OllaChuga Oc
JF-Expert Member
- Jul 4, 2016
- 21,161
- 24,116
Ile ngoma ya HAUTAKI ni the best song na Hilo halina ubishi. Mziki wa Arusha una impact kubwa Sana kwenye game ya bongo na kimataifa kwa ujumla.Si kamtolea mwanamke, kwani kwenye title ya ngoma kuna neno motra limeandikwa pale?
Kati ya motra na p nani kamfanya mwenzake aonekane zuzu?
Motra angetaka kuendelea kubakia japo na kaheshima kidogo anakopewa na baadhi ya watu asinge jaribu kutoa ngoma yeyote ya diss baada ya diss yake ya WEUPE. Kutoa tena ngoma ya diss kumemuondolea hako kaheshima kadogo alikokuwa anapewa na kale kakundi kalikokuwa kanampa heshima kameanza kumchukulia mwana kama boya
Hakutakiwa kutoa diss Na hata kama angetoa basi angetafuta utulivu na kutuliza akili kuipika ngoma ili iwe kali itakayoonesha ushindani kuliko hichi kituko cha HAUTAKI ambacho kimewaacha watu maswali mengi ya kujiuliza na kupelekea watu kupata mashaka kua kwa ubovu wa hii ngoma basi hata ile diss yake dhidi ya kikosi kazi huwenda hakuandika yeye.
Unaniambia nikasikilize ngoma ya WEUPE na wakati nimeweka hadi lyrics ambazo kawachana member wa kikosi kazi kwenye thread yangu? au katoa ngoma nyingine WEUPE part 2 ndio unani recommend nikaiskilize?
Kwa mfano Kama ingekuwa kweli, rapper kama Basta Rahymes au Evidence, au Rakaa achana na mtu Kama Nas au Rakim..ao wote hawawezi kupiga collabo na rappers wa mipasho Kama Nikk mbishi au songa, labda kidogo wakazi na Nash Mc ..unadhani ni kwanini? Hip-hop yao hao KIKOSI KAZI imekaa kimipasho Sana hawako really kabisa. Wanajikuta next level wakati hata Uganda tu hapo hawajulikani.
Hip-hop ya A Town imevuka boda kitambo mbele uko mziki unapigwa Sana ..nyie wazaramo pigeni mipasho hip-hop ni really.
Kwaya ya Cecilia wanapiga hela tamaduni wao wanatafuta attention..