NAHITAJI MSAADA WA KISHERIA JUU MIRATHI YA WAZAZI WANGU, Baba yangu alikuwa ni daktari na mama yangu muuguzi(Nurse midwife) wa hospitali ya serikali pale AMANA! walifariki nikiwa mdogo sana, walifariki mwaka 1993, toka wakati huo hakuna mirathi iliyofunguliwa na sasa nimekuwa mtu mzima, nimeajiriwa na watu na jamaa mbalimbali wamekuwa wakiniambia dai stahiki ya wazazi wako, kutoka mifuko yao ya pensheni,kazini na sehemu mbalimbali! sijui lolote na sijui hata nianzie wapi, mwenye uelewa wowote anisaidie, na pia niambie kama ni still possible kuweza kupata hizi stahiki! nitakuwa tayari kukutana na mwanasheria au mtu yoyote anayeweza kunisaidia!