Mnaobeza maamuzi ya TFF nikumbusheni ni lini CAF, CAS au FIFA zilitengua maamuzi/hukumu za TFF?

Shujaa Mwendazake

JF-Expert Member
Jul 11, 2015
3,734
6,292
Kuna mzee mmoja ni Jaji mstaafu kwa sasa, alishawahi kutuambia kuwa ukienda Mahakamani basi mlalamikaji na mlalamikiwa wote wanona wana haki. Hata kesi za jinai ukisikiliza upande wa mtuhumiwa ni ama anaonewa au ama anaalalamika kosa limekuzwa.

Nirejee hapa, sualal la Fei kihuruma linatazama upande mmoja tu wa mchezaji lakini watu hawajui kuwa kwa klabu mchezaji ni bidhaa. Yes, ni bidhaa na klabu imeingiza gharama kubwa sana kumlea na kumpandisha thamani huku ikimtimizia matakwa yake ya kimkataba ikiwemo kumlipa mshahara na posho.

Sijasikia kama Fei ana malimbikizo ya mishahara yake kuwa hajalipwa. Hivyo watu wapo tayari Fei apewe anachokitaka na kufinya haki ya klabu iliyompandisha thamaniambayo imemlipa kama walivyokubaliana.

Hoja ni kuwa kulinda kipaji cha mchezaji. Lakini hatuangalii kuwa klabu ilikuwa na mipango na mchezaji na wakati wa usajili hawakumuuza. Sasa kuondoka ghafla bila mipango au kuipa klabu muda wa kufanya replacement ambao si haraka hivyo si jambo litakaloiumiza Klabu?

Sasa TFF yenyewe imekaa kati kwenye Mzani ikiangalia maslahi ya mchezaji lakini pia ikilinda maslahi ya mwanachama wake (Klabu) pia yasidhulumiwe. TFF pia inafahamu uhuni wa Feisal ukipelekwa kisiasa na akaachiwa huru kama anavyotaka, je, madhara yake nini huko baadaye?

Kuna wanaoibeza TFF katika hili na kuamini hawajui kitu hasa watu wakiandika vitu kibao kuonesha kuwa TFF wamekosea. Jana pia baada ya Review bado watu wamekazana kuwa wamekosea na ikisisistizwa Fei aende CAS, bila kujua kuwa TFF wana semina nyingi wana uzoefu mwingi na wana wanasheria pia nguli kwenye maswala haya ya mpira. Fei na genge lake wanaujua ukweli kwa mbali kuliko sisi wapambe.

Taswira iliyopo ni kuwa TFF wamefanya hovyo au wanafanyaga hovyo na hawaaminiki katika hizi hukumu. Nachofahamu mimi labda wengine mnisaidie ni kuwa sijawahi kusikia hukumu ya TFF imewahi kubatilishwa CAS, CAF au FIFA kwa kiwango cha kusema kuwa jamaa siyo wakweli katika hukumu zao zaidi zaidi ni kelele za 'watuhumiwa' hasa Simba na Yanga ambao ili iitwe haki imetolewa ni lazima matakwa yao yashinde.

Kabla ya kumshauri Feisal aende CAS na kulipa hizo Dollar kadhaa, mwenye kumbukumbu ya kuonesha kuwa TFF wanahukumu kiubabaishaji waniletee memory lane ya maamuzi yao mawili kubatilishwa Kimataifa ili na mimi nianze kuwatilia mashaka.
 
Kuna mzee mmoja ni Jaji mstaafu kwa sasa, alishawahi kutuambia kuwa ukienda Mahakamani basi mlalamikaji na mlalamikiwa wote wanona wana haki. Hata kesi za jinai ukisikiliza upande wa mtuhumiwa ni ama anaonewa au ama anaalalamika kosa limekuzwa.

Nirejee hapa, sualal la Fei kihuruma linatazama upande mmoja tu wa mchezaji lakini watu hawajui kuwa kwa klabu mchezaji ni bidhaa. Yes, ni bidhaa na klabu imeingiza gharama kubwa sana kumlea na kumpandisha thamani huku ikimtimizia matakwa yake ya kimkataba ikiwemo kumlipa mshahara na posho.

