Msaada mtoto anaharisha.

mapipando

JF-Expert Member
Jun 8, 2015
2,921
3,549
Habari wakuu,
Mwanangu anatimiza umri wa miezi minne keshokutwa,siku ya jumamosi usiku alianza kuharisha na kesho yake tukampeleka hospitali akapimwa na kuonekana hana malaria bali kuna dawa alipewa ya kuzuia kuharisha.

Kwa namna moja ama nyingine dawa zimesaidia angalau kupunguza idadi ya kuharisha kwa siku, mfano usiku wa jana hakuharisha kabisa bali kuanzia mchana hadi jioni aliharisha mara tatu tu.

Usiku wa kuamkia leo pia hajaharisha ila asubuhi kaharisha na mwishoni akawa anatoa choo kilichochanganyikana na damu kwa mbali.
Na hapo ikumbukwe kuwa mara ya kwanza alipoanzakuhara alikuwa akitoa choo chenye damu kwa mbali.

Nimeleta tatizo hili kwenu ili nipate kusaidiwa ushauri.

Jambo lingine,je kumbadilishia mtoto maziwa ya Lactogen1 na kumpa ya ngo'mbe ni sawa?

Natanguliza shukrani zangu za dhati kwenu wakuu.
 
Mkuu chemsha maji kama kitre moja weka 1/4 kijiko cha chai chumvi na kijiko kimoja cha chai sukari yachanye mpe mtoto anywe wakati mnakwenda hospitali
 
Mkuu chemsha maji kama kitre moja weka 1/4 kijiko cha chai chumvi na kijiko kimoja cha chai sukari yachanye mpe mtoto anywe wakati mnakwenda hospitali
Na vp kuhusu kumbadilishia maziwa mkuu.
 
Mimi hua nachukulia kuharisha au kutapika kama kitu kizuri. Mfano nimapokuwa na Malaria, nikitapika hasa nikitapika nyongo basi hiyo ni dalili ya kupona na hata kama najisikia vibaya, basi huwa napata ahueni.
Pia kama nimekula kitu kibaya naumwa tumbo, nikiharisha natoa kile chakula kichafu na baada ya muda napata ahueni.
Sijui wenzangu mnachukuliaje but for me naona ndio pona yangu...
 
Pole sana mdau,mwezi uliopita wanangu walikuwa na tatizo hilo.
Kwanza hakikisha kila anapoharisha mpe maji ya ORS ni muhimu sana kwasababu yanarudisha nutrients anazopoteza kwa kuharisha.
Pili,muone Dr wa watoto haraka sana.Fuata ushauri wa Dr ndugu.

Kuhusu maziwa ya Ngo'mbe.Nakushauri acha kabisa kumpa mtoto kwasababu kwenye maziwa ya Ngo'mbe kuna bacteria huwa hafi hata yachemke vipi ndo maana inashauriwa kumpa mtoto maziwa ya KOPO uliyoyataja kwasababu hayana huyo bacteria. KUMBUKA MAZIWA MAZURI NI YA MAMA TU.

Nikemkuta mtu anampa maziwa ya Ngo'mbe mwanangu...atanikoma. First born ametusumbua sana kwasababu alikuwa na bili kabisa ya maziwa ya Ngo'mbe.


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mimi hua nachukulia kuharisha au kutapika kama kitu kizuri. Mfano nimapokuwa na Malaria, nikitapika hasa nikitapika nyongo basi hiyo ni dalili ya kupona na hata kama najisikia vibaya, basi huwa napata ahueni.
Pia kama nimekula kitu kibaya naumwa tumbo, nikiharisha natoa kile chakula kichafu na baada ya muda napata ahueni.
Sijui wenzangu mnachukuliaje but for me naona ndio pona yangu...
Oya.kile kitabu ulipata.the perfect bet.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
1. Kwa nini unampa maziwa ya kopo katika umri huo? (Hii ni wk ya unyonyeshaji) Inashauriwa mtoto asipewe chochote hadi miezi 6.
2. Kama walivyoshauri waliotangulia mpe ors na ped zinc kwa siku 10 hata kama amefunga.
3. Mara nyingi husababishwa na virus, hivyo antibiotic haina nafasi.
4. Aendelee kunyonya.
5. Usafi ni muhimu kuzingatiwa hasa vyombo unavyompia maziwa.
Wengine wataongezea.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mkuu chemsha maji kama kitre moja weka 1/4 kijiko cha chai chumvi na kijiko kimoja cha chai sukari yachanye mpe mtoto anywe wakati mnakwenda hospitali


umnikumbusha mbali! nakumbuka siku 1 mwanangu amehara had amelegea,yaan nilijua nampoteza mtoto wetu! mama m1 hosp akaknipokea mtoto hosp akampa ORS!..jaman pale pale katoto kakaniangalia na macho yakiwa na uzima tena!toka hapo naiheshim sana hii dawa jaman
 
Back
Top Bottom