Mkuu wa Taasisi ya Teknolojia Dar es Salaam, Prof Ndomba hana uwezo wa kuiongoza Taasisi hiyo, abadilishwe

TUHUMA ZINAZOMHUSU Mkuu wa Taasisi ya Teknolojia Dar es Salaam, Prof. Ndomba HAZINA UKWELI WOWOTE

Nikiwa mmoja wa wadau wa maendeleo ya TANZANIA, nimesikitishwa sana na tuhuma zilizoelekezwa kwa mkuu wa taasisi ya teknolojia ya Dar es Salaam, Prof. Ndomba.

Napenda kuwasilisha hoja kinzani ya habari zinazohusu mkuu wa Taasisi wa teknolojia ya Dar es Salaam zinazolenga kudhoofisha juhudi za mkuu huyo wa Taasisi, Prof. Preskedis Ndomba. Baada ya kutafakari hoja za mwandishi (ambaye siyo academician) na maneno yanayojirudia katika hoja zake, na aina ya maneno anayoyatumia katika lugha zote anazotumia kila mara, nimeridhika kwa asilimia kubwa kuwa ni mmoja wa watumishi wa DIT.

Kurejea hoja yetu:

Tukubaliane kuwa, si jambo la ajabu kuwa na mawazo na hisia zinazokinzana kati ya watu wawili tofauti. Kama kila ushauri ungekuwa unakubaliwa na kiongozi, ni wazi kuwa matokeo ya maamuzi yake yangekuwa yanayotia wasiwasi. Naamini kwamba Prof. Ndomba ni msikivu sana. Ofisi ya Mkuu wa taasisi iko wazi tofauti na baadhi ya watendaji wengine wa taasisi kama hii. Mimi ni shahidi katika hili. Kama ni ushauri wa busara na wenye kukidhi dira ya Taasisi, ningeshangaa kama ningesikia Prof. Ndomba anaukataa. Hizi anazoziita facts, kimsingi hazina proofs hata kidogo, maana hata mfano wa anazoziita facts hajaziweka hapa. Anachotaka ni kuiaminisha umma wa watanzania kwamba yeye ndiye mwenye kuchambua hizo facts bila kuieleza umma anaojaribu kuaminisha.

Kama mwandishi huyu angekuwa anajua sheria kama anavyojinadi, angejua kwamba Prof. Ndomba, ambaye amekuwa katika kitendo cha rasilimali watu kwa muda mrefu katika chuo kikuu cha Dar es Salaam (UDSM) yenye wasomi lukuki, angepata kashfa ya kutishia kufukuza watu. Ifahamike kwamba kila kiongozi anapitia changamoto nyingi hasa ya kuchukuliana na watu mbalimbali, na njia iliyo rasmi ni kupitisha changamoto kama hizo kwenye organs zinazokubalika kwa mujibu wa sheria. Hivyo kwa kupeleka mtumishi kwenye disciplinary committee (kamati ya kinidhamu) ni utaratibu halali tena wa busara ili kumpa mtumishi huyo nafasi ya kufahamu mapungufu yake na ikibidi kukabiliana na tuhuma husika. Mwandishi anataka kuaminisha umma kwamba hiyo kamati pia ina mapungufu! Mwandishi afahamu kwamba, kamati ya nidhamu ndiyo njia njema kumpa nafasi mtumishi kujitetea. Kwa miaka yote ambayo Prof. Ndomba amekaa DIT hakuna mtumishi hata mmoja aliyefukuzwa kazi, pamoja na mapungufu mengi ya watumishi kiutendaji ambayo mkuu huyo anayapata na kuchukuliana nayo. Nirejee kusema tena, kwa utaratibu huo, Prof. Ndomba atakuwa anamtendea mtumishi huyo haki zote na pengine kumsaidia. Hii inaonyesha mwandishi ndiye hana elimu ya sheria za kazi.

Kwa madai ya kujengea hofu wafanyakazi, napenda kumfahamisha mwandishi huyo kwamba, anayejijengea hofu ni yeye mwandishi mwenyewe, maana watumishi wa Taasisi hii ya teknolojia wanajua haki zao ambazo kwenye mabaraza ya wafanyakazi ambayo yanayo uwakilishi wa kila sehemu wanahudhuria. Katika kikao chochote, mwenyekiti anayo madaraka yake. Kama hoja inayojadiliwa haiendani na ajenda ya wakati huo, ni haki ya mwenyekiti kuongoza. Hata kama maamuzi ya mwenyekiti ndiyo yanayopitishwa, mwandishi huyu anaitukana wajumbe wa vikao hivyo kwamba hawawezi kujenga hoja zao kama zinatofautiana na za mwenyekiti. Niweke wazi kwamba, pamoja na ukweli kwamba hoja za wajumbe wa vikao yanaweza kufautiana lakini katibu wa vikao husika anaandika maamuzi ya wajumbe. Na kikao kinachofuata, wajumbe hurejea minutes na kupitisha zote. Mwandishi kwa kumbukumbu zake aiambie umma kwamba ni minutes za kikao kipi cha ndani ya taasisi ambayo kikao kilishindwa kupitisha kwa sababu siyo hoja zao? Mwandishi atupe heshima zetu kama watumishi wa taasisi na siyo watu wanaoweza kuburuzwa kama anavyoiaminisha umma wa watanzania!

Mwandishi anasema Prof. Ndomba anadhalilisha hata wasaidizi wake! Hivi, kwa akili ya kawaida, unaweza kuamini kuwa Prof. Nsimama na Dr. Najat wanaweza kukubali kudhalilika? Unadhani kwamba hawa viongozi wetu wangeshindwa kukemea hilo? Kwa taarifa ni kwamba, hata kama kungekuwa na tofauti zao, ambayo sitarajii kuwa yasiwepo, Prof. Nsimama anajua wapi anaweza kujisemea na siyo kukusubiri wewe uwe msemaji wake.

Mwandishi huyu anaonyesha mapungufu yake katika uelewa wa kisheria. Katika Taasisi hii kuna ASA, THTU, RAAWU, ambao kama wafanyakazi wananyimwa stahiki zao, vyombo hivyo vingewasemea watumishi hao. Kwa mfano, maswala ya extra duty yako kisheria na yanatolewa kwa miongozo na barua husika inayosema hilo. Kwa kumbukumbu zangu, sikumbuki mtumishi yeyote ambaye anakubalika kupata hizo extra duties akakosa. Siyo kila kazi ya msingi inatolewa extra duty. Mfano, mtumishi anayetumika katika kazi yake ya msingi ya ajira hawezi kudai extra duty! Hoja kama hizi zinaletwa katika baraza la wafanyakazi na yanajadiwa na kupatiwa majibu. Nitashangaa kama mkuu wa taasisi anaweza kutumia kodi na pesa za walala hao kumlipa mtumishi extra duty ambaye tayari analipwa mshahara kwa kazi yake ya msingi. Hivi, mwandishi anaposema Prof. Ndomba analipa kiasi kidogo, kiasi kikubwa ni kipi? Tufahamu kwamba kila kazi inayo malipo yake stahiki na halali. Kuna madai mengine hata yanaweza kutengenezwa kwa namna ambayo siyo halali. Kama kiongozi asipokuwa makini anaweza kuipelekea taasisi na serikali hasara. Namshauri mwandishi aulize ofisi zote zinazopitia na kupitisha malipo ajue mambo yanayokuwa huko! Kila malipo yanafanyiwa ukaguzi na lazima yakidhi sifa!

Madai mazito ya kwamba Prof. Ndomba hana utu, na kwamba hajali maslahi ya wafanyakazi ni ya mwandishi mwenyewe na bahati mbaya hajayaweka wazi. Kwa kweli niseme kwamba, kwa aliyekuja DIT miaka ya nyuma na sasa ataona tofauti. Nilidhani hapa kwa kutengeneza pavement za DIT tungeona kama mafanikio na kwamba sasa yale madimbwi yamekwisha. Ajabu hili kwa mwandishi ni mapungufu! Sidhani kama anajua mikakati mikubwa ya taasisi. Kwa maswala ya ofisi kwa watumishi, ni kwamba, kuna miradi mikubwa miwili mikubwa ambayo inaandaa kutolea majibu mambo ya hostels na ofisi. Lakini pia, kila semester wataalamu wanakuja kupiga dawa katika hostels zote za DIT kama mwandishi hana habari huko alipo, amuulize estate manager kwanza kabla ya kukurupuka kuandika upotoshaji huu!

Na ajabu kuona sasa DIT LIBRARY ilivyo sasa baada ya kufanya kazi usiku na mchana, badala ya kumpa pongezi Prof. Ndomba, lakini yeye anamlaumu. Sisi watumishi wengine tulioshiriki kwa vitendo na tumefurahishwa na hili. Tulipitia kila wakati hatua zote n ahata kutoa ushauri bila kujali taaluma zetu. Kila penye malengo lazima tunapaswa kushikamana kama Taasisi. Kama ni sifa kwa Prof. Ndomba ndiyo mwandishi anaona shida, basi sisi kama watumiaji wa library na waumishi, hili tunastahili sifa wote. Kwa kudai kwamba tulitaka ifunguliwe na waziri mkuu, kwetu sisi ndiyo, tulipenda iwe hivyo. Ninaamini Waziri Mkuu naye angependa kufanya hivyo. Namshauri mwandishi aitembelee library hata sasa na ataona tofauti.

Inashangaza kuona haya mafanikio kwa mwandishi ni mabaya tu. Binafsi sina taarifa ya kwamba Prof. Ndomba anafanya DIT kuwa stepping stone, ila kama ikiwapendeza wateuzi, watakapokuwa wamempa nafasi ingine kubwa zaidi, tunaomba wampendekeze mwenye maono kama haya ya Prof. Ndomba.

Nimshauri mwandishi awe anaandika ualisia na siyo maoni elekezi. Mwandishi anasema, Prof. Ndomba anapenda kila kitu kiandikiwe paper. Labda mwandishi ana uelewa finyu katika hili. DIT kuna tofauti kubwa ya watumishi, tofauti ya elimu, umri, lakini pia taaluma. Mwandishi ajue kwamba, hakuna Project yoyote ya EU ambayo inaopatikana bila uandishi wa proposal. Na isingekuwa rahisi kwa kuipata hiyo project ambayo mwandishi anadai kama haina project concept paper. Kwa kifupi paper kuwekwa ili iwe rahisi kueleweka kwa wana taasisi ambao mwisho wake ndiyo watendaji wa hiyo project ni jambo jema kabisa. Mwandishi ajikite kwenye taaluma yake na siyo hizi za kitaaluma ambayo hana uelewa nayo.

Niombe mwandishi ajue kwamba dhana ya Teaching Factory ni la taasisi pamoja na kwamba inasimamiwa pia na Prof. Ndomba. Katika hili, wale wote ambao hawajitumi na walizoea kudanganya katika tawala zilizopita wanaona ni taabu sana. Teaching factory, inatoa mianya kwa taasisi kushirikisha wadau wengine katika kufundisha waalimu na wanafunzi pia. Hatua ya sasa itakuwa ngumu kwa wenye mawazo kama haya ya mwandishi kuelewa. Namsihi ajishirikishe na mkuu wake wa karibu au wadau tulioielewa dhana ajifunze.

Prof. Ndomba amewapa wengi elimu ya miradi ambayo yeye binafsi ameandaa semina ya kufundisha hili na baada ya elimu hiyo, kuna wana taaluma wengi wameisha ingia katika miradi mingi ya ndani na nje. Kwa kujua hiyo potential iliyopo DIT ndiyo maana tunayo mradi wa world bank ambayo DIT inanufaika, TELMS, na mingine mingi ya ndani.

Waalimu wengi waliokuwa wanahangaika kufundisha nje ya taasisi kwa kukosa miradi kwa sasa wanajikita kwenye miradi. Nina Imani mwandishi amejipima ameona hana viwango vya DIT ya sasa na anajihami. Namshauri mwandishi arejee mikakati na ajione kama anafaa kubaki katika miradi mikubwa ya DIT au aanze mradi mwingine wa binafsi aliyoizoea.

Binafsi, nashangazwa kuona Mh. Pro. Ndalichako anahusishwa katika hili eti kwa swala la family friend. Hili nimuombe waziri wetu, mama yetu mpendwa, ufahamu kwamba hili ni wazo la binafsi na siyo ya DIT community!

Niombe wanataasisi tubaki na umoja wetu. Wakuu wetu wasichoke na sisi na kujua kwamba tuna watu wenye mawazo tofauti na changamoto zetu.

Asanteni
 
Prof. Ndomba analalamikiwa na wengi. Kuna kitu, sio bure. Kondoro alikaa DIT muda mrefu na pamoja na madhaifu yake lakini Ndomba ameanza kuharibu mapema.

Ki-tovuti cha DIT nowadays utadhani kimetengenezwa na mwanafunzi anayejifunza coding.

Nimeshangaa kukuta Challo bado yupo DIT
Kondoro alikuwa Jembe sana, yule jamaa.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
TUHUMA ZINAZOMHUSU Mkuu wa Taasisi ya Teknolojia Dar es Salaam, Prof. Ndomba HAZINA UKWELI WOWOTE

Nikiwa mmoja wa wadau wa maendeleo ya TANZANIA, nimesikitishwa sana na tuhuma zilizoelekezwa kwa mkuu wa taasisi ya teknolojia ya Dar es Salaam, Prof. Ndomba.

Napenda kuwasilisha hoja kinzani ya habari zinazohusu mkuu wa Taasisi wa teknolojia ya Dar es Salaam zinazolenga kudhoofisha juhudi za mkuu huyo wa Taasisi, Prof. Preskedis Ndomba. Baada ya kutafakari hoja za mwandishi (ambaye siyo academician) na maneno yanayojirudia katika hoja zake, na aina ya maneno anayoyatumia katika lugha zote anazotumia kila mara, nimeridhika kwa asilimia kubwa kuwa ni mmoja wa watumishi wa DIT.

Kurejea hoja yetu:

Tukubaliane kuwa, si jambo la ajabu kuwa na mawazo na hisia zinazokinzana kati ya watu wawili tofauti. Kama kila ushauri ungekuwa unakubaliwa na kiongozi, ni wazi kuwa matokeo ya maamuzi yake yangekuwa yanayotia wasiwasi. Naamini kwamba Prof. Ndomba ni msikivu sana. Ofisi ya Mkuu wa taasisi iko wazi tofauti na baadhi ya watendaji wengine wa taasisi kama hii. Mimi ni shahidi katika hili. Kama ni ushauri wa busara na wenye kukidhi dira ya Taasisi, ningeshangaa kama ningesikia Prof. Ndomba anaukataa. Hizi anazoziita facts, kimsingi hazina proofs hata kidogo, maana hata mfano wa anazoziita facts hajaziweka hapa. Anachotaka ni kuiaminisha umma wa watanzania kwamba yeye ndiye mwenye kuchambua hizo facts bila kuieleza umma anaojaribu kuaminisha.

Kama mwandishi huyu angekuwa anajua sheria kama anavyojinadi, angejua kwamba Prof. Ndomba, ambaye amekuwa katika kitendo cha rasilimali watu kwa muda mrefu katika chuo kikuu cha Dar es Salaam (UDSM) yenye wasomi lukuki, angepata kashfa ya kutishia kufukuza watu. Ifahamike kwamba kila kiongozi anapitia changamoto nyingi hasa ya kuchukuliana na watu mbalimbali, na njia iliyo rasmi ni kupitisha changamoto kama hizo kwenye organs zinazokubalika kwa mujibu wa sheria. Hivyo kwa kupeleka mtumishi kwenye disciplinary committee (kamati ya kinidhamu) ni utaratibu halali tena wa busara ili kumpa mtumishi huyo nafasi ya kufahamu mapungufu yake na ikibidi kukabiliana na tuhuma husika. Mwandishi anataka kuaminisha umma kwamba hiyo kamati pia ina mapungufu! Mwandishi afahamu kwamba, kamati ya nidhamu ndiyo njia njema kumpa nafasi mtumishi kujitetea. Kwa miaka yote ambayo Prof. Ndomba amekaa DIT hakuna mtumishi hata mmoja aliyefukuzwa kazi, pamoja na mapungufu mengi ya watumishi kiutendaji ambayo mkuu huyo anayapata na kuchukuliana nayo. Nirejee kusema tena, kwa utaratibu huo, Prof. Ndomba atakuwa anamtendea mtumishi huyo haki zote na pengine kumsaidia. Hii inaonyesha mwandishi ndiye hana elimu ya sheria za kazi.

Kwa madai ya kujengea hofu wafanyakazi, napenda kumfahamisha mwandishi huyo kwamba, anayejijengea hofu ni yeye mwandishi mwenyewe, maana watumishi wa Taasisi hii ya teknolojia wanajua haki zao ambazo kwenye mabaraza ya wafanyakazi ambayo yanayo uwakilishi wa kila sehemu wanahudhuria. Katika kikao chochote, mwenyekiti anayo madaraka yake. Kama hoja inayojadiliwa haiendani na ajenda ya wakati huo, ni haki ya mwenyekiti kuongoza. Hata kama maamuzi ya mwenyekiti ndiyo yanayopitishwa, mwandishi huyu anaitukana wajumbe wa vikao hivyo kwamba hawawezi kujenga hoja zao kama zinatofautiana na za mwenyekiti. Niweke wazi kwamba, pamoja na ukweli kwamba hoja za wajumbe wa vikao yanaweza kufautiana lakini katibu wa vikao husika anaandika maamuzi ya wajumbe. Na kikao kinachofuata, wajumbe hurejea minutes na kupitisha zote. Mwandishi kwa kumbukumbu zake aiambie umma kwamba ni minutes za kikao kipi cha ndani ya taasisi ambayo kikao kilishindwa kupitisha kwa sababu siyo hoja zao? Mwandishi atupe heshima zetu kama watumishi wa taasisi na siyo watu wanaoweza kuburuzwa kama anavyoiaminisha umma wa watanzania!

Mwandishi anasema Prof. Ndomba anadhalilisha hata wasaidizi wake! Hivi, kwa akili ya kawaida, unaweza kuamini kuwa Prof. Nsimama na Dr. Najat wanaweza kukubali kudhalilika? Unadhani kwamba hawa viongozi wetu wangeshindwa kukemea hilo? Kwa taarifa ni kwamba, hata kama kungekuwa na tofauti zao, ambayo sitarajii kuwa yasiwepo, Prof. Nsimama anajua wapi anaweza kujisemea na siyo kukusubiri wewe uwe msemaji wake.

Mwandishi huyu anaonyesha mapungufu yake katika uelewa wa kisheria. Katika Taasisi hii kuna ASA, THTU, RAAWU, ambao kama wafanyakazi wananyimwa stahiki zao, vyombo hivyo vingewasemea watumishi hao. Kwa mfano, maswala ya extra duty yako kisheria na yanatolewa kwa miongozo na barua husika inayosema hilo. Kwa kumbukumbu zangu, sikumbuki mtumishi yeyote ambaye anakubalika kupata hizo extra duties akakosa. Siyo kila kazi ya msingi inatolewa extra duty. Mfano, mtumishi anayetumika katika kazi yake ya msingi ya ajira hawezi kudai extra duty! Hoja kama hizi zinaletwa katika baraza la wafanyakazi na yanajadiwa na kupatiwa majibu. Nitashangaa kama mkuu wa taasisi anaweza kutumia kodi na pesa za walala hao kumlipa mtumishi extra duty ambaye tayari analipwa mshahara kwa kazi yake ya msingi. Hivi, mwandishi anaposema Prof. Ndomba analipa kiasi kidogo, kiasi kikubwa ni kipi? Tufahamu kwamba kila kazi inayo malipo yake stahiki na halali. Kuna madai mengine hata yanaweza kutengenezwa kwa namna ambayo siyo halali. Kama kiongozi asipokuwa makini anaweza kuipelekea taasisi na serikali hasara. Namshauri mwandishi aulize ofisi zote zinazopitia na kupitisha malipo ajue mambo yanayokuwa huko! Kila malipo yanafanyiwa ukaguzi na lazima yakidhi sifa!

Madai mazito ya kwamba Prof. Ndomba hana utu, na kwamba hajali maslahi ya wafanyakazi ni ya mwandishi mwenyewe na bahati mbaya hajayaweka wazi. Kwa kweli niseme kwamba, kwa aliyekuja DIT miaka ya nyuma na sasa ataona tofauti. Nilidhani hapa kwa kutengeneza pavement za DIT tungeona kama mafanikio na kwamba sasa yale madimbwi yamekwisha. Ajabu hili kwa mwandishi ni mapungufu! Sidhani kama anajua mikakati mikubwa ya taasisi. Kwa maswala ya ofisi kwa watumishi, ni kwamba, kuna miradi mikubwa miwili mikubwa ambayo inaandaa kutolea majibu mambo ya hostels na ofisi. Lakini pia, kila semester wataalamu wanakuja kupiga dawa katika hostels zote za DIT kama mwandishi hana habari huko alipo, amuulize estate manager kwanza kabla ya kukurupuka kuandika upotoshaji huu!

Na ajabu kuona sasa DIT LIBRARY ilivyo sasa baada ya kufanya kazi usiku na mchana, badala ya kumpa pongezi Prof. Ndomba, lakini yeye anamlaumu. Sisi watumishi wengine tulioshiriki kwa vitendo na tumefurahishwa na hili. Tulipitia kila wakati hatua zote n ahata kutoa ushauri bila kujali taaluma zetu. Kila penye malengo lazima tunapaswa kushikamana kama Taasisi. Kama ni sifa kwa Prof. Ndomba ndiyo mwandishi anaona shida, basi sisi kama watumiaji wa library na waumishi, hili tunastahili sifa wote. Kwa kudai kwamba tulitaka ifunguliwe na waziri mkuu, kwetu sisi ndiyo, tulipenda iwe hivyo. Ninaamini Waziri Mkuu naye angependa kufanya hivyo. Namshauri mwandishi aitembelee library hata sasa na ataona tofauti.

Inashangaza kuona haya mafanikio kwa mwandishi ni mabaya tu. Binafsi sina taarifa ya kwamba Prof. Ndomba anafanya DIT kuwa stepping stone, ila kama ikiwapendeza wateuzi, watakapokuwa wamempa nafasi ingine kubwa zaidi, tunaomba wampendekeze mwenye maono kama haya ya Prof. Ndomba.

Nimshauri mwandishi awe anaandika ualisia na siyo maoni elekezi. Mwandishi anasema, Prof. Ndomba anapenda kila kitu kiandikiwe paper. Labda mwandishi ana uelewa finyu katika hili. DIT kuna tofauti kubwa ya watumishi, tofauti ya elimu, umri, lakini pia taaluma. Mwandishi ajue kwamba, hakuna Project yoyote ya EU ambayo inaopatikana bila uandishi wa proposal. Na isingekuwa rahisi kwa kuipata hiyo project ambayo mwandishi anadai kama haina project concept paper. Kwa kifupi paper kuwekwa ili iwe rahisi kueleweka kwa wana taasisi ambao mwisho wake ndiyo watendaji wa hiyo project ni jambo jema kabisa. Mwandishi ajikite kwenye taaluma yake na siyo hizi za kitaaluma ambayo hana uelewa nayo.

Niombe mwandishi ajue kwamba dhana ya Teaching Factory ni la taasisi pamoja na kwamba inasimamiwa pia na Prof. Ndomba. Katika hili, wale wote ambao hawajitumi na walizoea kudanganya katika tawala zilizopita wanaona ni taabu sana. Teaching factory, inatoa mianya kwa taasisi kushirikisha wadau wengine katika kufundisha waalimu na wanafunzi pia. Hatua ya sasa itakuwa ngumu kwa wenye mawazo kama haya ya mwandishi kuelewa. Namsihi ajishirikishe na mkuu wake wa karibu au wadau tulioielewa dhana ajifunze.

