Luteni
JF-Expert Member
- Jan 9, 2010
- 2,274
- 302
MAKAMU Mwenyekiti wa CCM Tanzania Bara, Pius Msekwa, ameamriwa kulipa kiasi cha sh 7,072,000 ndani ya miezi mitatu kabla ya kuchukuliwa hatua zaidi.
Amri ya kulipa fedha hizo ilitolewa jana na Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali, John Cheyo wakati alipokutana na viongozi wa juu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa.
Cheyo alisema fedha hizo zilichukuliwa na Msekwa kutoka kwenye Ubalozi wa Tanzania nchini Ufaransa kati ya mwaka 2003 na 2004 kwa ajili ya matibabu ya mtoto wake.
Mwenyekiti huyo aliwaeleza waandishi wa habari ndani ya Ukumbi wa Ofisi Ndogo ya Bunge Dar es Salaam baada ya kumaliza kikao na wizara hiyo kuwa kamati yake ilielezwa malipo hayo yalitakiwa kufanyika ndani ya kipindi cha miezi 10.
Kamati imeelezwa kwamba Msekwa alikopa fedha hizo kwa ajili ya matibabu ya kijana wake aliyeugua ghafla huko Ufaransa, akaahidi kulipa deni hilo kwa kiasi cha sh milioni moja kila mwezi.
Lakini mpaka leo ulipaji wa deni hilo unasuasua, ndiyo maana tumeiagiza wizara kuwasiliana na mdeni wao ili kurudisha fedha hizo katika kipindi kisichozidi miezi mitatu, alisisitiza Cheyo ambaye pia ni Mbunge wa Bariadi Mashariki na kuongeza kwamba kinyume cha hapo kamati itajua nini cha kufanya.
Awali, Katibu Mkuu wa wizara hiyo, Sazi Salula aligoma kumtaja mdeni huyo kutokana na wadhifa wake ndani ya CCM, akimwelezea kuwa ni kigogo hivyo hakustahili kutajwa mbele ya waandishi wa habari na kwamba si muajiriwa wa serikalini.
Hata hivyo, Salula alisema kigogo huyo ameandikiwa barua akikumbushwa kuhusu deni lake mara kadhaa ingawa mpaka sasa amelipa sh milioni tatu tu.
Katika maelezo ya wizara hiyo kwa kamati ya Bunge, inadaiwa Msekwa alikopeshwa kiasi cha euro 5,924 sawa na sh 10,072,000 mwaka 2003/04 na kwamba ulipaji wake umefanyika kwa stakabadhi tofauti.
Stakabadhi zilizotumika katika malipo ya fedha hizo ni zenye namba 33065088 ya Januari 15 na 33065118 ya Aprili 20 zote za mwaka jana.
Mheshimiwa tumejitahidi kufuatilia fedha hizi, ndiyo maana hata Januari 8 mwaka huu tumemwandikia barua yenye kumbukumbu namba BA43/518/79 kumkumbusha kuhusu deni la sh 7,072,000, alisema Salula bila kumtaja madaiwa kwa msisitizo kuwa wadhifa wake alionao hastahili kutajwa mbele ya vyombo vya habari.
Akizungumza na Tanzania Daima kwa njia ya simu kutoka Arusha, Msekwa alilithibitisha kudaiwa na Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa kiasi cha sh milioni sita na si saba kama inavyodaiwa.
Ni kweli mwanangu anayefanya kazi London alipata matatizo, nikaomba Wizara ya Mambo ya Nchi za Nje inilipie gharama za matibabu pale Ufaransa nikakubaliwa, hivyo sikuona kama ni kosa, alisema Msekwa.
Alisema baada ya kupata fedha hizo, mwanaye ambaye hakumtaja kwa jina aliendelea kupata matibabu hadi alipopona na kurudi kazini Uingereza bila tatizo.
Kuanzia hapo nikiwa Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano sikudaiwa hata siku moja na mimi nilinyamaza nikitambua kwa vile mwanangu ni mfanyakazi wao, basi atakuwa amelipiwa fedha hizo ambazo ni sh milioni 10, lakini haikuwa hivyo.
Nikiwa sijui kinachoendelea nilishutukia naletewa barua na Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na kunieleza kwamba wamefanyiwa ukaguzi wa mahesabu na kukuta kiasi hicho hakipo sasa nikashangaa nikijua wazi wanalipa wao kwa vile ni mfanyakazi wao, basi nilikubaliana nao, alisema.
Alisema baada ya taarifa hiyo, alianza kulipa deni hilo kama alivyotakiwa kufanya.
Nalikubali deni hili ni langu. Tulikubaliana kila mwezi niwe nalipa sh milioni moja, mpaka sasa nimebakiza milioni sita tu, sina ubishi ni kweli hata risiti zote ninazolipa deni ninazo. Pia kumbuka mimi ni Spika mstaafu hivyo nalipa kutokana pensheni yangu ninayopata, alisema Msekwa.
