Mkuu wa Wilaya Urambo mkoani Tabora awafuta kazi wakuu wa shule 10

Mambo mengine yote yalikuwa sawasawa ikiwa ni pamoja na walimu wa kutosha na mazingira mazuri ya kufundishia na kujifunzia? Jamani naomba job description ya ma-DC.
Mwalimu kazi yake ni kufundisha. Kusoma na kujifunza ni kazi ya mwanafunzi akisaidiwa na mazingira mazuri ya kujifunza hasa nyumbani. Kama mtoto wa shule ya kata anarudi nyumbani anakuta ng'ombe wanamsubiri awapeleke malishoni akirudi atembee kilometer kadhaa kutafutwa maji, je huyu atasoma kweli? Mwalimu anafanya sehemu ndogo sana ya mafanikio ya mwanafunzi "kumwonyesha maji yako wapi na hawezi kuwalazimisha wayanywe". Hivyo hawa waalimu wameonewa.
 
Je hizo shule zina walimu wa kutosha? na je tatizo la hizo shule ni uongozi?.Mimi napata shida na viongozi wakuu wengi ambao walikuwa walimu. wanawaharasi sana walimu wenzao kweli kikulacho kipo nguoni mwako.Yeye mwenyewe alikuwa ni mwalimu sijuwi alikuwa anawafaulisha vipi wanafunzi kwenye masomo yake naomba yeyote aliyewahi fundishwa naye anieleze.Tabia hii ni sawa na ya Mkuu wa mkoa wa Tanga Mwantumu Mahiza.
 
viongozi wa chini wanajichukulia sheria mkononi na kufanya hata yale ambayo hawana mamlaka nayo. wa huko juu yao nao hawajui la kufanya maana hakuna anayejua tafsiri sahihi ya 'jipu' au 'hapa kazi' isipokuwa mkuu wa nchi. kwa kweli tunakoelekea ni giza tororo
 
wacha wakuonyeshe madoido sizonje,we sema tu unataka vya mafuta au vya Nazi,ha ha haaa!
 
Inatakiwa na yeye awajibishwe kwa vile kosa hilo limetokea wilayani kwake akiwa kiongozi. Hapa huyo DC ameamua kukimbia uwajibikaji na kupakazia wanyonge. Hivi serikalini hakuna performance appraisals?
 
Hii serikali kila kiongozi anafukuzafukuza tu bila au ni moja ya kazi walipangiwa
 
Kama wamevuliwa madaraka ,hawakufukuzwa rekebisha kichwa cha habari. Moderetor msaidieni mdau.
 
Acheni kuwa na chuki iliyopitiliza kwa Jk.mtu akifanya vizuri mnamsifia mtu binafsi na mtu akikosea mnamlaumu Jk.mbona Magu kateua wote walikuwepo utawala wa Jk?? Unafikiri kuna aliyeteuliwa hakuwemo serikali iliyopita?? Huyo Dc kachemka kwa uwezo wake duni tu.tupunguze chuki
 
Mkuu wa wilaya ya Urambo bibi Queen Mlonzi amewavua nyadhifa wakuu wa shule Kumi kufuatia shule zao kufanya vibaya katika matokeo ya kidato cha pili. Aidha DC huyo amesema ameamua kuchukua hatua hizo ili iwe funzo kwa walimu wengine.
Kuna utaratibu wa utumishi wa uma,nadhani serikali inabidi iliangalie hili maana tunapo elekea boss akiamka vibaya tu hiyo siku basi anaenda kufukuza watu,nadhani kwa utaratibu huu badala ya kujenga tutakuwa tunabomoa.
 
Je, yeye ndiye aliwaajiri? Pili, je kuna policy iliyowekwa wazi kabla ya haya inayosema mwalimu atavuliwa wadhifa wa kazi endapo wanafunzi wa form 2 wakifanya vibaya mitihani? Je, ni hii wilaya tu wanafunzi wamefanya vibaya? Na kama jibu ni sio, ni sawa kuwavua wadhifa wa kazi hawa wakati wengine wanaendelea kufanya kazi kwa wadhifa wao? Hii nchi inahitaji kuwepo utaratibu wa kufanya kazi (standards of operations ) ili kuhakikisha kuwa wote wa nao kwenda against utaratibu wanaadhibiwa wote. Huu utaratibu wa mkuu wa wilaya kuwa demote waalimu anavyojisikia is not leadership bali ni udikiteta. This should strongly be condemned.


Hapo ndio nchi ya tz ilipofikia.
 
