Mpango mzima wa kuihusisha CHADEMA na ugaidi mpya huu hapa

LOWASA Vs ZITTO KABWE NDANI YA VYAMA VYAO VYA SIASA
Watu Wanamfananisha Lowasa na Zitto, Wanasema Kama Lowasa Akihama CCM au Asipoteuliwa kuwa Mgombea Uraisi 2015 kwa Ticket ya CCM Basi CCM Itapasuka Vipandevipande na Wengine Kusema Itakufa Kabisa Kama Inavyopasuka Chadema na Kuelekea KIFO kwa sasa. Ifahamike ya Kwamba Vijana wa CCM na Wana CCM kwa Ujumla ni Tofauti Kabisa na Vijana wa Chadema na Wanachadema kwa Ujumla.Vijana wengi wa Chadema Walijiunga na Chadema Kwa Sababu ya Kuvutiwa na Zitto Kabwe, Uwezo na Umahiri Mkubwa Aliokuwa nao Katika Kujenga Hoja na Kuibua Kashfa,Siri Nyingi za Mafisadi.Hawakuwa na Malengo Binafsi ndani ya Chama na Siasa kwa Ujumla
Vijana wengi wa Chadema na Wanachadema kwa Ujumla Walijiunga na Chadema kwa sababu Kuu Zifuatazo
1. Walivutiwa na ZITTO KABWE, Dr Willbroad Slaa,Tundu Lissu au John Mnyika
2. Wanahasira na Serikali juu ya Kushindwa Kutatua Maslahi yao Binafsi
3. Walivutiwa na Chadema kwa Kuibua Kashifa za MAFISADI ie EPA, MELEMETA….
4. Waliongopewa ya Kwamba Chadema Inawapenda Sana Vijana na ni Mkombozi wa Taifa
5. Ndio Chama cha Upinzani Kilichokuwa na Nguvu Miaka ya 2009-2010…,Hivyo watu wanaopenda Upinzani Wakajikuta wamejiunga na Chadema
6. Wengine wamejiunga na Chadema kwa Sababu tu wao ni WACHAGA,Wanaamini Chadema ni Chama Chao
Vijana wengi wa CCM na WanaCCM kwa Ujumla Wamejiunga na CCM kwa Sababu Kuu Zifuatazo
1. Mapenzi yao ya Dhati na CCM,
2. Wana Malengo ya Kuwa Viongozi wa Kisiasa na Serikali wa Sasa na Badae
3. Nguvu ya Kisiasa na Kimtandao ya CCM ndani ya CCM na Serikali
4. Nafasi za Kiungozi ndani ya CCM ni Nyingi sana Ukilinganisha na Vyama Vingine vya Siasa
5. Nafasi ya CCM Kushinda Uchaguzi Mkuu na Kuunda Serikali ni Kubwa Kuliko Vyama vya Upinzani,Hivyo wana Matumaini ya Kuwa Sehemu ya Serikali
Ukitazama Sana Sababu Hizo Hapo Juu Utagundua ya kwamba Hata Lowasa Akihama CCM Basi Atahama yeye na Familia Yake na Hakuna MwanaCCM Atakaemfuata.Lowasa Atakuwa Raisi wa Tanzania Kama Kamati Kuu ya CCM na NEC Wakipendekeza Jina Lake na Kushinda Katika Kura za Maoni na Si Vinginevyo.Hata Kama Lowasa Hatashinda kwenye Kura za Maoni au Akakatwa Jina Lake Hata HAMA CCM, Atabaki CCM na Kuendelea Kuwa Mwanachama na Kiongozi wa CCM.
Vijana wa CCM na Wana CCM kwa Ujumla Wanakipenda Chama na Si Mtu Ndani ya Chama,Mimi Nawapenda Sana Viongozi wa CCM Wazalendo,Wanaowajali na Kupigania Maslahi ya Watanzania Lakini Wakihama CCM SINTOWAFUATA WAENDAKO,Nitabaki kuwa LOYAL na CCM Maana Kila Mtu Anamalengo yake ndani ya Chama cha Siasa,Kama Unamfuata Mtu Huwezi kuwa Stable Maana Umejenga Imani yako kwa Mtu na Si Chama.
FAHAMU
CCM Imejengwa Juu ya Mwamba,Ni Imara sana,Mizizi yake ni Mirefu na Imara Mno
CCM Inatawala Leo, Itatawala Kesho na Kuendelea Kutawala Mpaka Kitakapopatikana Chama sahihi Ambacho ni Mbadala wa CCM Lakini Sio Hivi Vyama vya KIKABILA…
CCM Inawajali Wazee na Vijana Hivyo Inapata Baraka za Pande Zote Tofauti na Vyama Vingine vilivyo Watenga Wazee na Kuona ni Watu waliopitwa na Wakati.