Prof. Ndomba amewapa wengi elimu ya miradi ambayo yeye binafsi ameandaa semina ya kufundisha hili na baada ya elimu hiyo, kuna wana taaluma wengi wameisha ingia katika miradi mingi ya ndani na nje. Kwa kujua hiyo potential iliyopo DIT ndiyo maana tunayo mradi wa world bank ambayo DIT inanufaika, TELMS, na mingine mingi ya ndani.

Waalimu wengi waliokuwa wanahangaika kufundisha nje ya taasisi kwa kukosa miradi kwa sasa wanajikita kwenye miradi. Nina Imani mwandishi amejipima ameona hana viwango vya DIT ya sasa na anajihami. Namshauri mwandishi arejee mikakati na ajione kama anafaa kubaki katika miradi mikubwa ya DIT au aanze mradi mwingine wa binafsi aliyoizoea.

Binafsi, nashangazwa kuona Mh. Pro. Ndalichako anahusishwa katika hili eti kwa swala la family friend. Hili nimuombe waziri wetu, mama yetu mpendwa, ufahamu kwamba hili ni wazo la binafsi na siyo ya DIT community!

Niombe wanataasisi tubaki na umoja wetu. Wakuu wetu wasichoke na sisi na kujua kwamba tuna watu wenye mawazo tofauti na changamoto zetu.

Asanteni
Hongera sana kwa majibu mazuri ya kumtetea kiongozi wako.maswali kadhaa ya msingi hujayajibu na hujasema kama yapo au la.
1.Je ni kweli kuna mtu amekaimu zaidi ya miezi 20?..kinyume cha sheria
2.Je watumishi hawapandishwi vyeo licha ya kuwa na vigezo?
3. Watumishi kutopata huduma ya NHIF kwa sababu ya fedha kutopelekwa limetokea?. Hili ndiyo baya zaidi kama ni kweli.
 
Hongera sana kwa majibu mazuri ya kumtetea kiongozi wako.maswali kadhaa ya msingi hujayajibu na hujasema kama yapo au la.
1.Je ni kweli kuna mtu amekaimu zaidi ya miezi 20?..kinyume cha sheria
2.Je watumishi hawapandishwi vyeo licha ya kuwa na vigezo?
3. Watumishi kutopata huduma ya NHIF kwa sababu ya fedha kutopelekwa limetokea?. Hili ndiyo baya zaidi kama ni kweli.


Ndugu Ngika90,
Ninashukuru kwa maswali yako.

Sina sababu ya kumjibia mkuu wa kambi, Prof. Ndomba, hoja hizi maana hajanituma kufanya hivyo, bali mimi nilijibu hoja ambazo zilipitiliza na kumnanga na lawama zilizoelekezwa kwa mkuu huyo hata kwa yale aliyofanya mazuri na angepaswa kupewa pongezi.

Mtazamo wangu unaweza kuwa tofauti wa wengi katika hili kulingana na jinsi tunavyoliona na uelewa pia. Silazimishi wote kukubaliana na mimi pia. Ni matarajio yangu kuwa hoja zinazokinzana zisilete uadui na chuki binafsi.
Kwa msingi huo nirudie tena, sipo kumtetea kiongozi huyo katika kila jambo maana nitakuwa naikosea umma wa watanzania. Na pengine nikawa ninaipotosha umma kwa kujibu nisiyoyajua. Hivyo nitabakia kutetea yale tu ambayo nina uhakika nayo.

1.Je ni kweli kuna mtu amekaimu zaidi ya miezi 20?..kinyume cha sheria
Jibu: SIJUI

Tafakari:
Ukweli, sina jibu la moja kwa moja. Ninaamini hata mwandishi hana jibu hilo. Turejee nafasi ya mkuu wa taasisi katika hili. Nitaanza kwa kuuliza pia “Je ni nani ambaye ana madaraka ya kukaimisha nafasi ya mtumishi huyo kwa miezi yote hiyo? Je ni mkuu wa taasisi peke yake ndiye ana madaraka ya kumbadili kutoka kaimu hadi nafasi husika? Kama ni maamuzi ya ngazi zaidi ya moja, je ni mkuu wa taasisi peke yake ndiye anapaswa kuwajibika katika hilo? Kama kuna wajibu wa mkuu wa taasisi, je kuna uhakika kwamba mkuu wa taasisi hajafanya anayopaswa kufanya? Je kuna uhakika gani kwamba ngazi zingine hazihusiki na hili libakie tu hapa kwa mkuu wa taasisi? Maswali haya yananipokonya haki ya kujibu swali hili maana sijui kama mkuu huyu hajatoa mapendekezo hayo kwa wenye mamlaka husika! Vipi kama ameshatoa mapendekezo yake na mamlaka husika ndiyo bado inaendelea na utaratibu wake? Sina majibu hapa.

2.Je watumishi hawapandishwi vyeo licha ya kuwa na vigezo?

Serikali inayo miongozo ya vigezo vya kupandisha vyeo na mishahara watumishi wa umma! Kwa taasisi kubwa kama DIT yenye idara ya rasilimali watu na uongozi wake kwa ujumla wanajua utaratibu huo na wanaufuata. Hivi itakuingia akilini kwamba RAAWU, THTU na ASA wangekaa kimya kama kungekuwa na ukiukwaji wa haki namna hiyo? RAAWU, THTU na ASA inaongozwa na madaktari tena wenye nafasi zao katika bodi ya taasisi, pia wanayo nafasi na haki ya kuonana na serikali kuu, wangenyamaza? Hili sihitaji akili ya kuambiwa na za upotoshaji kama anavyosema mwandishi.

3. Watumishi kutopata huduma ya NHIF kwa sababu ya fedha kutopelekwa limetokea?. Hili ndiyo baya zaidi kama ni kweli

Nashukuru kwa kuuliza hili la NHIF na huduma zingine.
Hili lilitokana na utendaji pia wa ndani ya NHIF. Kama unavyojua, malipo yote ya taasisi za serikali inalipwa kwa control namba. NHIF walitoa control namba ambayo ilikuwa na kasoro, fedha zilipelekwa, baada ya kutokea tatizo ndiyo wakafuatilia na kurekebisha hilo na huduma ikarejea kama kawaida.

Nikumbushe kwamba hata kwa viongozi wa nyuma kulitokea wakati fedha za mifuko ya pensheni hazikupelekwa kwa takribabi mwaka na zaidi! Hili bado linatesa wastaafu mpaka leo. Tukubaliane wote kwamba kuna mapungufu katika utendaji wa ndani ya taasisi pia. Hapa bado sijajua ni kwa nini pesa kama hizi serikali isizikate moja kwa moja na kuzipeleka kunakohitajika ili kupunguza dhama kama hili. Tutoe pole kwa wale wote waliopata shida na taabu kutokana na tatizo hili la NHIF. Ila ieleweke kwamba kosa analibeba mkuu kama CEO lakini watendaji wanaohusika na hili wa ndani na nje ya taasisi pia wanapaswa kuwajibika. Nina uhakika kwamba mkuu wa taasisi hakukaa kimya katika hilo. Hata jitihada ya kurejesha hali kuwa ya kawaida alihusika kwa hali ya juu.

Pale ambapo hakuna sababu ya kulaumu, bali tusaidiane, tushauriane, ili kuboresha, kurekebisha, na kuimarisha taasisi hii.
 
Ndugu Ngika90,
Ninashukuru kwa maswali yako.

Sina sababu ya kumjibia mkuu wa kambi, Prof. Ndomba, hoja hizi maana hajanituma kufanya hivyo, bali mimi nilijibu hoja ambazo zilipitiliza na kumnanga na lawama zilizoelekezwa kwa mkuu huyo hata kwa yale aliyofanya mazuri na angepaswa kupewa pongezi.

