUNGENI....

Msanii

Platinum Member
Jul 4, 2007
22,603
29,748
MAONI YA MSEMAJI WA KAMBI RASMI YA UPINZANI BUNGENI, WIZARA YA SHERIA NA KATIBA, MHESHIMIWA TUNDU A.M. LISSU KUHUSU
MUSWADA WA SHERIA YA MAREKEBISHO YA SHERIA
YA MABADILIKO YA KATIBA, SHERIA NA. 8 YA 2011
(Kanuni ya 86(6) ya Kanuni za Kudumu za Bunge, 2007)

Mheshimiwa Spika,
Tarehe 18 Novemba, 2011 Bunge lako tukufu lilipitisha Muswada wa Sheria ya Mabadiliko ya Katiba ya mwaka 2011. Siku kumi na moja baadaye, yaani tarehe 29 Novemba, 2011, Mheshimiwa Rais Jakaya Kikwete alitoa kibali cha Muswada huo kuwa Sheria kwa mujibu wa ibara ya 97(1) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, 1977, na kanuni ya 92(1) ya Kanuni za Kudumu za Bunge, 2007. Kwa mujibu wa kifungu chake cha 1(2), Sheria ya Mabadiliko ya Katiba, Na. 8 ya 2011, ilianza kutumika tarehe 1 Desemba, 2011, yaani siku mbili tu baada ya kupata kibali cha Rais.


Mheshimiwa Spika,

Leo ni siku arobaini na moja tangu Sheria hii ipate kibali cha Mheshimiwa Rais, na siku thelathini na tisa tangu ipate nguvu za kisheria ili ianze kutumika. Tumekutana hapa leo hii ili Bunge lako tukufu lipate fursa nyingine tena ya kuitafakari Sheria hii. Kila mmoja wetu humu ndani, na kila Mtanzania anayefuatilia mchakato wa kutengeneza Katiba Mpya, anafahamu kwamba tendo la kwanza lililoidhinishwa na Sheria hii, yaani kuteuliwa kwa Tume ya Mabadiliko ya Katiba, halijafanyika hadi sasa. Tumekutana hapa leo hii ili kujadili, na kama Bunge lako tukufu litaridhika, kupitisha Muswada wa Marekebisho ya Sheria ya Mabadiliko ya Katiba, 2011 unaopendekezwa na Serikali, na hivyo kumwezesha Mheshimiwa Rais kutenda tendo hilo la kwanza kwa mujibu wa Sheria hii.


MAJADILIANO YA CHADEMA NA RAIS


Mheshimiwa Spika,

Tarehe 20 Novemba, 2011 Kamati Kuu ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) iliunda Kamati Maalum ya wajumbe saba iliyopewa jukumu la kuonana na Mheshimiwa Rais kuhusu Sheria hii na mustakbali wa taifa letu. Siku mbili baadae, yaani tarehe 22 Novemba, 2011,
........

Download nakala ya hotuba
 

Attachments

  • The Amending Bill Final.doc
    91 KB · Views: 481
Tundu Lissu ni jembe, uwepo wake bungeni umesaidia saana.

Hayo yote ni matunda ya kuwa na Katibu Mkuu wa Chama mwelewa ; Dr. Slaa; anajua kuipanga timu yake ya kazi vyema katika kufanya kile ambacho CHADEMA tunataka!
 
Hongereni wanaCDM wote

Sawa tuko pamoja hadi kieleweke! Wafuasi wengi wa CCM ni mbumbumbu ndo maana hawawezi kujua nini CDM wanapigania - ila mwisho na hao mbumbumbu watafaidika kwani tunachokitafuta ni kwa ajili ya Taifa zima na wala si kwa ajili ya wanachadema tu!
 
Sijui kwanini Mibunge ya CCM migumu sana kuelewa? Mbowe, Silinde, Arfi, Machali wameongea vizuri sana lakini nahisi wanataka kutumia wingi wao kulazimisha wakuu wa Wilaya
 
Congrats to all stakeholders (the govt, various parties, civil societies etc) for showing a high level of political maturity in resolving this crucial matter
 
ambaye yupo kwenye laptop naomba aidownload atuwekee hapa. wengine tunatumia simu. ova
 
Congrats to all stakeholders (the govt, various parties, civil societies etc) for showing a high level of political maturity in resolving this crucial matter

Hebu soma kifungu hiki cha mwisho

"Mheshimiwa Spika,
Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni inafarijika kwamba Kamati ya Katiba, Sheria na Utawala ya Bunge lako tukufu imeridhia na kukubali mapendekezo yote ya Muswada huu na Jedwali la Marekebisho la Serikali. Kwa sababu zote hizi, Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni sio tu inaunga mkono Muswada wa Marekebisho ya Sheria ya Mabadiliko ya Katiba, 2011, bali pia inatoa rai kwa waheshimiwa Wabunge wote, bila kujali the narrowness of our political party affiliations, tuungane na Mheshimiwa Rais katika kulipatia taifa letu utaratibu wa kutengeneza Katiba Mpya wenye muafaka wa kitaifa.

Mheshimiwa Spika, kwa mara ya kwanza, naomba kuunga mkono hoja hii.



---------------------------------------------------------------

Tundu Antiphas Mughwai Lissu (MB)

MSEMAJI, KAMBI RASMI YA UPINZANI BUNGENI

&

WAZIRI KIVULI, KATIBA NA SHERIA


FEBRUARI 9, 2012 "



IT was a very nice presentation. We hope the interests of the majority have been given paramount importance at last!
 
Back
Top Bottom