Msaada sticker ya fire

Mess

JF-Expert Member
Mar 2, 2009
661
181
Jamani nimelipia Motor vehicle licence nikaambiwa wameongeza na elfu ishirini ya fire sticker then nikachukue kule bure. Wakanielekeza jengo la ushirika TRA hao 1st floor nimeenda kule nimemkuta receptionist akaniambia pale hawatoi ila nipeleke fire wakakague fire extinguisher then watanipa sticker. Nimeenda kule gari kukaribia tu akaja mlinzi nikamuuliza akasema inabidi ulipe elfu kumi ndo unapata fire sticker. Ndio utaratibu huo?
Msaada.
 
hii kitu inamix kweli.....mwenye kujua atuweke bei ya fire kulingana na cc za gari.....
 
hii kitu inamix kweli.....mwenye kujua atuweke bei ya fire kulingana na cc za gari.....

utaratibu huu mgunu sana, TRA wanakwambia hutakiwi kulipa kitu ukienda kule wanakwambia lazima ulipe elfu kumi, mimi inanichanganya. Hakuna connection kati ya wafanyakazi wa serikali wanakurupuka tu kuanza utaratibu kwa kuwa wanakusanya pesa basi. two days nakimbizana nayo maana najijua traffic akinishika tutaanza mabishano ndo maana naitafuta sana, ili nisiwe na kosa lakini serikali inanilazimisha nikutwe na kosa ili ikusanye tena barabarani elfu 30,000
 
Ni kweli sasa hivi sticker ya fire inalipiwa TRA ikiunganishwa pamoja na Motor vehicle licence LAKINI baada ya hapo hakuna malipo mengine.......unaenda ofisi za Fire na hiyo receipt ya malipo na mtungi wako wa gas, wanatakiwa waukague na kama hauna kasoro wanatakiwa wakuandikie sticker,period.
 
Ni kweli sasa hivi sticker ya fire inalipiwa TRA ikiunganishwa pamoja na Motor vehicle licence LAKINI baada ya hapo hakuna malipo mengine.......unaenda ofisi za Fire na hiyo receipt ya malipo na mtungi wako wa gas, wanatakiwa waukague na kama hauna kasoro wanatakiwa wakuandikie sticker,period.

lakini ndio inavyofanywa hivyo?
 
lakini ndio inavyofanywa hivyo?

Inashangaza sana wakuu. Huku Arusha unalipia 40,000 TRA pamoja na renewal ya road license. Serikali inaongozwa na kichwa cha nazi, kimejaa maji. Wezi wakubwa 40,000 bila mtungi just stiker tu, wanyonyaji wakubwa.
 
Kumbaku:- Huo ndio utaratibu, nadhani ukishajua utaratibu then kinyume cha hapo utajua unatapeliwa,,,,,,,,itakuwa ni juu yako kukomaa usilipe hicho cha juu au uwalipe upewe sticker,,,,,,,binafsi sijawahi kulipa tofauti na inavyotakiwa
 
Hawa wanafanya wizi. Mm nimelipia m/licence mwezi wa tana mwaka huu tar.8 wakalazimisha nilipie fire 20,000, cha ajabu baada ya kupewa naona inaanza tar 1 julai 2011 na kuexpire 30 june mwaka huu, si wizi huo? Kwann isiwe kama ya motorvehicle ambayo inaexpire 2013? Inabidi nikate nyingine sasa hv. Huu ni wizi wa waziwazi kabisa.
 
hii kitu inamix kweli.....mwenye kujua atuweke bei ya fire kulingana na cc za gari.....

preta, tatizo sio kujua ni kiasi gani.

Je kuna uhalalina justification wa kulipa hicho kiasi?

Kwa nini ulipe 30,000 kwa ajili ya kukagua fire extinguisher ndogo inayokaa kwenye gari? Ujazo wa hiyo fire extinguisher kwa kwa bei hiyo, je kiwanda kama breweries au TCC watatakiwa kulipa kiasi gani? Kama wao wanalipa kidogo ni nini kigezo cha wao kupunguziwa?

The million dollar question, gari ni yangu, nimeinunua kwa jasho na nguvu zangu kwa nini unilazimishe niweke fire extinguisher. Tukizilea sheria kama hizi, kesho watakuja BASATA na kusema kuwa shauri kuna redio kwenye gari basi tulipie miziki tunayosikiliza ndani ya gari.

Hii sheria haifai, watuachie tukatae kulipa watupele mahakamani ili tujitetee wanantumia mgongo wa TRA kupata hizo fee za kidhalimu kirahisi.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom