Msaada: Gari inawaka taa ya ‘check engine’

Mar 29, 2020
6
3
Habari za leo,

Ndugu zangu naamini kuna mafundi wazuri tu humu na wazoefu wa masuala ya magari
Nina tatizo ktk gari yangu aina ya Toyota Grand Mark 2 (Gx 110 injini ni 1G kavu). Kwa masiku kadhaa ya wiki iliyopita hapa Dar kulikuwa na mvua sana.

Historia fupi ya tatizo
Sasa kwa maeneo nayokaa kuna madimbwi makubwa mawili nikipita gari inazama hasaaa na tairi nimefunga ni saizi 15 hivyo ipo chini.

Pia nina shamba maeneo ya Mkuranga ndani ndani kdg ambapo huwa naenda sana hasa ktk wakati huu wa mvua kutokana na uwekezaji nilioweka huko. Sasa barabara ukweli zina madimbwi sana makubwa kwa madogo. Kwa masiku ya karibuni imekuwa nikipita kuna taa kwenye dash board inawaka baada ya kutembea.

Nikiizima gari na nikiiwasha tena taa inakuwa imezima. Lakini nikipita tu katika madimbwi inafanya hivi baada ya mwendo kidogo. Je, inawezekana ikawa shida ni maji yameingia katika sensa au injini ina tatizo?

Kuna fundi umeme (hakufanya diagnosis) nilimwendea na kumuuliza akasema ni kwa sababu ya maji tu huenda yanaingia kwenye sensa nisiwe na khofu.

Naomba ushauri wenu.

20200424_120214.jpg

Naambatanisha na picha niliipiga wakati ilipowaka

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Nilichogundua mark2 gx110 zinazo hilo tatizo la check ingine, gari yangu ya kwanza kumiliki ilikuwa gx110 na ilikuwa na tatizo hilo hilo ambalo ilifanyika diagnosis na kugundua plug moja ya vvti ilikufa. Na jamaa yangu nae juzi ya kwake ilikuwa hivyo hivyo akatengeneza sijui tatzo lilkuwa nini.

Mimi sio fundi nimetoa uzoefu wangu tu kuhusiana na gx110.
 
Nilichogundua mark2 gx110 zinalo hilo tatizo la check ingine, gari yangu ya kwanza kumiliki ilikuwa gx110 na ilikuwa na tatzo hilo hilo ambalo ilifanyika diagnosis na kugundua plug moja ya vvti ilikufa. Na jamaa yangu nae juzi ya kwake ilikuwa hivyo hivyo akatengeneza sijui tatzo lilkuwa nini.

Mimi sio fundi nmetoa uzoefu wangu tu kuhusiana na gx110.
Ahsante Mkuu
Je, kuna dalili gani nyingine ilikuwa inaonyesha zaidi ya hy ya kuwaka taa ya check injini?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Jana tu nilioona GX110 Machinga complex ina shida hio hio ila walishaitatua yenyewe oil ilikua haipandishi juu
 
its not an error, its a warning

its not general, it is code-specific
Mkuu inaweza isiwe error ila taa ya check engine ipo general inaweza ikawaka sababu ya vitu vingi. ndo maana nikamshauri aende kwa mtu mwenye diagosis tool ili aweze kuona hiyo code ya kitu sababishi kilichofanya hiyo taa iwake
 
Hapana, hakuna mabadiliko ya muungurumo na nilipita kwa fundi makenika mmoja wa injini kuuliza baadhi ya mambo juu ya injini na akawasha gari akasema ipo sawa

Sent using Jamii Forums mobile app
Sasa fanya reset ya ECU yako. Jinsi ya kureset, Chomoa betri subiri dakika chache kadhaa, irudishe tena. Washa gari tembelea kama kawaida, ikiwaka tena, ipeleke ikafanyiwe diagnosis. kama haijawaka baada ya kilomita nyingi (walau 100KM ivi) ujue ilikuwa na hashuo tu.

Ikiwaka tena, hebu fungua coils na plugs zitizame hali yake, kama zina dalili kuwa zimepata maji japokuwa it is hard to imagine vipi maji ya mvua yafike kwenye coils na plugs wakati una bonnet.

