Ruhazwe JR
JF-Expert Member
- Jan 31, 2011
- 3,403
- 920
naomba kujua juu ya baba na mama wanapotengana,na baba akataka apewe mtoto wake lakini mtotohuyu ana umri wa miaka 2 na nusu je utaratibu unakuaje?
mkuu nashukuru sana kwa kunipa mwelekeo kwani kaka yangu yamemkuta na inaonekana kabisa shemeji hata weza kumlea mtoto kwa sababu za kitabiaKulingana na sheria za Tanzania wazazi wanapotengana, uamuzi wa mahakama kuwa nani akae na watoto huwa unaangalia kanuni ya 'welfare of the child',' je mtoto akikaa na nani kati ya wazazi wake atapata malezi na makuzi mazuri'. Pia kuna dhana inayokanushika kuwa mtoto chini ya miaka saba (7) anapaswa kuwa chini ya uangalizi wa mama yake.
Nidhahiri kuwa mtoto wa miaka miwili na nusu anapaswa kuwa chini ya uangalizi wa mama yake,mama anaweza kunyimwa kukaa na mtoto ikiwa kuna sababu maalum mfano ana matatizo ya akili au anamyanyasa mtoto n.k.
NB: kama una kesi kama hii ni vyema ukatafta mwanasheria akupe ushauri zaidi.