Mshana Jr
Platinum Member
- Aug 19, 2012
- 269,640
- 697,940
Wandugu, jamaa na rafiki zangu wanyonge.. Nimekuja kwenu rasmi kwa ushauri na msaada.. Nimekwama na niko njiapanda. Msaada wako kimawazo na ushauri ni muhimu sana kipindi hiki kigumu nilichonacho
Mimi ni Mwenyekiti na Mkuu wa Kijiji chetu. Naomba nisikitaje jina kwa sasa. Kwa sababu maalum mbalimbali
Iko hivi mwezi uliopita hapo kijijini kwetu kulitokea tatizo kidogo.. In fact hilo tatizo limetokea huko vijiji vya mbali mpaka kufika kwetu. Basi mimi nikajiongeza. Jioni moja nikamuita kwa siri sangoma wetu mkuu hapo kijijini kwetu.. Tukakaa nje penye giza pembeni ya kilabu chetu cha ugimbi. Nikamnunulia KIPIMO kimoja na mimi nikaagiza KIPIMO
Tukanywa tukafurahi. Mimi nina kautaalam kidogo na vipimo hivyo sangoma alifurahi sana mpaka nikamuongeza na kingine (pengine hapa ndio niliharibu) kwakuwa katika jambo nililomuitia akanishauri kwa kipindi hiki nikimbie maramoja kijijini kuwasalimia wazee na nikirudi lile tatizo litakuwa limekwisha kwakuwa linapita tu tena ni la muda mfupi
Nimeapa kutoamini tena ushauri wa kilabuni.. Maana sasa napata tabu sana... Ubao wa matangazo kijijini kwetu hauishi kuandika vijembe juu yangu.. Naambiwa eti nimekimbia kaya na kwenda kujificha kwetu.. Eti kwamba mkubwa wote mimi bado muoga halafu napenda kudeka sana
Natamani sana kurudi kwangu.. Tena sana lakini sijui naanzia wapi... Hapa nilipo ni usiku mwingi lakini sina usingizi wala amani ni mawazo tele kichwani... Nitarudije kwangu? Naona wana kijiji wanachonga sana juu yangu
Uso umeumbwa na soni kama sio haya.. Lakini hilo sio tatizo.. Tatizo langu kubwa ni hofu je kule kwangu wakati nikiwa sipo hawajanitegea mbigili kweli? Unajua wabaya wapo popote?
Nishauri kwa hekima
Nishauri kwa weledi
Au nishauri vyovyote
Nahitaji msaada wako kimawazo nimechoka kukaa kijijini nataka nirudi kwangu
Kuna bundi analia hapo nje sijui anataka nini tena huyu.. Sijui katumwa?
Jr
Mimi ni Mwenyekiti na Mkuu wa Kijiji chetu. Naomba nisikitaje jina kwa sasa. Kwa sababu maalum mbalimbali
Iko hivi mwezi uliopita hapo kijijini kwetu kulitokea tatizo kidogo.. In fact hilo tatizo limetokea huko vijiji vya mbali mpaka kufika kwetu. Basi mimi nikajiongeza. Jioni moja nikamuita kwa siri sangoma wetu mkuu hapo kijijini kwetu.. Tukakaa nje penye giza pembeni ya kilabu chetu cha ugimbi. Nikamnunulia KIPIMO kimoja na mimi nikaagiza KIPIMO
Tukanywa tukafurahi. Mimi nina kautaalam kidogo na vipimo hivyo sangoma alifurahi sana mpaka nikamuongeza na kingine (pengine hapa ndio niliharibu) kwakuwa katika jambo nililomuitia akanishauri kwa kipindi hiki nikimbie maramoja kijijini kuwasalimia wazee na nikirudi lile tatizo litakuwa limekwisha kwakuwa linapita tu tena ni la muda mfupi
Nimeapa kutoamini tena ushauri wa kilabuni.. Maana sasa napata tabu sana... Ubao wa matangazo kijijini kwetu hauishi kuandika vijembe juu yangu.. Naambiwa eti nimekimbia kaya na kwenda kujificha kwetu.. Eti kwamba mkubwa wote mimi bado muoga halafu napenda kudeka sana
Natamani sana kurudi kwangu.. Tena sana lakini sijui naanzia wapi... Hapa nilipo ni usiku mwingi lakini sina usingizi wala amani ni mawazo tele kichwani... Nitarudije kwangu? Naona wana kijiji wanachonga sana juu yangu
Uso umeumbwa na soni kama sio haya.. Lakini hilo sio tatizo.. Tatizo langu kubwa ni hofu je kule kwangu wakati nikiwa sipo hawajanitegea mbigili kweli? Unajua wabaya wapo popote?
Nishauri kwa hekima
Nishauri kwa weledi
Au nishauri vyovyote
Nahitaji msaada wako kimawazo nimechoka kukaa kijijini nataka nirudi kwangu
Kuna bundi analia hapo nje sijui anataka nini tena huyu.. Sijui katumwa?
Jr