KIDUMU CHAMA CHA MAPINDUZI…

Ukiandika habari na kuweka kitu ambacho unadhani ni ukweli ni lazima utoe chanzo chake ni nini? Huwezi kutwambia Vijana wengi chadema wamejiunga kwa sababu ya Zitto, lete chanzo kinachodhibitisha hilo lasivyo haya ni mawazo yako tu mkuu!.

Kwa mfano mdogo tu hebu umbuka zile kura zilizopigwa hapa JF mwezi uliopita nani alipata kura nyingi kati ya Zitto na CC ya chadema dhidi ya uamuzi wa CC wa kumvua vyeo Zitto? Unaweza ukachukua labda Mikutano ya Zitto kule Kigoma kama kigezo lakini huo ni mkoa mmoja halafu ni nyumbani kwao, hivyo huwezi kuhitimisha kuwa Jamaa anawafuasi wengi Chadema.

Nadhani kama wewe ni moja wa washauri wake, basi mmesaidia kwa kiasi kikubwa kmpotezea Zitto ulaji wake chadema maana madam angejua kuwa umaarufu aliokuwa nao ni kwa sababu ya chadema angekuwa mnyenyekevu na kuomba msamaha na angesamehewa tu. Lakini kwa kuwa na kiburi cha kuwa na wafuasi wa kufikirika mmemfanya apoteze kila kitu.

Mimi binafsi nilikuwa ninaona future yake ilikuwa very bright, lakini amekosa uvumilivu na hili ataambiwa na watu wote wenye busara na akili nyingi!
 
ndg mohamed mtoi,
kutokana na kutumia qur'an nashawishika kuamini kuwa wewe ni muislam,tena safi. naomba nikuulize kidogo tu kutokana na ulichotuletea hapa mtandaoni; je, unaamini kuwa kuna siku ya mwisho ambayo kila mtu ataulizwa kuhusu kile alichokifanya? basi nikukumbushe tu kuwa usijisahau sana maaana naona uko bize kutumikia mabwana kiasi hisia zimekutawala kuliko uhalisia wa mambo! vitisho vinatolewa waziwazi vya kila namna hata humu mtandaoni...mahakamani watu wameandaliwa, tena na mh. wakawatusi na kuwazomea na kuwarushia mawe watu fulani, ikiwezekana. yote wakati yanatokea MUISLAM wewe umekaa kimya. leo hii watu wamepigwa unajitokeza na kuzushazusha hiko ulichozusha na visingizio kibao. na hapo sijataja waliopigwa ndani ya mikutano halali ya chama. nina hakika wewe si muislam, hakuna muislam mnafiki kiasi hiki,tena asiye na haya!!!!

Mkuu.

Naomba kurudia tena kama nilivyo muambia mchangiaji mmoja hapo juu.

Mojawapo ya vitu ambavyo huwa navisema dhahiri ni kwamba, kama kuna kitu CCM imefanikiwa kwenye Taifa hili basi si kingine bali ni kuharibu mfumo wetu wa elimu na hivyo kujikuta maskini ya Mungu wengi wenu ambao hamkubahatika angalau kujibidiisha kusoma vitabu mbalimbali vya kujiongezea maarifa, mmejikuta uwezo wenu wa tafakuri tunduizi uko chini ya matendegu ya vitanda. (Sorry to say).

Kwenye uchambuzi wa thread husika uliyo changia naweza kuthubutu kusema kuwa umechangia ukiwa umeeleekea KIBLA wakati maskini ya Mungu kwenye thread hii ulitakiwa kuona mantiki huku ukichambua, kukusanya, na kuunganisha nukta kwa tafakuri tunduizi bila kuanza kusimama kwenye mkeka nakuanza kuiona imani ya mleta mada huku ukiacha mantiki ya mada yenyewe!

Mkuu, Kwa nini usinge chambua hoja na kubomoa hoja kwa hoja, moja baada ya nyingine bila kuondoka kwenye mkondo wa hoja wenye tafakuri jadidi na matokeo yake umeanza kahamia kwenye mkondo wa imani kana kwamba uchambuzi ulihusu imani za kidini?!

Nikushauri urudi na kusoma upya mada yote huku ukiwa umetulia halafu uje tuwekeane mguu chini hoja kwa hoja bila kusimama kwenye mkeka na kugeukia kibla. Halafu tukimaliza kama ni muda wa swala tutie nia tukaswali huku tuliyojadili yakibaki kuwa maoni binafsi yasiyo shawishiwa na imani za kidini bali maoni yaliyojijenga kwenye misingi ya tafakuri tunduizi.
 
