Msaada wa kumshitaki mgombea huyu

johnmashilatu

JF-Expert Member
Sep 16, 2010
725
710
Msaada wa kumshitaki mgombea huyu.
Mimi nikiwa ni mkazi wa jiji la Mwanza nakuja haopa jamvini kutafuta msaada ili kuchukuahatua stahiki dhidi ya kitendo kisichofaa cha Mgombea ubunge wa Jimbo la Nyamagana pamoja na washirika wake kwa kuingilia mawasiliano yangu bila ridhaa yangu.

Mnamo oktoba 15 mwaka 2015 muda wa saa tano na dakuika 15 asubuhi nilipokea ujumbe kutoka kwa mtu anayejitambulisha kuwa ni Stanslaus Mabula wenye lengo la kunishawishi nimpigie kura ya ndiyo ifikapo Oktoba 25 mwaka huu.

Ingawa Ujumbe huo aukusema huyo ni mgombea kupitia chama gani lakini ni ukweli uliowazi kuwa mgombea mwenye jina hilo anatokea CCM.

Ujumbe huo umenisababishia usumbufu kwani muda huo nilikuwa natekeleza majukumu yangu lakini nikalazimika kusitisha na kusoma ujumbe huo ambao sikutarajia au kuutaka. Pamoja na matumizi ya njia za kisasa za mawasiliano kufanya kampeni nimeumizwa na ujumbe huo kwani ni ushahidi kuwa Namba zetu za simu SIO SALAMA na mtu anaweza kuzipata na kuzitumia bila kuchukuliwa hatua.

Nimejaribu kuwasiliana na kampuni ya VODACOM ambao ndio naitumia kwa mawasiliano yangu lakini wamesema hawahusiki kutoa namba za wateja wao kwani hicho ni kitu cha siri kati yao na mteja. Suala kubwa ninalojiuliza ni kuwa wapi mtu huyu na washirika wake wake wamepata namba yangu?

Ujumbe uliotumwa umemlenga kijana, akiwa na maana ya kuwa na tgaarifa sahihi za mlengwa kwani nimewauliza wazee kadhaa ambao wameeleza kuwa hawajapata ujumbe huo. Hawa watu wamepata wapi namba yangu. Kuna usalama kweli wa kuendelea kutumia mitando hii ya simu?, kwanini waingilie mawasiliano yangu? Kama sasa wameweza kufanya hivi, huko nyuma wamefanya nini bila mimi kufahamu?, ile sharia ya makosa ya mitandao inawahusu wakina nani?

Naomba kupitia jukwaa hili nipate msaada wa kulifikisha suala hili mahakamani ili iwe fundisho kwa Mgombea huyo na washirika wake kwa kuijngilia mawasiliano yangu
 
Msaada wa kumshitaki mgombea huyu.
Mimi nikiwa ni mkazi wa jiji la Mwanza nakuja haopa jamvini kutafuta msaada ili kuchukuahatua stahiki dhidi ya kitendo kisichofaa cha Mgombea ubunge wa Jimbo la Nyamagana pamoja na wash...

Hiii kali sana mzee. ukiisha fanikiwa na mimi unijulishe niwastaki twaweza kwa kunitumia tafiti matokeo ya uongo yakupika kuhusu uchaguzi kwani sikuwaomba na walinisababishia nipoteze usingizi wangu ....walinichefua sana...
 
hata Kawe KIPPI WARIOBA anatusumbua sana aisee,ukipata msaada nipe mrejesho na mimi nimshughulikie huyu wangu

Mkuu,

Wote wanaokerwa na hatua hii hatuwezi kuungana ili kudhibniti vitendo hivi vya kuingilia mawasiliano yetu, kwani ni lazima wanaofikishwa mahakamani wawe ni wanaowatuhumu wengine kufa au kulishwa sumu?
 
Msaada wa kumshitaki mgombea huyu.
Mimi nikiwa ni mkazi wa jiji la Mwanza nakuja haopa jamvini kutafuta msaada ili kuchukuahatua stahiki dhidi ya kitendo kisichofaa cha Mgombea ubunge wa Jimbo la Nyamagana pamoja na wash...