Mtazamo wangu unaweza kuwa tofauti wa wengi katika hili kulingana na jinsi tunavyoliona na uelewa pia. Silazimishi wote kukubaliana na mimi pia. Ni matarajio yangu kuwa hoja zinazokinzana zisilete uadui na chuki binafsi.
Kwa msingi huo nirudie tena, sipo kumtetea kiongozi huyo katika kila jambo maana nitakuwa naikosea umma wa watanzania. Na pengine nikawa ninaipotosha umma kwa kujibu nisiyoyajua. Hivyo nitabakia kutetea yale tu ambayo nina uhakika nayo.

1.Je ni kweli kuna mtu amekaimu zaidi ya miezi 20?..kinyume cha sheria
Jibu: SIJUI

Tafakari:
Ukweli, sina jibu la moja kwa moja. Ninaamini hata mwandishi hana jibu hilo. Turejee nafasi ya mkuu wa taasisi katika hili. Nitaanza kwa kuuliza pia “Je ni nani ambaye ana madaraka ya kukaimisha nafasi ya mtumishi huyo kwa miezi yote hiyo? Je ni mkuu wa taasisi peke yake ndiye ana madaraka ya kumbadili kutoka kaimu hadi nafasi husika? Kama ni maamuzi ya ngazi zaidi ya moja, je ni mkuu wa taasisi peke yake ndiye anapaswa kuwajibika katika hilo? Kama kuna wajibu wa mkuu wa taasisi, je kuna uhakika kwamba mkuu wa taasisi hajafanya anayopaswa kufanya? Je kuna uhakika gani kwamba ngazi zingine hazihusiki na hili libakie tu hapa kwa mkuu wa taasisi? Maswali haya yananipokonya haki ya kujibu swali hili maana sijui kama mkuu huyu hajatoa mapendekezo hayo kwa wenye mamlaka husika! Vipi kama ameshatoa mapendekezo yake na mamlaka husika ndiyo bado inaendelea na utaratibu wake? Sina majibu hapa.

2.Je watumishi hawapandishwi vyeo licha ya kuwa na vigezo?

Serikali inayo miongozo ya vigezo vya kupandisha vyeo na mishahara watumishi wa umma! Kwa taasisi kubwa kama DIT yenye idara ya rasilimali watu na uongozi wake kwa ujumla wanajua utaratibu huo na wanaufuata. Hivi itakuingia akilini kwamba RAAWU, THTU na ASA wangekaa kimya kama kungekuwa na ukiukwaji wa haki namna hiyo? RAAWU, THTU na ASA inaongozwa na madaktari tena wenye nafasi zao katika bodi ya taasisi, pia wanayo nafasi na haki ya kuonana na serikali kuu, wangenyamaza? Hili sihitaji akili ya kuambiwa na za upotoshaji kama anavyosema mwandishi.

3. Watumishi kutopata huduma ya NHIF kwa sababu ya fedha kutopelekwa limetokea?. Hili ndiyo baya zaidi kama ni kweli

Nashukuru kwa kuuliza hili la NHIF na huduma zingine.
Hili lilitokana na utendaji pia wa ndani ya NHIF. Kama unavyojua, malipo yote ya taasisi za serikali inalipwa kwa control namba. NHIF walitoa control namba ambayo ilikuwa na kasoro, fedha zilipelekwa, baada ya kutokea tatizo ndiyo wakafuatilia na kurekebisha hilo na huduma ikarejea kama kawaida.

Nikumbushe kwamba hata kwa viongozi wa nyuma kulitokea wakati fedha za mifuko ya pensheni hazikupelekwa kwa takribabi mwaka na zaidi! Hili bado linatesa wastaafu mpaka leo. Tukubaliane wote kwamba kuna mapungufu katika utendaji wa ndani ya taasisi pia. Hapa bado sijajua ni kwa nini pesa kama hizi serikali isizikate moja kwa moja na kuzipeleka kunakohitajika ili kupunguza dhama kama hili. Tutoe pole kwa wale wote waliopata shida na taabu kutokana na tatizo hili la NHIF. Ila ieleweke kwamba kosa analibeba mkuu kama CEO lakini watendaji wanaohusika na hili wa ndani na nje ya taasisi pia wanapaswa kuwajibika. Nina uhakika kwamba mkuu wa taasisi hakukaa kimya katika hilo. Hata jitihada ya kurejesha hali kuwa ya kawaida alihusika kwa hali ya juu.

Pale ambapo hakuna sababu ya kulaumu, bali tusaidiane, tushauriane, ili kuboresha, kurekebisha, na kuimarisha taasisi hii.
Tatizo ni akili ndogo kujaribu kuongea na akili kubwa. Nikulize swali dogo tu; umeshawahoji hao viongozi wa hizo taasisi za wafanyakazi au umewaza mabo yako ya nyumbani? Kwa taarifa wanaobezwa zaidi na huyo beberu ni hao hao viongozi. Huyu mtu hafai kabisa, tuliongea na hao viongozi na kugundua hakuna mwenye imani nae, kwani hana uchungu na Taasisi wala watumishi katika taasisi. Ananyanyasa mpaka ofisi ya rasilimali watu, kiasi cha kushindwa kufuatilia masuala ya wafanyakazi. Kwanza tusaidie; Hivi hoko alikotoka kulikuwa salama kweli, maana kuna tetesi kwamba alipoondoka huko, waliokuwa nae walifanya sherehe. Huyu jamaa alishawahi pata mafunzo ya uongozi? Hivi alipopelekwa DIT alipitia mchakato gani; maana inasemekana kuna tundu alipitia na kubebwa. Kwa hali ilivyo hapo DIT, ni ya kutia huruma sana. na huyu jama Bebwa hajui hata kwamba baadhi ya idara ziko hatarini kufungwa kabisa, kutokana na kukosa sasilimali watu na vifaa vya kufundishua. Hata viongozi wa Taaluma hawashirikishwi katika maswala ya bajeti na hivyo kupelekea kushindwa kuwalipa walimu wa musimu, na haki nyingine za wafanyakazi.
Inatoa pole wewe, wewe, wewe. Alitakiwa atoe pole yeye, hawezi kwa sababu anafurahia au hajali kabisa. Nasikia anaitwa Mr Not Approved, Mr. Kaachini na anayafurahia hayo majina.
Nasisitiza huko alikotoka alikuwaje?
Je yeye hatakiwi kuona wafanyakazi wake wana amani ya kufanya kazi?
Je yeye anaumia kuona wafanyaka wake hawapandi?
Je kweli ukimuuliza matatizo ya chuo chake anayajua?
Je Jina la DIT linapanda au linashuka?
Je Umahiri wa ufundishaji na taaluma unapanda au unashuka.
Kimsingi hata wanafunzi, wanaogopa uwepo wa huyo mtu, wanahisi hari ya walimu wao imeshuka.

Hizo ni zakutoka jikoni
 
Tena ngoja nitafiti zaidi, maana naona hata vyou kama NIT sasa vimeshaipiku DIT ya toka 1958. Nakule kuna kiongozi ambaya ni tunda la DIT. Huyu wa kutoka huko kwao, naona kama anataka kuua hicho chuo.
 
TUHUMA ZINAZOMHUSU Mkuu wa Taasisi ya Teknolojia Dar es Salaam, Prof. Ndomba HAZINA UKWELI WOWOTE

Nikiwa mmoja wa wadau wa maendeleo ya TANZANIA, nimesikitishwa sana na tuhuma zilizoelekezwa kwa mkuu wa taasisi ya teknolojia ya Dar es Salaam, Prof. Ndomba.

Napenda kuwasilisha hoja kinzani ya habari zinazohusu mkuu wa Taasisi wa teknolojia ya Dar es Salaam zinazolenga kudhoofisha juhudi za mkuu huyo wa Taasisi, Prof. Preskedis Ndomba. Baada ya kutafakari hoja za mwandishi (ambaye siyo academician) na maneno yanayojirudia katika hoja zake, na aina ya maneno anayoyatumia katika lugha zote anazotumia kila mara, nimeridhika kwa asilimia kubwa kuwa ni mmoja wa watumishi wa DIT.

