Msaada wa Kisheria tafadhali.

The FaMa

Senior Member
Oct 6, 2011
125
27
Wakuu, salaamu.

Ninaomba msaada wenu wa kisheria au ushauri kisheria kwa jambo hili. Nimeombwa ushauri nami si Mwanasheria, sina ushauri sahihi wa kutoa kwa mtu aliyeniomba ushauri huo.

Jambo lenyewe liko hivi;(mfano) Mimi ninaishi Mwanza, ninahitaji kununua gari toka kwa mtu anayefanya biashara hiyo huko Dar. Bei tuliyoafikiana ni TSh. 7,000,000/- (7.0m/-). Nikaomba nimlipe kwa awamu wakati naye akifanya mchakato wa kuliweka sawa hilo gari (usajili nk). Kwa vile akaunti zetu zipo katika benki tofauti, huyo muuzaji alinipatia akaunti namba ya rafiki yake ambaye iko benki moja na yangu ili iwe rahisi kwangu kumtumia malipo hayo ya awamu ya kwanza. Hivyo, malipo ya kwanza ya TSh. 5,000,000/- (5.0m/-) yakafanyika kupitia akaunti ya huyo rafiki yake muuzaji.

Baada ya muda (say mwezi), nikafika Dar na kuonana na muuzaji katika moja ya Ofisi (siyo yake) na kumkabidhi kiasi cha pesa kilichosalia pasipo kuandikishana popote (yaani kuaminiana) na muuzaji huyo kunieleza kuwa gari husika litakuwa tayari after 2 weeks toka siku hiyo.

Sasa, baada ya hizo 2weeks kupita, huyo muuzaji akaanza kutoa sababu mbalimbali za kwa nini ameshindwa kunipatia hilo gari na kunitaka niendelee kuwa na subira. Tumeendelea kuwasiliana kwa simu (kwa kuwa mimi niko Mwanza na yeye yuko Dar) na kila mara ananiomba samahani kwa kunicheleweshea gari na kwamba anaendelea kuhangaika kulitoa huko bandarini.

Baada ya muda wa miezi 6 kupita pasipo kupata gari yangu, niliamua kumfuata Dar na kumtaka anirejeshee kiasi changu cha pesa nilichompatia (TSh. 7.0m/-). Hivyo, aliniomba tukutane katika ofisi moja ya ndugu yake na kuniomba nimpe muda wa miezi mitatu ya kunirejeshea fedha zangu. Nilikubali na tukaandikishana hapo Ofisini kwa ndugu yake na huyo ndugu yake akiwa shahidi wa makubaliano yetu hayo ya mimi kurejeshewa fedha zangu. Aidha, wakati tukiwasiliana kwa simu (messages na calls), nilikuwa nikihifadhi messages zote tulizokuwa tukiwasiliana wakati nafuatilia gari langu. Pia, siku hiyo ya makubaliano ya kurejeshewa fedha zangu, nilikuwa nikirekodi mazungumzo yetu pasipo wao kujua. Hivyo, ninazo messages na rekodi ya mazungumzo yetu pamoja na ile karatasi ya kuwekea pesa (pay in slip) kwa yale malipo ya kwanza kupitia akaunti ile ya rafiki yake na makubaliano ya kurejeshewa pesa zangu tuliyoandikishana.

Sasa, tatizo nililoombwa ushauri hapa ni, endapo huyo muuzaji akakiuka makubaliano ya kumrejeshea jamaa fedha zake kama walivyoandikishana, je;
1. Atakuwa na nguvu kisheria kumshitaki kudai fedha zake (kwamba anao ushahidi wa kutosha (sufficient evidence))?
2. Kama ndiyo, atamshitaki katika mahakama ipi-ya mwanzo au wilaya au mkazi?
3. Atamshitaki katika Mahakama ya wapi - Mwanza au Dar?
4. Anaweza kuweka Wakili?

Naombeni ushauri ili nimfikishie huyu mtu, kwani ana wasiwasi kuwa huenda ndo keshapoteza fedha zake.

Ni hayo tu, natanguliza shukurani.

 
Haraka Haraka tu huyo jamaa ana ushahidi wa kutosha wa kumshitaki kwa kuwa waliandikishana na amerekodi kila kitu.
Ukija katika swala la mahakama ipi, itakuwa ni mahakama ya wilaya kwa kuwa mahakama ya mwanza uwezo wake wa kusikiliza kesi za madai unakomea kwenye 5,000,000/= na kwa kuwa itakuwa kwenye mahakama ya wilaya basi atakuwa na haki ya kumuweka wakili kama atakuwa na uwezo wa kumlipa.
Kuhusu kisi hii ifunguliwe wapi, kuna maswali kadhaa ya kujiuliza, swali la kwanza ni 'where did the course of action arise' yani hii biashara ilikuwa inafanyikia wapi dar au mwanza au huo mkataba wa kulipana uliingiliwa wapi dar au mwanza?, kwa mfano wako itakuwa ni dar, pia unaweza ukaangalia mdaiwa anapoishi au kufanyia kazi, kama anaishi dar then kesi itafunguliwa dar. kwa hiyo kutokana na mfanao wako basi itakuwa vizuri kama kesi ikafunguliwa katika mahakama ya wilaya ya katika mkoa wa Dar es Salaam.
Naomba kuto radhi kwa kiswakili changu kama kitakuwa hakieleweki but ni matumaini yangu makubwa kwamba nimejibu maswali yako.
For more details email me on Kabarega2012@gmail.com
 
Mkuu Makoroboi, shukrani kwa kunipatia pa kuanzia ushauri. Naamini nitakutafuta kwa ushauri zaidi kupitia anuani yako hiyo.

