Mpango wa kummaliza Dr. Slaa sasa umeiva na kazi imeanza kutekelezwa

Kagemro

JF-Expert Member
Jan 11, 2010
1,433
633
Mambo ndani ya usalama sasa yanakwenda vibaya, mpango wa kummaliza kabisa Dr Slaa umeiva.

Wakurugenzi wa usalama walikaa kikao chao wiki iliyopita na kufikia maamuzi ya kumuondoa kwenye sura ya dunia Dr Slaa wakiamini kwamba Slaa ndiye mzizi katika Chadema na anaweza kuiangusha CCM 2015 kama alivyofanya 2010 lakini kwa bahati wakafanikiwa kuchakachua kura zake. wameona mazingira ya kuchakachua 2015 ni magumu sana.


Njia pekee ni kuondoa wagombea ambao ni tishio na wenye ushawishi wa kuhamishia wanasiasa wengine walio ccm kwenda Chadema.
Waliopewa kutekeleza zoezi hili ni vijana wawili, wa kwanza ni yule yule anayetuhumiwa kumdhuru Dr. ulimboka.

Huyu aliitwa na mkurugenzi akaambiwa hawa jamaa wa Chadema wana habari zako zote na wanataka kukumaliza. Akaambiwa Idara inaweza kukulinda endapo tu CCM itaendelea kuwa madarakani, lakini hawa Chadema wakichukua, wewe na familia yako mtatoweka kabisa. Salama yako ni kuhakikisha Chadema hawaingii madarakani. Jamaa akapendekeza kutumia kikosi chake kile kile alichokitumia kwa Ulimboka ili kuwashughulikia Chadema atakaoelekezwa kufanya hivyo.

Mkurugenzi akamwambia kikosi hicho hakifai, wakashauriana watumie kikosi kilichomkosakosa Kubenea (wale majambazi wanne). Kidogo ikaonekana hiyo inaweza kuwa na mafanikio. Hapa ndipo akaletwa yule bwana mdogo aliyekuwa akitumia wale majambazi wanne, (majambazi wanne wote wanafahamika) Huyu kijana tayari ameshaanza mazungumzo na hao watu na ameshawapa mgawo wao wa kwanza.

Hawa majamaa wanakamilisha taarifa za kuwasaidia utekelezaji. Tishio hili ni dhahiri na litatekelezwa.

Kwenye kikao chao cha kidhalimu, mmoja wao akapendekeza matumizi ya ama uchawi au sumu inayoua taratibu. Huyu aliyependekeza anahofia kuwa njia yoyote itakayofanana na ile ya Ulimboka italeta kelele na dunia nzima itagundua. Anajaribu kuwashawishi wenziwe waachane na hiyo, isipokuwa watumie njia hizi mbili mbadala; sumu au uchawi.

Jamaa wanamiliki wachawi wengi sana na wachawi hawa wako makundi mawili. Kundi la kwanza ni lile linalotumika kumlinda JK na huwa linaenda ikulu kila wiki mara moja. Kundi hili liko kwenye payrol ya mkurugenzi. Kundi la pili ni lile la wachawi waliotaka kumuua Mwakyembe kipindi fulani. Kundi hili liko katika mazungumzo kwa ajili hiyo.

Hivi sasa, hata hivi navyoandika, mtuhumiwa wa kumdhuru Ulimboka yuko kwenye kikao kizito na mkurugenzi wakijadiliana habari hii, wanamfanyia timing kipindi hiki Slaa atakaporudi kutoka Ghana. Mtuhumiwa huyu ana furaha sana na ameonekana kuwa mtu mwenye matumaini makubwa akiamini kwamba ile habari yake imesahaulika kwenye jamii.

Anapewa pesa nyingi sana kwa ajili ya kazi hii. Kimakazi, hivi sasa anaishi Tabata, ametazamana na gate la Chuo cha ualimu st. Mary's. Amepewa gari Mazda, T506 BEL. Kikazi bado anatumia yale maficho yaliyopo Ada estate karibu na Best Bite. Ni mtu hatari sana, amekula kiapo cha kumuangamiza Slaa na kummalizia Ulimboka, anasema Ulimboka naye lazima afe kwa sababu iko siku ataropoka tena.

Jambo jengine baya sana ni kwamba wana mpango wa kuua kwa njia hiyo hiyo wabunge ambao wanaamini hawahongeki kabisa kifedha ili wasiibue ile kashfa ya Ridhiwani na madawa ya kulevya Uchina kwa sababu ya connection yake na suala la madini, hasa uranium na wachina.

Wanasema sasa hivi wanajiendesha kisayansi. Walipom-brief JK naye akaona safari hii watafanikiwa.

CHANZO: Josephine Mushumbusi (Mama Slaa) on Facebook - http://www.facebook.com/jmushumbusi

attachment.php
 

Attachments

  • josephine-timeline.jpg
    josephine-timeline.jpg
    25.1 KB · Views: 2,553
Dah! haya mambo mengine inakuaga ngumu kumeza, sasa hata wewe mleta habari tutakuamini vipi, au ndio tahadhali tu. Usije wewe ukawa umetumika kupeleka watu kushoto halafu mambo yanatokea kulia. Vyovyote vile hao hawataweza kufanikiwa. Chadema walianza na Mungu na watamaliza na Mungu. Akina Dr. Slaa sasa wapo wengi, sasa sijui watawaua wangapi!. Hakuna mtu yupo juu ya sheria 50 zako zikifika utanyea debe tu.
 
