Mlolongo wa Ajali za Barabarani Tanzania 2007-2011

Poleni sana majeruhi na waliopoteza wapendwa wao. Inahuzunisha sana jamani, hadi lini mambo haya jamani. Mungu utusaidie.
 
Inasikitisha sana, hii ngorika ilikuwa inaelekea Tanga...waliokufa ni 06 na ni abiria wa Hiace. Ngorika bado ipo pale na polisi walifika katika eneo la tukio na kuchukua miili ya waliokufa kwenye ajali hiyo.
Majeruhi nao walikimbizwa hospital.
MUNGU AZILAZE ROHO ZA MAREHEMU MAHALI PEPA PEPONI...AMEN!!!
 
Asubuhi hii basi la Ngorika lililokuwa linatoka arusha kwenda dar limegongana na Hiace imeandika Shalom katika daraja la Makumira nje kidogo ya jiji la Arusha watu wamekufa na wengine wamejeruhiwa..
Mungu aziwe mahali pema roho za marehemu.. Amen
Hakuna mtu ambae alikuwa hajui kuwa Ngorika ipo siku litauwa,nadhani hata police na vyombo vingine vya barabarani vilikuwa vinasubiri tu siku.ngorika ni kampuni ya mabasi ambayo tangu enzi ilikuwa inasifika kwa speed kali barabarani nahata baadhi ya askari wanajua hilo na walikuwa hata wakidiriki kusifia mwendo wa yale mabasi.binafsi nilishaapa kutopanda lile basi milele baada ya kuona jinsi linavyoenda na hata ukiangalia wahudumu wa bus lile kuanzia conductor hadi dereva ni mirungi tu kwa kwenda mbele,kwa ufupi ni mabasi ambayo yanaonekana matatizo yake yameanzia kwa tajiri wao.
nashauri waziri husika na viongozi wa jeshi la police usalama barabarani wajiuzulu kwa hili.maana tumeshachoka na ajali kila siku.
 
Madereva wa ngorika na chakito ndo wanaongoza kwa mwendo kasi ili wafike wa kwanza.wamewekewa utaratibu na maajenti wa tiketi kuwa gari ya kwanza kufika ubungo driver anapewa 50,000 ili kuvutia abiria wafanyabiashara wanaopenda kuwahi...

this is really shocking kama ni kweli mkuu... Yani wanachezea maisha ya watu hivi hivi kisa 50,000??... Na hao polisi wa kudhibiti mwendo kasi wapo wapi?? Si huwa naskia kila basi huwa linapewa time chart yake na expected time of arrival?? Mbn inakua ivyo sasa??
 
imetokea ajali mbaya maeneo ya makumira Arusha kati ya hiace na ngorika...watu 9 wamekufa hapohapo..!habari zaidi zitawajia..!

Mi kipindi hiki naogopa sana kusafiri yaani mpaka matatizo nayahailisha.
Poleni wafiwa poleni majeruhi.
Madereva watatumaliza
 
ni ukweli hata polisi walikua wanajua tu kwamba kuna siku wataua hawa jamaa maana hakuna mtu asiyejua mwendo wa mabasi haya kweli wanateketeza viumbe wa mungu na hata sisi abiria kwanini huwa hatuwaambii hawa madereva?wapunguze mwendo?
this is really shocking kama ni kweli mkuu... Yani wanachezea maisha ya watu hivi hivi kisa 50,000??... Na hao polisi wa kudhibiti mwendo kasi wapo wapi?? Si huwa naskia kila basi huwa linapewa time chart yake na expected time of arrival?? Mbn inakua ivyo sasa??
 
Pamoja na sababu za usalama barabarani, sababu nyingine inayochangia ajali nyingi siku hizi hapa Tanzania ni kutokana na kuwa na viongozi washirikina ambao wamelipeleka taifa zima kwenye ushirikina. Hivyo mashetani na mapepo wanayoyaabudu wanapata haki ya kunywa damu za watanzania. Suala hapa ni serikali kuacha kuunga mkono ushirikina wa Babu Loliondo na wagawa vikombe wote walioibuka kwani kufanya hivyo wanampa shetani haki ya kunywa damu za watanzania.
 
Hapo inabidi idara nzima ya polisi wa usalama barabarani wajivue gamba.Kazi yao ni kukinga mikono wapate pesa na sio kutekeleza majukumu yao.
Ni kweli kabisa, na pia mpaka pale wamiliki wa mabasi watakapoamua kupunguza hizo ajali.

Kuna dereva mmoja aliwahi kuendesha mabasi yaliyojulikana kama mabasi ya ligi, yalikuwa yanasafiri kati ya Dar na Nyanda za juu, huyu jamaa akapata kazi Scandinavia baadaye, huwezi kuamini alikuwa anapunguza mwendo ili madereva wenzie wampite kitu ambacho hakikuwezekana alipokuwa na makampuni mengine
 
tatizo ni serekali kutotaka kufana upanuzi wa barabara, si rahisi kumaliza ajali za barabarani bila kuwa na utatuzi wa barabara. imefika wakati nchi yetu iwe na double rod za kwenda na kurudi, apo tunaweza kupunguza ajali.

Mkuu labda umesahau kitu kimoja. barabara nyingi ni double standar, yaani gari moja inauwezo wa kupishana na gari moja nyingine, kama kuna na mwendesha baskeli, either mmojawapo asimame kila mtumia barabara akilazimisha ndo yaliyotokea leo! Mungu awatie nguvu walio fiwa, na majeruhi wapone haraka. (Kumbuka kuwa mi ni si-pest kila jambo hivo sisemi RP kwani mtu anarest in peace kwa kuandaa maisha yake baada ya hapa duniani wanaobaki hawawezi kukuombea kwa Mungu.
 
Mungu awatie nguvu ndugu jamaa, pia majeruhi tunawaombea wapone haraka.
 
Ngorika bus linalo fanya safari zake Dar to Arusha limepata ajali mbaya sana hapa USA RIVER Arusha karibu na chuo kiku cha Tumaini makumira. Limegongana uso kwa uso na haice. Kwa muonekano, abiria walioko kwenye haice ndio walio fariki na wengine kumia kwa wingi.
 
Kuna ajali mbaya imetokea Kati ya Ngorika na kiford kugongana watu wengi wamekufa mwenye taarifa kamili atujulishe.
 
Ngorika wapipwe ban miezi 3, harafu mkuu wa usalama barabarani arusha ajipangue mwenyewe. Lakini kwa vile, katiba yetu haitowi mwanya wa uwajibikaji tutalia kwa muda na maisha yanaendelea. The same story itatokea in the near future harafu tunalia tunazikana na kusahau.

Niko nchi fulani, nilimhadithia rafiki yangu mmoja kuwa mama yangu alishafariki kwa kuugua na malaria, akashangaa sana na maswali yake mengi. Kiufupi tunahitaji kupunguza vifo vitokanavyo uzembe kama hivyo.
 
RIP Poleni wafiwa!! Duh, Madereva wengine bora Hata Tungefundisha wanyama wangekuwa wanaogopa Maisha yao, Kwani sasa madereva hawaogopi Kufa!! Haraka zote hizo za nini? Wanakimbilia wapi?
 
Back
Top Bottom