jmushi1
Platinum Member
- Nov 2, 2007
- 24,989
- 22,521
Waungwana na hasa Mushi,
Mbona mnakuwa wasahaulifu namna hii? Je mmesahau kuwa tuhuma hizi kuwa hawa jamaa walitoa Rushwa zilipandwa na Vigogo wa CCM ili Mollel na Laizer wapakwe madoa na kuondolewa Kugombea viti vya NEC CCM?
Je mmesahau kuwa Mollel na Laizer wanajulikana ni maadui wa Lowassa na ilikuwa kampeni marudufu karibu kukigawa CCM mkoani Arusha ili kuhakikisha watu wa Lowassa wanaingia NEC?
Je mmesahau baada ya tuhuma za Ufisadi zilizosababisha Kikwete kuvunja Baraza la Mawaziri kutokana na Lowassa kujiuzulu kwa tuhuma za Richmond, zilisababisha kikao cha NEC na CC Butiama kiwe mshike mhike baada ya baadhi ya Wajumbe kuhoji iweje Watuhumiwa wa Ufisadi Lowassa, Chenge, Karamagi, Mramba, Msabaha na Rostam waendelee kuwa wajumbe wa NEC na CC huku wanatuhuma za kuhujumu Taifa na kwa nini hawavuliwi huo ujumbe na kuwekewa pingamizi kama Mollel na Laizer walivyofanyiwa?
Ukweli ni kuwa Kesi hii ilikuwa ya Haramu, TAKUKURU walitumiwa na CCM kupaka matope kina Mollel, Laizer na wenzao ili Uchaguzi wa CCM Arusha ufanyike kwa matakwa ya Lowassa na wenzake.
Wakulaumiwa si Mahakama, ni TAKUKURU kwa kukimbilia kushitaki kina Mollel na Laizer kwa jambo la uzushi na ushahidi wa kuzusha huku wanawaachia kina Chenge wanapeta!
Hii ni aibu kubwa kwa CCM na kama jinsi tunavyoshupalia Wangwe afukuzwe, basi sasa mpira uwageukie CCM.
Hili ni doa na tuwapake matope na mavi ya farasi, ng'ombe na nguruwe CCM iendelee kunuka Rushwa!
Kwa nini CCM iliogopa kuwaufukuza Ujumbe wa NEC na CC Lowassa, Chenge, Msabaha, Karamagi, Mramba na Rostam huku wakiwa na tuhuma? Je CCM kinaliambia nini Taifa ikiwa kinafanya mambo kwa Upendeleo na kugawanya wanachama?
Jee CCM ni mali ya Lowassa, Chenge, Msabaha, Karamagi na Rostam au ni mali ya wanachama Wakulima na Wafanyakazi wa Tanzania?
Kila kitu kiwekwe wazi...Kuwa UAMUZI WA KWANZA ULIKUWA TAKUKURU, NA PIA UAMUZI WA PILI NI WAO TAKUKURU!
SASA HIZO ASSUMPTIONS ZA KINA LOWASSA ZITAWEKWA WAZI HAPO HAO TAKUKURU WATAKAPOJIELEZA KUWA NI KIVIPI WAGANYIKE KWENYE ISSUE NYETI KAMA HIYO KAMA KWELI WOTE NIA YAO NI MOJA!
NA HAPO TUNARUDI KWENYE FACT KUWA TAKUKURU IS NOT RELIABLE NA MAAMUZI YAO YACHUNGUZWE NA WAITWE BUNGENI KUHOJIWA NA SI KUWAACHIA WAENDELEE KUTOWA KAULI NA MMAMUZI YA KISIASA!