Ni kweli tatizo la uwezo wa kuchambua mambo, linalosababishwa na ubutu wa elimu yetu, ni kubwa sana! Wengi wenye vyeti na madegree wamelipia tu, siyo kuyasomea na kufaulu! Kuna ushabiki pia, ule usimba na uyanga unawekwa kwenye mambo ya msingi! Watu wanashabikia hoja za 'kijinga' kabisa kisa kasema fulani, na hoja zenye mashiko zinazomewa, hata bungeni, kisa kasema fulani, ambaye si mwenzetu!

Tatizo kubwa la baadhi ya wachangiaji wengi wa mada mbali mbali humu ni kuwa huwa hawasomi mada husika vizuri na kufanya critical analysis. They don't read between the lines. Wao wanaangalia nani katoa mada na kumrukia yeye badala ya kuichambua mada husika critically. Nakubaliana na wewe kabisa kuwa tatizo kubwa la wachangiaji wengi ni elimu. Na bahati mbaya sana kwa elimu yetu ni kuwa tumeaminishwa kuwa kujua kusoma, kuandika na kuhesabu ndio kuelimika! Na tumeenda mbele zaidi na kuamua kuwa si lazima mtu ajue kusoma, kuandika na kuhesabu ndipo tukaamua kuwa kila anayekwenda shule aendelee mpaka kidato cha nne kwani cha msingi ni kuangalia miaka mtu aliyokwenda shule. Kufikia hapo ndipo tukaanza kuwafaulisha kwenda sekondari wanafunzi wasiojua kusoma, kuandika na kuhesabu ambapo taarifa ya serikali mwakajana ilionesha kuwa wanafunzi zaidi ya 5200 wasiojua kusoma "walifaulu" na kujiunga na sekondari. Sasa jiulize huko sekondari wanafanya nini?! Katika hali hiyo si ajabu kumsikia waziri katika wizara ya elimu akisema Tanzania ni muungano wa visiwa vya Zimbabwe na Tanganyika uliofanyika mwaka 11964. Kwahiyo watu wengi wanasoma kwakuwa wanajua kusoma lakini hawaelewi! Ndio maana utashangaa mtu anajibu nje ya mada kabisa. Watu wana degree wengine ni madaktari na maprofesa lakini ukiwasikiliza ndipo utachoka kabisa. Kuna rais mmoja wa nchi ya kadikika anajidai ni mchumi kwakuwa ana shahada ya uchumi. Alipoulizwa kwanini nchi yako ni masikini pamoja na utajiri wa raslimali zilizojaa tele humo nchini, aliruka futi 100 moja kuwa hata yeye haelewi sababu kwanini nchi yake ni masikini! Sasa ndio usishangae akasema kazi yake kubwa ni kuizunguka dunia kuhemea vibaba ili watu wake wasife njaa kwa kuwa kwa "elimu" yake ya uchumi hajui chanzo cha umasikini katika nchi yake na hana namna ya kuifanya nchi yake ijitegemee kwa rasmali ilizonazo zaidi ya kuwapa wageni kisha yeye kufunga safari baadaye kwenda kwa hao wageni (yeye anawaita wawekezaji) kuhemea! Hiyo ndiyo Danganyika ya wadanganyika!
 
Mohamedi Mtoi wewe kweli tambara la deki, ninguwa Mod ninge kupiga Ban, na upuuzi wako, Yaani hili nalo utummwa na mabwana zako au ndio kujipendekeza tu kwa Mtei.wewe tulia tu kifaranga, tuwashughulikie hawa MAGAIDI.

Nilitegemea ujibu hoja na sio kutoa matusi kwa mtoa hoja. Nilitegemea na wewe umletee facts zaidi ilione alichoandika ni kweli/sio kweli.
 
Sasa hivi hata likitokea janga la njaa nchini lazima litakuwa limesababishwa na CHADEMA,Hata litokee TETEMEKO la ARDHI nchini itakuwa ni kazi ya CHADEMA, Hata yatokee MAFURIKO nchini lazima yatakuwa yamesababishwa na CHADEMA.Watanzania tumekuwa wapumbavu kiasi hiki kweli cha kurubuniwa na watu wa CCM wasio itakia mema nchi yetu????????????????????.Niwaambie tu WATANZANIA kwamba Mungu anaweza kukutoa kwenye shida/matatizo kwa kutumia matatizo mengine, wewe ukajua Mungu amekuacha kumbe yuko na wewe bega kwa bega.Yanayotokea kwa chadema sasa hivi ni kama DHAHABU inapopitishwa kwenye moto ili itoke ikiwa safi kwa ajili ya kutumika.Mimi binafsi nayafurahia sana haya yanayoendelea sasa kwa CDM Kwa sababu yanakikomaza chama zaidi na zaidi na hii itakisaidia sana chama kufanya kazi kwa ufanisi zaidi baada ya kuchukua jukumu la kuipeleka KANANI nchi yetu hapo baada ya kushinda uchaguzi mwaka 2015.
well said.nilikua siamini kama zzk anakisaliti chama,ila kwa mlolongo wa matukio tangu alipovuliwa uongozi hadi matokeo ya kesi aliyokifungulia chama,kila kitu kimekua wazi,amejivua nguo,anajimaliza kisiasa,muda si mrefu atakua kwenye level ya mzee lyatonga au chini zaidi.
 
Hivi umejishughulisha hata kusoma analyisis yote.....? Au umeandika huku ukiongozwa na hisia chafu na kuangalia jina la mleta thread....? Hili ndilo tatizo la sisi wabongo...

Naamini hujasoma mada bali umeangalia jina la mleta mada....Ungesoma mada yote hakika ungekaa kimya au ungetoa hoja za msingi...

Elimika..

Bavicha hamjawahi kuadmit facts. Mkizidiwa sana sana mnawatoa watu akili!

Mna mtazamo kuwa kukubali ukweli ni kukihujumu chama.
 
Kwahiyo kwa mujibu wa Mtoi huyu kamanda aliyeokotwa pale mitaa ya Ununio ni mwongo? hakuumia? hakupigwa?

Au alipigwa na CCM?
 
Tulianza na Mungu,tutamaliza na Mungu.Mafisadi wanataka kuua ndoto za wengi,na watashindwa.:A S 100::A S 100::A S 100:
 
Sasa uaminiwe wewe uliyesoma gazeti na kutoa maoni yako dhaifu au aliyetaka kuuawa. Mimi nadhani walidhani wamemwua kumbe Mungu yu pamoja na Yona. Yona una Mungu na cdm ni ya shetani. Watashindwa na kulegea. Yeyote anayetetea umafia, woga, uzandiki na upuuzi wa aina hii Mungu atamwonyesha njia. Mohamed angalau mwogope Mtume wa jina lako, lakini ukibaki hivyo jehanam. Sikuhukumu na wala sina uwezo huo hila inabidi umwombe Mungu akuondolee unafiki, kwani Mungu alisema mnafiki motoniiiiiiiiiiiiiiiii
 
mimivkama mtanzania wa leo na jana,nimeiona ccm kwa muda mrefu.

1,Ni ukweli usiopingika sasa kwamba ZZK alipewa fedha nyingi na ccm,ili kufanikisha mkakati wao ili kuiangamiza chadema.ushahidi ni jinsi serikali ya ccm inavyotumia nguvu kuivuruga CDM.na jinsi ccm inavyojitokeza kuwa rafiki wa karibu wa kabwe na kuwa mtetezi wake mkuu.
2,Ili mkakati huo utimie ni lazima ingepaswa zitto awe ndani ya mfumo wa chadema,tofauti na akiwa nje ya mfumo wa cdm,kama ambavyo ameshtukiwa mapema na uongozi ndani ya cdm. jambo ambalo linakuwa ni hasara kwa ccm kwani tayari alikwisha lipwa pesa nyingi na hivyo kitendo cha yeye kutimuliwa mapema ni maumivu kwa pande zote yaani ccm na zzk.
3,hivyo ndio maana sasa tunaona hii plan B ya mkakati wa kuivuruga cdm kwa kumtumia huyohuyo zzk,ili pesa zisipotee bure.
¤Ole wenu na hakika woote mnaojifanya kutouona ubaya huu wa siasa chafu za ccm ndani ya nchi kwa malipo hayo mnayopewa lakini muelewe siku na saa itafika na hakika haya yoote yana mwisho,yuko wapi Moi na KANU yake?yuko wapi Chiluba?,yuko wapi Kamuzu Banda,yuko wapi Mobutu sese seko?,

Kila jambo malipo ni hapahapa duniani,ccm damu yote inayomwagika kwa uroho wenu wa madaraka na uoga wa kufikishwa mahakamani kwa ufisadi na ujangili wenu mkumbuke malipo yake ni hapahapa kama hamuamini Jiulizeni yaliyomkuta marehemu Ghadaffi.na wanae leo wanaozea jela huku familia ikiishi kwa fadhila za majirani.

Jikumbusheni majina haya.
*Hosni mubararak.
*Pelves musharaf
*Omar bongo.
*Gnasimbe eyadema nk.

JIBU MNALO!
 
Kwahiyo kwa mujibu wa Mtoi huyu kamanda aliyeokotwa pale mitaa ya Ununio ni mwongo? hakuumia? hakupigwa?

Au alipigwa na CCM?

Unadhani ni nani anayejeruhi watu TZ?Ulimboka, mwangosi, etc .....Zitto naye anajiweka pabaya sana..hizi kelele anazopiga kawapa sana mabwana zake nafsi ya kumdespose wadai ni CDM kwa mategemeo ya kufanya shambulizi la mwisho ktk PR ya CDM....itakuwa ni suicide kwa Zitto....
 
Asanteni kutufungua macho ya ndani.Hata hivyo juhudi za kuikomboa Tanganyika hazitasimama,kwanza ndiyo zimeshika kasi ya ajabu.
Kutekwa na kuteswa Mwenyekiti wa Temeke; Mpango mzima wa kuihusisha CHADEMA huu hapa;

Jana majira ya saa 3.30 asubuhi, watu wapatao watano ambao ni wanachama wa CHADEMA mamluki wa Timu ya Zitto na CCM, wakiwa eneo moja la ofisi ya umma wakisubiri huduma ya muhimu sana, walipokea simu ya taarifa kuwa Mwenyekiti wao wa chama wilaya ya Temeke, Josephat Yona Patrick alikuwa amekutwa mahali fulani Dar es Salaam baada ya kutekwa, kuteswa na kuumizwa na watu wasiojulikana.

Wale watu mara tu baada ya kupokea habari hizo, wakamtafuta mtu waliyekuwa wakimwita kwenye simu jina la Mchange (wala si mwingine ni Mhange huyo huyo anayefahamika katika masuala hayaya circles za usaliti dhidi ya CHADEMA).

Wakamwambia habari hiyo (inavyoonekana yeye alikuwa tayari anaijua na alikuwa mahali fulani kwa mwanasheria). Akawauliza wanaweza kumtaja mtu (a watu) yeyote wanayetaka ahusishwe kwenye tukio hilo kisha afunguliwe kesi. Mtu ambaye akihusishwa itakuwa rahisi kwa viongozi wakuu wa chama na hatimaye chama kizima kuhusishwa kwenye tukio hilo.

Wale watu wakamwambia ili kumalizana na ‘biashara’ ya CHADEMA kabisa kwa kuwahusisha viongozi na hatimaye chama kizima katika tukio hilo ambalo linaweza kukuzwa na kuoneshwa kuwa ni UGAIDI, wako tayari kumtajia majina ya watu wawili ambao wamekuwa wakikihami na kukitetea sana CHADEMA Temeke, hivyo ni kikwazo kwa mikakati yao ya kukihujumu CHADEMA katika eneo hilo.

Kama inavyojulikana kwa upande wa Dar es Salaam, mikakati ya kuihujumu CHADEMA imekuwa ikifanyika kwa kiasi kikubwa sana Temeke.

Wale watu wakamtajia huyo mtu waliyekuwa wakimtaja kwa jina la Mchange, majina ya watu wawili, Mzee Salum Zinga na Bernard Mwakyembe. Wote hawa ni makamanda kweli kweli hapo Temeke, kiasi kwamba Mwenyekiti wa sasa wa CHADEMA Wilaya ya Temeke amekuwa akimhofia sana Mwakyembe kwamba anaweza kuchukua nafasi yake wakati wa uchaguzi ujao wa ndani ya chama hicho.

Baada ya kumtajia majina hayo, wakamwambia wanapitia ofisi ya wilaya ya chama hicho mara moja, kisha wakutane kituo cha polisi ili wakafungue malalamiko dhidi ya watu hao wawili kuwa wamehusika na tukio la kutekwa, kuteswa na kuumizwa kwa mwenyekiti huyo. Mpango mzima ukawa umekamilika na ukatekelezwa.

Tunavyozungumza hapa sasa tayari Mzee Salum Zinga ambaye ni Mwenyekiti wa Wazee Jimbo la Temeke ameshakamatwa na polisi na sasa jeshi hilo linamtafuta Mwakyembe. Lakini kwa namna ambavyo mpango huo umepangwa na utakavyotekelezwa, lengo ni kuwafikia viongozi wa juu.

Mpango huo uliozungumzwa na watu hao watano pale Temeke kwa kuwasiliana na Mchange ndiyo msingi wa kauli za Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Suleman Kova, kutamka kwa kuihusisha CHADEMA huku akijigamba kuwa watamkamata mtu yeyote bila kujali cheo chake. Akilenga viongozi wakubwa wa chama hicho.

