Rev. Kishoka
JF-Expert Member
- Mar 7, 2006
- 4,526
- 1,530
Ni lini tutaamka tukiwa na hasira za kweli na kufanya kweli?
Leo hii tunapingana na kubishana kuhusu Rostam, Lowassa, Lukaza, Chenge, Karamagi, Jeetu na wengine wengi ambao wamehujumu nchi yetu. Lakini mkondo wa haki na sheria ni butu, vyombo vya dola vinaogopa wahujumu hawa maarufu kama mafisadi, wanasiasa na wakubwa wa mashirika wanashirikiana na hawa mafisadi kuhujumu nchi na hakuna anayediriki kuona soni na kuwajibika au kukaripia uhujumu na ufisadi.
Sasa kama tuliowapa dhamana ya kutulinda na kutoa haki wanashindwa kazi zao na kila tukichagua watu wapya, tunakuta mizizi iliyokomaa ya hujuma na ufisadi imetambaa kama gonjwa la Ukimwi au Satarani, basi kwa nini tusichukue hatua mikononi?
Leo mwizi wa kuku, redio au tairi la gari hupewa mkong'oto mkali na huswekwa jela akibahatika kufika huko akiwa hai, lakini wanaotuhujumu kwa mabilioni, ndio kwanza wanakaribishwa kukata tepe, wanapokelewa kwa maandamano na bado wanaendelea kupelelezwa kisa eti ushahidi hautoshi au wapepelezi na waendesha mashitaka wanasubiri ridhaa ya Rais kufungua mashitaka?
Nasema bila woga, pamoja na kuwa ni kinyume cha haiba yangu, wakati umefika, tujichukulie hatua mikononi, tuanze kuwapiga mawe na kuwachapa kila aliyeshindwa kazi na kutuingiza katika umasikini kwa kutuhujumu.
Sijali awe Rostam, Mkapa, Chenge, Karamagi, Lowassa, Lukaza, Vithlani, Patel au Mattaka, kama kuna kiongozi au mtendaji ambaye ametuingizia hasara ambayo ni kutokana na uhujumu, sherti tumchape viboko akiwa ma ta ko wazi hadharani, kisha tumtembeze nchi nzima akiwa uchi kama tunakimbiza Mwenge au wale vikojozi mtaani azomewe, achapwe mijeledi na hata tumpige mawe.
Labda hapo tutakapoamka na kujichukulia sheria mkononi, Wanasiasa wetu watakuwa na adabu na kujifunza kuchapa kazi na kuwa waadilifu na wanyenyekevu!
Leo hii tunapingana na kubishana kuhusu Rostam, Lowassa, Lukaza, Chenge, Karamagi, Jeetu na wengine wengi ambao wamehujumu nchi yetu. Lakini mkondo wa haki na sheria ni butu, vyombo vya dola vinaogopa wahujumu hawa maarufu kama mafisadi, wanasiasa na wakubwa wa mashirika wanashirikiana na hawa mafisadi kuhujumu nchi na hakuna anayediriki kuona soni na kuwajibika au kukaripia uhujumu na ufisadi.
Sasa kama tuliowapa dhamana ya kutulinda na kutoa haki wanashindwa kazi zao na kila tukichagua watu wapya, tunakuta mizizi iliyokomaa ya hujuma na ufisadi imetambaa kama gonjwa la Ukimwi au Satarani, basi kwa nini tusichukue hatua mikononi?
Leo mwizi wa kuku, redio au tairi la gari hupewa mkong'oto mkali na huswekwa jela akibahatika kufika huko akiwa hai, lakini wanaotuhujumu kwa mabilioni, ndio kwanza wanakaribishwa kukata tepe, wanapokelewa kwa maandamano na bado wanaendelea kupelelezwa kisa eti ushahidi hautoshi au wapepelezi na waendesha mashitaka wanasubiri ridhaa ya Rais kufungua mashitaka?
Nasema bila woga, pamoja na kuwa ni kinyume cha haiba yangu, wakati umefika, tujichukulie hatua mikononi, tuanze kuwapiga mawe na kuwachapa kila aliyeshindwa kazi na kutuingiza katika umasikini kwa kutuhujumu.
Sijali awe Rostam, Mkapa, Chenge, Karamagi, Lowassa, Lukaza, Vithlani, Patel au Mattaka, kama kuna kiongozi au mtendaji ambaye ametuingizia hasara ambayo ni kutokana na uhujumu, sherti tumchape viboko akiwa ma ta ko wazi hadharani, kisha tumtembeze nchi nzima akiwa uchi kama tunakimbiza Mwenge au wale vikojozi mtaani azomewe, achapwe mijeledi na hata tumpige mawe.
Labda hapo tutakapoamka na kujichukulia sheria mkononi, Wanasiasa wetu watakuwa na adabu na kujifunza kuchapa kazi na kuwa waadilifu na wanyenyekevu!