Kagemro
JF-Expert Member
- Jan 11, 2010
- 1,433
- 633
Mambo ndani ya usalama sasa yanakwenda vibaya, mpango wa kummaliza kabisa Dr Slaa umeiva.
Wakurugenzi wa usalama walikaa kikao chao wiki iliyopita na kufikia maamuzi ya kumuondoa kwenye sura ya dunia Dr Slaa wakiamini kwamba Slaa ndiye mzizi katika Chadema na anaweza kuiangusha CCM 2015 kama alivyofanya 2010 lakini kwa bahati wakafanikiwa kuchakachua kura zake. wameona mazingira ya kuchakachua 2015 ni magumu sana.
Njia pekee ni kuondoa wagombea ambao ni tishio na wenye ushawishi wa kuhamishia wanasiasa wengine walio ccm kwenda Chadema.
Waliopewa kutekeleza zoezi hili ni vijana wawili, wa kwanza ni yule yule anayetuhumiwa kumdhuru Dr. ulimboka.
Huyu aliitwa na mkurugenzi akaambiwa hawa jamaa wa Chadema wana habari zako zote na wanataka kukumaliza. Akaambiwa Idara inaweza kukulinda endapo tu CCM itaendelea kuwa madarakani, lakini hawa Chadema wakichukua, wewe na familia yako mtatoweka kabisa. Salama yako ni kuhakikisha Chadema hawaingii madarakani. Jamaa akapendekeza kutumia kikosi chake kile kile alichokitumia kwa Ulimboka ili kuwashughulikia Chadema atakaoelekezwa kufanya hivyo.
Mkurugenzi akamwambia kikosi hicho hakifai, wakashauriana watumie kikosi kilichomkosakosa Kubenea (wale majambazi wanne). Kidogo ikaonekana hiyo inaweza kuwa na mafanikio. Hapa ndipo akaletwa yule bwana mdogo aliyekuwa akitumia wale majambazi wanne, (majambazi wanne wote wanafahamika) Huyu kijana tayari ameshaanza mazungumzo na hao watu na ameshawapa mgawo wao wa kwanza.
Hawa majamaa wanakamilisha taarifa za kuwasaidia utekelezaji. Tishio hili ni dhahiri na litatekelezwa.
Kwenye kikao chao cha kidhalimu, mmoja wao akapendekeza matumizi ya ama uchawi au sumu inayoua taratibu. Huyu aliyependekeza anahofia kuwa njia yoyote itakayofanana na ile ya Ulimboka italeta kelele na dunia nzima itagundua. Anajaribu kuwashawishi wenziwe waachane na hiyo, isipokuwa watumie njia hizi mbili mbadala; sumu au uchawi.
Jamaa wanamiliki wachawi wengi sana na wachawi hawa wako makundi mawili. Kundi la kwanza ni lile linalotumika kumlinda JK na huwa linaenda ikulu kila wiki mara moja. Kundi hili liko kwenye payrol ya mkurugenzi. Kundi la pili ni lile la wachawi waliotaka kumuua Mwakyembe kipindi fulani. Kundi hili liko katika mazungumzo kwa ajili hiyo.
Hivi sasa, hata hivi navyoandika, mtuhumiwa wa kumdhuru Ulimboka yuko kwenye kikao kizito na mkurugenzi wakijadiliana habari hii, wanamfanyia timing kipindi hiki Slaa atakaporudi kutoka Ghana. Mtuhumiwa huyu ana furaha sana na ameonekana kuwa mtu mwenye matumaini makubwa akiamini kwamba ile habari yake imesahaulika kwenye jamii.
Anapewa pesa nyingi sana kwa ajili ya kazi hii. Kimakazi, hivi sasa anaishi Tabata, ametazamana na gate la Chuo cha ualimu st. Mary's. Amepewa gari Mazda, T506 BEL. Kikazi bado anatumia yale maficho yaliyopo Ada estate karibu na Best Bite. Ni mtu hatari sana, amekula kiapo cha kumuangamiza Slaa na kummalizia Ulimboka, anasema Ulimboka naye lazima afe kwa sababu iko siku ataropoka tena.
Jambo jengine baya sana ni kwamba wana mpango wa kuua kwa njia hiyo hiyo wabunge ambao wanaamini hawahongeki kabisa kifedha ili wasiibue ile kashfa ya Ridhiwani na madawa ya kulevya Uchina kwa sababu ya connection yake na suala la madini, hasa uranium na wachina.
Wanasema sasa hivi wanajiendesha kisayansi. Walipom-brief JK naye akaona safari hii watafanikiwa.
