Moyo wa Shukrani na Utayari...😇

Kasie

Platinum Member
Dec 29, 2013
21,248
36,301
Habari ya muda huu popote pale ulipo wana jamvi.

Kama ulipo haijadondoka tarehe 25/12/2023 basi endelea kuvuta subira itafika tuu punde si punde.

Ni sikukuu leo ya kuadhimisha kukumbuka kuzaliwa kwa Kiongozi wa waumini wa dini ya Kikristo.

Heri ya Sikukuu na Maandalizi ya Mwaka Mpya 2024.

Mpendwa, kama hadi muda huu hujajua sikukuu inaendaje usipate msongo wa mawazo. Shukuru kwa uzima na afya uliyonayo, siku itapita na maisha yataendelea.

Imezoeleka sikukuu ni siku ya kula chakula kizuri, uvae nguo mpya, ukatembee mahala ambapo mtafurahia mandhari na chakula na vinywaji kishe mrejee nyumbani kulala au wengine kulala hukohuko, ama ualike wageni waje kula na kunywa au ualikwe mahala...

Ndugu, kama hukufanikiwa kusafiri, hukufanikiwa kuwa na gari jipya, hukufanikiwa kuwapa familia yako nguo mpya au mlo maalum (pilau nyama) wa sikukuu basi....

Kaa na familia yako mjadiliane kwa amani na upendo namna gani mnavuka mwaka mpya.

Inapendeza ukiwa na mahitaji yote hayo ila si lazima, ukipata sawa ila ukikosa basi usikumbatue huzuni.

Furahini katika Bwana tena Nasema Furahini....

Kila mwenye furaha ashiriki furaha yake na asiye nayo.

Sina mpangilio mzuri wa nini nataka kusema ila ikiwa huu ujumbe umekulenga. Amka, kaoge, kamshukuru Mungu, andaa kile ulichonacho jikoni basi furahi na nafsi, ndugu jamaa au marafiki walio karibu nawe hata kwa simu tuu.

Wale wanaopitia changamoto za ugonjwa, misiba, kesi mahakamani, polisi, nawaombea mpate ahueni.

Ntatupia picha baadae ya kile nilichobarikiwa nacho.

Kasinde Matata 🙂.
 
Habari ya muda huu popote pale ulipo wana jamvi.

Kama ulipo haijadondoka tarehe 25/12/2023 basi endelea kuvuta subira itafika tuu punde si punde.

Ni sikukuu leo ya kuadhimisha kukumbuka kuzaliwa kwa Kiongozi wa waumini wa dini ya Kikristo.

Heri ya Sikukuu na Maandalizi ya Mwaka Mpya 2024.

Mpendwa, kama hadi muda huu hujajua sikukuu inaendaje usipate msongo wa mawazo. Shukuru kwa uzima na afya uliyonayo, siku itapita na maisha yataendelea.

Imezoeleka sikukuu ni siku ya kula chakula kizuri, uvae nguo mpya, ukatembee mahala ambapo mtafurahia mandhari na chakula na vinywaji kishe mrejee nyumbani kulala au wengine kulala hukohuko, ama ualike wageni waje kula na kunywa au ualikwe mahala...

Ndugu, kama hukufanikiwa kusafiri, hukufanikiwa kuwa na gari jipya, hukufanikiwa kuwapa familia yako nguo mpya au mlo maalum (pilau nyama) wa sikukuu basi....

Kaa na familia yako mjadiliane kwa amani na upendo namna gani mnavuka mwaka mpya.

Inapendeza ukiwa na mahitaji yote hayo ila si lazima, ukipata sawa ila ukikosa basi usikumbatue huzuni.

Furahini katika Bwana tena Nasema Furahini....

Kila mwenye furaha ashiriki furaha yake na asiye nayo.

Sina mpangilio mzuri wa nini nataka kusema ila ikiwa huu ujumbe umekulenga. Amka, kaoge, kamshukuru Mungu, andaa kile ulichonacho jikoni basi furahi na nafsi, ndugu jamaa au marafiki walio karibu nawe hata kwa simu tuu.