Huyo Kova ambaye kwa sababu ameshajitambulisha kuwa ni bingwa wa kugeuza matukio haya ya ukatili kuwa ni ‘filamu’ ya kuficha ukweli na kuanza kusaka uongo, hatuna haja ya kumjadili zaidi ya hapo. Ila ajue tu kuwa mpango mzima unajulikana.

Ndiyo maana sehemu ya mpango huo ni kumlazimisha Yona arudi na kulazwa Moi ambako alikuwa ameagwa jana hiyo hiyo baada ya kubainika hana majeraha makubwa na angetakiwa kurudi baada ya wiki mbili. Hiyo ilikuwa ni baada ya CHADEMA kuwa wamesimamia matibabu yake, ikiwemo kumlipia gharama za hospitali na usafiri kumpeleka nyumbani.

Akiwa hapo hospitalini amezungumza na vyombo vya habari kwa namna tofauti tofauti, kwa mtazamo wa kila chombo na kadri ya maelekezo…

Mpango mzima unaandaliwa pia kupitia vyombo vya habari;

Angalia kutoka magazetini

Kama mlivyoona leo kwenye kurasa za mbele za magazeti yote yaliyotoka leo, habari hii imepewa uzito mkubwa, ingawa kwa namna tofauti tofauti, kulingana na uwezo, sera za vyombo vya habari na MALENGO ya chombo husika, hasa katika kufanya kazi za watawala dhidi ya CHADEMA.

Lengo lingine ni kubeba agenda za makundi ya kuwania urais ndani ya CCM, ambayo CHADEMA ndiyo tishio pekee la wao kufanikiwa kwenda ikulu, hivyo yanafanya kila jitihada kukiumiza chama hicho kwa propaganda nyepesi kama ya tukio hilo.

Kwa upande wako fanyia kazi PICHA zilizotumika leo katika magazeti yote. Zimepigwa wakati gani? Eneo gani? Saa ngapi huyo mpiga picha maalum alikuwa ameandaliwa kwa ajili ya kupiga hizo picha zinazooenakaana kupigwa kwa ustadi na kifaa kizuri? Kuna maswali mengi sana ukizingatia kuwa picha zilizotumika katika habari hiyo ni za aina moja! Nani kazipiga?

Hapa tunaweza kujadili habari kutoka katika magazeti kadhaa;

Mtanzania

Gazeti hili limeipatia habari hii kichwa kisemacho INATISHA. Ndani ya habari gazeti hilo kwa malengo linalojua yenyewe, labda likiongozwa na kile kinachoweza kuitwa aina ya weledi wa aina yake wa taaluma ya habari, sera za chombo hicho na malengo ya wamiliki, limewahusisha viongozi wa CHADEMA katika tukio hilo kwa hali ambayo inaacha maswali mengi sana.

Mathalani kwenye moja ya nukuu zake, wamemnukuu Yona akisema

“Bernard na Mwakyembe walinisalimia na kuondoka, baada ya hapo, wakaja watu wengine wane ambao siwajui, wakajitambulisha kwangu kuwa ni polisi wanatoka kituo cha kati, hivyo basi wananihitaji kwa ajili ya mahojiano.”

Waandishi wa gazeti hili wangekuwa na nia ya kufanya uandishi unaowajibika kwa jamii, wangefanya kazi yao kidogo tu wangebaini kuwa Yona katika hilo alikuwa amewadanganya au amewaambia kitu ambacho kinahitaji kufanyiwa kazi zaidi.

Kwa sababu kama umefuatilia mtiririko wa taarifa hii, kuna mtu anaitwa Bernard Mwakyembe (mtu mmoja), lakini hapa Yona ametaja kwamba hao ni watu wawili tofauti. Gazeti lilipaswa kufanya kazi yake badala ya kutumika kuwa karatasi ya kufanyia propaganda za CCM dhidi ya CHADEMA.

Katika aya mbili zinazofuata ndiyo zinaliacha gazeti hilo uchi kabisa kwamba limeamua kutumika kwenye mkakati unaoandaliwa na CCM kupitia vyombo vya dola. Limeandika hivi;

“Tulibishana sana tena ni muda mrefu, mwisho nikawaambia wanionyeshe kibali cha kunikamata lakini walinijibu kuwa wao ni polisi, napaswa kutii amri kama kuna mahojiano zaidi yatafanyika kituoni, nikapanda gari lao na kuondoka,” alisema Patrick.

Soma na aya inayofuata ambayo gazeti hilo limeandika kama vile lilikuwepo wakati tukio linatokea. Kwa sababu lilipaswa kuandika maneno ya Yona ni madai…allegations.

“Alipohoji sababu ya watu hao kujitambulisha ni polisi wakati anawajua kuwa si wanausalama, walianza kumshurutisha kuingia ndani ya gari alipogoma walimsukuma kwa nguvu ndani ya gari hilo na kumwambia kuwa wanampeleka kituo cha kati.”

