Honorables
New Member
- Feb 26, 2020
- 2
- 3
Uzi huu ni msaada mkubwa kwa kijana mwenye malengo na focus ya mafanikio.
"Huku" wapi mkuu ?Kuna gold detectors za aina nyingi huku ila nataka kujua ipi ni nzuri na je nikileta ntauza?
Zipo za Mjerumani nzuri sana zingine mpaka 15m
AiseeNdugu we muongo faida EF 2 au EF 3
Nina rafik angu anachukua dhahabu msumbiji eneo la kaguruwe ana kuja uza dar kila baada ya wiki moja,
gram 100 Sawa na milioni 10 gram ananunua laki sokoni inacheza laki na 25 ivi,
this time Mara ya mwisho katoka dar na faida ya 1.8million akitoa process zingne ndio anabaki na iyo 1.8 m
Au labda sijaelewa maelezo yako vizuri lakin kama ndio ayo hapo juu faida ef 3 big no ukitaka nikupe na namba ya simu muulize ata kwambia na kama upo dar wiki hii anakuja apo kuuza dhahabu muulize.
Aaah sawa, ngoja basi nikitulia nitakueleza kwa ufahamu trend ya utafutaji wa dhahabu ili pamoja na wadau wengine tufanye tathmini ya pamoja kama biashara ya vipimo kwa sasa itafaa au haitafaa.UK
Dili lipo mkuu au unazijua nzuri
Kuna gold detectors za aina nyingi huku ila nataka kujua ipi ni nzuri na je nikileta ntauza?
Zipo za Mjerumani nzuri sana zingine mpaka 15m
Nitakujibu kwa majibu marefu kidogo, kuwa mvumilivu, tiririka nami.
Majibu haya ni kwa mujibu wa my personal experience (nimezaliwa na kukulia katika moj ya maeneo ya uchimbaji wa madini ya dhahabu nchini Tanzania)
Hivyo kunaweza kuwa na mabadiliko kidogo katika hoja zangu kulingana na hali ilivyo katika maeneo yenye madini nchini.
Tutazame kwanza mabadiliko ya trends za teknolojia za kupata dhahabu na nyakati zake.
1. Kuokota dhahabu maeneo mbalimbali (kwenye surface land) hasa ya maeneo ya mitoni, n.k :
Hizi ni zama za zamani sana, hasa kabla ya uhuru na kabla ya kuja watu weupe barani Afrika. Kama umeshawahi kusikia kwamba zamani dhahabu zilikua zinatumika kama "kete" za kuchezea bao. It was that simple, that abundant.
2. Kuchimba ili kupata "mchanga wa dhahabu" na kuosha ili kuipata dhahabu yenyewe (kusekesa/kuchekecha, kupiga kalai):
Hapa kilichokua kinatafutwa ni "mchanga wa dhahabu", na hatimaye unaoshwa kwa njia nilizotaja hapo juu ili kupata madini ya dhahabu. Ni njia ambayo inahitaji maji na kinachopatikana hapa tunaweza kusema ni "pure gold".
3. Kuchimba mashimo marefu (long bases) ili kutafuta MIAMBA inayoambatana na dhahabu:
Katika njia hii miamba hiyo hulainishwa (kuwa mawe madogo madogo), kutwangwa (kupata unga unga) na hatimaye "kukamatishwa" kwa kutumia Mercury ili kupata dhahabu. Mercury inafanya selective extraction ya gold kutoka kwenye unga (Ore) inayojumuisha metali nyingine.
Baada ya kazi ya Mercury, yale mabaki ("baada ya dhahabu" kuwa extracted) yalikua ama yakitupwa, au kutunzwa kwa ajili ya kurudia zoezi la extraction ya Mercury wakati ujao yatakapokua mengi zaidi. Logic hapa ni kwamba Mercury haifanyi extraction ya 100%. Katika point namba 5 tutaanzia hapa kwenye haya MABAKI au MARUDIO au MASAINENTI.
