Mnada wa samaki waliokamatwa kwa wavuvi haramu wadoda

Pdidy

JF-Expert Member
Nov 22, 2007
50,956
22,150
Mnada wa samaki waliokamatwa kwa wavuvi haramu wadoda
broken-heart.jpg
Peter Edson na Aika Mushi

KAMPUNI ya udalali ya Yono Auction Mart jana ilishindwa kuanza kazi yake ya kuuza tani 70 za samaki waliovuliwa eneo la Tanzania ndani ya Bahari ya Hindi kutokana utofauti mkubwa wa bei.

Hatua hiyo iliilazimu kampuni hiyo kuahirisha mnada huo wa wazi baada ya wafanyabiashara wengi waliofika katika mnada huo kutaka kununua samaki kwa bei ya Sh1,500 hadi 2,000 kwa kilo chini ya iliyopangwa na serikali ya Sh 7,000.

Katika vuta nikuvute huku idadi ya wachuuzi ikiwa kubwa kuliko ya wafanyabiasha wakubwa wa samaki, uongozi wa Yono uliamua kuitisha kikao cha dharula ambacho hadi mchana kilikuwa kikiendelea kutafuta ufumbuzi baina yake na wafanyabaishara wanaotaka kununua samaki hao kwa bei ya chini.

Akizungumza jana katika eneo la tukio Afisa wa Serikalini, Geofrey Nanyaro alisema suala la kuuza samaki hao kwa bei ya jumla litashindikana kwa kuwa mnunuzi atashindwa kupata kibali cha kuwauza samaki hao katika soko la nje.

“Samaki hawa ni wazuri na wenye uzito mkubwa, tunaweza kuwauza kwa wafanyabaishara hawa wanaotaka kununua kwa wingi lakini wao wanataka kwa ajili ya kuwasafirisha nje, jambo ambalo ni vigumu kufanyika, kwani hawatapata vibali,” alisema Nanyaro.

Naye Mkurugenzi wa kampuni ya Royal Africa, Rabstar Muhamed Alhabase alisema pamoja na kuwa na nia ya kununua samaki wote, ameshindwa kuafikiana na kampuni ya Yono kutokana na tatizo la upatikanaji wa kibali cha kusafirisha nje ya nchi.

“Mimi naweza kuwachukua samaki hawa, lakini tatizo liko serikalini, hawana vibali vya kuruhusu samaki hao kuuzwa nje ya nchi,” alisema Alhabase.

Naye mfanyabishara maarufu wa samaki jijini Ahmed Kombe alisema kuwa yeye alikwua anahitaji samaki wa Sh9 milioni, lakini ilishikana kufikia muafaka kutokana na bei aliyokuwa anataka auziwe.

“Hawa jamaa wanauza kilo moja kwa Sh7,000 mimi nataka tani moja kwa Sh400,000 jambo ambalo limeshindikana kupatiwa ufumbuzi,” alisema Kombe.

Hata hivyo, Mkurugenzi wa Yono, Scholastica Kavela, alisema kuwa samki hao wanauzwa kulingana bei ambayo serikali inadhani kuwa haitaweza kuleta hasara wala faida kubwa.

Alisema kufuatia hali hiyo hawataendelea na mnada huo hadi watakapojadiliana na serikali kuhusina na hali hiyo. Hivi karibuni Waziri wa Maendeleo ya Mifugo na Uvuvi, John Magufuli alifanikiwa kudhibiti maliasili za baharini baada ya kunasa meli iliyokuwa imebeba tani 70 za samaki waliovuliwa eneo la Tanzania ndani ya Bahari ya Hindi.
 
wanafikiri bei ya sh. 7000 watanunuwa watanzania kwa vile wote wanakipato kinachofanana wabunge. Hivi hawajui hali halisi ya maisha ya watanzania. Wanafikiri hao samaki wanauzwa kwenye soko la ulaya au Marekani?. Wafanyabiashara wakinunua sh. 7000 kwa kilo wao wakauze kwa sh. ngapi na kwa nani (may be wakawauzie waheshimiwa wabunge. Kama ndio njia ya kurudisha gharama za kuwahifadhi hao samaki, naona hiyo gia imekwama jaribuni nyingine.
 