Kurejea hoja yetu:

Tukubaliane kuwa, si jambo la ajabu kuwa na mawazo na hisia zinazokinzana kati ya watu wawili tofauti. Kama kila ushauri ungekuwa unakubaliwa na kiongozi, ni wazi kuwa matokeo ya maamuzi yake yangekuwa yanayotia wasiwasi. Naamini kwamba Prof. Ndomba ni msikivu sana. Ofisi ya Mkuu wa taasisi iko wazi tofauti na baadhi ya watendaji wengine wa taasisi kama hii. Mimi ni shahidi katika hili. Kama ni ushauri wa busara na wenye kukidhi dira ya Taasisi, ningeshangaa kama ningesikia Prof. Ndomba anaukataa. Hizi anazoziita facts, kimsingi hazina proofs hata kidogo, maana hata mfano wa anazoziita facts hajaziweka hapa. Anachotaka ni kuiaminisha umma wa watanzania kwamba yeye ndiye mwenye kuchambua hizo facts bila kuieleza umma anaojaribu kuaminisha.

Kama mwandishi huyu angekuwa anajua sheria kama anavyojinadi, angejua kwamba Prof. Ndomba, ambaye amekuwa katika kitendo cha rasilimali watu kwa muda mrefu katika chuo kikuu cha Dar es Salaam (UDSM) yenye wasomi lukuki, angepata kashfa ya kutishia kufukuza watu. Ifahamike kwamba kila kiongozi anapitia changamoto nyingi hasa ya kuchukuliana na watu mbalimbali, na njia iliyo rasmi ni kupitisha changamoto kama hizo kwenye organs zinazokubalika kwa mujibu wa sheria. Hivyo kwa kupeleka mtumishi kwenye disciplinary committee (kamati ya kinidhamu) ni utaratibu halali tena wa busara ili kumpa mtumishi huyo nafasi ya kufahamu mapungufu yake na ikibidi kukabiliana na tuhuma husika. Mwandishi anataka kuaminisha umma kwamba hiyo kamati pia ina mapungufu! Mwandishi afahamu kwamba, kamati ya nidhamu ndiyo njia njema kumpa nafasi mtumishi kujitetea. Kwa miaka yote ambayo Prof. Ndomba amekaa DIT hakuna mtumishi hata mmoja aliyefukuzwa kazi, pamoja na mapungufu mengi ya watumishi kiutendaji ambayo mkuu huyo anayapata na kuchukuliana nayo. Nirejee kusema tena, kwa utaratibu huo, Prof. Ndomba atakuwa anamtendea mtumishi huyo haki zote na pengine kumsaidia. Hii inaonyesha mwandishi ndiye hana elimu ya sheria za kazi.

Kwa madai ya kujengea hofu wafanyakazi, napenda kumfahamisha mwandishi huyo kwamba, anayejijengea hofu ni yeye mwandishi mwenyewe, maana watumishi wa Taasisi hii ya teknolojia wanajua haki zao ambazo kwenye mabaraza ya wafanyakazi ambayo yanayo uwakilishi wa kila sehemu wanahudhuria. Katika kikao chochote, mwenyekiti anayo madaraka yake. Kama hoja inayojadiliwa haiendani na ajenda ya wakati huo, ni haki ya mwenyekiti kuongoza. Hata kama maamuzi ya mwenyekiti ndiyo yanayopitishwa, mwandishi huyu anaitukana wajumbe wa vikao hivyo kwamba hawawezi kujenga hoja zao kama zinatofautiana na za mwenyekiti. Niweke wazi kwamba, pamoja na ukweli kwamba hoja za wajumbe wa vikao yanaweza kufautiana lakini katibu wa vikao husika anaandika maamuzi ya wajumbe. Na kikao kinachofuata, wajumbe hurejea minutes na kupitisha zote. Mwandishi kwa kumbukumbu zake aiambie umma kwamba ni minutes za kikao kipi cha ndani ya taasisi ambayo kikao kilishindwa kupitisha kwa sababu siyo hoja zao? Mwandishi atupe heshima zetu kama watumishi wa taasisi na siyo watu wanaoweza kuburuzwa kama anavyoiaminisha umma wa watanzania!

Mwandishi anasema Prof. Ndomba anadhalilisha hata wasaidizi wake! Hivi, kwa akili ya kawaida, unaweza kuamini kuwa Prof. Nsimama na Dr. Najat wanaweza kukubali kudhalilika? Unadhani kwamba hawa viongozi wetu wangeshindwa kukemea hilo? Kwa taarifa ni kwamba, hata kama kungekuwa na tofauti zao, ambayo sitarajii kuwa yasiwepo, Prof. Nsimama anajua wapi anaweza kujisemea na siyo kukusubiri wewe uwe msemaji wake.

Mwandishi huyu anaonyesha mapungufu yake katika uelewa wa kisheria. Katika Taasisi hii kuna ASA, THTU, RAAWU, ambao kama wafanyakazi wananyimwa stahiki zao, vyombo hivyo vingewasemea watumishi hao. Kwa mfano, maswala ya extra duty yako kisheria na yanatolewa kwa miongozo na barua husika inayosema hilo. Kwa kumbukumbu zangu, sikumbuki mtumishi yeyote ambaye anakubalika kupata hizo extra duties akakosa. Siyo kila kazi ya msingi inatolewa extra duty. Mfano, mtumishi anayetumika katika kazi yake ya msingi ya ajira hawezi kudai extra duty! Hoja kama hizi zinaletwa katika baraza la wafanyakazi na yanajadiwa na kupatiwa majibu. Nitashangaa kama mkuu wa taasisi anaweza kutumia kodi na pesa za walala hao kumlipa mtumishi extra duty ambaye tayari analipwa mshahara kwa kazi yake ya msingi. Hivi, mwandishi anaposema Prof. Ndomba analipa kiasi kidogo, kiasi kikubwa ni kipi? Tufahamu kwamba kila kazi inayo malipo yake stahiki na halali. Kuna madai mengine hata yanaweza kutengenezwa kwa namna ambayo siyo halali. Kama kiongozi asipokuwa makini anaweza kuipelekea taasisi na serikali hasara. Namshauri mwandishi aulize ofisi zote zinazopitia na kupitisha malipo ajue mambo yanayokuwa huko! Kila malipo yanafanyiwa ukaguzi na lazima yakidhi sifa!

Madai mazito ya kwamba Prof. Ndomba hana utu, na kwamba hajali maslahi ya wafanyakazi ni ya mwandishi mwenyewe na bahati mbaya hajayaweka wazi. Kwa kweli niseme kwamba, kwa aliyekuja DIT miaka ya nyuma na sasa ataona tofauti. Nilidhani hapa kwa kutengeneza pavement za DIT tungeona kama mafanikio na kwamba sasa yale madimbwi yamekwisha. Ajabu hili kwa mwandishi ni mapungufu! Sidhani kama anajua mikakati mikubwa ya taasisi. Kwa maswala ya ofisi kwa watumishi, ni kwamba, kuna miradi mikubwa miwili mikubwa ambayo inaandaa kutolea majibu mambo ya hostels na ofisi. Lakini pia, kila semester wataalamu wanakuja kupiga dawa katika hostels zote za DIT kama mwandishi hana habari huko alipo, amuulize estate manager kwanza kabla ya kukurupuka kuandika upotoshaji huu!

Na ajabu kuona sasa DIT LIBRARY ilivyo sasa baada ya kufanya kazi usiku na mchana, badala ya kumpa pongezi Prof. Ndomba, lakini yeye anamlaumu. Sisi watumishi wengine tulioshiriki kwa vitendo na tumefurahishwa na hili. Tulipitia kila wakati hatua zote n ahata kutoa ushauri bila kujali taaluma zetu. Kila penye malengo lazima tunapaswa kushikamana kama Taasisi. Kama ni sifa kwa Prof. Ndomba ndiyo mwandishi anaona shida, basi sisi kama watumiaji wa library na waumishi, hili tunastahili sifa wote. Kwa kudai kwamba tulitaka ifunguliwe na waziri mkuu, kwetu sisi ndiyo, tulipenda iwe hivyo. Ninaamini Waziri Mkuu naye angependa kufanya hivyo. Namshauri mwandishi aitembelee library hata sasa na ataona tofauti.