4. Kutumia "vipimio" (Gold detectors) kupata dhahabu:
Hii hasa ni kwa ajili ya kupata dhahabu zilizo kwenye surface (hazikuonekana kwa macho na kuokotwa hapo zamani), zile za kwenye "mchanga wa dhahabu" na kwa uchache kwenye "miamba yenye dhahabu".
Kwa huku kwetu, teknolojia hii imeanza kuchipukia mwaka 2000, imekuja ku peak miaka ya 2005-2010. Kuanzia miaka ya 2010 kuja juu vipimio vilianza kupungua kutokana na uhaba wa "aina ya dhahabu" ambazo vinagundua. Hivyo wenye vipimio walianza kwenda maeneo ya mbali (kutoka huku niliko) ili kutafuta dhahabu zinazoweza kutambuliwa na hivi vipimio. Mfano Mpanda, Maeneo ya nchi ya Msumbiji, Zambia n.k
Ila kwa ujumla ni kwamba kwa sasa kumiliki kipimio imekua kama ni old fashioned way ya kutafuta dhahabu, siku za kulala njaa zinakua ni nyingi sana. Kwa maneno mengine hapa nakuambia kwamba kuwa makini sana kama kweli utaamua kuleta hivyo vifaa. Hali yake ndivyo ilivyo.
Mifano ya "aina" za vipimio (gold detectors) iliyokua maarufu ni kama vile GP, SD, XT, GMT, Fisher, n.k
5. Ujio wa "Leaching plants" pamoja na "Elution" ili KUOZESHA "marudio" (Rejea point namba 3 hapo juu) na hatimaye kupata kupata dhahabu:
Yale mabaki au marudio baada ya shughuli ya Mercury, hapa yanaozeshwa kwa kutumia kemikali kadhaa kwenye mtambo wa uchenjuaji dhahabu na hatimaye kuchomwa ili kuipata dhahabu yenyewe.
Kutokana na hili, the more marudio unazalisha, the more likely kwamba utachenjua mara nyingi na hivyo utapata dhahabu kwa wingi zaidi.
Maana yake sasa, utahitaji maeneo mengi yenye miamba ya dhahabu, utahitaji mitambo mingi ya kusaga mawe (yanaitwa makarasha, yaani crushers) kutengeneza "marudio" mengi zaidi.
Kwa sasa teknolojia hii ya kumiliki "makarasha" ndio ina peak sana kwa "huku kwetu".
6. CIP & CIL Major plants:
Hii ni advanced level ya njia namba 5 hapo juu, inakua na ufanisi mkubwa zaidi katika kuozesha, inachukua large volumes ya marudio at a time na pia ina extract more gold.
Hata hivyo inahitaji mtaji mkubwa na miundombinu thabiti (hasa umeme) ili kuiendesha. Kwahiyo hizi bado ni chache sana.
Unaweza ukaona kuwa katika scenario zote 6 hapo juu (of course kuna zaidi) utaona dhahabu ni ileile, ila kinachobadilika ni TEKNOLOJIA inayotumika kuipata.
Hivyo nakusihi ufanye maamuzi juu ya biashara hiyo kulingana na uhalisia wa mambo yalivyo.
NB: Hii inahusu zaidi wachimbaji wadogo na angalau kidogo wachimbaji wa kati.
Andiko langu si msimamo wa sekta ya madini ya nchi nzima, ila angalau kwa 80% liamini na uliafuate.
Ukitaka nieleze fursa "za kibiashara" zilizopo katika sekta ya madini na mnyororo wake wa thamani, nitafanya mambo mawili yafuatayo:-
A. Nitakuomba unipe muda
B. Nitakueleza kinagaubaga.
Uwe na siku njema.
