Msaada: External HD inaandika Format kila nikiiweka kwenye PC

Masterproud

JF-Expert Member
Sep 14, 2012
440
116
Habari ya saa hizi wana JF. Samahani naombeni msaada, Eternal Hard Disk yangu (Transcend 500 GB) Inaandika Format kila nikiichomeka kwenye PC. ndani ina data zangu nyingi sana muhimu. Nimejaribu kuiweka kwenye computer mbalimbali bado kila nikiiweka kabla ya kufunguka inaleta msg kuwa natakiwa niiformat. juzi nimejaribu kutaka kuiformat lakini pia ikagoma kuformat ikaandika msg 'window is unable to format'. Naombeni msaada nifanyeje? Je ikiwezekana kuformat data zangu zinawezaje kupatikana tena? Asante
 
Naomba uingie youtube u search kuhusu tatizo lako. Kuna tutorial nying sana zinazoeleza kuhusu issue yako.
Mm km kuna kitu kinanishinda naingia google moja kwa moja
 
Ukiformat data zinapotea zote,, jaribu kuiscan kwa antivirus ambayo iko active, kma ikidetect virus wafute..

Jaribu njia hyo,,ikikataa (japo najua itakubali 89%) tumia hivyohivyo bt uwe una *cancel kile kiwindow cha kuformat.
 
Anagalia kwanza kuptia disk management ipo katika format gan??? NTFS au RAW
 
Habari ya saa hizi wana JF. Samahani naombeni msaada, Eternal Hard Disk yangu (Transcend 500 GB) Inaandika Format kila nikiichomeka kwenye PC. ndani ina data zangu nyingi sana muhimu. Nimejaribu kuiweka kwenye computer mbalimbali bado kila nikiiweka kabla ya kufunguka inaleta msg kuwa natakiwa niiformat. juzi nimejaribu kutaka kuiformat lakini pia ikagoma kuformat ikaandika msg 'window is unable to format'. Naombeni msaada nifanyeje? Je ikiwezekana kuformat data zangu zinawezaje kupatikana tena? Asante
Possibly ilichomolewa bila kufuata utaratibu hivyo hata ukiformat haitakubali
 
Hdd huwa haifi wadau so kama kuna data sensitive peleka kwa watala wwtaziondoa then utaitupa
 
Kama ni RAW hiyo ni ya kutupa huwezi kui recover
Hapana mkuu, kama ipo kwenye format ya RAW anaweza kurecover data zake na kuformat katika file system nyingine, cha muhimu inategemea na uwezo wake kwenye suala la IT tu, mi nimekuwa nikiletewa hdd nyingi za namna hiyo na zinapona
 
kama sio hardware failure leta tukusaidie ku recover. kuanzia 100 000 kutegemeana na condition ya HDD. Non refundable in any case
 
usiiweke ktk computers au kujaribu kufanya chochote. Unazidi kupoteza uwezekano wa kuzipata data zako
 
Hapana mkuu, kama ipo kwenye format ya RAW anaweza kurecover data zake na kuformat katika file system nyingine, cha muhimu inategemea na uwezo wake kwenye suala la IT tu, mi nimekuwa nikiletewa hdd nyingi za namna hiyo na zinapona
Flash disk ikiwa na format ya RAW unafanyaje kui recover?
 
Flash disk ikiwa na format ya RAW unafanyaje kui recover?
Kuna njia kibao, kama unataka command line au software inategemeana na skills za anayefanya kazi hiyo ya kuformat haswa kwenye masuala ya IT, May be we unataka njia ipi nikupe namna ya kufanya!?
 
Kuna njia kibao, kama unataka command line au software inategemeana na skills za anayefanya kazi hiyo ya kuformat haswa kwenye masuala ya IT, May be we unataka njia ipi nikupe namna ya kufanya!?
Sotware naona ndo itakuwa rahisi zaidi. Nipe link nidownload hiyo software
 
Sotware naona ndo itakuwa rahisi zaidi. Nipe link nidownload hiyo software
Best software ya kurecover data ambayo huwa natumia na nikubali ni EaseUS Data Recovery, Hii ni ya kununua ila kama huwezi kununua unaweza kutafuta cracked kwenye torrents website.
Baada ya kufanya data recovery kwa kutumia EaseUS Data Recovery unaweza ukatumia aidha kati aya hizi Software kubadili RAW file system kwenda NTFS file system
1. M3 RAW Drive recovery (inauzwa ila unaweza kutafuta cracked)
2. TestDisk (freeware)
3. MiniTool Partition Wizard (freeware na ya kuuza) mi huwa naikubali sana hii kwa sababu una options nyingi kulingana na cause ya hiyo RAW file system, maana RAW file system huwa inasababishwa na factors mbalimbali kama vile damage partition table, bad sectors, virus attacks, power outage, file system structural damage, na nyingine nyingi tu, sasa kwa kutumia hii Software ina uwezo wa kusolve tatizo kulingana na causes ya hiyo RAW file system
NB: Ukitumia EaseUS Data Recovery (kwa ajili ya data recovery) na MiniTool Partition Wizard (drive recovery) unaweza kuokoa data na hdd ikiwa utakuwa na uzoefu wa kuzitumia au utazitumia effectively unless tatizo liwe ni physical hdd damage hapo itakuwa 50/50
 
Back
Top Bottom