Yale Yale yaliyofanyika kumbomoa Mbowe mwaka 2005 ndio wanarudia makosa yaleyale, Chadema tunaweza kuwa wajinga lakini sio wajinga hivyo maana Chadema sio Dr.Sllaa isipokuwa ni zake fikra pevu ktk kupambana na utawala huu..Kina Dr.Slaa wapo wengi na wanazidi kuzaliwa.
 
Mwenyezi Mungu ninakuomba kwa dhati kabisa kuwa hawa wenye nia mbaya na watetezi wetu uwaponye kama ambavyo ulimponya Sauli akienda kuwatesa watu wako.

Baba katika Jina la Yesu Kristo ninakuomba uwaponye na kutubu kabisa kabla hawajatenda maovu haya maana shetani atafurahi sana. Dhambi zao imulikwe na kuwekwa wazi na waaibike kabla hawajafanikisha mambo yao. Na wachawi hawa washukiwe na Roho mtakatifu ili waokoke na kubatizwa katika jina la Yesu.

Pia Ninakuomba utembee na Dr Slaa na Ulimboka popote walipo na Wengine wote kwenye hiyo list ya kuuwawa ili wasipatwe na Janga kama ambavy shetani anavyopanga. Mashetani hawa najua wanapambana na nguvu zako baba na hawaamini kuwa wewe ndo mwenye mamlaka juu ya uhai wa binadamu.

Ninaomba haya machache kupitia jina la Mwanao Yesu Kristo. Amen.
 
Bahati mbaya star wetu wa bongo movie amefariki, dah...au tumpe arnold? huh huh naona tumpe Rambo...hapana bwana tumpe bruce lee.

Hii tuifanye transcript mkuu, ili tukawauzie makomandoo watengeneze bonge la movie. UNAONAJE?
 
Wao wana pesa, sis tuna Mungu!! Whatever they do, it will be revealed before the sunset!!
 
...Hali inatisha hasa ukitilia maanani kauli za "CCM itatawala Tanzania milele." na "Kamwe hatuwezi kukabidhi dola kwa wahuni wa CHADEMA."

Wanajua fika wakishapoteza uchaguzi basi ndio chama chao kitakuwa kinazikwa rasmi, sasa watahakikisha wafanye kila wawezalo ili kubaki madarakani. Kuua wameshaanza rasmi ila idadi ya watakaouawa itaongezeka zaidi kadri tutakapokuwa tunakaribia uchaguzi.
 
sikuamini hapo mwanzo kuwa nchi hii imeoza hivi. lakini baada ya kupata taarifa za ndani kabisa usalama wa taifa ndio unaliangamiza taifa hili kwa biashara ya madawa ya kulevya i was shocked.....lakini nilipokatiwa ishu zaidi familia ya rais na usalama wa taifa fulani ambao wanajiona wako revel na mkuu wa nchi....i was speechless. ndio maana nikaona kwanini huyu dada amina baada ya kutoa tamko la drug deal mjengoni mauti yake yalikuwa speed....just think!? hata kama ni ugonjwa mwingine wapo wangapi ambao ni wagonjwa lakini wapo....hata huyo mwenye nchi hii tunajua maradhi yake lakini bado yupo na wabunge wengi kibao. hiyo ilikuwa ni sumu kwa amina ambayo ilimchukua na mumewe pia ili kuifanya hii kitu was natural....dots hizi ukiunganisha bayana unajua nini kinachoendelea katika nchi hii.
Mungu pekee ndiye anayejua nini hatima ya nchi hii....
 
Aisee, hali ni mbaya!
Kumbe kung'oa usultani kazi sana? Manake nimezaliwa nikaukuta uhuru wa bendera.
Chadema lazma mchukue hatua za tahadhari.
 
mhhhh hivi naota amakweli???? Ngoja nianawe kwanza uso na kutoa tongotongo kisha nitarejea
 
Hii ni kali ya mwaka, wamuue kwa uchawi? Wakisha mmaliza kwa ndumba,UN wataunda tume ifanye uchunguzi na itaongozwa na yule mchawi wa Obama anae ishi white house.
 
Bahati mbaya star wetu wa bongo movie amefariki, dah...au tumpe arnold? huh huh naona tumpe Rambo...hapana bwana tumpe bruce lee.

Hii tuifanye transcript mkuu, ili tukawauzie makomandoo watengeneze bonge la movie. UNAONAJE?
You're not spared to be ignorant! wake up dude.!
 
Another story from Shigongo chipolopolo! Baad ya kuona ile ya madawa ya kulevya imeshtukiwa. Hebu jamani hata kama tunataka kudanganya tujue namna ya kudanganya basi duh!
 
Back
Top Bottom