Mpaka sasa Serikali ipo kimya juu ya Watu 49 pamoja na watu sita wa familia moja waliofariki wakimuaga Rais Magufuli

SOPINTO

Senior Member
Oct 19, 2020
155
385
Ni kama vile hakuna jambo lolote la kuhuzunisha na kusitikitisha lililotokea wakati wa kuaga mwili wa aliyekuwa Rais wa awamu ya tano, mpaka sasa hakuna kilichofanyika kwa wafiwa si kwa serikali ya ngazi ya wilaya au mkoa wa DSM.

Kutokana na mkanyagano huo , Familia moja jijini Dar Es Salaam iliepoteza watu sita katika mkanyagano uliotokea wakati maelfu ya wakaazi wa jiji hilo walipojitokeza kuuaga mwili wa Rais John Magufuli. Kijana mmoja kwa jina la Dennis Mtuwa amepoteza mke wake, watoto wawili, na wapwa zake wawili. Walienda kumuaga aliyekuwa Rais wao jana Jumapili katika Uwanja wa Uhuru, lakini hawakurejea tena nyumbani, lakini cha kushangaza serikali ipo kimya si wakati wa msiba na hata baada ya mazishi gharama zote zimetolewa na familia iliyopata maafa.

Serikali iangalie Familia hizi zilizopoteza wapendwa wao , sio jambo tu la RPC kutaja majeruhi pamoja na idadi ya vifo kama vile ni sherehe , lakini pia familia hizi zijue zina haki zao kisheria zikiweza zitafute mwanasheria msomi hili zifungue kesi.

Msimamizi wa shughuli yote ya kuaga mwili wa hayati JPM alikuwa serikali lakini kutokana na uzembe walieshindwa kujipanga kuweka mazingira mazuri ya usalama wa Raia , matokeo yake kusababisha maafa.

Wanasheria mnasemaje kuhusu hili?

L.jpg
 
Lab

labda useme system inaonewa .....
Serikali inatakiwa ifanyeje na watu wameshakufa? Hivi wale watu waliokanyagana kwenye kukanyaga mafuta kwa mwamposa nani aliwajibika?
.
.
Vitu vingine ni vya bahati mbaya kutokana na situation yenyewe , ni Jambo la bahati mbaya..ajali.
Hakuna alie walazimisha kwenda, ilikuwa kwa mapenzi yao, wamekufa bahati mbaya basi maisha yaendelee.
 
Majaliwa, Mambo yaliratibiwa vizuri mpaka tukampumzisha mpendwa wetu chato.......kazi ziendelee kama Rais wetu Samia alivyoshauri.

Nota bene:wafiwa wangetazwamwa kwa jicho la huruma na kamati ya PM
 
Serikali inatakiwa ifanyeje na watu wameshakufa? Hivi wale watu waliokanyagana kwenye kukanyaga mafuta kwa mwamposa nani aliwajibika?
.
.
Vitu vingine ni vya bahati mbaya kutokana na situation yenyewe , ni Jambo la bahati mbaya..ajali.
Hakuna alie walazimisha kwenda, ilikuwa kwa mapenzi yao, wamekufa bahati mbaya basi maisha yaendelee.
Wamekufa kwa uzembe. Siyo bahati mbaya.
 
Hivi kulikuwa na ulazima gani kwa huyo mama kwenda kuaga na watoto wadogo.huyo denis ilikuwaje akamruhusu mkewe kwenda uwanjani na watoto wadogo
 
Wamekufa kwa uzembe. Siyo bahati mbaya.
Haya, kwahiyo marehemu walipwe? Na wao walikuwa wazembe..wapo walioona msongamano ni mkubwa wakaahirisha wakaondoka.
Mtu unaendaje sehemu Kama ile na watoto? Kwanza watoto kuaga maiti ni kuwaonea...halafu hata sio ndugu yao.
 
Wewe
Serikali inatakiwa ifanyeje na watu wameshakufa? Hivi wale watu waliokanyagana kwenye kukanyaga mafuta kwa mwamposa nani aliwajibika?
.
.
Vitu vingine ni vya bahati mbaya kutokana na situation yenyewe , ni Jambo la bahati mbaya..ajali.
Hakuna alie walazimisha kwenda, ilikuwa kwa mapenzi yao, wamekufa bahati mbaya basi maisha yaendelee.
Wewe husiseme kama vile unakunywa maji na husifananishe kwa mwamposya na public issue kama ile, think twice na sio simple kama unavyofikiri wewe ..eti maisha yaendeleee ... jua katika public issue kama ile kila mtu anawajibu wake sasa kuna uzembe ulifanyika ....
 
Hivi kulikuwa na ulazima gani kwa huyo mama kwenda kuaga na watoto wadogo.huyo denis ilikuwaje akamruhusu mkewe kwenda uwanjani na watoto wadogo
... kuna watu wana akili za ajabu hadi wanashangaza!
 
Wewe

Wewe husiseme kama vile unakunywa maji na husifananishe kwa mwamposya na public issue kama ile, think twice na sio simple kama unavyofikiri wewe ..eti maisha yaendeleee ... jua katika public issue kama ile kila mtu anawajibu wake sasa kuna uzembe ulifanyika ....
Hata wazazi walioenda na watoto wadogo wakafa ni wazembe.
 
Hivi kulikuwa na ulazima gani kwa huyo mama kwenda kuaga na watoto wadogo.huyo denis ilikuwaje akamruhusu mkewe kwenda uwanjani na watoto wadogo
swala la ulazima au sio lazima hiyo ilihakikishwa na mamlaka husika , hatujaji marehemu tunamjaji msimamizi we ukiandaa issue yako alafu wakaja wageni then likatokea tatizo hata moto au ukuta kuanguka wageni wakafa au kuumia utamjaji marehemu kwanini alikaa pale? au utamuuliza msimamizi kwanini aliweka wageni katika utaratibu mbovu... ...
 
Back
Top Bottom