Mmea Jr
JF-Expert Member
- May 20, 2016
- 551
- 1,222
Habari zenu wakuu , tafadhari naombeni msaada wa mawazo katika hili tatizo lilomkuta mdogo wangu.
Moja kwa moja kwenye maada . Hapa nyumbani ninapoishi ninaishi na mdogo wangu wa kiume . Lengo la kuishi naye ni ili aweze kunisaidia katika biashara yangu ya duka nililolifungua hapa nyumbani .
Sasa huyu mdogo wangu katika hii biashara ya duka imetokea ameanzisha mahusiano ya kimapenzi na mfanyakazi (beki tatu )wa jirani ya yangu mahusiano ambayo yalikuwa ya siri baina yao .
Sasa katika siku ya jumapili ( tarehe 3/7/. jirani yangu alinifuata na kuniambia kuwa mfanyakazi wake wa kike kamuibia kiasi cha pesa cha shilingi laki nne . Ukweli nilistaajabu na kumpa pole za dhati kabisa huyu jirani yangu na kumuuliza sasa amechukua hatua gani ?.
Akaniambia kutoka na uchunguzi aliyofanya amegundua huyo mfanyakazi wake wa kike (ambaye bado anaishi naye ) ana mahusiano ya kimapenzi na mdogo wangu. Hivyo anahisi baada ya binti huyu kuiba pesa kiasi cha tsh 400,000/= . basi amempa huyu mdogo wangu wa kiume amfichie ( ukweli nilishangaa sana ) .
Ikabidi tumuite mdogo wangu wa kiume na kuumuliza juu ya shutuma zinazomkabili , mdogo wangu kweli kajibu alikuwa ana mahusiano na huyo binti (mfanyakazi wangu ) na katika mahusiano yao mdogo wangu wa kiume ndiyo amewahi kumpa binti tsh 5000/= tu . Na siyo kinyume chake .
Sasa changamoto inakuja hapa huyu jirani yangu moja anatangaza kwa watu kuwa huyu mfanyakazi wake wa kike anayemuhisi kamuibia pesa amempa huyu mdogo wangu wa kiume amfichie , lakini pia aenda mbali zaidi na kuwaambia watu anaenda polisi kumfungulia kijana wangu wa kiume kesi ya wazi , kuwa ameshirikiana na mfanyakazi wake wa kike kumuibia kiasi tsh 400,000/= .
Sasa naombeni ushauri wanaJamiiForums mnishauri ni hatua gani za kuchukua juu ya huyu mtu maana binti wamemuuliza kataa kuwa hajaiba, wamempiga lakini pia binti kagoma pia . Sasa nifanyaje juu ya huyu kiumbe
Moja kwa moja kwenye maada . Hapa nyumbani ninapoishi ninaishi na mdogo wangu wa kiume . Lengo la kuishi naye ni ili aweze kunisaidia katika biashara yangu ya duka nililolifungua hapa nyumbani .
Sasa huyu mdogo wangu katika hii biashara ya duka imetokea ameanzisha mahusiano ya kimapenzi na mfanyakazi (beki tatu )wa jirani ya yangu mahusiano ambayo yalikuwa ya siri baina yao .
Sasa katika siku ya jumapili ( tarehe 3/7/. jirani yangu alinifuata na kuniambia kuwa mfanyakazi wake wa kike kamuibia kiasi cha pesa cha shilingi laki nne . Ukweli nilistaajabu na kumpa pole za dhati kabisa huyu jirani yangu na kumuuliza sasa amechukua hatua gani ?.
Akaniambia kutoka na uchunguzi aliyofanya amegundua huyo mfanyakazi wake wa kike (ambaye bado anaishi naye ) ana mahusiano ya kimapenzi na mdogo wangu. Hivyo anahisi baada ya binti huyu kuiba pesa kiasi cha tsh 400,000/= . basi amempa huyu mdogo wangu wa kiume amfichie ( ukweli nilishangaa sana ) .
Ikabidi tumuite mdogo wangu wa kiume na kuumuliza juu ya shutuma zinazomkabili , mdogo wangu kweli kajibu alikuwa ana mahusiano na huyo binti (mfanyakazi wangu ) na katika mahusiano yao mdogo wangu wa kiume ndiyo amewahi kumpa binti tsh 5000/= tu . Na siyo kinyume chake .
Sasa changamoto inakuja hapa huyu jirani yangu moja anatangaza kwa watu kuwa huyu mfanyakazi wake wa kike anayemuhisi kamuibia pesa amempa huyu mdogo wangu wa kiume amfichie , lakini pia aenda mbali zaidi na kuwaambia watu anaenda polisi kumfungulia kijana wangu wa kiume kesi ya wazi , kuwa ameshirikiana na mfanyakazi wake wa kike kumuibia kiasi tsh 400,000/= .
Sasa naombeni ushauri wanaJamiiForums mnishauri ni hatua gani za kuchukua juu ya huyu mtu maana binti wamemuuliza kataa kuwa hajaiba, wamempiga lakini pia binti kagoma pia . Sasa nifanyaje juu ya huyu kiumbe