Inashangaza kuona haya mafanikio kwa mwandishi ni mabaya tu. Binafsi sina taarifa ya kwamba Prof. Ndomba anafanya DIT kuwa stepping stone, ila kama ikiwapendeza wateuzi, watakapokuwa wamempa nafasi ingine kubwa zaidi, tunaomba wampendekeze mwenye maono kama haya ya Prof. Ndomba.

Nimshauri mwandishi awe anaandika ualisia na siyo maoni elekezi. Mwandishi anasema, Prof. Ndomba anapenda kila kitu kiandikiwe paper. Labda mwandishi ana uelewa finyu katika hili. DIT kuna tofauti kubwa ya watumishi, tofauti ya elimu, umri, lakini pia taaluma. Mwandishi ajue kwamba, hakuna Project yoyote ya EU ambayo inaopatikana bila uandishi wa proposal. Na isingekuwa rahisi kwa kuipata hiyo project ambayo mwandishi anadai kama haina project concept paper. Kwa kifupi paper kuwekwa ili iwe rahisi kueleweka kwa wana taasisi ambao mwisho wake ndiyo watendaji wa hiyo project ni jambo jema kabisa. Mwandishi ajikite kwenye taaluma yake na siyo hizi za kitaaluma ambayo hana uelewa nayo.

Niombe mwandishi ajue kwamba dhana ya Teaching Factory ni la taasisi pamoja na kwamba inasimamiwa pia na Prof. Ndomba. Katika hili, wale wote ambao hawajitumi na walizoea kudanganya katika tawala zilizopita wanaona ni taabu sana. Teaching factory, inatoa mianya kwa taasisi kushirikisha wadau wengine katika kufundisha waalimu na wanafunzi pia. Hatua ya sasa itakuwa ngumu kwa wenye mawazo kama haya ya mwandishi kuelewa. Namsihi ajishirikishe na mkuu wake wa karibu au wadau tulioielewa dhana ajifunze.

Prof. Ndomba amewapa wengi elimu ya miradi ambayo yeye binafsi ameandaa semina ya kufundisha hili na baada ya elimu hiyo, kuna wana taaluma wengi wameisha ingia katika miradi mingi ya ndani na nje. Kwa kujua hiyo potential iliyopo DIT ndiyo maana tunayo mradi wa world bank ambayo DIT inanufaika, TELMS, na mingine mingi ya ndani.

Waalimu wengi waliokuwa wanahangaika kufundisha nje ya taasisi kwa kukosa miradi kwa sasa wanajikita kwenye miradi. Nina Imani mwandishi amejipima ameona hana viwango vya DIT ya sasa na anajihami. Namshauri mwandishi arejee mikakati na ajione kama anafaa kubaki katika miradi mikubwa ya DIT au aanze mradi mwingine wa binafsi aliyoizoea.

Binafsi, nashangazwa kuona Mh. Pro. Ndalichako anahusishwa katika hili eti kwa swala la family friend. Hili nimuombe waziri wetu, mama yetu mpendwa, ufahamu kwamba hili ni wazo la binafsi na siyo ya DIT community!

Niombe wanataasisi tubaki na umoja wetu. Wakuu wetu wasichoke na sisi na kujua kwamba tuna watu wenye mawazo tofauti na changamoto zetu.

Asanteni
Hizi ni hoja zako mwenyewe, hazijatoka kwa wanataasisi.
 
Wengine tulisoma Enzi za Kandolo DIT,Mbosoli TCA na Zuberi MTC


Sent from my iPhone using JamiiForums
[/QUOTE

Zuberi alikuwa mtu mwema sana ila Kilagane na Kunjumu walikuwa makauzu sana kwa wafanyakazi na wanafunzi
 
Sawa Sawa Acha Ituue
Anaweza Kuachia Ngazi Soon!!!
Atatenguliwa Punde, Anywe Funda La Mwisho La Maji
Utafiti unaonyesha 99% ya haya ni kweli. Ila kuna watu kama watatu hivi ni maswaiba wake sana, na wote amewapa nafasi kubwa kuliko uwezo wao, hao hawaelewanani na wenzao.
 
Fanyeni kama Elihuruma na Lumola walimnyosha Profesa mpaka leo hawezi sahau.

Sent using Jamii Forums mobile app
Nilikuwa first year pale daaah lumola ana ushawishi balaa nili join movement jaama ana hoja alisimama kwenye vimbweta pale nikaona lissu huyu hapa..akaja singo akase wewe kijana ww una haribu chuo!!lumola ni hatari anajenga hoja halafu ana ushawishi

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mkuu wa Taasisi ya Teknolojia Dar es Salaam, Prof Ndomba, hana uwezo wa kuiongoza DIT kwa ufanisi na hivyo inapaswa abadilishwe. Sababu kuu za kutaka abadilishwe ni kama zifuatavyo:

Hakubali kushaurika, hasikilizi na ni mbishi: Ukimshauri kama hapendi unachomshauri atakikataa hata haka hana hoja za msingi za kukataa. Kwa vile yeye ni Prof, inatarajiwa akatae kwa hoja na si kwa amri na bila hoja. Hata akishauriwa kitaalam, with facts, kama hapendi, atakataa hata bila sababu za msingi. Wakati mwingine, kabla hajasikiliza hoja yako ya msingi, atakukatatisha na kukuzuia kuendelea kuongea. Kiongozi wa namna hii hafai kuongoza taasisi ya Umma kama DIT

Anawatishia kuwafukuza wafanyakazi wanapokuwa na mawazo tofauti na yake: Wafanyakazi kadhaa wameshapelekwa kwenye disciplinary committee na baadhi amewatishia kuwaandikia barua za kinidhamu. Anaongea na wafanyakazi matured, kama anavyoongea na mtoto mdogo bila staha, anakutisha utafikiri hujui sheria za kazi.

Amwemwandika barua hadi dereva wake eti kwa sababu alienda kumpokea Naibu Katibu Mkuu wizara ya Elimu. Anatengeneza hofu kwa wafanyakazi. Kwa sababu hii, vikao vingi, na maamuzi yanafanyika kama anavyotaka yeye na kwa sababu amewajengea wafanyakazi uoga, na wengi hataki kupoteza muda kubishana nae.

Anadhalilisha wafanyakazi, wakiwemo hata wasaidizi wake: Ikiwa ni pamoja na kuwafokea hata wasaidizi wake mbele ya wafanyakazi wengine, kuwaamurisha wafanyakazi, wakiwemo wakuu ma maidara, kukaa chini hata kama wanatoa hoja za msingi kwenye vikao.

Halipi wafanyakazi stahiki zao ambazo ni halali kisheria: Malipo mbalimbali yakiwemo extra duty, perdiem wakati wa safari za kikazi. Yeye, anaposafiri analipwa stahiki zake zote kisheria. Kuna mfanyakazi aligoma kwenda China kuwapeleka wanafunzi kutembelea chuo kimoja huko China, kwa sababu mkuu alitaka waende bila malipo stahiki, tena wakiwa wanasafiri na wanafunzi. Kila mara Mkuu huwa anautoa huo mfano kama mfano mbaya kwa wafanyakazi.

Wakati wa registration, wafanyakazi wanafanya kazi hadi usiku, lakini wanapoomba stahiki zao, mkuu anaamua kuwalipa kiasi kidogo, bila sababu na wakati wanafunzi wamelipa registration fee. Walimu wa part time, hawalipwi kwa wakati, wanafundisha semester nzima bila malipo. In fact, walimu wa part time wameongezeka kwa sababu walimu wengi walikaa kuchukua extra load teaching load kwa sababu alikataa kuwalipa, hivyo sasa hivyi walimu wa part time wanalipwa zaid ya milioni 400.