CHANZO: Josephine Mushumbusi (Mama Slaa) on Facebook - http://www.facebook.com/jmushumbusi
Wakurugenzi wa usalama walikaa kikao chao wiki iliyopita na kufikia maamuzi ya kumuondoa kwenye sura ya dunia Dr Slaa wakiamini kwamba Slaa ndiye mzizi katika Chadema na anaweza kuiangusha CCM 2015 kama alivyofanya 2010 lakini kwa bahati wakafanikiwa kuchakachua kura zake. wameona mazingira ya kuchakachua 2015 ni magumu sana.
Njia pekee ni kuondoa wagombea ambao ni tishio na wenye ushawishi wa kuhamishia wanasiasa wengine walio ccm kwenda Chadema.
Waliopewa kutekeleza zoezi hili ni vijana wawili, wa kwanza ni yule yule anayetuhumiwa kumdhuru Dr. ulimboka.
Huyu aliitwa na mkurugenzi akaambiwa hawa jamaa wa Chadema wana habari zako zote na wanataka kukumaliza. Akaambiwa Idara inaweza kukulinda endapo tu CCM itaendelea kuwa madarakani, lakini hawa Chadema wakichukua, wewe na familia yako mtatoweka kabisa. Salama yako ni kuhakikisha Chadema hawaingii madarakani. Jamaa akapendekeza kutumia kikosi chake kile kile alichokitumia kwa Ulimboka ili kuwashughulikia Chadema atakaoelekezwa kufanya hivyo.
Mkurugenzi akamwambia kikosi hicho hakifai, wakashauriana watumie kikosi kilichomkosakosa Kubenea (wale majambazi wanne). Kidogo ikaonekana hiyo inaweza kuwa na mafanikio. Hapa ndipo akaletwa yule bwana mdogo aliyekuwa akitumia wale majambazi wanne, (majambazi wanne wote wanafahamika) Huyu kijana tayari ameshaanza mazungumzo na hao watu na ameshawapa mgawo wao wa kwanza.
Hawa majamaa wanakamilisha taarifa za kuwasaidia utekelezaji. Tishio hili ni dhahiri na litatekelezwa.
Kwenye kikao chao cha kidhalimu, mmoja wao akapendekeza matumizi ya ama uchawi au sumu inayoua taratibu. Huyu aliyependekeza anahofia kuwa njia yoyote itakayofanana na ile ya Ulimboka italeta kelele na dunia nzima itagundua. Anajaribu kuwashawishi wenziwe waachane na hiyo, isipokuwa watumie njia hizi mbili mbadala; sumu au uchawi.
Jamaa wanamiliki wachawi wengi sana na wachawi hawa wako makundi mawili. Kundi la kwanza ni lile linalotumika kumlinda JK na huwa linaenda ikulu kila wiki mara moja. Kundi hili liko kwenye payrol ya mkurugenzi. Kundi la pili ni lile la wachawi waliotaka kumuua Mwakyembe kipindi fulani. Kundi hili liko katika mazungumzo kwa ajili hiyo.
Hivi sasa, hata hivi navyoandika, mtuhumiwa wa kumdhuru Ulimboka yuko kwenye kikao kizito na mkurugenzi wakijadiliana habari hii, wanamfanyia timing kipindi hiki Slaa atakaporudi kutoka Ghana. Mtuhumiwa huyu ana furaha sana na ameonekana kuwa mtu mwenye matumaini makubwa akiamini kwamba ile habari yake imesahaulika kwenye jamii.
Anapewa pesa nyingi sana kwa ajili ya kazi hii. Kimakazi, hivi sasa anaishi Tabata, ametazamana na gate la Chuo cha ualimu st. Mary's. Amepewa gari Mazda, T506 BEL. Kikazi bado anatumia yale maficho yaliyopo Ada estate karibu na Best Bite. Ni mtu hatari sana, amekula kiapo cha kumuangamiza Slaa na kummalizia Ulimboka, anasema Ulimboka naye lazima afe kwa sababu iko siku ataropoka tena.
Jambo jengine baya sana ni kwamba wana mpango wa kuua kwa njia hiyo hiyo wabunge ambao wanaamini hawahongeki kabisa kifedha ili wasiibue ile kashfa ya Ridhiwani na madawa ya kulevya Uchina kwa sababu ya connection yake na suala la madini, hasa uranium na wachina.
Wanasema sasa hivi wanajiendesha kisayansi. Walipom-brief JK naye akaona safari hii watafanikiwa.
CHANZO: Josephine Mushumbusi (Mama Slaa) on Facebook - http://www.facebook.com/jmushumbusi