wanafikiri bei ya sh. 7000 watanunuwa watanzania kwa vile wote wanakipato kinachofanana wabunge. Hivi hawajui hali halisi ya maisha ya watanzania. Wanafikiri hao samaki wanauzwa kwenye soko la ulaya au Marekani?. Wafanyabiashara wakinunua sh. 7000 kwa kilo wao wakauze kwa sh. ngapi na kwa nani (may be wakawauzie waheshimiwa wabunge. Kama ndio njia ya kurudisha gharama za kuwahifadhi hao samaki, naona hiyo gia imekwama jaribuni nyingine.

Si bora ku-comment kwa namna hiyo. Kama wewe huwezi nunua kwa bei hiyo, basi wenzako wananunua. Hawa jamaa wa mnada tatizo lao hawajajipanga vema. Lakini samaki hao wana thamani kubwa sana. Hata Pale Ferry bei iko humo humo.
 
Si bora ku-comment kwa namna hiyo. Kama wewe huwezi nunua kwa bei hiyo, basi wenzako wananunua. Hawa jamaa wa mnada tatizo lao hawajajipanga vema. Lakini samaki hao wana thamani kubwa sana. Hata Pale Ferry bei iko humo humo.

Ni vyema nikacoment hivyo. Kumbuka hao samaki wamekaa kwenye friji muda mrefu hata radha wameshapoteza. Gharama zilizotumika kuwatunza ni zaidi ya thamani halisi ya hao samaki. Na wakiendelea kutonunuliwa ni kuwa tutaendelea kugharamia gharama za kuwahifadhi. Samaki wenyewe ni perishable hivyo wanatakiwa wawe disposed haraka ili wasituingizie gharama zisizo za lazima.
 
Si bora ku-comment kwa namna hiyo. Kama wewe huwezi nunua kwa bei hiyo, basi wenzako wananunua. Hawa jamaa wa mnada tatizo lao hawajajipanga vema. Lakini samaki hao wana thamani kubwa sana. Hata Pale Ferry bei iko humo humo.


Tatizo letu ni kwamba walikaa wachache wakaamua kunadi, wanadhani kunadi vyakula na vitu perishables ni kama kunadi magari na magodoro kama huyo yono alivyozoea!!! Bullshit!!

They needed to a a right research na in some cases kama unataka international bidders then you a right international dalali

Garbage in-garbage out = that what we got from this flop auction

Probably it was a move without proper preparation and market research, but that is not unexpected from our dear government and researchers
 
Probably it was a move without proper preparation and market research, but that is not unexpected from our dear government and researchers

Mkuu MTM;apo kidogo nabisha,hawa jamaa ma dear am sure kabisa walifanya research na kujua kilo ni sh ngapi..upumbavu ulio wajaa ni tamaa ya dunia hii ndio inawaangamiza na ndio maana biblia inasema watu wangu wanaangamia kwa kukosa maarifa..unafikiri awajui mwanza sh ngapi kilo...oooo yeah
tatizo mnada kama huo ma br unawajumuisha wengi wapo waliompa tender YONO nao wanaitaji mgao wao...wapo waliokuwa wakihifadhi wana mgaoo wao sasa nasoma vichekesho vingine wanataka kumuuzia samaki jamaa mmoja ambae ndie anaziihifadhi ati akauze nje;hivi tutakuwa manyangau mpaka lini..huyo mtu ananunua hata kama ni kwa alfu tano anaenda kuuza doller 15-20........ wizi mtupu...kwa hiyo ni tamaa tu ndio inayowafanya washinwe kujua umuhimu wa mtanzania;mnakamata samaki then kwa kosa la kupeleka nje..halafu mnazirudisha nje tena si mngefanya makubaliano na mliowakamata wawasaidie kusafirisha.....sh ngapi mna loose kulaza lile meli pale;;;demn wizi mtupuuuuuuuu
 
Si bora ku-comment kwa namna hiyo. Kama wewe huwezi nunua kwa bei hiyo, basi wenzako wananunua. Hawa jamaa wa mnada tatizo lao hawajajipanga vema. Lakini samaki hao wana thamani kubwa sana. Hata Pale Ferry bei iko humo humo.

