Ben Saanane
JF-Expert Member
- Jan 18, 2007
- 14,581
- 18,124
Kwanza kabisa nianze kwa kupongeza hatua moja ya kumfikisha Mhe.Mramba na Mhe.Daniel Yona mahakamani ili kujibu mashitaka yao ya matumizi mabaya ya madaraka yaliyolisababishia taifa letu hasara kubwa
Mramba ni mbunge wa kuchaguliwa na wapiga kura wa Jimbo la Rombo.kiti cha ubunge wa jimbo la Rombo ni ofisi ya umma.Hadi sasa mhe.Mramba ameonyesha utovu mkubwa wa nidhamu katika ofisi ya umma,hafai kuwa na mamlaka katika ofisi ya umma.Leo hii wananchi wa jimbo la Rombo watanufaika vipi na mbunge wao kama haruhusiwi hata kutoka nje ya Dar es salaaam?
Anahimiza vipi shughuli za maendeleo?
Pia,katika sifa zilizomfanya Mramba kuwa waziri au kupewa dhamana kubwa kama hiyo katika ofisi nyeti na inayogusa maisha ya kila siku ya mtanzania ni pamoja na kupigiwa kura na wananchi wa jimbo la Rombo.Hii ilikua ni heshima kubwa si kwake pekee bali hata kwa wananchi na wapiga kura wake wa jimbo la Rombo.Leo hii mramba kutumia mamlaka na dhamana aliyopewa vibaya imegeuka kuwa dharau,aibu na kejeli kwa wapiga kura wake.
Mramba amewadhalilisha wapiga kura wake,ni jukumu la kila mwananchi na mpiga kura wa jimbo la Rombo kumkataa Mramba na mambo yake yote.Kumkubali Mramba maanke ni kumkubali na aibu zake zote.Mambo aliyoyatenda akiwa waziri wa fedha,ni matusi makubwa kwa wapiga kura wake ambao wapo walio wengi wamezongwa na umaskini,waliokosa elimu nk. Leo hii hospitali kuu ya jimbo lake Huruma hospital ina upungufu mkubwa wa madawa,vitanda nk.Sasa leo mbunge anapandishwa kizimbani kwa kutumia mamlaka vibaya ili kujinufaisha yeye na wazungu huku wananchi wake wakiwa katika hali ya umaskini wa kutisha na mateso makali
Ni jukumu la watu woote wenye maslahi katika jimbo la Rombo kokote waliko huko Tanzania na duniani kuungana bega kwa bega kwa kumshinikiza mtuhumiwa Basil Pesambili Mramba aachie ngazi ili kuunga mkono juhudi za kupambana na ufisadi. warombo kuweni sehemu ya vita dhidi ya ufisadi kwa kumkataa Basil Mramba kuwa mbunge wenu
Onyesheni dira ya Tanzania tuitakayo
Basil Pesambili Mramba Step Down Nooow!
Mramba ni mbunge wa kuchaguliwa na wapiga kura wa Jimbo la Rombo.kiti cha ubunge wa jimbo la Rombo ni ofisi ya umma.Hadi sasa mhe.Mramba ameonyesha utovu mkubwa wa nidhamu katika ofisi ya umma,hafai kuwa na mamlaka katika ofisi ya umma.Leo hii wananchi wa jimbo la Rombo watanufaika vipi na mbunge wao kama haruhusiwi hata kutoka nje ya Dar es salaaam?
Anahimiza vipi shughuli za maendeleo?
Pia,katika sifa zilizomfanya Mramba kuwa waziri au kupewa dhamana kubwa kama hiyo katika ofisi nyeti na inayogusa maisha ya kila siku ya mtanzania ni pamoja na kupigiwa kura na wananchi wa jimbo la Rombo.Hii ilikua ni heshima kubwa si kwake pekee bali hata kwa wananchi na wapiga kura wake wa jimbo la Rombo.Leo hii mramba kutumia mamlaka na dhamana aliyopewa vibaya imegeuka kuwa dharau,aibu na kejeli kwa wapiga kura wake.
Mramba amewadhalilisha wapiga kura wake,ni jukumu la kila mwananchi na mpiga kura wa jimbo la Rombo kumkataa Mramba na mambo yake yote.Kumkubali Mramba maanke ni kumkubali na aibu zake zote.Mambo aliyoyatenda akiwa waziri wa fedha,ni matusi makubwa kwa wapiga kura wake ambao wapo walio wengi wamezongwa na umaskini,waliokosa elimu nk. Leo hii hospitali kuu ya jimbo lake Huruma hospital ina upungufu mkubwa wa madawa,vitanda nk.Sasa leo mbunge anapandishwa kizimbani kwa kutumia mamlaka vibaya ili kujinufaisha yeye na wazungu huku wananchi wake wakiwa katika hali ya umaskini wa kutisha na mateso makali
Ni jukumu la watu woote wenye maslahi katika jimbo la Rombo kokote waliko huko Tanzania na duniani kuungana bega kwa bega kwa kumshinikiza mtuhumiwa Basil Pesambili Mramba aachie ngazi ili kuunga mkono juhudi za kupambana na ufisadi. warombo kuweni sehemu ya vita dhidi ya ufisadi kwa kumkataa Basil Mramba kuwa mbunge wenu
Onyesheni dira ya Tanzania tuitakayo
Basil Pesambili Mramba Step Down Nooow!