Eddo Sambai
JF-Expert Member
- Aug 1, 2013
- 2,351
- 1,780
Tupeni up-dates
Hivi mbona wale waliojitanabaisha kupinga muungano siwasikii tangia Ile hotuba ya Warioba? Nini kimetokea jamani.
Ngoja tusubiri siku ya mkutano hope tutapata live streaming.
Tupeni up-dates
si wako na katiba inasema 'zanzibar ni nji', asa wanataka kudai nji gani tena?
Haya someni hili tangazo linalosambazwa mitandaoni halafu wale waliokuwa wakiniita mchochezi na nina chuki binafsi kwa wazanzibari wajiulize kwanza....
KUMEKUCHA!! SASA MAMLAKA KAMILI NI LAZIMA KAMA HAKUNA 3 NA MBILI HAZIPO WAZANZIBARI WOTE KUKUTANA KIWANJA CHA DEMOKRASIA 26/3/2014
,Haya haya wazanzibari! Kumekucha! La mgambo likilia kuna jambo! Chama cha wananchi CUF kinawatangazia wanachama, wapenzi na wazanzibari wote wa mikoa mitatu ya Unguja, wazalendo na wapenda nchi yao kwa jumla kuhudhuria kwa wingi katika mkutano mkubwa wa hadhara wa aina yake , wa kihistoria utakaofanyika siku ya Jumatano ya tarehe 26/03/2014 katika viwanja vya Demokrasia, Kibanda Maiti kuanzia saa 8:00 barabara za Mchana mpaka saa 12:00 za jioni.
Mgeni rasmi katika Mkutano huo ni Nahodha wa safari ya kuelekea katika mamlaka kamili ya Zanzibar, Simba wa nyika, tishio la vibaraka wauza nchi yetu, kipenzi cha wazanzibari, mwenye uzalendo wa hali ya juu na mapenzi makubwa kwa Zanzibar na wazanzibari, Makamo wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar na Katibu Mkuu wa CUF, Alhakiir Maalim Seif Sharif Hamad. Mkutano utaanza saa 8:00 barabara za mchana mpaka saa 12:00 jioni.
Agenda kuu katika mkutano ni jee safari ya kuelekea mamlaka kamili imefikia wapi? Jee Kikwete, CCM na vibaraka wachache wa Zanzibar wataweza kutuondosha katika mstari wa madai yetu? Jee mpango wa CCM wa kumtanguliza Warioba kwa kuvunja kanuni za Bunge la Katiba kwa lengo la Kumleta Kikwete kuponda mapendekezo ya Warioba utafanikiwa kusitisha safari hii ya wazanzibari? Nini wazanzibari wanapaswa kutarajia?
Maswali yote hayo yatapatiwa majibu pamoja na mambo kadhaa muhimu. Hatumwi mototo!
Shime wazanzibari wote kuhudhuria kwa wingi bila ya kukosa!
TUNATAKA NCHI YETU SASA TUMECHOKA TAFRANI!
HAKI!
KILA LA KHERI JAMAA ZETU, SISI TUMEISHATAYARISHA KARATASI NA KALAMU KUANDIKA TALAKA...
Mbona wazanzibar wa mikoa mitatu ya Unguja?
mambo live yatakuwa hapo! aiye mwana aeleke jiwe, twataka zanzibar yetu nanyi mpate tanganyika yenu, tuishi kwa ujirani mwema, sio kama kikwete atakavyo mwamunyange aje atupindue !!!!
Chuchu FM Live by Dr. Fauz! -
dogo vipi mbona povu jingi.. hoja ni kuwa kwanini wawaachie MAGAIDI YA UAMSHO !!?? mambo ya lema, msigwa na uislamu yameingiaje!!?? punguza ukilaza
mambo live yatakuwa hapo! aiye mwana aeleke jiwe, twataka zanzibar yetu nanyi mpate tanganyika yenu, tuishi kwa ujirani mwema, sio kama kikwete atakavyo mwamunyange aje atupindue !!!!
Chuchu FM Live by Dr. Fauz! -
Yaani kujiita Remote halafu kuweka avatar unakata mauno kuliko mamako inadhihirisha unafanya mchezo wa KIKRISTO
Asante sana Mkuu,
Kwa kupitia kwako Mzenji73 naomba kupitisha Samahani zangu na familia yangu kwa dhambi tuliifanya ya kuwatawala (kuwa koloni la Tanganyika)
tunataka nchi yetu zanzibar - YouTube
Wakuu, nimepita kwenye hiyo Link hapo nusura machozi yanitoke, alafu nikapitia na hotuba ya Lisu jibu nililopata Watanganyika tunalaana ya Wanzanzibar.
Funga ------ wako huo usi waletewe Watu taabu kinembe weweSIO WAZANZIBAR NI WAPEMBA Hivi unajua kuwa Maalim yeye uchu wake Madaraka? unajua kuwa yeye ndiye chanzo cha Aboud Jumbe kutolewa Urais baada ya Maalim seif kumsingizia anataka kuvunja muungano ili mradi urais apate yye?so maalim ni mroho wa madaraka wala si mtetezi wa hii zanzibar.....wapemba ndio wanaomshabikia kwa wingi kwani walimpromise lazima akahutubie umoja wa mataifa Pemba stand up lakin nchi hapati