Aaa haina hiyo.....kwani si wamewapata bure?kinachotakiwa labda warudishe gharama za kuwahifadhi.Otherwise inaonekana hilo ni CHEZO tayari
 
Probably it was a move without proper preparation and market research, but that is not unexpected from our dear government and researchers

Mkuu MTM;apo kidogo nabisha,hawa jamaa ma dear am sure kabisa walifanya research na kujua kilo ni sh ngapi..

Ndugu yangu, kuna mengi hapo; the net income kwa serikali tusipoangalia tutaambiwa ne zero kwasababu ya storage etc. hawakufanya research ya market; uuzaji wa tani mia tatu kamwe usingeangalia soko la ndani pekee unapoweza kununua kwa buku mbili per Kg.

PDidy, its more than that; hii ni procurement process iliyo wazi katika maandiko na target number one would be a one bulk purchasers it could be through direct auction but inviting fish export companies [in and out of tanzania]; kwetu tanzania kila procurement kunakuwa na malicious deed utake usitake

HAWAKUFANYA RESEARCH PROPER, WALICONSULT A FEW "SO CALLED EXPERIENCED" WAKAISHIA NA YONO-- DUH!!!

I HOPE WALIWASILIANA NA BODI ZA MAZAO YA BIASHARA KUPATA INSIGHT NA CONSULTATION

ANYWAY, MAYBE NI KWELI SOKO LA SAMAKI HAO LILIKUWA HIVYO, NISIJE BISHA KUMBE NAUNGUA NA JUA
 
Kwanza wapendwa hiyo tenda ilitoka lini mpaka akapewa mheshimiwa sana Yono,kama sikosei huyu ni mbunge wa Njombe,je haya mambo si ndio hatuyataki? na pia siku zote walikuwa wapi kupanga jinsi ya kuwauza hao samaki,mimi naamini wangeanza muda muda mrefu na wangeuza kwa bei nafuu hao samaki wangekuwa wamekwisha lakini sababu wakubwa wana ten percent yao hayo ndio matokeo.
 
Wa Okeleki
user_online.gif

Wa Okeleki has no status.
Junior Member
Join Date: Fri Mar 2009
Posts: 6
Thanks: 0
Thanked 0 Times in 0 Posts
Rep Power: 0
reputation_pos.gif
reputation_pos.gif
reputation_pos.gif
reputation_pos.gif
reputation_pos.gif
reputation_highpos.gif
reputation_highpos.gif
reputation_highpos.gif

Credits: 9,165


icon1.gif
Re: Mnada wa samaki waliokamatwa kwa wavuvi haramu wadoda

Quote:


Si bora ku-comment kwa namna hiyo. Kama wewe huwezi nunua kwa bei hiyo, basi wenzako wananunua. Hawa jamaa wa mnada tatizo lao hawajajipanga vema. Lakini samaki hao wana thamani kubwa sana. Hata Pale Ferry bei iko humo humo.




Aaa haina hiyo.....kwani si wamewapata bure?kinachotakiwa labda warudishe gharama za kuwahifadhi.Otherwise inaonekana hilo ni CHEZO tayari

JAMANI BIBLIA SI INASEMA WAZI MMEPATA BURE TOENI BURE SASA HII MIJAMAA INATAKA UTAJIRI HUMOHUMO....WAMRUIE MUNGU HATA KIDOGO....ATAWAFUNULIA ZAIDI...NJE YAHAPO NAWAMBIA HATA PESA ZITAKAZOPATIKANA MTAAMBIWA ZIMEPELEKWA KWENYE KILIMO...KALAGHABAO....