Thanx.
 
Wakuu, salaamu.

Ninaomba msaada wenu wa kisheria au ushauri kisheria kwa jambo hili. Nimeombwa ushauri nami si Mwanasheria, sina ushauri sahihi wa kutoa kwa mtu aliyeniomba ushauri huo.

Jambo lenyewe liko hivi;(mfano) Mimi ninaishi Mwanza, ninahitaji kununua gari toka kwa mtu anayefanya biashara hiyo huko Dar. Bei tuliyoafikiana ni TSh. 7,000,000/- (7.0m/-). Nikaomba nimlipe kwa awamu wakati naye akifanya mchakato wa kuliweka sawa hilo gari (usajili nk). Kwa vile akaunti zetu zipo katika benki tofauti, huyo muuzaji alinipatia akaunti namba ya rafiki yake ambaye iko benki moja na yangu ili iwe rahisi kwangu kumtumia malipo hayo ya awamu ya kwanza. Hivyo, malipo ya kwanza ya TSh. 5,000,000/- (5.0m/-) yakafanyika kupitia akaunti ya huyo rafiki yake muuzaji.

Baada ya muda (say mwezi), nikafika Dar na kuonana na muuzaji katika moja ya Ofisi (siyo yake) na kumkabidhi kiasi cha pesa kilichosalia pasipo kuandikishana popote (yaani kuaminiana) na muuzaji huyo kunieleza kuwa gari husika litakuwa tayari after 2 weeks toka siku hiyo.

Sasa, baada ya hizo 2weeks kupita, huyo muuzaji akaanza kutoa sababu mbalimbali za kwa nini ameshindwa kunipatia hilo gari na kunitaka niendelee kuwa na subira. Tumeendelea kuwasiliana kwa simu (kwa kuwa mimi niko Mwanza na yeye yuko Dar) na kila mara ananiomba samahani kwa kunicheleweshea gari na kwamba anaendelea kuhangaika kulitoa huko bandarini.

Baada ya muda wa miezi 6 kupita pasipo kupata gari yangu, niliamua kumfuata Dar na kumtaka anirejeshee kiasi changu cha pesa nilichompatia (TSh. 7.0m/-). Hivyo, aliniomba tukutane katika ofisi moja ya ndugu yake na kuniomba nimpe muda wa miezi mitatu ya kunirejeshea fedha zangu. Nilikubali na tukaandikishana hapo Ofisini kwa ndugu yake na huyo ndugu yake akiwa shahidi wa makubaliano yetu hayo ya mimi kurejeshewa fedha zangu. Aidha, wakati tukiwasiliana kwa simu (messages na calls), nilikuwa nikihifadhi messages zote tulizokuwa tukiwasiliana wakati nafuatilia gari langu. Pia, siku hiyo ya makubaliano ya kurejeshewa fedha zangu, nilikuwa nikirekodi mazungumzo yetu pasipo wao kujua. Hivyo, ninazo messages na rekodi ya mazungumzo yetu pamoja na ile karatasi ya kuwekea pesa (pay in slip) kwa yale malipo ya kwanza kupitia akaunti ile ya rafiki yake na makubaliano ya kurejeshewa pesa zangu tuliyoandikishana.

Sasa, tatizo nililoombwa ushauri hapa ni, endapo huyo muuzaji akakiuka makubaliano ya kumrejeshea jamaa fedha zake kama walivyoandikishana, je;
1. Atakuwa na nguvu kisheria kumshitaki kudai fedha zake (kwamba anao ushahidi wa kutosha (sufficient evidence))?
2. Kama ndiyo, atamshitaki katika mahakama ipi-ya mwanzo au wilaya au mkazi?
3. Atamshitaki katika Mahakama ya wapi - Mwanza au Dar?
4. Anaweza kuweka Wakili?

Naombeni ushauri ili nimfikishie huyu mtu, kwani ana wasiwasi kuwa huenda ndo keshapoteza fedha zake.

Ni hayo tu, natanguliza shukurani.


Ushahidi ulio nao unatosha sana, hasa ule wa maandishi. Electronic evidence inakubalika mahakamani. sasa sijui admissibility ya recorded sound as evidence, maana mtu anaweza kuigiza sauti!!!!
Unayemdai yupo Dar hivyo fungua Dar
Mahakama lazima iwe ya wilaya- primary court haina jurisdiction ya kiwango hicho cha hela-
Hopefully this will shade some light
 
1.kinachopelekea mtu kushitaki/kufungua kesi sio ushahidi bali ni "cause of Action" ambayo mpaka hapo kwa maelezo yako unayo dhidi ya huyo mdaiwa wako.

2. unapopeleka mahakamani madai kama hayo usidai ile principal amount peke yake bali pia weka loss of income kama hiyo gari ilikuwa kwa ajili ya biashara ni kiasi gani cha pesa ungepata kwa siku so piga hesabu hadi siku unafungua kesi plus interest.

3. kwa maana hiyoitazidi jurisdiction ya mahakama ya mwanzo.
 
kimsingi nakubaliana na ushauri wa wenzangu waliotangulia ila nadhani ni vyema pia ukajiridhisha na uliyo yaandika katika mkataba wenu yaani "contractual contents" ili kama kuna chochote hakiko vizuri ukishughulikie mapema
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom