Mpango Huu wa Lowassa ulifanikiwa vipi?

Mzee Mwanakijiji

Platinum Member
Mar 10, 2006
33,476
39,995
SERIKALI imeweka bayana mkakati mpya wa muda mfupi na mrefu utakaosaidia kupunguza msongamano wa magari katika Jiji la Dar es Salaam.

Akizungumza na waandishi wa habari jana baada ya kumaliza kikao na viongozi wa Mkoa wa Dar es Salaam, Waziri Mkuu, Edward Lowassa, alisema barabara za Morogoro na Ali Hassan Mwinyi, zitagawanywa ili kupunguza msongamano nyakati za asubuhi na jioni.

Lowassa, alisema nyakati hizo magari katika Barabara ya Morogoro yatakayokuja mjini, yatatumia barabara tatu na moja itatumika kwa magari yanayotoka katikati ya mjini kwenda nje ya mji, na kuongeza kuwa utaratibu huo utafanyika pia kwenye Barabara ya Alli Hassan Mwinyi.

Katika mkutano huo, viongozi hao wamekubaliana kuwa zinunuliwe taa za barabarani kwa vile taa zilizopo sasa ni chakavu na nyingine hazifanyi kazi.

Mkoa wa Dar es Salaam, una taa 3,021 zinazofanyakazi wakati nyingine tisa ni mbovu, hivyo viongozi hao wameiagiza Wizara ya Miundombinu kutumia sheria ya manunuzi ya mwaka 2004 ili kuweka taa mpya katika jiji hilo.

Kadhalika, wamekubaliana kuongeza idadi ya polisi wa usalama barabarani ili kupunguza tatizo la foleni linalochelewesha ukuaji wa uchumi nchini.

“Jamani tatizo la foleni ni letu sote, tushirikiane na mamlaka husika kuwaelimisha wananchi kuhusu matumizi sahihi ya barabara na sheria zake…naamini tutapunguza kwa kiasi kikubwa kero hii,” alisema Waziri Mkuu.

Aidha, maamuzi ya kikao hicho ni kutowavumilia wapiga debe na kuwataka waondoke, kwa madai kuwa wanachangia msongamano wa magari na kuwataka wenye malori kutopita katikati ya jiji.

Hata hivyo aliutaja mpango wa muda mrefu kuwa ni ule wa ujenzi wa barabara za pembezoni zitakazounganisha wilaya hadi wilaya.

Wakati huo huo, Waziri wa Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI), Mizengo Pinda, alisema mradi wa mabasi yaendayo kasi utaanza wakati wowote kuanzia sasa na kwamba serikali imedhamiria kutoa sh bilioni 10 kama mchango wake katika kufanikisha mradi huo.

Pinda, alisema mradi huo unafadhiliwa na Benki ya Dunia na utatekelezwa kwa awamu sita, na kuzitaja barabara husika kuwa ni Morogoro, Kilwa, Ali Hassan Mwinyi na Kawawa.

Habari Leo??
 
Akizungumza na waandishi wa habari jana baada ya kumaliza kikao na viongozi wa Mkoa wa Dar es Salaam, Waziri Mkuu, Edward Lowassa, alisema barabara za Morogoro na Ali Hassan Mwinyi, zitagawanywa ili kupunguza msongamano nyakati za asubuhi na jioni.

Waziri wa Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI), Mizengo Pinda, alisema mradi wa mabasi yaendayo kasi utaanza wakati wowote kuanzia sasa na kwamba serikali imedhamiria kutoa sh bilioni 10 kama mchango wake katika kufanikisha mradi huo.

Hii ni habari ya lini?

 
Mpango wa njia tatu uliongeza ajali kwa waenda kwa miguu hasa wakti wa kuvuka barabara, ulianza bila elimu kwa waeanda kwa miguu, watu walivuka bila kuangalia kama kuna magari mengine
 
Hii ndiyo mipango ya viongozi wetu!
Hivi serikalini si kuna kitu inaitwa OPRAS, kwanini watu wanaokubaliana na wananchi kutekeleza mambo fulani, na wasitekeleze, bado wanaendelea kuajiriwa?
 
Hii ndiyo mipango ya viongozi wetu!
Hivi serikalini si kuna kitu inaitwa OPRAS, kwanini watu wanaokubaliana na wananchi kutekeleza mambo fulani, na wasitekeleze, bado wanaendelea kuajiriwa?

Mkuu tatizo hata hiyo OPRAS wanaoiratibu ambao ndio Ofisi ya Rais Menejiment ya Utumishi wa Umma ndio hawana habari kabisaaaaa!!! Sasa nani atamshika mwenzake uchawi?
 
Huu mpango ulisababisha ajali na uliuwa wavuka kwa miguu wengi sana maeneo ya Sayansi, Makumbusho na Victoria, ulikuwa ni mpango mbovu na usio na elimu kwa watumiaji wa barabara.....na hakika kwa nguvu za mwenyezi damu yao haitapotea hivihivi.

Sema Ameni....
 
utekelezaji umeanza na daraja la kigamboni unaotarajiwa kuanza wakati wowote kuanzia sasa yaani january 2012
 
wengi wanashangaa kuwa mwanakijiji anasema nini hawamwelewi.

kama daraja la kigamboni wanasema kuwa lilianza kuzungumziwa miaka 35 iliyopita na baada ya hiyo miaka 35 ndio wamesaini mkata wa kuanza kwa ujenzi basi na story kwani miaka 35 imekwisha kianzi cha kuanza utekelezaji?
 
Haaaaaaaaaa Mzee Mwanakijiji kama kawaida Siju kama Mzee wangu Pinda amekuelewa kupitia ujumbe huu.Nimependa sana kwa kuwa kama alikuwa Waziri wa TAMISEMI akatoa ahadi kuwa mradi wa mabasi yaendayo kwa kasi yako karibu kuanza kazi 2007 na wakati huo waziri wake mkuu EL akitoa matamko ya kupambana na foleni na elimu kwa umma kuhusiana na matumizi ya barabara leo hiii 2012 aliyekuwa Waziri wa TAMISEMI ni Waziri mkuu miaka miatano baadae mambo ni yale yale tena ndio hapatoshi,na huo mradi wa mabasi ambayo ulitarajiwa kuanza 2007 miaka mitano kwishney bila harufu yoyote hata ya uda mpya barabarani.

Hakika Mwanakijiji ili ni somo kubwa kwa Mzee Pinda.
 
Huu mpango ulisababisha ajali na uliuwa wavuka kwa miguu wengi sana maeneo ya Sayansi, Makumbusho na Victoria, ulikuwa ni mpango mbovu na usio na elimu kwa watumiaji wa barabara.....na hakika kwa nguvu za mwenyezi damu yao haitapotea hivihivi.

Sema Ameni....

Mkuu umesema vizuri, elimu kwa watumia barabara ilikosekana lakini mpango wenyewe ulikuwa mzuri na ulikuwa unasaidia kupunguza foleni wakati wa peak hours. Tatizo lingine ni kwamba traffic police walishindwa kuusimamia mpango huu kabisa. Otherwise, mtindo huu wa njia tatu unatumika katika baadhi ya nchi na unafanya kazi vizuri sana na kusaidia kupunguza trafic jam.

Tiba
 
Komredi mleta mada,TATIZO LA FORENI DAR AU NCHI NZIMA SIYO BARABARA.
Tatizo ni magari yanakwenda wapi ndo tatizo,?
Wanaoshughulika na maswala haya awajuii tatizo hili,kuwa magari yanakwenda wapi.?
Dar hatuna tatizo la barabara ata kidogo ni wausika kukosa ufumbuzi wa wapi magari yanakwenda.?
 
Mimi sifahamu kuwa ulitaka kutueleza nini.
Soma heading na contents utaelewa maana kaanza na swali kuwa mpango huu wa EL ulifanikiwa vipi? Na akafuatia na maelezo ya mpango wenyewe ambao ulibuniwa 2007 na EL, kwakuwa tatizo la msongamano jijini Dar bado ni kubwa MM alitaka kujua ni kwa vipi mpango ule ulifanikiwa..
 
Kutumia barabara tatu kulisababisha ajali nyingi kwa waendao kwa miguu na vyombo ya usafiri pia. hT Insurance companies couldn't compesate these accidents kwani zilikuwa zinatokea kwenye wrong side of the driving lane!
 
Huu mpango ulisababisha ajali na uliuwa wavuka kwa miguu wengi sana maeneo ya Sayansi, Makumbusho na Victoria, ulikuwa ni mpango mbovu na usio na elimu kwa watumiaji wa barabara.....na hakika kwa nguvu za mwenyezi damu yao haitapotea hivihivi.

Sema Ameni....
Amen. Nashukuru kuwa kule kwenye double lane huu mpango ulikufa natural death. lakini kile kipande cha Moroco na Mwenge bado ni hatari sana kwa sababu wameweka lane tatu na wakati mwingine vigumu sana kujua ile lane ya katikati ni nani ana haki ya kuitumia. Na huu ukichaa wa madereva wetu, basi waenda miguu tunaendelea kuteseka sana eneo hili
 
Mbona sielewi licha ya kusoma.
Maana yake mleta mada anajaribu kuonyesha kuwa Bwn Edward Ngoyai Lowasa ana influence kubwa bado kwenye hii serikali ya Kikwete pamoja kuwa yeye ni mwizi mkubwa wa fedha zetu!!!!!!!!!! Hakuna mtu wa kumshika mwizi huyu, si Mizwengwe Pinda PM wala Mkuu wa Magogoni the man is above the law!!!!!!!!!!!!!

 
Back
Top Bottom