Hiii kali sana mzee. ukiisha fanikiwa na mimi unijulishe niwastaki twaweza kwa kunitumia tafiti matokeo ya uongo yakupika kuhusu uchaguzi kwani sikuwaomba na walinisababishia nipoteze usingizi wangu ....walinichefua sana...

Mkuu

Binafsi nimepata usumbufu ambao ninahitaji kupata remedy hata kama ile ya maji Vs Mengi.Hatuna wakili wa kutusaidia katika hili?
 
Msaada wa kumshitaki mgombea huyu.
Mimi nikiwa ni mkazi wa jiji la Mwanza nakuja haopa jamvini kutafuta msaada ili kuchukuahatua stahiki dhidi ya kitendo kisichofaa cha Mgombea ubunge wa Jimbo la Nyamagana pamoja na washirika wake kwa kuingilia mawasiliano yangu bila ridhaa yangu.

Mnamo oktoba 15 mwaka 2015 muda wa saa tano na dakuika 15 asubuhi nilipokea ujumbe kutoka kwa mtu anayejitambulisha kuwa ni Stanslaus Mabula wenye lengo la kunishawishi nimpigie kura ya ndiyo ifikapo Oktoba 25 mwaka huu.

Ingawa Ujumbe huo aukusema huyo ni mgombea kupitia chama gani lakini ni ukweli uliowazi kuwa mgombea mwenye jina hilo anatokea CCM.

Ujumbe huo umenisababishia usumbufu kwani muda huo nilikuwa natekeleza majukumu yangu lakini nikalazimika kusitisha na kusoma ujumbe huo ambao sikutarajia au kuutaka. Pamoja na matumizi ya njia za kisasa za mawasiliano kufanya kampeni nimeumizwa na ujumbe huo kwani ni ushahidi kuwa Namba zetu za simu SIO SALAMA na mtu anaweza kuzipata na kuzitumia bila kuchukuliwa hatua.

Nimejaribu kuwasiliana na kampuni ya VODACOM ambao ndio naitumia kwa mawasiliano yangu lakini wamesema hawahusiki kutoa namba za wateja wao kwani hicho ni kitu cha siri kati yao na mteja. Suala kubwa ninalojiuliza ni kuwa wapi mtu huyu na washirika wake wake wamepata namba yangu?

Ujumbe uliotumwa umemlenga kijana, akiwa na maana ya kuwa na tgaarifa sahihi za mlengwa kwani nimewauliza wazee kadhaa ambao wameeleza kuwa hawajapata ujumbe huo. Hawa watu wamepata wapi namba yangu. Kuna usalama kweli wa kuendelea kutumia mitando hii ya simu?, kwanini waingilie mawasiliano yangu? Kama sasa wameweza kufanya hivi, huko nyuma wamefanya nini bila mimi kufahamu?, ile sharia ya makosa ya mitandao inawahusu wakina nani?

Naomba kupitia jukwaa hili nipate msaada wa kulifikisha suala hili mahakamani ili iwe fundisho kwa Mgombea huyo na washirika wake kwa kuijngilia mawasiliano yangu

Rudia kusoma ulichoandika uone kama kuna kesi hapo! Unapoteza muda wako nenda kaendelee na shuguli zako za kutafuta riziki
 
msaada wa kumshitaki mgombea huyu.
Mimi nikiwa ni mkazi wa jiji la mwanza nakuja haopa jamvini kutafuta msaada ili kuchukuahatua stahiki dhidi ya kitendo kisichofaa cha mgombea ubunge wa jimbo la nyamagana pamoja na washirika wake kwa kuingilia mawasiliano yangu bila ridhaa yangu.

Mnamo oktoba 15 mwaka 2015 muda wa saa tano na dakuika 15 asubuhi nilipokea ujumbe kutoka kwa mtu anayejitambulisha kuwa ni stanslaus mabula wenye lengo la kunishawishi nimpigie kura ya ndiyo ifikapo oktoba 25 mwaka huu.

