Sildenafil Citrate
JF-Expert Member
- Jan 29, 2021
- 573
- 2,553
Habari wakuu,
Hali yangu kiafya siyo njema sana, nikiwa natoka kutibiwa kwenye mojawapo ya hospitali humu jijini Dsm nimekutana na jambo baya linalosikitisha sana.
Dereva mmoja mwenye gari iliyo na usajiri wa T 546 DGV (Mimi sio mtaalamu sana wa magari, sijaweza kugundua upesi ni gari aina gani) ametaka kusababisha msiba mkubwa kwa Taifa kwenye kona ya kwanza iliyo na mteremko wa kasi wa Barabara inayoelekea Saranga kutokea Kimara Temboni.
Dereva huyu kalewa sana, akiwa na speed kubwa kashindwa kuhimili kona iliyopo kwenye mteremko huo hivyo kuvivaa vibanda vya wanawake wajasiriamali wanaofanya kazi zao za urembo, stationery n.k
Bila gari ile kugonga nguzo mojawapo ya fremu zile na kusimama mtaroni ni dhahiri kuwa eneo hilo kwa leo lingeshuhudia mauaji makubwa yanayoweza kuepukika.
Kibaya zaidi, katika hali ile ya taharuki huku manusura wakiwa na wenge kubwa la kusalimika, dereva anaanza kumwagia watu pombe zilizobaki kwenye gari huku akiwafukuza wasitoe msaada.
Najua baadae trafiki mtafika hapo. Chukueni hatua kali dhidi ya kijana huyo mwenye tabia ya hovyo isiyoelezeka.
Picha ya Mwisho: Kijana aliyevaa suruali ya khaki na shati jeusi mikono mirefu ndiye dereva.
Uhai ukipotea haurudi. Usiendeshe gari ukiwa umelewa.
Hali yangu kiafya siyo njema sana, nikiwa natoka kutibiwa kwenye mojawapo ya hospitali humu jijini Dsm nimekutana na jambo baya linalosikitisha sana.
Dereva mmoja mwenye gari iliyo na usajiri wa T 546 DGV (Mimi sio mtaalamu sana wa magari, sijaweza kugundua upesi ni gari aina gani) ametaka kusababisha msiba mkubwa kwa Taifa kwenye kona ya kwanza iliyo na mteremko wa kasi wa Barabara inayoelekea Saranga kutokea Kimara Temboni.
Dereva huyu kalewa sana, akiwa na speed kubwa kashindwa kuhimili kona iliyopo kwenye mteremko huo hivyo kuvivaa vibanda vya wanawake wajasiriamali wanaofanya kazi zao za urembo, stationery n.k
Bila gari ile kugonga nguzo mojawapo ya fremu zile na kusimama mtaroni ni dhahiri kuwa eneo hilo kwa leo lingeshuhudia mauaji makubwa yanayoweza kuepukika.
Kibaya zaidi, katika hali ile ya taharuki huku manusura wakiwa na wenge kubwa la kusalimika, dereva anaanza kumwagia watu pombe zilizobaki kwenye gari huku akiwafukuza wasitoe msaada.
Najua baadae trafiki mtafika hapo. Chukueni hatua kali dhidi ya kijana huyo mwenye tabia ya hovyo isiyoelezeka.
Picha ya Mwisho: Kijana aliyevaa suruali ya khaki na shati jeusi mikono mirefu ndiye dereva.
Uhai ukipotea haurudi. Usiendeshe gari ukiwa umelewa.