Hakika wewe umetema pointi za maana na zinazoonyesha uhalisia wa biashara tofauti na wengi wetu hupenda kusikia stori za vijiweni, maake kama faida ingekuwa kubwa sana tunavyoaminishwa basi wengi wangefanya.Hii biashara ni tofaut na tunavyohadithiana.kwanza inahtaj roho ngumu na ukatil ndani yake.na ukiwa mtu Wa dini huwezi Fanya hii bizn..kiufup kwenye biashara kama hz kutoboa ni ngekewa ya MTU.ili upate faida ni lazima uwe mdanganyifu.faida ya dhahabu inatokana na umenunuaje na ubora wake..mana sio kwamba hiyo 130000 ni kwa kila dhahabu.apana hiyo ni kwa zile pure yani karat 24.na wengi wanafeli kwenye hili unaenda porini unanunua kwa 95000 per gram.unakuja sokoni unakuta ni karat 18 ambayo ukitajiwa bei unaweza lia.bei unambiwa hii tunanunua 75000.ukipiga hesabu apo kila grm imekata 20000.bado ikichomwa inapungua.kama ulikuwa umebeba grm 50 lazma ikate 2.5,au tatu kabisa.kwa hiyo apo ni kucheza na soko +asilimia na kuminya mzani.ukipoteza point moja ni sawa na kudondisha 10000..ila ukiipatia unawezatoa ushuda aljazeera a
Mkuu mimi nanunua dhahabu. Mara nyingi inakuja dhahabu IL yopembuliwa, ila Kuna wakati yanakuja mawe nayadhamini mwenye nayo anasaga kisha ananiuzia dhahabu. Hivyo kuwa na karasha imepanua wigo mwingine wa miradi yangu maana mwezi October nitatoa mlima. Nilikuwa nasagia kwa jamaa kabla sijachonga, jamaa juzi kachenjua mlima kapata kilo na gm miambili. Hivyo marudio yanalipa vizuri ila uwe na mtaji na usimamie kwa karibu zaidi.Mkuu mcrounmj kwanini umeamua kupanua uwekezaji wako kwa kutaka kuchonga karasha ?
Kwa ufahamu na uzoefu wangu (mi ni mzaliwa wa Chunya) najua kwamba kuendesha karasha kuna risks kubwa kuliko biashara ya kununua dhahabu.
Kwanini usiongeze mtaji katika ununuzi wako au ukaamua kuomba leseni ya mnunuzi mkubwa (dealer) ?
Mkuu IBRA wa PILI usimbishie Narubongo kuwa faida ya dhahabu ni 2000 hadi 3000 kwa gram. Mkuu iko ivii, inategemea na maeneo. Kwa sababu ya ushindani wa kibiashara unakuta sehemu watu wanainunua dhahabu kwa bei ya juu kuzidi hata bei elekezi ya serikali. Hivyo huambulia faida kiduchu au kupata hasara. Yapo maeneo wanunuzi wa dhahabu wanapata faida maradufu sababu wanaelewana na wananunua dhahabu kwa bei elekezi. Mfano Mimi juzi nilikuwa sokoni nikiwa na 93g nilipoyeyusha ikatoka 91g. Polini nimetumia mil. 7.5, narudi na mil 9.2. Hapo hata Kama nimekaa wiki mbili bado inalipa mnoo.Ndugu we muongo faida EF 2 au EF 3
Nina rafik angu anachukua dhahabu msumbiji eneo la kaguruwe ana kuja uza dar kila baada ya wiki moja,
gram 100 Sawa na milioni 10 gram ananunua laki sokoni inacheza laki na 25 ivi,
this time Mara ya mwisho katoka dar na faida ya 1.8million akitoa process zingne ndio anabaki na iyo 1.8 m
Au labda sijaelewa maelezo yako vizuri lakin kama ndio ayo hapo juu faida ef 3 big no ukitaka nikupe na namba ya simu muulize ata kwambia na kama upo dar wiki hii anakuja apo kuuza dhahabu muulize.
