Hello mwezi uliopita nlikuja kuomba ushauri humu kuhusu nmekwama kufanyiwa recategorazation sababu nmesoma tax na watu wakanishauri nkamwone RAS sasa kuna mtu alikwenda kuongea na RAS na akasema akipata nafasi ataangalia vizuri kwenye muundo..sasa kiukweli Mimi natamani tu kuacha kazi ila nakosa msaada kwa watu wanaonizunguka hakuna hata mmoja anaekubaliana na Mimi,,maana nawaza je RAS akisema hyo nafasi hakuna kabisa niendelee kuwa mhudumu wa afya milele?no siko tayari na mi hivi kabla sijapata hii kazi nlipata kazi ya data clerk water reed program na kiukweli mshahara ulikuwa mzuri lakni watu wanashauri ni bora niende serikalini lakni serikali yenyewe ndo hii na recategorazation imebuma jamani naomba mnishaur nfanyeje ili hawa watu wangu muhimu wanielewe niache tu kazi na si kwamba hawana uwezo wa kunipa mtaji wanao ila mmoja anaamini kwamba serikalini tu ndo ntafanikiwa(mzazi) mwngne kila siku ananilaumu sana kwa kuacha kazi water Reed maana hakutaka kabisa (mume) lakini hana msaada wowote na huko anakofanya kazi nkimwambia anitafutie kazi anasema kuliko Mimi kufanya kazi mgodini bora tuachane ..jamani Mimi nahitaji kuacha kazi kiroho safiii kabisa maana siwezi kuwa mhudumu wa afya milele never ila ntumie njia gani Hawa watu wanielewe na wanipe mtaji na hata wakikataa mtaji naweza nkapata ila ndo watu wangu wa karbu hawataki nshaurini..watu wangapi wanafanya biashara na wako vizuri tu ..plz mnishauri Mimi kama mdogo wenu nko kwenye mawazo makubwa sana najiona mkosefu kuacha kazi yangu ya mwanzo