Msekwa amshukia Kingunge

masopakyindi

Platinum Member
Jul 5, 2011
17,882
13,172
attachment.php



  • Asema hajui kanuni, amepitwa na wakati
  • Mtaturu(katibu CCM Mwanza): heshima ya Kingunge imeshuka

Makamu Mwenyekiti Mstaafu CCM Pius Msekwa amesema tuhuma zinazotolewa na mwanasia mkongwe nchini , Kingunge Ngombale Mwiru dhidi ya vikao vya juu vya chama hazina ukweli wowote.

Msekwa alisema, tatizo linalomkumba Mzee Kinunge ni kuganda kwenye utartibu uliokuwa ukitumika wakati yeye alipokuwa Mjumbe wa Kamati Kuu miaka mingi iliyopita

Aliongeza kuwa Mzee Kingunge hana habari na kanuni zinazotumiaka sasa na hajataka uzifaamu.

Katika hatua nyingine. Katibu wa CCM mkoa wa Mwanza. Miraji Mtaturu, amesema Mzee Kingunge amejipotezea heshima aliyojijengea kwa miaka mingi kutokana na kauli zake.

"Nashangazwa na kauli iliyotolewa na Mzee Kingunge akiwatuhumu (wazee) kuendesha vikao vya mchakato wa kumpata mgombea urais kwa mizengwe na ajenda ya siri"

"Ukiona mtu anabadilika ujue amenunuliwa...!

Chanzo:
Gazeti la Uhuru:p 1, pg4

MY TAKE
Kingunge anatikisa mzinga wa nyuki!
(mods thanks for the clarity)
 
Ukisoma umetulia kauli ya Msekwa ni ya kisiasa zaidi kuliko uhalisia. Kingunge kasema kanuni na taratibu zilizopo ambazo hazijahuishwa, mbona Msekwa hakusema zilibadilishwa lini?

Unataka kusema hata hao akina Nchimbi na wenzake ambao ni wajumbe wa kamati Kuu hawakufahamu hizo Kanuni zilizobadilishwa? Na hao akina Mtaturui wanaisdhi katika maisha ya zamani ambayo kilichosemwa adharani na mwenyekiti hapaswi kupingwa.

Ingawa mimi ni mmoja wa wale waliokuwa wanapinga kuteuliwa Lowassa lakini kwa maoni yangu huyu Mzee amejirejeshea heshima kwa jamii kwa kusimamia uvunjifu wa taratibu na kanuni.
 
ukitaka kujua wana CCM wenzangu ni hamnazo,we waseme kwenye mambo yenye ukweli watakutuna bila kuungalia sura wala umri wako,wamewaambukiza mpaka CHADEMA nao hawapendi kuambiwa ukweli
 
Kwa hiyo kama Kingunge hazijui hizo kanuni kwa vile ni mpya jee na Nchimbi, Kimbisa na Sofia Simba nao hawazijui wakati ni wajumbe was KK?
Msekwa anyamaze tuu kwa vile CCM wameumbuka kupitia Kingunge
 
angezitaja hizo mpya ili kingunge akajisomee ,tofauti na hapo Tutamfuata Lowasa Popote (TLP)
 
Ukisoma umetulia kauli ya Msekwa ni ya kisiasa zaidi kuliko uhalisia. Kingunge kasema kanuni na taratibu zilizopo ambazo hazijahuishwa, mbona Msekwa hakusema zilibadilishwa lini?

Unataka kusema hata hao akina Nchimbi na wenzake ambao ni wajumbe wa kamati Kuu hawakufahamu hizo Kanuni zilizobadilishwa? Na hao akina Mtaturui wanaisdhi katika maisha ya zamani ambayo kilichosemwa adharani na mwenyekiti hapaswi kupingwa.

Ingawa mimi ni mmoja wa wale waliokuwa wanapinga kuteuliwa Lowassa lakini kwa maoni yangu huyu Mzee amejirejeshea heshima kwa jamii kwa kusimamia uvunjifu wa taratibu na kanuni.

Kingunge anaweza kuwa sahihi..ila angeonekana nguli kweli kweli kama angekuwa anawaongelea watia nia wote walioachwa....yeye kaonekana kulalia upande wa kuaminisha jamii kuwa ni Lowassa ndiye aliyeonewa pekee...na kwa kuwa toka awali alionekana kuwa ni mtia nia aliyekuwa anamsapoti, tumeishia kujumlisha 1 + 1 = 3...
 
Msekwa nilikuwa namheshimu sana lakini naanza kumdharau kama lapulapu la kudekia choo cha stendi
 
Kwa hiyo kama Kingunge hazijui hizo kanuni kwa vile ni mpya jee na Nchimbi, Kimbisa na Sofia Simba nao hawazijui wakati ni wajumbe was KK?
Msekwa anyamaze tuu kwa vile CCM wameumbuka kupitia Kingunge

Msekwa ni fisi
 
Back
Top Bottom