Sijasikia kama Fei ana malimbikizo ya mishahara yake kuwa hajalipwa. Hivyo watu wapo tayari Fei apewe anachokitaka na kufinya haki ya klabu iliyompandisha thamaniambayo imemlipa kama walivyokubaliana.

Hoja ni kuwa kulinda kipaji cha mchezaji. Lakini hatuangalii kuwa klabu ilikuwa na mipango na mchezaji na wakati wa usajili hawakumuuza. Sasa kuondoka ghafla bila mipango au kuipa klabu muda wa kufanya replacement ambao si haraka hivyo si jambo litakaloiumiza Klabu?

Sasa TFF yenyewe imekaa kati kwenye Mzani ikiangalia maslahi ya mchezaji lakini pia ikilinda maslahi ya mwanachama wake (Klabu) pia yasidhulumiwe. TFF pia inafahamu uhuni wa Feisal ukipelekwa kisiasa na akaachiwa huru kama anavyotaka, je, madhara yake nini huko baadaye?

Kuna wanaoibeza TFF katika hili na kuamini hawajui kitu hasa watu wakiandika vitu kibao kuonesha kuwa TFF wamekosea. Jana pia baada ya Review bado watu wamekazana kuwa wamekosea na ikisisistizwa Fei aende CAS, bila kujua kuwa TFF wana semina nyingi wana uzoefu mwingi na wana wanasheria pia nguli kwenye maswala haya ya mpira. Fei na genge lake wanaujua ukweli kwa mbali kuliko sisi wapambe.

Taswira iliyopo ni kuwa TFF wamefanya hovyo au wanafanyaga hovyo na hawaaminiki katika hizi hukumu. Nachofahamu mimi labda wengine mnisaidie ni kuwa sijawahi kusikia hukumu ya TFF imewahi kubatilishwa CAS, CAF au FIFA kwa kiwango cha kusema kuwa jamaa siyo wakweli katika hukumu zao zaidi zaidi ni kelele za 'watuhumiwa' hasa Simba na Yanga ambao ili iitwe haki imetolewa ni lazima matakwa yao yashinde.

Kabla ya kumshauri Feisal aende CAS na kulipa hizo Dollar kadhaa, mwenye kumbukumbu ya kuonesha kuwa TFF wanahukumu kiubabaishaji waniletee memory lane ya maamuzi yao mawili kubatilishwa Kimataifa ili na mimi nianze kuwatilia mashaka.

Mkuu wa Bongo si unajua ujuaji mwingi kumbe hamna mtu ajualo ni ile kutaka kuonekana ktk wapiga zumari na wewe umo…

Mwenyewe Toto ya zenj akikaa pekee yake moyoni anajutia alivyo laghaiwa
 
Mkuu wa Bongo si unajua ujuaji mwingi kumbe hamna mtu ajualo ni ile kutaka kuonekana ktk wapiga zumari na wewe umo…

Mwenyewe Toto ya zenj akikaa pekee yake moyoni anajutia alivyo laghaiwa
Tunawaita Bush Lawyers..

Ambao hata Maktaba full wa Fei na Yanga hawajausoma.

Watataka utolewe hadharani, Je kesi ina PUBLIC INTEREST mpaka nyaraka zote zitolewe hadharani?
 
Kama wakienda CAS Fei akishinda TFF na kamati yake itadharauriwa sana na kuonekana wa hovyo kitu ambacho TFF hatoruhusu kamwe kitokea atapambana kwa njia zote ilu kulinda heshima yao.
 
Wewe ni mjinga kweli.

Hasa unaposema TFF imekaa kati, kwa kulinda maslahi ya mchezaji na.mwanachama wake [klabu] yasidhulumiwe.

Hapo ndio umekiri TFF inaingiliwa na wanasiasa kudhulumu haki za mchezaji, hakuna popote penye haki mbili kwenye shauri moja, ulichoandika hapo ni ujinga wa PhD.
 