Hana utu/ubinadam (hana empath) na hajali maslahi wa wafanyakazi: Watu wanapoenda kumuona kwa shida mbalimbali, anawajibu majibu ya kukatisha tamaa. Ameshindwa kusimami matumizi ya fedha kiasi kwamba pesa za bima ya Afya ya Wafanyakazi huwa wakati mwigine anashindwa kuzipeleka NHIF kwa wakati na kufanya wafanyakazi wafungiwe huduma za bima za afya, kitu hatarishi kwa afya za wafanyakazi. Akilalamikiwa hajai.

Anayapa kipaumbele mambo ya kumpa sifa na si mambo ya kusaidia taasisi kukua kitaaluma: Kujenga pavement wakati kuna walimu wana office mbovu, zina vumbi na viti vibovu. Mabweni ya wanafuzi ni mabovu kupindukia, kunguni wamejaa kila kona. Mfano mwingine ni Library - wakati inakarabitiwa watu walikuwa wanafanya kazi usiku na mchana ili kuzinduliwa na Waziri Mkuu, ambaye hakuweza kuja kwenye uzinduzi wakati wa Graduaration December.

Toka kipindi hicho, kila kitu kilisimama hadi leo. Alikuwa anafanya kazi usiku na mchana ili aje apate sifa kuwa amekarabati library imependeza, na siyo kwa sababu anataka library iishe haraka ili wanafunzi waitumie kusoma kabla semester haijaisha.

Hiyo nguvu ya kutengeneza library usiku na mchana mbona haipo sasa hivi? Mambo ambayo anafanya ni yale yatakayomfanya aonekanane kwa viongozi kuwa anafanya kazi nzuri ili apate sifa. Anatumia DIT kama stepping stone, ili aonekane kuwa yeye ni bora ili apate uteuzi mwingine, na hana lengo la kuijenga taasis kitaaluma. Ndo maana hata kujenga pavement tu, au kukarabati library anamwalika Rais, Waziri Mkuu au Waziri kuja kuifungua/kuizindua!

Hapandishi Wafanyakazi madaraja kwa vigezo vyake binafsi: Kuna urasimu katika kupandisha wafanyakazi madaraja. Pamoja na kuwa wanakuwa wamekidhi vigezo vyote, anasema "hamjakidhi vigezo kama kule kwetu UDSM". Wakati mwingine anasema "Mtakuwa Maprofesa wa DIT", anataka kutumia vigezo vya vyou vingine katika kupandisha madaraja wafanyakazi wa DIT. Kama anaona vigezo vina mapungufu, apendekekeze viwe reviewed?

Anapenda kuabudiwa: Anataka kila kitu lazima aandikiwe paper au kuwe na formal submission - hata mambo ambayo hayahitaji kuandikiwa paper wala hayahitaji formal submission yeye anataka iwe hivyo. Kuna Dr wamekosa kushiriki kwenye Project ya EU kwa sababu alikataa kusaini project agreement kwa kigezo kuwa hajaandikiwa paper kuombwa asaini.

Kwenye hiyo agreement, kuna maelezo yote ya lengo la project, involvement ya taasis na impacts za project. UDSM na vyou vingine vimepata hiyo project and DIT tumekosa kwa sababu ya Tabia ya Mkuu wa Taasisi. Utumie muda kuandika proposal, tena upeteze muda kumwandikia mkuu wa taasis ombi la kukubali kusaini!

Anadanganya viongozi kuhusu dhana ya Teaching Factory: Kwamba kazi zote wanafanya wanafunzi na walimu. Siyo kweli, zaidi ya asilimia 90 ya kazi kwenye miradi ya ujenzi wa pavements na library zimefanywa na vibarua, lakini wakati wa uzinduzi Waziri wa Elimu alidanganywa kuwa kazi yote ya ujenzi wa pavement imefanywa na wanafuzi na wafanyazi, ili kujipatia tu sifa za uongo.

Anamdharau kila mtu - kila mara anasema DIT hamna watu: DIT ni chuo cha ufundi ambacho kina PhD holders wengi kuliko chuo chochote cha ufundi hapa nchini. Wote hao anawadharau, anasema hana mtu wa kufanya naye kazi. Ukweli ni kwamba, DIT kuna potential resource ambayo Mkuu wa Taasisi hajaweza kuitumia kwa sababu ya tabia yake ya kutosikiliza, kutoheshimu mawazo ya watu wengine na kudharau.

Hivyo, wengi wameamua kufanya mambo yao binafsi ya kimaendeleo kuliko kubishana na Mkuu wa Taasisi. In fact, kuna watu ni very bright, intelligent kuliko hata Mkuu mwenyewe na wamesoma vyou bora zaidi kuliko hata chuo alichosoma yeye, lakini bado anapokuwa anaongea nao, anawadharau na hawasikilizi.

Why waste time with such a person! Hii resource, inayolipwa mishara na pesa za walipa kodi, haitumiki ipaswavyo kwa sababu ya Tabia ya Mkuu wa Taasisi. Hii ni hasara kubwa sana kwa Taifa. DIT imetoa viongozi mbalimbali: Prof Mganilwa (Rector NIT), Dr Mgaya (Deputy Rector Academic, NIT), Dr Masika (Aliyekuwa Mkuu wa Chuo Arusha Tech), Deputy Rector wa sasa hivi wa Arusha Tech, Aliyekuwa mkuu wa Chuo cha Maji, Mkuu wa chuo wa sasa wa DMI, nk.

Na bado kuna huge potential ya PhDs. Prof Ndomba haoni hii potential, na hata hataki wasaidizi wake watoke DIT kwa sababu ya dharau. Deputy Principal Academic amekaimu zaidi ya miezi 20 kinyume na sheria, ila hataki awe confirmed kwa sababu zake binafsi.

DIT ni taasisi muhimu sana ya elimu ya ufundi, hasa katika kipindi hiki ambacho tunaelekea katika uchumi wa kati wa viwanda. Taasisi isipoendeshwa kwa weledi, hatutaweza kupata wahitimu wenye elimu ya ufundi itakayowasaidia katika kuendeleza na kusimamia miradi mikubwa inayoendelea kuwekezwa hapa nchini.

Kutokana na tabia yake na namna ambavyo anakiongoza chuo, walimu na wafanyakazi wote wamekata tamaa na wamekuwa na mgomo usio wa wazi. Hii ina madhara makubwa sana kwa wanafunzi, na kiwango na ubora wa elimu ya ufundi itashuka. Na pia potential kubwa ya wafanyakazi wenye PhD inapotea bure, kupelekea hasara kwa Taifa.

Hivyo basi, kwa manufaa ya taifa, Wizara ya Elimu imbadilishe Mkuu wa Taasisi ya DIT, Prof Ndomba. Waziri wa Elimu, Prof Ndalichako, Prof Ndomba ni family friend, umembeba sana. Hata UDSM ali-underperform akapewa sabbatical leave kama njia ya kumtoa kwenye nafasi aliyokuwa akitumikia. Naomba ufungue mbeleko, atambee kwa miguu yake mwenyewe!

Tunaomba uteue kiongozi mwenye weledi na mawazo mtambuka atakayesimamia DIT na kuendeleza elimu ya ufundi hapa nchini na atakaeweza kutumia kwa ufanisi rasmali watu iliyopo DIT kwa manufaa ya taifa!
Mkuu nimeanza kuamini maneno yako, waulize waalimu wa part time wanavyohenya kulipwa, yaani ni nusu mwaka sasa hawajalipwa toka january. Yaani mpaka unawaonea huruma wanakosa hata ari ya kufundisha wanaishia kufuatilia malipo badala ya kufundisha. Imagine kwa miezi 6 hujalipwa hela yako na unatakiwa ufundishe....utaweza? Hata yeye Ndomba ukimwambia akae miezi 6 apige kazi bila kulipwa hatoweza ila ndio hivyo watoto wa watu wanawafanyia hivyo bila kujali athari kwa wanafunzi wanaolipa ada lakini walimu hawalipwi licha ya kuwa pia chuo cha serikali
 
Back
Top Bottom