-Viongozi waandamizi wa CCM wameongea sana na kumchafua Lowassa kwamba ni fisadi bila kutoa uthibitisho popote pale kwa muda mrefu. Tena kuna wengine ambao wana madoa zaidi ya chui lakini sasa hivi wanajiona wasafi zaidi ya theluji kwa sababu tu wanaficha maovu yao kwa jina la Lowassa
-Lowassa hayuko serikalini kwa miaka mingi na pia hayuko CCM lakini kinachoshangaza ni kwamba jina lake bado linatumika vibaya kwa ajili ya kuficha ukweli.
-Nawaombeni ndugu watanzania tujiulize kwamba hili suala la “ Hewa hewa” kila idara ni dili ya nani ndani ya CCM na serikalini. Tunaambiwa kuna wafanyakazi, wanafunzi, bajeti nk hewa, Je nani aliyekuwa anasimamia ufisadi huu wa kutengeneza taarifa zisizo sahihi serikalini tangia uhuru hadi sasa?
-Naomba nijue wanafunzi na wafanyakazi hewa walitoka wapi? Nina amini huu ni mchezo uliofanywa na mafisadi wa CCM na hao watu wapo na yawezekana wanajulikana lakini hawasemwi kwasababu ndio wale wenye maneno mengi na matusi ndani ya CCM.
#Huu ufisadi wa HEWA HEWA kila idara ni wa nani?
-Lowassa hayuko serikalini kwa miaka mingi na pia hayuko CCM lakini kinachoshangaza ni kwamba jina lake bado linatumika vibaya kwa ajili ya kuficha ukweli.
-Nawaombeni ndugu watanzania tujiulize kwamba hili suala la “ Hewa hewa” kila idara ni dili ya nani ndani ya CCM na serikalini. Tunaambiwa kuna wafanyakazi, wanafunzi, bajeti nk hewa, Je nani aliyekuwa anasimamia ufisadi huu wa kutengeneza taarifa zisizo sahihi serikalini tangia uhuru hadi sasa?
-Naomba nijue wanafunzi na wafanyakazi hewa walitoka wapi? Nina amini huu ni mchezo uliofanywa na mafisadi wa CCM na hao watu wapo na yawezekana wanajulikana lakini hawasemwi kwasababu ndio wale wenye maneno mengi na matusi ndani ya CCM.
#Huu ufisadi wa HEWA HEWA kila idara ni wa nani?