Ingawa ujumbe huo aukusema huyo ni mgombea kupitia chama gani lakini ni ukweli uliowazi kuwa mgombea mwenye jina hilo anatokea ccm.

Ujumbe huo umenisababishia usumbufu kwani muda huo nilikuwa natekeleza majukumu yangu lakini nikalazimika kusitisha na kusoma ujumbe huo ambao sikutarajia au kuutaka. Pamoja na matumizi ya njia za kisasa za mawasiliano kufanya kampeni nimeumizwa na ujumbe huo kwani ni ushahidi kuwa namba zetu za simu sio salama na mtu anaweza kuzipata na kuzitumia bila kuchukuliwa hatua.

Nimejaribu kuwasiliana na kampuni ya vodacom ambao ndio naitumia kwa mawasiliano yangu lakini wamesema hawahusiki kutoa namba za wateja wao kwani hicho ni kitu cha siri kati yao na mteja. Suala kubwa ninalojiuliza ni kuwa wapi mtu huyu na washirika wake wake wamepata namba yangu?

Ujumbe uliotumwa umemlenga kijana, akiwa na maana ya kuwa na tgaarifa sahihi za mlengwa kwani nimewauliza wazee kadhaa ambao wameeleza kuwa hawajapata ujumbe huo. Hawa watu wamepata wapi namba yangu. Kuna usalama kweli wa kuendelea kutumia mitando hii ya simu?, kwanini waingilie mawasiliano yangu? Kama sasa wameweza kufanya hivi, huko nyuma wamefanya nini bila mimi kufahamu?, ile sharia ya makosa ya mitandao inawahusu wakina nani?

Naomba kupitia jukwaa hili nipate msaada wa kulifikisha suala hili mahakamani ili iwe fundisho kwa mgombea huyo na washirika wake kwa kuijngilia mawasiliano yangu

kama hupo karibu na mnara wa mtandao unaotumia ; na yeye kalipia free massage;

ukifika karibu na manara unapokea mesage hiyo; ata vyuoni wakati wa uchaguzi i kitu cha kawaida

ushauri; angalia jina la mnara ; block huo mnara
ama huo mnara .
 
Inabidi Nec watwambie kama walikuwa wanachukua anwani zetu za mawasiliano ikiwemo simu zetu za mikononi kwa ajili ya kuwapa Wagombea ili watusumbue kwa namna tunayoiona.Binafsi naona watu waliotoa namba zetu za simu kwa hawa wagombea ni Nec.
 
Asante mkuu RB

kwa maelezo yako ni kuwa mgombea huyu anashirikiana na makampuni ya simu ambayo mimi nimeongea nao jana saa tatu usiku wakakataa kuwa hawahusiki. tunahitaji kulindwa kama mtu anauwezo wa kulipia hizo free message inaweza kuwa usumbufu mkubwa kwa taifa. wale watu wanaowalinda wateja wa huduma za simu wanapatikana wapi


Na kuhusu ushauri wako kama nita-"Block" huo mnara nitapata mawasiliano kweli?
 
Labda mahakama za ulaya, lakini hizi zetu hapana. Sheria zetu tumeiga uingereza lakini hatutumii vema kulinda privacy ya mtu.

Mkuu,

muda wa mahakama zetu kuanza kutekeleza wajibu wa kulinda haki ya faragha umewadia. Lakini pia mamlaka husika ziko wapi katika hili?
 
namba zinazotuma sms ni za kawaida mfano: 0766.... au ni zile special mfano; 15566???
Mkuu, yawezekana ni hizozenye tarakimu tano yaani 15566 na sio hizi tunazotumia kwani iliyotumika huwezi kuipiga na kinachojitokeza ni mwisho wa ujumbe ni jina MABULA kana kwamba niliwahi kuhifadhi namba yake. Hivi siwezi mwenyewe kwenda mahakamani na kufungua shauri?
 
Back
Top Bottom