Kiroroma
JF-Expert Member
- Feb 6, 2009
- 370
- 114
Wana-JF,Naingia hapa jamvini kama mdau mchanga sana,Kwenu naomba ushauri wa janga hili;Shoga yake na wife ambaye ni jirani yetu hapa maskani alinikamata mguu miaka kama mitatu imepita kwa kisingizio kwamba ndani kwake hapati huduma stahili.Anaye mdau kama mimi ila nililong'amua ni kwamba mdau kazi zimemzidia na kinywaji sana.Sasa sihitaji kuendelea na maisha haya.Nimempa mpango huo live haelekei kuelewa ndo kwanza anaweka shinikizo kali na mkwara kibao.Nimekata mguu lakini hataki kuachia ngazi.Hanigharimu kitu chochote kwa maana ya mali au hata fedha lakini dhamira yangu inanishtaki sana.Uhusiano wa kifamilia ni mzuri kabisa wife hata fununu hana!Kwani shoga ni msiri hata kuliko Misri,hafanyi kosa yeye shida yake kubwa huduma tuu.Nifanyeje wajemeni?Roho haitaki tena udhalimu huu.