Wale wanaopitia changamoto za ugonjwa, misiba, kesi mahakamani, polisi, nawaombea mpate ahueni.

Ntatupia picha baadae ya kile nilichobarikiwa nacho.

Kasinde Matata .
Naomba nialike kwako nije kula

Sent from my SM-J410F using JamiiForums mobile app
 
Nilikuwa nanyi humu tukifurahi maisha lakini huu mwaka ulikuwa mgumu sana kwangu. Sikuwahi kupitia magumu kama haya toka nizaliwe. Namshukuru Mungu kwa yote
Mkuu kama ni ule utani wa kwenye mpira ni mambo ya kawaida. Lakini kinyume na hapo basi,pole sana na Mungu akutie nguvu, maumivu tumeumbiwa wanadamu tuyabebe hadi kifo kitakapo tufika.
 
Nilikuwa nanyi humu tukifurahi maisha lakini huu mwaka ulikuwa mgumu sana kwangu. Sikuwahi kupitia magumu kama haya toka nizaliwe. Namshukuru Mungu kwa yote

Pole na hongera kwa kukabiliana na changamoto ulizokutana nazo.
Endelea kuwa na moyo wa shukrani kwani katika kushukuru baraka humiminika maishani mwetu.

Ikawe heri kwako kwa 2024.
 
Mkuu kama ni ule utani wa kwenye mpira ni mambo ya kawaida. Lakini kinyume na hapo basi,pole sana na Mungu akutie nguvu, maumivu tumeumbiwa wanadamu tuyabebe hadi kifo kitakapo tufika.

Ni jambo jema kuendelea kutiana moyo kwenye safari hii ya maisha.
 
Namshukuru Mungu sana, 2023 umekua ni mwaka mzuri kwangu, kuna vitu vingi vizuri vimetimia🙏 , hongereni kwa wote ambao wishes zenu zimetimia na kama hazijatimia wakati wa Mungu ni wakati sahihi let's keep on praying atajibu kwani sikio lake si zito hata asisikie.

I wish you all a Merry Christmas and happy new year 🙏
 
Mpendwa, kama hadi muda huu hujajua sikukuu inaendaje usipate msongo wa mawazo. Shukuru kwa uzima na afya uliyonayo, siku itapita na maisha yataendelea.

Hapa ndio pa muhimu...

Kasinde ubwabwa twaula wapi leo?
 
Namshukuru Mungu sana, 2023 umekua ni mwaka mzuri kwangu, kuna vitu vingi vizuri vimetimia🙏 , hongereni kwa wote ambao wishes zenu zimetimia na kama hazijatimia wakati wa Mungu ni wakati sahihi let's keep on praying atajibu kwani sikio lake si zito hata asisikie.

I wish you all a Merry Christmas and happy new year 🙏

Asante kwa salamu, na kwako pia.

Ashukuriwe aliye juu kwa kufanikisha mengi kwa upande wako. Ikawe heri na neema tele kwa 2024.

Hongera pia kwa kujawa na moyo wa shukrani.
 
Hapa ndio pa muhimu...

Kasinde ubwabwa twaula wapi leo?

Aahahahhaaa shugaaa mamboo...!

Leo jiko na mwiko havijanitupa best, ubwabwa umefika mezani ukiwa na viwango vya SGR...😋😋😋

Kama kawaida ya sikukuu kipimo huongezwa. Bado pishi lipo, karibu sana Msafiri.

Ila namshukuru Mungu nimeushinda moyo kwa kutupia mbali wazo la kutoka na kuzifata Desperado nizishushie na barafu nyumbani... sema pia nafasi ilijaa ubwabwa hivyo Desperado zikapotezewa kirahisi 😁.
 
Asante kwa salamu, na kwako pia.

Ashukuriwe aliye juu kwa kufanikisha mengi kwa upande wako. Ikawe heri na neema tele kwa 2024.

Hongera pia kwa kujawa na moyo wa shukrani.
Amina ahsante Kasie hivi bado lile jina Kasie mahaba linaendelea kutumika mtumishi?

Kuna kitu natamani kikatimie 2024, Mungu ni mwema🙏
 
Back
Top Bottom