Pambana mkuu, in'shallah utafikaUmeni insipire sana, nilisha sikia habari za hii biashara kupitia kipindi cha E-fm (ubaoni-ripoti ya leo) kuna mdada alikuwa ana simulia jinsi mume wake alivyo kuwa akipambana na hii biashara mpaka kufanikiwa na alianza na 2M's pekee naona na wewe una nizidishia ukali wakusaka capital ili niingie humo kupambana kazi ninayo ifanya kwa sasa balipwa 250k so ina hitaji uvumilivu ili kufikisha mtaji hata wa 3M's maana hiyo hiyo 250k nina takiwa nihakikishe na weka akiba pia nakula na vaa kwa hyo hiyo 250k ila naamini nita fika tu kikubwa ni juhudi na kumuomba sana mungu atufungulie milango iliyo fungwa.
Pori unalochukulia lipo wapi? Na soko lipo wapi?Mkuu IBRA wa PILI usimbishie Narubongo kuwa faida ya dhahabu ni 2000 hadi 3000 kwa gram. Mkuu iko ivii, inategemea na maeneo. Kwa sababu ya ushindani wa kibiashara unakuta sehemu watu wanainunua dhahabu kwa bei ya juu kuzidi hata bei elekezi ya serikali. Hivyo huambulia faida kiduchu au kupata hasara. Yapo maeneo wanunuzi wa dhahabu wanapata faida maradufu sababu wanaelewana na wananunua dhahabu kwa bei elekezi. Mfano Mimi juzi nilikuwa sokoni nikiwa na 93g nilipoyeyusha ikatoka 91g. Polini nimetumia mil. 7.5, narudi na mil 9.2. Hapo hata Kama nimekaa wiki mbili bado inalipa mnoo.
Nitakujibu kwa majibu marefu kidogo, kuwa mvumilivu, tiririka nami.
Majibu haya ni kwa mujibu wa my personal experience (nimezaliwa na kukulia katika moj ya maeneo ya uchimbaji wa madini ya dhahabu nchini Tanzania)
Hivyo kunaweza kuwa na mabadiliko kidogo katika hoja zangu kulingana na hali ilivyo katika maeneo yenye madini nchini.
Tutazame kwanza mabadiliko ya trends za teknolojia za kupata dhahabu na nyakati zake.
1. Kuokota dhahabu maeneo mbalimbali (kwenye surface land) hasa ya maeneo ya mitoni, n.k :
Hizi ni zama za zamani sana, hasa kabla ya uhuru na kabla ya kuja watu weupe barani Afrika. Kama umeshawahi kusikia kwamba zamani dhahabu zilikua zinatumika kama "kete" za kuchezea bao. It was that simple, that abundant.
2. Kuchimba ili kupata "mchanga wa dhahabu" na kuosha ili kuipata dhahabu yenyewe (kusekesa/kuchekecha, kupiga kalai):
Hapa kilichokua kinatafutwa ni "mchanga wa dhahabu", na hatimaye unaoshwa kwa njia nilizotaja hapo juu ili kupata madini ya dhahabu. Ni njia ambayo inahitaji maji na kinachopatikana hapa tunaweza kusema ni "pure gold".
3. Kuchimba mashimo marefu (long bases) ili kutafuta MIAMBA inayoambatana na dhahabu:
Katika njia hii miamba hiyo hulainishwa (kuwa mawe madogo madogo), kutwangwa (kupata unga unga) na hatimaye "kukamatishwa" kwa kutumia Mercury ili kupata dhahabu. Mercury inafanya selective extraction ya gold kutoka kwenye unga (Ore) inayojumuisha metali nyingine.
Baada ya kazi ya Mercury, yale mabaki ("baada ya dhahabu" kuwa extracted) yalikua ama yakitupwa, au kutunzwa kwa ajili ya kurudia zoezi la extraction ya Mercury wakati ujao yatakapokua mengi zaidi. Logic hapa ni kwamba Mercury haifanyi extraction ya 100%. Katika point namba 5 tutaanzia hapa kwenye haya MABAKI au MARUDIO au MASAINENTI.
4. Kutumia "vipimio" (Gold detectors) kupata dhahabu:
Hii hasa ni kwa ajili ya kupata dhahabu zilizo kwenye surface (hazikuonekana kwa macho na kuokotwa hapo zamani), zile za kwenye "mchanga wa dhahabu" na kwa uchache kwenye "miamba yenye dhahabu".
