Moshi: Mzazi ampiga na kumjeruhi mwalimu shuleni kwa kosa la kumuadhibu mwanae

Bushmamy

JF-Expert Member
Aug 18, 2019
8,848
15,253
Hali ya taharuki imetokea katika shule ya msingi Narumu, katika Kijiji cha Narumu wilaya ya Hai mkoani Kilimanjaro, baada ya mama mmoja ajulikanae kwa jina la Valentina Kweka, kuingia ofisi ya walimu na kumpiga Mwalimu.

Mwalimu huyo ambaye ni wa kike (jina limehifadhiwa) alijeruhiwa hivyo kupelekea kutoka damu puani kwa kile kinachodaiwa kuwa ni mwalimu huyo kumchapa mwanafunzi huyo wa darasa la tano fimbo moja kwa kosa la kukataa kudeki darasa.

Mtoto huyo alienda kusema kwa mamake huku akilia ndipo mzazi huyo alipochukua jukumu la kwenda hadi shuleni na kumpiga mwalimu huyo na kumjeruhi.

Aidha mwenyekiti wa kijiji hicho Bwana Ismael Urassa pamoja na diwani wa kata hiyo wamethibisha kutokea kwa tukio hilo na kusema kuwa tukio hilo limefika ofisi ya kata na linashughukiwa.
 
Tatizo mwandishi ameamua kuchagua kuwa upande wa waalimu bila hata kutumia akili, hivi kweli mtoto achapwe fimbo moja halafu mzazi aje kufanya fujo shuleni?

Fanyeni uchunguzi kidogo kabla ya kuleta habari kwenye public.

- Inawezekana mtoto ana matatizo ya afya ndio maana alikataa kudeki, so mwalimu kabla ya kukurupuka kutumia mafimbo angemshirikisha mzazi(siku hizi simu zipo kila mahali).

- Semeni ukweli alimchapa vipi na alitoa maneno gani wakati anamchapa au wakati mzazi alipokuja shuleni.

UCHUNGU WA MWANA AUJUAYE MZAZI.
 
Karma is a bitch.
Huyo mtoto Hana muda mrefu atakua mgeni wa serikali Kama sio kisongo Basi Ni karanga. Huko ndio kwa wenzake wanaoendana naye.
Una uhakika ni kweli alikataa kudeki akachapwa fimbo moja tu? Kabla ya kutoa laana upande mmoja hebu jiridhishe kidogo nini kilitokea.

Nakupa mfano mmoja mdogo, mtoto wa jirani yangu alikuwa mgonjwa wa pumu na alitakiwa asifanye kazi ngumu kwa muda aliokuwa anatumia dozi fulani na taarifa mzazi alipeleka shuleni.

Akaja mwalimu fulani mgeni akaintroduce program ya kukimbia asubuhi kama mazoezi, so kwakuwa yule dogo alikuwa ana kamwili fulani yule mwalimu akajua dogo mzembe tu na akamlazimisha akimbie ili apungue, mzazi alivyoskia vile bado kidogo aje ale kichwa cha yule mwalimu ndio waalimu wengine wakaomba msamaha.

Kumbuka mtoto hawezi kujieleza vizuri ni jukumu la mwalimu kumuelewa haraka kwanini hataki kazi fulani na kuchukua hatua stahiki ila sio kukimbilia kuchapa mtoto kama punda. Rudia tena kutoa comment kistaarabu
 
Una uhakika ni kweli alikataa kudeki akachapwa fimbo moja tu? Kabla ya kutoa laana upande mmoja hebu jiridhishe kidogo nini kilitokea.

Nakupa mfano mmoja mdogo, mtoto wa jirani yangu alikuwa mgonjwa wa pumu na alitakiwa asifanye kazi ngumu kwa muda aliokuwa anatumia dozi fulani na taarifa mzazi alipeleka shuleni.

Akaja mwalimu fulani mgeni akaintroduce program ya kukimbia asubuhi kama mazoezi, so kwakuwa yule dogo alikuwa ana kamwili fulani yule mwalimu akajua dogo mzembe tu na akamlazimisha akimbie ili apungue, mzazi alivyoskia vile bado kidogo aje ale kichwa cha yule mwalimu ndio waalimu wengine wakaomba msamaha.

Kumbuka mtoto hawezi kujieleza vizuri ni jukumu la mwalimu kumuelewa haraka kwanini hataki kazi fulani na kuchukua hatua stahiki ila sio kukimbilia kuchapa mtoto kama punda. Rudia tena kutoa comment kistaarabu
Una point, lkn mzazi naye ana mdomo, angeweza kuongea na walimu sio kuchukua Sheria mkononi.

Unafikiri mtoto atakua anajisikiaje akijua walimu hawatamuadhibu Tena.
Unafikiri Kuna mwalimu hapo shuleni atashughulika na huyo mtoto?
Yuko mzazi mmoja Dar alikwenda shuleni kwa lengo la kumpiga mwalimu lkn walimu wanamtetea mwenzao na kumuambia huyo mzazi, kuanzia leo hatuta shughulika na huyo mtoto wako hata akiumwa hakuna atakaye kupigia simu.
Mzazi alidhani Ni utani.
 
Mwalimu mbona unamkingia sana kifuabmwalimu mwenzio? Yani kamchapa fimbo? Kweli mwalimu huu ndio ukweli?

Hata hivyo acha wazazi tulinde watoto wetu maana tunaona namna mnawashambulia wanetu huku mkiwarekodi na kutuonyesha mtandaoni.

Popote ulipo mzazi mlinde mwanao kwa gharama yoyote walimu wa leo vijanavijana hawa sio watu sahihi kwa usalama wa watoto wetu mambo yamebadilika sana.
 
Siku moja nilitoa kichapo kwa mwanafunzi mmoja wa kike wa darasa la kike baada ya kukataa kunipikia chai asubuhi. Baada ya kumchapa viboko kadhaa kwa ubishi wake alikimbia nyumbani kwao kumleta baba yake.

Mzazi alikuja amefura hasira mpaka nyumbani kwa walimu eneo la shule akakosa mwalimu yupi amshambulie kwa kuwa walimu tulichanganyikana huku wengine wakiwa ni watu wazima na wenye miili mikubwa iliyojazia. Mzazi alirudi nyumbani kwake huku akitoa ole wake huyo mwalimu aliyemchapa mtoto wake angepigana naye. Tangu siku hiyo niliona isiwe taabu kuwatumia wanafunzi kwenye shughuli zangu binafsi.

Kuna mkuu mmoja wa shule ni wa kike alikuwa ni mbabe, mzazi akijitia kiherehere kwenda shuleni kuleta fujo alikuwa anamkwida na kumzabatua makofi na ngumi huku akimuambia anampeleka polisi. Wazazi wengine shuleni hawaji ila watatengeneza manuever kumkomoa mwalimu aliyechapa watoto wao. Mwalimu anaweza kujikuta katundikwa juu ya mti kalala huko usiku wote kimazingara. Wengine hufanyiwa vitendo vya kishirikina usiku
 
Visa vya wazazi kuvamia shule ni vingi. Kuna mwanafunzi mmoja alichapwa na mkuu wa shule, akakimbia kwenda kwao, akaja na mzazi wake huku wameshika mapanga. Mwalimu alijificha ofisini kwake hawakumuona. Mwingine naye aliingiliwa usiku na mchawi, kumbe naye yuko fiti kwenye ulimwengu huo wa kichawi alimuadhibu mchawi hukohuko uchawini nusura amgandishe mchawi uchi mpaka asubuhi wakamalizana yaishe isiwe aibu. Walimu wengine wa kike wao walichoshwa kupelekewa moto usiku na vibabu hasa. Vibabu ni vikongwe vikawa vinajilia tani yao hao walimu ikabidi waikimbie hiyo shule. Mi niliambiwa mti wa shule huwaka moto usiku na ngoma huchezwa hapo mbele ya majengo ya shule niliogopa sana maana niliishi nyumba ya shule peke yangu usiku nisivamiwe na washirikina baada ya kuwachapa watoto wao, ila sikuwahi kuona ushirikina shuleni hapo zaidi ya kusifiwa na majirani kuwa nina ulinzi wa mkubwa hakuna mshirikina anaweza kuja eneo nilipo akafanya atakavyo. Sio walimu tu hata watumishi wengine kijijini hukutana na mikasa hiyo
 
Huko si ndio inasemekana elimu iliwahi kuingia, wanajitambua. Wazee wa shule kila kijiji .Hii nchi kutoka Maghabiri mpaka Mashariki, Kusini mpaka Kaskazini ni walewale tu waliokunywa uji wa mgonjwa. Vurugu tupu.
 
Back
Top Bottom