Mi ningekushauri uende kufanya engine diagnosis ujue fitna iko wapi
 
taa inawaka sababu kuna sehem kuna shida au kuna hali siyo yakawaida imerepotiwa na kwakuwa gari huwa unaidumbukiza kwenye maji basi yawezekana kabisa kuna mahala maji huwa yanaingia na kureport shida taarifa zinakwenda kwenye ECU .

Hapo kwa urahisi zaidi nenda kampime pindi gari imewaka taa utapata jibu sahihi huwa inawaka kwasababu gani.. au kama unaweza mm naweza nikakuelekeza ukaipima mwenyewe manually na ukishanipa jibu la fault gani inasoma nitakwambia shida ni nn hapo??. au naweza nikakupa kila kitu umalize mwenyewe
 
taa inawaka sababu kuna sehem kuna shida au kuna hali siyo yakawaida imerepotiwa na kwakuwa gari huwa unaidumbukiza kwenye maji basi yawezekana kabisa kuna mahala maji huwa yanaingia na kureport shida taarifa zinakwenda kwenye ECU . hapo kwa urahisi zaidi nenda kampime pindi gari imewaka taa utapata jibu sahihi huwa inawaka kwasababu gani.. au kama unaweza mm naweza nikakuelekeza ukaipima mwenyewe manually na ukishanipa jibu la fault gani inasoma nitakwambia shida ni nn hapo??. au naweza nikakupa kila kitu umalize mwenyewe
Mkuu kwa manufaa ya umma, naomba utupe hiyo elimu ya kupima manually unafanya je?
 
Msaada jaman,
Gearbox ya gar yang aina ya corollar 4E 111 imezingua ikatafuna baadh ya meno hasa pinion, fundi wang anasema Automatic gearbox haitengenezeki. Je n kwel swez kuitengeneza ikarud kama mwanzo?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
taa inawaka sababu kuna sehem kuna shida au kuna hali siyo yakawaida imerepotiwa na kwakuwa gari huwa unaidumbukiza kwenye maji basi yawezekana kabisa kuna mahala maji huwa yanaingia na kureport shida taarifa zinakwenda kwenye ECU . hapo kwa urahisi zaidi nenda kampime pindi gari imewaka taa utapata jibu sahihi huwa inawaka kwasababu gani.. au kama unaweza mm naweza nikakuelekeza ukaipima mwenyewe manually na ukishanipa jibu la fault gani inasoma nitakwambia shida ni nn hapo??. au naweza nikakupa kila kitu umalize mwenyewe
Naomba elimu hy ya kuipima Mkuu kwa wote hapa ubaoni

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mrejesho
Sijafanya jambo lolote ie diagnosis nk. Nilichukua ushauri tu wa fundi umeme mmoja niliebahatika kuonana nae kuwa kuna uwezekano maji hufika mahala ambapo si sahihi kufika ndiyo maana taa inawaka, alitumia kigezovha gari ipo chini sana. TAA YA CHEKI INJINI HAIJAWAKA TENA TOKA NILIVYORIPOTI jambo hili hapa na kwa umbali nimeshatembea zaidi ya kilomita 500 kwa sasa. Na nimepita tena kwenye maji lkn haijawaka

Je nitakuwa sahihi?
Nilichoamua kufanya nimeipandisha juu kidogo kwa kuweka spacer za mm 20 hv na kisha nataka nifunge tairi saizi 18 nyembamba. Lengo likia ni kuiinua juu kdg kutoka tairi size 15. Wataalam hili mwalionaje? Au mnaushauri gani? cc
LEGE

Sent using Jamii Forums mobile app
 
taa inawaka sababu kuna sehem kuna shida au kuna hali siyo yakawaida imerepotiwa na kwakuwa gari huwa unaidumbukiza kwenye maji basi yawezekana kabisa kuna mahala maji huwa yanaingia na kureport shida taarifa zinakwenda kwenye ECU . hapo kwa urahisi zaidi nenda kampime pindi gari imewaka taa utapata jibu sahihi huwa inawaka kwasababu gani.. au kama unaweza mm naweza nikakuelekeza ukaipima mwenyewe manually na ukishanipa jibu la fault gani inasoma nitakwambia shida ni nn hapo??. au naweza nikakupa kila kitu umalize mwenyewe
Mkuu hii ishu imenitokea sasa hivi baada ya leo asubuhi kumwagia maji kwenye kioo cha mbele kukisafisha! Naomba nielekeze cha kufanya
 
Back
Top Bottom