Kwa huku kwetu, teknolojia hii imeanza kuchipukia mwaka 2000, imekuja ku peak miaka ya 2005-2010. Kuanzia miaka ya 2010 kuja juu vipimio vilianza kupungua kutokana na uhaba wa "aina ya dhahabu" ambazo vinagundua. Hivyo wenye vipimio walianza kwenda maeneo ya mbali (kutoka huku niliko) ili kutafuta dhahabu zinazoweza kutambuliwa na hivi vipimio. Mfano Mpanda, Maeneo ya nchi ya Msumbiji, Zambia n.k
Ila kwa ujumla ni kwamba kwa sasa kumiliki kipimio imekua kama ni old fashioned way ya kutafuta dhahabu, siku za kulala njaa zinakua ni nyingi sana. Kwa maneno mengine hapa nakuambia kwamba kuwa makini sana kama kweli utaamua kuleta hivyo vifaa. Hali yake ndivyo ilivyo.
Mifano ya "aina" za vipimio (gold detectors) iliyokua maarufu ni kama vile GP, SD, XT, GMT, Fisher, n.k
5. Ujio wa "Leaching plants" pamoja na "Elution" ili KUOZESHA "marudio" (Rejea point namba 3 hapo juu) na hatimaye kupata kupata dhahabu:
Yale mabaki au marudio baada ya shughuli ya Mercury, hapa yanaozeshwa kwa kutumia kemikali kadhaa kwenye mtambo wa uchenjuaji dhahabu na hatimaye kuchomwa ili kuipata dhahabu yenyewe.
Kutokana na hili, the more marudio unazalisha, the more likely kwamba utachenjua mara nyingi na hivyo utapata dhahabu kwa wingi zaidi.
Maana yake sasa, utahitaji maeneo mengi yenye miamba ya dhahabu, utahitaji mitambo mingi ya kusaga mawe (yanaitwa makarasha, yaani crushers) kutengeneza "marudio" mengi zaidi.
Kwa sasa teknolojia hii ya kumiliki "makarasha" ndio ina peak sana kwa "huku kwetu".
6. CIP & CIL Major plants:
Hii ni advanced level ya njia namba 5 hapo juu, inakua na ufanisi mkubwa zaidi katika kuozesha, inachukua large volumes ya marudio at a time na pia ina extract more gold.
Hata hivyo inahitaji mtaji mkubwa na miundombinu thabiti (hasa umeme) ili kuiendesha. Kwahiyo hizi bado ni chache sana.
Unaweza ukaona kuwa katika scenario zote 6 hapo juu (of course kuna zaidi) utaona dhahabu ni ileile, ila kinachobadilika ni TEKNOLOJIA inayotumika kuipata.
Hivyo nakusihi ufanye maamuzi juu ya biashara hiyo kulingana na uhalisia wa mambo yalivyo.
NB: Hii inahusu zaidi wachimbaji wadogo na angalau kidogo wachimbaji wa kati.
Andiko langu si msimamo wa sekta ya madini ya nchi nzima, ila angalau kwa 80% liamini na uliafuate.
Ukitaka nieleze fursa "za kibiashara" zilizopo katika sekta ya madini na mnyororo wake wa thamani, nitafanya mambo mawili yafuatayo:-
A. Nitakuomba unipe muda
B. Nitakueleza kinagaubaga.
Uwe na siku njema.
Mkuu hizo CIP na CIL major plants ni "bigger versions" za hizi normal Leaching plants.Mkuu asante kwa maelezo ya uhakika. Najua kuhusu leaching plants pamoja na elution plants ila sijawahi kusikia kuhusu hizo CIP & CIL Major plants. Naomba utolee maelezo zaidi hizo kama hutojali. Fursa na changamoto zake, mtaji wa kuanzia nk.
Aidha kati ya kuwekeza kwenye plants na kwenye uuzaji wa machinery na madawa ya uchenjuanji ni wapi kuna fursa zaidi na lesser risky?