Rutashubanyuma
JF-Expert Member
- Sep 24, 2010
- 219,470
- 911,174
Wengi hawaelewi ni kwa nini tunataka katiba mpya................ni kwa sababu tunataka raia wote tushiriki kuitunga katiba hiyo kupitia wawakilishi ambao tutawachagua sisi wenyewe kwa kazi hiyo tu...........hatutaki wabunge waturekebishie katiba iliyopo kwa sababu wataongozwa na masilahi yao binafsi.......na hivyo kutelekeza masilahi ya raia wengi wanyonge.................
Huko nyuma CCM walipokuwa wanafanya marekebisho ya katiba ya 13 walijaribu kuwatumia mawaziri katika kuinadi kile walichokiita ni "WHITE PAPER" ambayo ilizingatia masilahi ya viongozi tu..............................kwa kujineemesha wenyewe..........na walipoipitisha walijisifu sana kuwa ilikuwa imeandaliwa na wananchi jambo ambalo halikuwa la kweli hata kidogo........................................
Hili sasa limekuja kugundulika kuwa siyo la kweli hata chembe kwa sababu kiu ya watanzania kujipatia katiba yetu wenyewe badala ya hii iliyopo ya kuwalinda viongozi ipo pale pale...............................................
Sasa katiba mpya tutaipima kuwa hii ni mpya kama itazingatia vigezo vifuatavyo katika kuiandika:-
a) Bunge litapitisha sheria ya kuanzishwa mchakato wa wapigakura kuchagua wawakilishi wao wenyewe kupitia majimbo yao ya uchaguzi na wilaya zao kupata watakaoiandika katiba mpya...........................
b) Katika uwakilishi huo watumishi serikalini wakiwemo wanasiasa watazuiwa kuwemo kama wajumbe wa MKUTANO huo wa KIKATIBA...............................wanasiasa hao ni wale ambao wanashikilia nyadhifa za aina yoyote ndani ya vyama vyao vya siasa au wanashikilia nyadhifa zozote serikalini ikiwemo Bungeni......................
c) MKUTANO huo wa KIKATIBA utaratibiwa shughuli zake na kamati ya wataalamu ambao usaili wake utafanywa na Kamati ya Bunge inayoshughulikia masuala ya sheria na katiba.....na wajumbe hao wateule wa MKUTANO wa KIKATIBA kupitishwa na Bunge baada ya nafasi hizo kuwa zilitangazwa kwenye magazeti na waombaji kujitokeza.................
Mchujo utafanywa na Kamati hiyo ya Bunge tajwa..........................
d) MKUTANO huo wa KIKATIBA unapaswa uwe umemaliza kazi yake katika kipindi cha miaka miwili kwa sababu watapewa mapendekezo mengi kutoka kwa wadau mbalimbali hivyo hawana sababu ya kupoteza muda mwingi katika kukusanya maoni......ingawaje watafanya vikao vya wazi na umma maeneo mbalimbali nchini kukusanya maoni hayo................kwa muda maalumu........................
e) Baada ya kukamilisha mapendekezo yao watayakabidhi kwa MWANASHERIA MkUU ambaye atapaswa ndani ya siku 90 awe amewakilisha mapendekezo ya sheria ya kujadiliwa Bungeni.......na kupitishwa...................
f) Baada ya Bunge kuyapitia na kuyapitisha mapendekezo ya Katiba Mpya wananchi wapewe nafasi ya kupiga kura ya maoni...........hivyo tunahitaji sheria ya kura ya maoni kwa kazi hiyo na nyinginezo zitakazojitokeza..................
g) Iundwe mahakama maalumu ya kusikiliza kero za wananchi juu ya kero za raia zitakazojitokeza wakati mchakato huu wa kuandika katiba mpya unaendelea.................
Haya ni maeneo machache ambayo ninaona yafaa kuwa ni uangalizi wa kuhakikisha serikali iliyopo madarakani haitutupii changa la macho kwa kuiita ni KATIBA MPYA huku ni KATIBA ya viongozi tu kama zile zilizotangulia...................mwenye mchango wa ziada wa kuboresha haya mapendekezo anakaribishwa................
Huko nyuma CCM walipokuwa wanafanya marekebisho ya katiba ya 13 walijaribu kuwatumia mawaziri katika kuinadi kile walichokiita ni "WHITE PAPER" ambayo ilizingatia masilahi ya viongozi tu..............................kwa kujineemesha wenyewe..........na walipoipitisha walijisifu sana kuwa ilikuwa imeandaliwa na wananchi jambo ambalo halikuwa la kweli hata kidogo........................................
Hili sasa limekuja kugundulika kuwa siyo la kweli hata chembe kwa sababu kiu ya watanzania kujipatia katiba yetu wenyewe badala ya hii iliyopo ya kuwalinda viongozi ipo pale pale...............................................
Sasa katiba mpya tutaipima kuwa hii ni mpya kama itazingatia vigezo vifuatavyo katika kuiandika:-
a) Bunge litapitisha sheria ya kuanzishwa mchakato wa wapigakura kuchagua wawakilishi wao wenyewe kupitia majimbo yao ya uchaguzi na wilaya zao kupata watakaoiandika katiba mpya...........................
b) Katika uwakilishi huo watumishi serikalini wakiwemo wanasiasa watazuiwa kuwemo kama wajumbe wa MKUTANO huo wa KIKATIBA...............................wanasiasa hao ni wale ambao wanashikilia nyadhifa za aina yoyote ndani ya vyama vyao vya siasa au wanashikilia nyadhifa zozote serikalini ikiwemo Bungeni......................
c) MKUTANO huo wa KIKATIBA utaratibiwa shughuli zake na kamati ya wataalamu ambao usaili wake utafanywa na Kamati ya Bunge inayoshughulikia masuala ya sheria na katiba.....na wajumbe hao wateule wa MKUTANO wa KIKATIBA kupitishwa na Bunge baada ya nafasi hizo kuwa zilitangazwa kwenye magazeti na waombaji kujitokeza.................
Mchujo utafanywa na Kamati hiyo ya Bunge tajwa..........................
d) MKUTANO huo wa KIKATIBA unapaswa uwe umemaliza kazi yake katika kipindi cha miaka miwili kwa sababu watapewa mapendekezo mengi kutoka kwa wadau mbalimbali hivyo hawana sababu ya kupoteza muda mwingi katika kukusanya maoni......ingawaje watafanya vikao vya wazi na umma maeneo mbalimbali nchini kukusanya maoni hayo................kwa muda maalumu........................
e) Baada ya kukamilisha mapendekezo yao watayakabidhi kwa MWANASHERIA MkUU ambaye atapaswa ndani ya siku 90 awe amewakilisha mapendekezo ya sheria ya kujadiliwa Bungeni.......na kupitishwa...................
f) Baada ya Bunge kuyapitia na kuyapitisha mapendekezo ya Katiba Mpya wananchi wapewe nafasi ya kupiga kura ya maoni...........hivyo tunahitaji sheria ya kura ya maoni kwa kazi hiyo na nyinginezo zitakazojitokeza..................
g) Iundwe mahakama maalumu ya kusikiliza kero za wananchi juu ya kero za raia zitakazojitokeza wakati mchakato huu wa kuandika katiba mpya unaendelea.................
Haya ni maeneo machache ambayo ninaona yafaa kuwa ni uangalizi wa kuhakikisha serikali iliyopo madarakani haitutupii changa la macho kwa kuiita ni KATIBA MPYA huku ni KATIBA ya viongozi tu kama zile zilizotangulia...................mwenye mchango wa ziada wa kuboresha haya mapendekezo anakaribishwa................