Aya hizo mbili zilitosha kabisa kuwashtua waandishi au wahariri makini kuwa chanzo cha habari wanachozungumza nacho si cha kuaminika au kinazua maswali mengi mno.

Mtu aliyesema dakika kadhaa tu zilizopita kuwa walikuja watu wengine wanne hawajui, wanajitambulisha kuwa ni polisi, akawahoji vitambulisho, wakashindwa kutoa, akabishana nao sana maeneo ya baa (hakuna mtu aliyesikia?), cha ajabu akakubali kuondoka nao wakati yeye hawajui ni akina nani, ghafla tena anasema kuwa anawajua kuwa si wanausalama. Kuna maswali mengi sana?!

Kwa ujumla habari nzima ya Mtanzania kuhusu tukio hili, ilistahili kuandikwa na yale magazeti ‘----’ ya ajabu ajabu yaliyoko mtaani, chini ya waandishi na wahariri ambao hawajui wala hawathamini chembe hata moja ya maadili achilia mbali weledi wa kitaaluma.

Wameandika habari ile badala ya kutumia madai ya nafsi ya tatu umoja, wao wameandika kama vile walikuwepo hatua kwa hatua na mlalamikaji Yona, lengo zima ikiwa ni kuwahusisha viongozi wa CHADEMA na chama hicho katika sakata zima. Je Mtanzania maslahi yao katika hili ni yapi? Bila shaka ni makubwa sana.

Angalia aya hizi zilivyoandikwa kwa makusudi, kimkakati;

Patrick ambaye ni rafiki wa karibu na aliyekuwa Naibu Katibu Mkuu wa CHADEMA, Zitto alisema kuwa mgogoro wake na viongozi wakuu wa chama hicho ulianza tangu alipoitisha mkutano na waandishi wa habari wa kuitaka Kamati Kuu ya chama hicho kuitisha mkutano wa kujadili suala la kina Zitto, Samson Mwigamba na Dk. Kitila Mkumbo.

“Niliitisha mkutano ule ili kuwaambia viongozi wa CHADEMA kujadili suala la kina Zitto, Kitila na Mwigamba ndani ya chama na si kuwavua uanachama kama ilivyojitokeza jambo ambalo lilipingwa na viongozi wa chama hicho,” alisema Patrick.

Alisema, kutokana na hali hiyo viongozi wa chama hicho akiwemo Mwenyekiti wake Freeman Mbowe na Katibu Mkuu, Dk. Willibrod Slaa alimwita na kumuambia aache urafiki na Zitto la sivyo watamfukuza uanachama. (Walimwita lini, wapi kwa namna gani, hivi kweli viongozi wa juu namna hiyo wanaweza kumwita kiongozi wa wilaya hivi hivi tu, hicho chama si CHADEMA labda CHAUMA na viongozi hao hawawezi kuwa Mbowe wala Slaa, lakini kibaya kabisa, gazeti wala halikuwatafuta kutaka kujua upande wao na kupata hata ukweli. Uandishi wa hatari sana huu)

“Waliniita na kuniambia niachane na Zitto, nilipinga ndipo waliponiambia nijiondoe ndani ya chama hicho, niliendelea kupinga,” alisema.

Alisema kutokana na hali hiyo, viongozi hao walimwambia aitishe mkutano wa Kamati ya Utendaji ya Wilaya na kuwaambia wajumbe wa kamati kuwa yeye si rafiki wa Zitto na kwamba hawezi kumuunga mkono kwenye harakati zake, lakini aliendelea kukataa suala hilo. (Hivi gazeti makini linaweza kunukuu uongo kama huu na kusema limeandika habari kwa ajili ya watu kusoma. Kuna tofauti gani na magazeti ya Yule jamaa mtunga hadithi).

“Tangu nilipoitisha mkutano wa waandishi wa habari wa kupinga uamuzi wa kuwavua uanachama akina Zitto, Mwigamba na Kitila, nimekuwa kwenye mvutano mkubwa na viongozi wangu wa juu, nimepokea vitisho vingi ambavyo nilivirekodi kwenye simu yangu ya mkononi waliyoichukua,” alisema Patrick.

(Kwa trend ambayo chanzo hicho kimeonesha tanguy huko juu, huna haja ya kwenda hata darasa moja kujua kuwa huu ni uongo mkubwa unaosemwa na mtu anayejifunza kuzalisha fitna na majungu, lakini pia mwanafunzi wa kutengeneza mgogoro, lakini kikubwa kupika kesi. Mathalani mhariri makini hawezi kupitisha uchafu kama huu uwe habari, angeuliza tu, huyo Yona alifanya huo mkutano lini?, Ulihusu nini? Je ni kweli ulihusu kupinga kuwavua uanachama watu hao? Kwa nini kutumika kuandika uongo?).