Amri ya kulipa fedha hizo ilitolewa jana na Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali, John Cheyo wakati alipokutana na viongozi wa juu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa.
Cheyo alisema fedha hizo zilichukuliwa na Msekwa kutoka kwenye Ubalozi wa Tanzania nchini Ufaransa kati ya mwaka 2003 na 2004 kwa ajili ya matibabu ya mtoto wake.
Mwenyekiti huyo aliwaeleza waandishi wa habari ndani ya Ukumbi wa Ofisi Ndogo ya Bunge Dar es Salaam baada ya kumaliza kikao na wizara hiyo kuwa kamati yake ilielezwa malipo hayo yalitakiwa kufanyika ndani ya kipindi cha miezi 10.
Kamati imeelezwa kwamba Msekwa alikopa fedha hizo kwa ajili ya matibabu ya kijana wake aliyeugua ghafla huko Ufaransa, akaahidi kulipa deni hilo kwa kiasi cha sh milioni moja kila mwezi.
Lakini mpaka leo ulipaji wa deni hilo unasuasua, ndiyo maana tumeiagiza wizara kuwasiliana na mdeni wao ili kurudisha fedha hizo katika kipindi kisichozidi miezi mitatu, alisisitiza Cheyo ambaye pia ni Mbunge wa Bariadi Mashariki na kuongeza kwamba kinyume cha hapo kamati itajua nini cha kufanya.
Awali, Katibu Mkuu wa wizara hiyo, Sazi Salula aligoma kumtaja mdeni huyo kutokana na wadhifa wake ndani ya CCM, akimwelezea kuwa ni kigogo hivyo hakustahili kutajwa mbele ya waandishi wa habari na kwamba si muajiriwa wa serikalini.
Hata hivyo, Salula alisema kigogo huyo ameandikiwa barua akikumbushwa kuhusu deni lake mara kadhaa ingawa mpaka sasa amelipa sh milioni tatu tu.
Katika maelezo ya wizara hiyo kwa kamati ya Bunge, inadaiwa Msekwa alikopeshwa kiasi cha euro 5,924 sawa na sh 10,072,000 mwaka 2003/04 na kwamba ulipaji wake umefanyika kwa stakabadhi tofauti.
Stakabadhi zilizotumika katika malipo ya fedha hizo ni zenye namba 33065088 ya Januari 15 na 33065118 ya Aprili 20 zote za mwaka jana.
Mheshimiwa tumejitahidi kufuatilia fedha hizi, ndiyo maana hata Januari 8 mwaka huu tumemwandikia barua yenye kumbukumbu namba BA43/518/79 kumkumbusha kuhusu deni la sh 7,072,000, alisema Salula bila kumtaja madaiwa kwa msisitizo kuwa wadhifa wake alionao hastahili kutajwa mbele ya vyombo vya habari.
Akizungumza na Tanzania Daima kwa njia ya simu kutoka Arusha, Msekwa alilithibitisha kudaiwa na Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa kiasi cha sh milioni sita na si saba kama inavyodaiwa.
Ni kweli mwanangu anayefanya kazi London alipata matatizo, nikaomba Wizara ya Mambo ya Nchi za Nje inilipie gharama za matibabu pale Ufaransa nikakubaliwa, hivyo sikuona kama ni kosa, alisema Msekwa.
Alisema baada ya kupata fedha hizo, mwanaye ambaye hakumtaja kwa jina aliendelea kupata matibabu hadi alipopona na kurudi kazini Uingereza bila tatizo.
Kuanzia hapo nikiwa Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano sikudaiwa hata siku moja na mimi nilinyamaza nikitambua kwa vile mwanangu ni mfanyakazi wao, basi atakuwa amelipiwa fedha hizo ambazo ni sh milioni 10, lakini haikuwa hivyo.
Nikiwa sijui kinachoendelea nilishutukia naletewa barua na Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na kunieleza kwamba wamefanyiwa ukaguzi wa mahesabu na kukuta kiasi hicho hakipo sasa nikashangaa nikijua wazi wanalipa wao kwa vile ni mfanyakazi wao, basi nilikubaliana nao, alisema.
Alisema baada ya taarifa hiyo, alianza kulipa deni hilo kama alivyotakiwa kufanya.
Nalikubali deni hili ni langu. Tulikubaliana kila mwezi niwe nalipa sh milioni moja, mpaka sasa nimebakiza milioni sita tu, sina ubishi ni kweli hata risiti zote ninazolipa deni ninazo. Pia kumbuka mimi ni Spika mstaafu hivyo nalipa kutokana pensheni yangu ninayopata, alisema Msekwa.