LINGINE KINANIFURAHISHA ATI NIMEONA STORAGE NI USD 8 KWA SIKU NA MPAKA SASA WANADAIWA SH MILLION 189...JAMANI ZIMEKAA SIKU NGAPI HIZO DOLLER 8 SAWA NA SH ZA KITANZANIA 10,400 SASA189,000,000/10,400 = MMMMA SASA SIJUI TATIZO LA GAZETI AMA NDIO UFISADI WENYEWE
 
Anyway, maybe ni kweli soko la samaki hao lilikuwa hivyo, nisije bisha kumbe naungua na jua
__________________
na weye umo??? Am kid...kaka nafikiri kilichobaki ni maombi tu
 
Duh kata waChina ingiza wabongo, sasa wafanyabiashara wanataka njia ya mkato ya wao kuexport fish wa mnada? mie nilijua watapelekwa mahospitalini kama bado wanapikiwa, vyuo vya mafunzo, mashule ya bweni , majeshi nyumba za kutunzia watoto yatima, wenye taahira ya akili, wenye ulemavu and other disabilities na wanaoisho kwenye mazingira magumu, wazee , wenye ukoma n.k. Kumbe wafanyabiashara ndio wanaotaka mijifish!
 
wananchi maeneo yenye njaa wapewe tu bure angalau wabadili mlo!

Kwanza ni mali yao na raslimali ya nchi yao iliyokamatwa kwa wizi!
 
Nimesoma habari hii, iliyofupishwa, kwa masikitiko makubwa:
Tuna fish seized from foreign vessel fails to get market (2009-05-03 17:01:50 –by Correspondent Edwin Agola)


The auctioning of 299 tonnes of tuna fish recovered from a pirate vessel impounded while fishing illegally in the Tanzania Exclusive Economic Zone (EEZ) waters territories, failed to take place in Dar es Salaam yesterday for lack of potential buyers.

The low turn out of potential buyers has reportedly been aggravated by high quotation from the government side compared to actual price at the market.

The fish is currently being stored at the Bahari Food premises in Mikocheni area in the city.

The High Court of Tanzania recently mandated a court broker Yono Auction Mart Company to sell the fish, a fragile product, on behalf of the government….


Huu ni upuuzi kabisa! Yaani tungojee sijui “wawekezaji” wa kuja kununua hao samaki!

Rais JK, nakuomba leo hii, kama ukisoma habari hii, toa amri ili samaki hao WALIOTUIIBIA NA SISI KUWAPATA BURE, walishwe wagonjwa wetu mahospitalini, watoto yatima nchi, ikiwa ni pamoja na kuilisha mashule yetu, ILI KUPUNGUZA GHARAMA WAKATI WA KUYUMBA KWA UCHUMI!

Kwa nini tuendelee kulipia gharama za kuwatunza hao samaki hapo Bahari Food, Mikocheni?

Kwa nini tumlipe dalali Yono Auction Mart Company?

Si ajabu tukakaribisha ufisadi, shauri ya mnuso wa 10% au na zaidi!

 
Hatua hiyo iliilazimu kampuni hiyo kuahirisha mnada huo wa wazi baada ya wafanyabiashara wengi waliofika katika mnada huo kutaka kununua samaki kwa bei ya Sh1,500 hadi 2,000 kwa kilo chini ya iliyopangwa na serikali ya Sh 7,000.

Ha ha haaaaaaaaaaaaaaa, wakuu hiyo difference ni kubwa mno 2000 by 7000. Haini ingii akilini, watanzania/wafanyabiashara sio tabula lasa hawajaanza jana biashara hiyo ya samaki. Either kunamchezo mchafu or mtoa hoja kuna maelezo hajayaweka sawa
 
Back
Top Bottom