Lucas Mwashambwa
JF-Expert Member
- Jul 28, 2022
- 15,668
- 10,091
Ndugu zangu Watanzania,
Kama mwanadamu mwenye moyo wa nyama na mwenye Damu natambua kuwa hakuna anayependa kudhalilishwa, wala kushushiwa heshima yake. Hakuna binadamu mwenye akili Timamu anayeweza kufurahi kuona mama yake au baba yake au wazazi wake au walezi wake wakitukanwa au mama yake akitukanwa na kijana ambaye ni sawa kiumri. Rais Samia siyo mama yangu mzazi lakini kiumri ni sawa na mama yangu . Ni kweli Rais samia siyo mama wa watanzania bali ni Rais wa watanzania.
Lakini Rais Samia Ni Mwanadamu kama tulivyo sisi, mwenye moyo wa nyama na hisia za maumivu kama zetu. Ni jambo la kusikitisha kuumiza, kusononesha sana unapoona vijana wadogo kiumri wakitoa lugha za matusi, kuudhi, kudhalilisha na kumshushia heshima mh Rais wetu. Huwa najiuliza hawa vijana wenzangu wamekulia na kulelewa katika mazingira gani? Walizaliwa na kubebwa miezi tisa Tumboni na mama zetu? Walinyonya maziwa ya mama zetu? Walipata upendo wa mama? Walifunzwa adabu? Walikaa na mama zao katika makuzi yao?
Kijana mwenye adabu, maadili mema, hofu ya Mungu, nidhamu, staha, heshima unawezaje kumtukana na kutumia lugha za matusi na udhalilishaji kwa mh Rais? Unapata wapi ujasiri wa aina hiyo? Unaanzia wapi? Unaanzeje kuandika matusi mtandaoni kumkashifu mh Rais? Vijana tunavuta bangi? Tumezibuka akili? Tumekosa malezi?
Kwani hatuwezi kukosoa jambo pasipo kutumia matusi? Hatuwezi kuandika jambo kwa kutumia lugha za heshima ,staha na adabu? Kwani nani amewahi kuwa shujaa katika jamii kwa matusi? Kwanini Tumekosa adabu na heshima kiasi hiki? Nini shida yetu vijana? Tatizo nini? Nani katuroga? Mbona tumekuwa waropokaji na wenye mihemuko?
Kesho Ya Taifa letu ipo Hatarini sana kwa aina ya vijana Tuliopo Sasa. Ni vipi Tutapokea madaraka kwa wazee wetu na kulipeleka Taifa mbele kwa aina ya ujenzi wa hoja wa matusi? Ni vipi tutaaminiwa na watanzania na kupewa madaraka makubwa pasipo hofu ya kuliangamiza Taifa letu kwa midomo yetu na matendo yetu?
Vijana aina ya Salim hamed salimu walioshika madaraka katika umri wa miaka 22 wapo wapi kwa kizazi cha sasa? Wapo wapi akina Warioba wengine? Wapo wapi akina Samia wengine? Wapo wapi akina kinana,Kikwete,Mwandosya, kimiti? wapo wapi akina Nyerere wengine? Hawa ni vijana kwa wakati wao ambao waliaminiwa na kufanya vizuri katika Taifa letu.
Vijana Tubadilike,Tuache matusi,tuwe na adabu, heshima na staha kutoka katika vinywa vyetu. Tujifunze kuheshimu wengine hata pale tunapotofautiana mitizamo ,tuwe watulivu na wenye uadilifu wa hali ya juu sana,tuwe wenye subira na uvumilivu. Tujifunze kusikiliza zaidi kuliko kuongea sana na kuropoka. Tumheshimu Rais wetu na tumkosoe kwa lugha za heshima, staha na adabu. Rais wetu ni mwanadamu na siyo malaika na Taifa letu katu na kamwe halitaongozwa na malaika, hivyo lazima tufahamu ya kuwa hakuna aliye kamilika na hivyo katika kutokamilika huko yatupasa kukosoana na kushauriana kwa lugha za heshima.
Rais wetu ni msikivu na mwenye masikio yenye kusikia sauti zote, ni mnyenyekevu na mzalendo. Tumwambie kwa lugha za heshima atatusikia na kufanyia kazi mawazo yetu. Binafsi sipendi sana na nachukizwa sana napoona kijana mwenzangu anatumia lugha za matusi kwa Mh Rais ,Naumia sana na nakuwa naona uchungu sana kwa hatua mbaya ambayo baadhi yetu vijana tumefikia hatua ya kukosa adabu,staha na heshima.
Kazi iendelee, mama Ametufikia na kuwafikia watanzania kwa utumishi wake uliotukuka wa kugusa maisha ya watanzania wanyonge wasio na Sauti.
