Manyanza
JF-Expert Member
- Nov 4, 2010
- 9,526
- 14,399
Wakuu!
Jana asubuhi nilikuwa maeneo ya Kimara Temboni Upande wa kuelekea Mbezi huwa zinapaki Bajaji pamoja na Bodaboda kwa wingi, Kwa ndani kidogo kuna round about halafu kuna Mgahawa, nilienda kujipatia kifungua kinywa. Baada ya muda mfupi lilikuja basi la Mwendokasi lenye namba T 557 DWR halina abiria hata mmoja yupo dereva tu akashuka mule kwenye basi baada ya kulipaki.
Yaani alilipaki kwenye Kona na akauziba mpaka ule Mgahawa, aliposhuka kuna Jamaa akasema huyu naye kila Siku na huwa anamfuata Mwanamke na kweli baada ya kama dk 10 hivi akaja Mwanamke wakasallimia kwa kukumbatiana na alikuwa na Kishikwambi akampa yule Mwanamke , Yeye akaenda kwenye friji akachukua Pepsi baridi na Egg Chop akawa anakula , huko kwenye kona ikaanza foleni na yule Mwanamke aliyemfuata yupo kwenye gari kakaa. Na dereva alitumia karibu dakika 25 pale kwenye Mgahawa , anazunguzunguka anapiga porojo tu na wale Wafanyakazi wa ule Mgahawa.
Maswali yangu.
1. Huyu Dereva ni nani? Mbona anafanya vitu ambavyo kama Dereva anayeendesha usafiri wa abiria hasitahili kufanya?
2. Na yule Mwanamke aliyemfuata ni nani? Maana inasemekana mara nyingi sana huwa anaenda kumfuata pale?
3. Kwanini huyu Dereva analitoa basi la Mwendokasi na kulipeleka kwenye Barabara ambayo sio njia yake ? karibu 300 mita kutoka Morogoro road njia ya kuu na njia ya mwendokasi.
4. Kuna sheria gani inayomlinda huyu Dereva maana Sheria zilizopo kazivunja kwa makusudi
5. Je huyu ndio wale Wazee wa unanijua Mi nani?
6. Au ni ndugu wa Kigogo Mkubwa Serikalini?
Naomba Wahusika mlifuatilie pale Kimara Temboni, Upande wa kuelekea Mbezi unaingia ndani kidogo kuna round about na Mgahawamjaribu kupata maelezo ya kutosha. Anachokifanya huyo dereva sio sahihi kabisa.
Nawasilisha
Jana asubuhi nilikuwa maeneo ya Kimara Temboni Upande wa kuelekea Mbezi huwa zinapaki Bajaji pamoja na Bodaboda kwa wingi, Kwa ndani kidogo kuna round about halafu kuna Mgahawa, nilienda kujipatia kifungua kinywa. Baada ya muda mfupi lilikuja basi la Mwendokasi lenye namba T 557 DWR halina abiria hata mmoja yupo dereva tu akashuka mule kwenye basi baada ya kulipaki.
Yaani alilipaki kwenye Kona na akauziba mpaka ule Mgahawa, aliposhuka kuna Jamaa akasema huyu naye kila Siku na huwa anamfuata Mwanamke na kweli baada ya kama dk 10 hivi akaja Mwanamke wakasallimia kwa kukumbatiana na alikuwa na Kishikwambi akampa yule Mwanamke , Yeye akaenda kwenye friji akachukua Pepsi baridi na Egg Chop akawa anakula , huko kwenye kona ikaanza foleni na yule Mwanamke aliyemfuata yupo kwenye gari kakaa. Na dereva alitumia karibu dakika 25 pale kwenye Mgahawa , anazunguzunguka anapiga porojo tu na wale Wafanyakazi wa ule Mgahawa.
Maswali yangu.
1. Huyu Dereva ni nani? Mbona anafanya vitu ambavyo kama Dereva anayeendesha usafiri wa abiria hasitahili kufanya?
2. Na yule Mwanamke aliyemfuata ni nani? Maana inasemekana mara nyingi sana huwa anaenda kumfuata pale?
3. Kwanini huyu Dereva analitoa basi la Mwendokasi na kulipeleka kwenye Barabara ambayo sio njia yake ? karibu 300 mita kutoka Morogoro road njia ya kuu na njia ya mwendokasi.
4. Kuna sheria gani inayomlinda huyu Dereva maana Sheria zilizopo kazivunja kwa makusudi
5. Je huyu ndio wale Wazee wa unanijua Mi nani?
6. Au ni ndugu wa Kigogo Mkubwa Serikalini?
Naomba Wahusika mlifuatilie pale Kimara Temboni, Upande wa kuelekea Mbezi unaingia ndani kidogo kuna round about na Mgahawamjaribu kupata maelezo ya kutosha. Anachokifanya huyo dereva sio sahihi kabisa.
Nawasilisha