Kama wakienda CAS Fei akishinda TFF na kamati yake itadharauriwa sana na kuonekana wa hovyo kitu ambacho TFF hatoruhusu kamwe kitokea atapambana kwa njia zote ilu kulinda heshima yao.
Utopolo mmeanza kutetemeka

Naona kilichobaki sasa ni kujipa moyo tu.
 
Wewe ni mjinga kweli.

Hasa unaposema TFF imekaa kati, kwa kulinda maslahi ya mchezaji na.mwanachama wake [klabu] yasidhulumiwe.

Hapo ndio umekiri TFF inaingiliwa na wanasiasa kudhulumu haki za mchezaji, hakuna popote penye haki mbili kwenye shauri moja, ulichoandika hapo ni ujinga wa PhD.
NIKUELEWESHE AU , MAANA HUJANIELEWA
 
Wewe ni mjinga kweli.

Hasa unaposema TFF imekaa kati, kwa kulinda maslahi ya mchezaji na.mwanachama wake [klabu] yasidhulumiwe.

Hapo ndio umekiri TFF inaingiliwa na wanasiasa kudhulumu haki za mchezaji, hakuna popote penye haki mbili kwenye shauri moja, ulichoandika hapo ni ujinga wa PhD.

Jamaa una akili za kisenqe Sana... Kwahiyo unaona haki pekee nikushinda kesi kwa asiyestahili kushinda?. Ujuaji wakipuuzi hebu tuelezee huyu fei ni bora kuliko mane mwenye management iliyokamilika, hujui Kama mane ameomba maboresho ya mkataba/maslahi zaidi ya mwaka na liver hawakumpa!!, Uliona anataka kuvunja mkataba kijinga hivyo?,uliona anagomea timu?. Unajua sakata ka Theo na Asernal?. Jifunzeni kuheshimu taratibu sio kukomaza mishipa ya miqundu alooh!!.
 
Naomba mrejee ushauri wa mzee Aden Rage alisema pale panatakiwa itumike busara tu kuliko huko wanakodhan CAS watapata haki, kisheria Fei toto and makosa kimkataba kwasababu amevunja mkataba kihuni kwani mwajiri wake wa zaman hakuwa amekosea chochote kwenye mkataba wao baina ya yanga na Feisal. Akienda CAS atafeli . Hayo ni maneno ya mwanasheria na mwenyekiti wa zaman wa TFF na mshabiki nguli wa Simba.

Kitu cha msingi atafutwe aliyeko nyuma ya feisali ni nani na ambaye anajifanya kumdanganya huyu feisali na kuharibia kipaji chake. Yanga wanataka wapate faida kutoka kwa feisali na Feisali anataka apate faida ya kipaji chake. Wakae mezan wamalizane
 
Naomba mrejee ushauri wa mzee Aden Rage alisema pale panatakiwa itumike busara tu kuliko huko wanakodhan CAS watapata haki, kisheria Fei toto and makosa kimkataba kwasababu amevunja mkataba kihuni kwani mwajiri wake wa zaman hakuwa amekosea chochote kwenye mkataba wao baina ya yanga na Feisal. Akienda CAS atafeli . Hayo ni maneno ya mwanasheria na mwenyekiti wa zaman wa TFF na mshabiki nguli wa Simba.
Na aliwahi kuwa Mwenyekiti wa klabu yao na ndie muasisi wa kuwaita wanachama wa klabu ile ma "MBUMBUMBU".
 
Wewe ni mjinga kweli.

Hasa unaposema TFF imekaa kati, kwa kulinda maslahi ya mchezaji na.mwanachama wake [klabu] yasidhulumiwe.

Hapo ndio umekiri TFF inaingiliwa na wanasiasa kudhulumu haki za mchezaji, hakuna popote penye haki mbili kwenye shauri moja, ulichoandika hapo ni ujinga wa PhD.
No. 4
 
Utopolo mmeanza kutetemeka

Naona kilichobaki sasa ni kujipa moyo tu.
Huo ndio uhalisia Tff hatokubali kudhalilika kizembe ,hata Dundukaz kuna kipindi walitaka kushindana na Tff kubatilisha ubingwa wa Yanga kwa kuahidi kushitaki Fifa je walifika wapi ?
 
Back
Top Bottom