Aliongeza, suala hilo liliendelea hadi Dk. Slaa na Mbowe walipomwita na kumlazimisha aitishe tena kikao kingine cha kamati tendaji ili atangaze kujiuzulu mwenyewe nafasi yake kabla ya kumfukuza uanachama, jambo ambalo alilipinga tena. (Umakini wa waandishi na wahariri wa gazeti hilo haukuwatuma kuona umuhimu wa kuwatafuta viongozi hao walau wahalalishe huo uchafu walioamua kuuita ni habari ya kuwapelekea Watanzania. Hii ni hatari sana.)

“Dk. Slaa aliniandikia barua ya kunitaka niitishe mkutano nilipoona kelele zinazidi nikaamua kuitisha lakini wajumbe wa kikao nilichoitisha kwa pamoja wakaniunga mkono na kusema wana imani na mimi, hivyo basi hawataki niondoke.

“Baada ya hapo, Dk. Slaa akaniandikia barua na kuniambia kuwa kikao nilichoitisha ni batili na kwamba wanatakiwa kuitisha kuitisha kikao kingine Januari 10 mwaka huu.”

Kwa ujumla habari nzima ya Mtanzania ni ----. Na kuonesha dhahiri malengo na nia ovu waliyonayo dhidi ya CHADEMA kupitia tukio hilo la kusikitisha la kutekwa na kuteswa kwa Yona, gazeti hili ambalo limeandika mengi sana ya KUUMIZA, yanayokiuka maadili na weledi wa uandishi, likimnukuu mwenyekiti huyo akisema uongo dhidi ya Mbowe na Dk. Slaa, halikuwatafuta viongozi hao, lakini likamtafuta Zitto Kabwe.

Wanaandika hivi;

“Nikiangalia tukio langu na mgogoro uliopo ndani ya chama najua nimeumizwa kwa ajili ya kumtetea Zitto, kwa sababu nimekuwa nikipokea vitisho kutoka kwa viongozi wa juu wa chama na M4C,” alisema.

Kukamilisha mpango huo wa spinning ya kuwahusisha viongozi wa CHADEMA na hatimaye chama kizima katika sakata hilo, Zitto akatafutwa na akasema hivi;

Akizungumzia tukio hilo, Zitto amesema vurugu kamwe siyo suluhu ya siasa nchini na kwamba ni kitendo kinacholenga kuwaingiza watu katika woga na kuwatisha.

“Haya ni matendo ya kikatili na ya kumuogopesha kutokana na kupinga baadhi ya mapendekezo ya upande wa baadhi ya viongozi Kamati Kuu ya chama.

“Natoa changamoto kwa viongozi zote wa Chadema kwamba sasa wakanushe kuwa vurugu siyo silaha yao katika siasa,” alihitimisha Zitto.

Huyu mtu tayari alishajua na kuhitimisha kuwa viongozi na chama chake kinahusika na tukio hilo? Kwa nini anawahi kuhitimisha kuwasukumia tukio zito kama hilo ambalo linaweza kuharibu kabisa chama chake ambacho eti anataka kuwa mbunge na kiongozi wake. Au ni mwendelezo wa mkakati ule ule, wakakutanishwa kwenye kipindi cha Star tv asubuhi yeye na Mwigulu, Mwigulu Nchemba akajifanya anatoa habari ya ugaidi wa CHADEMA?

Habari za kiuchambuzi juu ya mkakati huu wa kutaka kurudisha taswira ya ugaidi na kuihusisha CHADEMA na matukio ya vurugu yanayohusisha umwagaji wa damu ikipangwa kwa ustadi na wale wale, kwa mtindo ule ule, kwa malengo yale yale, zitaongezwa baadae katika andiko hili;

Chanzo:Chadema diaspora.
 
Mohamedi Mtoi
hizi hekaya zenu za kutunga tumeshazizoea! sisi tunafuatisha ukweli kutoka kwa muhusika.

ukwel upi mbna unapotosha ukwel kijana unaish kwa ndoto ukwel mpk TCRA walete maongez tuyasikie ndo utakubali ukwel acha mambo ya kipmbav thn mbona ya mwakyembe na mwandosya kuwekewa sumu hamkufatilia ukwel?? au kwasababu ndo style yenu hata bomu mlisema chadema wamejipga wenyewe
 
Hivi kuna chama kinaitwa M4C? Kimesajiliwa lini na nani mwenyekiti wake??
 
Back
Top Bottom