Mwalimu kazi yake ni kufundisha. Kusoma na kujifunza ni kazi ya mwanafunzi akisaidiwa na mazingira mazuri ya kujifunza hasa nyumbani. Kama mtoto wa shule ya kata anarudi nyumbani anakuta ng'ombe wanamsubiri awapeleke malishoni akirudi atembee kilometer kadhaa kutafutwa maji, je huyu atasoma kweli? Mwalimu anafanya sehemu ndogo sana ya mafanikio ya mwanafunzi "kumwonyesha maji yako wapi na hawezi kuwalazimisha wayanywe". Hivyo hawa waalimu wameonewa.
Nadhani wewe umezaliwa na kukulia ulaya ambako wazazi huingia darasani kuwasaidia walimu kufundisha. Huku Africa wazazi wengi hawajaenda shule na wala hawajui umuhimubwa shule ndiyo maana mwalimu ana kazi kubwa sana. Mzazi anajua ni mwalimu ni kila kitu. Kumbe when we talk of conducive learning and teaching environment wewe huwa unatoka kapa. Watu kama nyie inawezekana mmesoma lakini hamjaelimika.
 
hizi chuki mwisho wake ni mbaya sana shule hazina walimu wa kutosha hazina vitabu mazingira mabovu yanayosababisha utoro njaa majumbani mwamko mdogo wa wazazi kuhusu elimu we mkuu wa wilaya unamdemote mwalimu huku umevaa sare ya chama chako na kadi ya chama chako mfukoni hii sio haki mbona walimu wanastrem yao ya uongozi na mwajiri wa mwalimu ki wilaya yupo chini ya mkurugenzi na kitaifa yupo chini ya ofisi ya waziri mkuu .Na kinachouma zaidi Mkuu wa wilaya ni political figure
Kwa kweli. Hawa Viongozi wajue kuwa waalimu hawa wanajitolea sana. Kitu wangefanya ni kufanya tathmini kwanza kabla ya kukurupuka na kuangalia factors zinazochangia wanafnzi kufeli na kuangalia jinsi ya kupata resources nk.
 
Je, yeye ndiye aliwaajiri? Pili, je kuna policy iliyowekwa wazi kabla ya haya inayosema mwalimu atavuliwa wadhifa wa kazi endapo wanafunzi wa form 2 wakifanya vibaya mitihani? Je, ni hii wilaya tu wanafunzi wamefanya vibaya? Na kama jibu ni sio, ni sawa kuwavua wadhifa wa kazi hawa wakati wengine wanaendelea kufanya kazi kwa wadhifa wao? Hii nchi inahitaji kuwepo utaratibu wa kufanya kazi (standards of operations ) ili kuhakikisha kuwa wote wa nao kwenda against utaratibu wanaadhibiwa wote. Huu utaratibu wa mkuu wa wilaya kuwa demote waalimu anavyojisikia is not leadership bali ni udikiteta. This should strongly be condemned.

Udikteta tuliusubiri kwa hamu sana bora uenee kila sehemu hasa Polisi, Jeshini na Mahakamani akikosea tu anatwangwa risasi hii nchi haitakiwi sheria tena watu wamekuwa wazembe kwa vigezo vya sheria
 
Mkuu wa wilaya ya Urambo bibi Queen Mlonzi amewavua nyadhifa wakuu wa shule Kumi kufuatia shule zao kufanya vibaya katika matokeo ya kidato cha pili. Aidha DC huyo amesema ameamua kuchukua hatua hizo ili iwe funzo kwa walimu wengine.
Anatenda asilolijua huyo

Kwanza kwenye organization chart ya mfumo wa elimu Mkuu wa wilaya hayupo kabisa. Yeye ni mteule wa rais na ninachokijua hana hata job description, Mteule .... ni mtu aloteuliwa sio kwa vigezo maalum bali kwa mapenzi / matakwa ya aliyemteua. ..... Kama nakosea mwenye wazo tofauti na hilo anijuze ...
 
Nimetoka juzi kijijini kwetu nimekuta kuna shule ya sekondari ina walimu wawili tu, tangu finguliwe haijawahi ktoa mtoto hata mmoja kwenda chuo au kidato cha tano, wazazi wanachoka kununua vifaa vya shule watotot wanarudi mtaani kuzurura, sasa hawa wawili nao wkafukuzwe kazi kwa kuwa watotot hawafaulu? Wanaangalia mazingira kwanza? shule kama hii watafaulu vipi hata kama mwalimu akiwa n anafanya kazi kwa spidi ya ajabu? Waache kukurupuka watafute sababu za msingi.
 
Back
Top Bottom