Lucas Hebel mwashambwa, Kijana mzalendo na mpenda nchi yangu.
0742-676627.
Kama mwanadamu mwenye moyo wa nyama na mwenye Damu natambua kuwa hakuna anayependa kudhalilishwa, wala kushushiwa heshima yake. Hakuna binadamu mwenye akili Timamu anayeweza kufurahi kuona mama yake au baba yake au wazazi wake au walezi wake wakitukanwa au mama yake akitukanwa na kijana ambaye ni sawa kiumri. Rais Samia siyo mama yangu mzazi lakini kiumri ni sawa na mama yangu . Ni kweli Rais samia siyo mama wa watanzania bali ni Rais wa watanzania.
Lakini Rais Samia Ni Mwanadamu kama tulivyo sisi, mwenye moyo wa nyama na hisia za maumivu kama zetu. Ni jambo la kusikitisha kuumiza, kusononesha sana unapoona vijana wadogo kiumri wakitoa lugha za matusi, kuudhi, kudhalilisha na kumshushia heshima mh Rais wetu. Huwa najiuliza hawa vijana wenzangu wamekulia na kulelewa katika mazingira gani? Walizaliwa na kubebwa miezi tisa Tumboni na mama zetu? Walinyonya maziwa ya mama zetu? Walipata upendo wa mama? Walifunzwa adabu? Walikaa na mama zao katika makuzi yao?
Kijana mwenye adabu, maadili mema, hofu ya Mungu, nidhamu, staha, heshima unawezaje kumtukana na kutumia lugha za matusi na udhalilishaji kwa mh Rais? Unapata wapi ujasiri wa aina hiyo? Unaanzia wapi? Unaanzeje kuandika matusi mtandaoni kumkashifu mh Rais? Vijana tunavuta bangi? Tumezibuka akili? Tumekosa malezi?
Kwani hatuwezi kukosoa jambo pasipo kutumia matusi? Hatuwezi kuandika jambo kwa kutumia lugha za heshima ,staha na adabu? Kwani nani amewahi kuwa shujaa katika jamii kwa matusi? Kwanini Tumekosa adabu na heshima kiasi hiki? Nini shida yetu vijana? Tatizo nini? Nani katuroga? Mbona tumekuwa waropokaji na wenye mihemuko?
Kesho Ya Taifa letu ipo Hatarini sana kwa aina ya vijana Tuliopo Sasa. Ni vipi Tutapokea madaraka kwa wazee wetu na kulipeleka Taifa mbele kwa aina ya ujenzi wa hoja wa matusi? Ni vipi tutaaminiwa na watanzania na kupewa madaraka makubwa pasipo hofu ya kuliangamiza Taifa letu kwa midomo yetu na matendo yetu?
Vijana aina ya Salim hamed salimu walioshika madaraka katika umri wa miaka 22 wapo wapi kwa kizazi cha sasa? Wapo wapi akina Warioba wengine? Wapo wapi akina Samia wengine? Wapo wapi akina kinana,Kikwete,Mwandosya, kimiti? wapo wapi akina Nyerere wengine? Hawa ni vijana kwa wakati wao ambao waliaminiwa na kufanya vizuri katika Taifa letu.
Vijana Tubadilike,Tuache matusi,tuwe na adabu, heshima na staha kutoka katika vinywa vyetu. Tujifunze kuheshimu wengine hata pale tunapotofautiana mitizamo ,tuwe watulivu na wenye uadilifu wa hali ya juu sana,tuwe wenye subira na uvumilivu. Tujifunze kusikiliza zaidi kuliko kuongea sana na kuropoka. Tumheshimu Rais wetu na tumkosoe kwa lugha za heshima, staha na adabu. Rais wetu ni mwanadamu na siyo malaika na Taifa letu katu na kamwe halitaongozwa na malaika, hivyo lazima tufahamu ya kuwa hakuna aliye kamilika na hivyo katika kutokamilika huko yatupasa kukosoana na kushauriana kwa lugha za heshima.
Rais wetu ni msikivu na mwenye masikio yenye kusikia sauti zote, ni mnyenyekevu na mzalendo. Tumwambie kwa lugha za heshima atatusikia na kufanyia kazi mawazo yetu. Binafsi sipendi sana na nachukizwa sana napoona kijana mwenzangu anatumia lugha za matusi kwa Mh Rais ,Naumia sana na nakuwa naona uchungu sana kwa hatua mbaya ambayo baadhi yetu vijana tumefikia hatua ya kukosa adabu,staha na heshima.
Kazi iendelee, mama Ametufikia na kuwafikia watanzania kwa utumishi wake uliotukuka wa kugusa maisha ya watanzania wanyonge wasio na Sauti.
Lucas Hebel mwashambwa, Kijana mzalendo na mpenda nchi yangu.
0742-676627.