Mu-sir
JF-Expert Member
- Oct 12, 2010
- 3,621
- 1,629
Wakuu, mimi ni kijana wa kiume na nina tatizo la muda mrefu kidogo ambalo linaninyima raha wakati linapotokea. Tatizo lenyewe ni kwamba hutokea nikiwa nimelala naanza kuota kama ndoto ambayo siwezi kuielezea na katika ndoto huja kitu mfano wa mtu(jinamizi) na kuni gandamiza kimazingara mwili mzima na ninashindwa hata kuinua mkono na kupambana nacho zaidi ya kutumia hisia zaidi. Yaani mwili wote unakuwa umekandamizwa kiasi kwamba siwezi kufanya chochote zaidi ya kutulia na kutumia hisia tu kukifukuza. Wakati mwingine pia wakati nikitokewa na hali hii pia hutokea kama ninashirikiana kimapenzi na kitu hicho (ambacho kihisia hutokea katika umbo la binadamu wa kiume) hali ambayo huninyima raha kabisa. Kiimani mimi ni mkristo na huwa nakikemea kihisia mara kinitokeapo kwa kuwa siwezi kuinua hata kidole kimoja kupambana na mara kiondokapo mimi hushtuka na kujikuta kumbe nilikuwa ndotoni tu. Naomba msaada wa mawazo kwani hali hii hujirudia mara kadhaa na haina interval maalum. Nifanyeje? Natanguliza shukrani.