Mohamed Dewji (MO) aliyepotea, apatikana. Amerudi nyumbani akiwa salama

Wanabodi,
Hii ni thread ya swali, nikipendekeza kwa kuuliza, maana siku hizi, ukiuliza kitu,, watu hawaonagi alama za kuuliza, wakadhani nimetoa statement.

Baada ya Mo kupatikana, baada ya juhudi kubwa sana za jeshi letu la polisi, baada ya ile ahadi ya motivation iliyopelekea hadi IGP kufanya press conference ya jana, hii imethibitisha kuwa kumbe Jeshi letu la polisi, linaweza, wala hatuhitaji wachunguzi wa nje. Jeshi letu la polisi sasa ndio linauwezo, au kama lilikuwa nao siku zote, then, likiamua, linaweza, ukijumlisha na ile ahadi ya motivation ya familia, bali limeweza kwa sababu, sasa ndio limeonyesha uwezo huo kwa kufanikisha Mo kupatikana akiwa mzima, salama uu salmini na bukheri wa Afya.

Sasa kwa vile familia tayari iliishatenga shilingi billion moja kwa atayefanikisha kupatikana kwa Mo, na waliofanikisha ni IGP Kamanda Sirro, na vijana wake, kwa ile Press Conference muhimu ya jana. Mimi Napendekeza hizo pesa apewe Kamanda Sirro na vijana wake, ili zitumike kuboresha jeshi letu la polisi nchini kwa kulijengea uwezo kuzuia matukio ya utekaji, kwa kuwa motivate, siku zote, mtu yoyote akitekwa au kushambuliwa na wasiojulikana, juhudi kama hizi za kumsaka MO, ikiwemo kuitisha press conference, zifanyike. Tena laiti kama tungelijua kabla namna ya kuwa motivate polisi wetu watimize wajibu wao, usikute hata Ben Saanane alipotoweka, tungejichanga tukatangaza dau, angepatikana,
Aliposhambuliwa Lissu, tungejichanga tukatangaza dau, wasiojulikana wale, wangepatikana, na alipopotea Azori Gwanda, sisi media tungejichanga tukatangaza dau, angepatikana, huwezi jua!, Bilioni moja jameni sii mchezo!.

Zamani tulizoea ahadi za motivation ni kwenye kutafutia kura tuu, lakini sasa, hata katika kutimiza wajibu!, tena naombeni msinielewe vibaya kwa hii hoja ya motivation, kwa the difference between Mo, Ben Saanane na Azori Gwanda ni status tuu, Mo ana motivational status iliyopelekea kuhangaikiwa kulikopelekea kupatikana.

Mungu Mkubwa, Pesa ndio kila kitu!, Mkono Mtupu Haulambwi!. Masikini Ben Saanane, masikini Azori Gwanda
Jumamosi Njema
P.
Mkuu cheki pm yangu
 
Hakuna taasisi yoyote ile point ya msingi mchango wa Raisi ulikua ni upi wakati hajatoa pole wala neno lolote lile la faraja au hata kuamrisha watu wake wampate haraka iwezekanavyo
kuna watu lukuki nyuma ya rais, walifanya kwa niaba yake, narudia "RAIS NI TAASISI":cool::cool::cool::cool:
 
Kwa wale tuliosoma st. Kayumba tunawafahamu wale walimu waliokuwa na tabia ya kuudhi ati akimaliza kukuchapa anakwambia sema ASANTE, na we kishingo upande unasema Asante mwalimu, Teh!
 
Kwahiyo ulitaka gari likamatwe na namba hizo hizo.

Akili za bavicha mnazijua wenyewe.

Kazi nzuri Jeshi la polisi.
mbona hili halina mahali pa kufunga spare tyre? Akili fupi zinawaponza! tazama walipozungushia
 
lema4.jpg


Imani kwa vyombo vya usalama inajengwa na haki .Ushujaa sio kutoa amri bali ni uwezo wa kubeba kweli,haki na uadilifu ktk wajibu.Suala la Mo kutekwa mpaka kupatikana limejaa wasiwasi.Kama MB nitaongea na niko tiyari kulipa gharama kwani mambo haya yakiendelea ni hatari kwa Nchi.

 
Imani kwa vyombo vya usalama inajengwa na haki .Ushujaa sio kutoa amri bali ni uwezo wa kubeba kweli,haki na uadilifu ktk wajibu.Suala la Mo kutekwa mpaka kupatikana limejaa wasiwasi.Kama MB nitaongea na niko tiyari kulipa gharama kwani mambo haya yakiendelea ni hatari kwa Nchi.
lini
 
Asante sana kwa taarifa. Ni haki yake kutoa maoni kama ambavyo wengine tunaendelea kutoa maoni. Hizo gharama anazoongelea ni zipi? Au ana mpango wa kuvuka mipaka?

Halafu mkuu jitahidi kuweka title fupi zenye mvuto. Hizi ndefu sana sio poa. Au unaonaje?
 
Lini?? Ongea sasa
Watakimbilia kukupeleka mahakamani hapo ndipo mtakapowanasa mabedhuli hawa
Ongea tu Lema hawa wanawanyamazisha ionekane sirikali haihusikii
Huu mchezo wao ufikie mwisho
Kama mmbwai na iwe mmbwai
 
Lema unajipendekeza tu wala hamna atakayekusikiliza.

Tokea useme ni heshima kwa Mungu kumzomea fisadi Lowasa alafu baadae wewe mwenyewe tena ukawa mbeba viatu wa Lowasa tulishakupuuza
 
Mnajua ukiweka siasa kila mahali kuna mambo ambayo unaweza usiyaone kwa macho hata yakwa mbele yako;

Kama Mo anagetekwa kisiasa tujue tu kwamba asingerudishwa.Never.
Mo ametekwa kibiashara na waliopanga ni mahasimu wake wa kibaishara kutoka nje ya Tanzania

Sitaki kuweka facts zote hapa kwa sababu bado nafuatilia baadhi ya taarifa ila kwa sasa kama na wewe ni mchinguzi jaribu kufuatilia maamuzi ya kisera yaliyofanyika siku za karibuni na serikali katika kulinda bidhaa za ndani na aina ya bidhaa ambazo MO amenza kuzitengeneza ikiwema bidhaa ambazo market share ilikuwa chini ya wageni kwa muda mrefu na wageni hawa wanajua kuwa hawatweza kushindana na MO kisha uniambie kama sio uhasimu wa kibiashara.

Lengo lao ilikuwa ni kumtisha tu na kumchomoa pesa ila walipoona na siasa zimeingia ndani na limekuwa tukio la kiulimwengu wamesita hasa baada ya kugundua kuwa hata wakimuua MO bado hawataweza kuzuia upepo wa vita unaowajia katika medani za ushindani wa kibiashara.

SO tuache kuweka siasa tujue tu kwamba this was all business nothing personal and nothing political
 
Kila mtu ni nabii wa Maisha yake kajitabiria kulipa gharama ajiandae kulipa gharama unabii wake utatimia pasipo Shaka yoyote hundred percent
 
Back
Top Bottom