mi_mdau
JF-Expert Member
- Oct 29, 2010
- 1,104
- 1,476
Kama mnakumbuka magazeti kadhaa ya jumamosi yalikuwa na habari zinazoelezea matumizi mabaya ya takribani bilioni 30 za kitanzania yaliyofanywa na mfuko wa taifa wa bima ya afya (NHIF). Fedha hizo zilitumika vibaya, pamoja na maeneo mengine, kwenye manunuzi yasiyofuata taratibu.
Pia kama mnakumbuka kuna post iliwahi kutolewa humu kipindi cha nyuma kidogo ikimtuhumu Mkurugenzi mkuu wa mfuko huo wa wakati huo ambaye ndiye bado yuko mpaka sasa kwa mambo mbalimbali ikiwemo ufujaji wa fedha, ubabe, kuhamisha wafanyakazi hovyo hovyo, upendeleo usio na tija na mengineyo. Kama malalamko haya yote yasingechukuliwa kwa masihara na wahusika basi pengine fedha hizi na hata nyingine ambazo hatuzijui, na ni zetu sisi wanachama zisingepotea.
Leo hii wanachama tunaendelea kulalamikia kiwango kidogo tunachowekewa kama limit ya kiwango cha matibabu huku baadhi ya watendaji wakiongozwa na Mkurugenzi mkuu huyo asiye na maadili na mwonevu wakifuja fedha zetu kujinufaisha.
Ni wakati sasa kwa wahusika kuchukua hatua sahihi ili pesa zetu wanachama zitunufaishe wengi na si wachache. Mkurugenzi mkuu wa mfuko huo ameshatuhumiwa pia kwa kujichukulia maamuzi yake binafsi bila kufuata ushauri sahihi wa watendaji walio chini yake.
Atafanya anachokiona yeye ni sahihi na chenye manufaa kwake binafsi. Hufikia hatua ya kuwatishia, kuwahamisha, kuwapa onyo na kuwachukia sana wale wote anawaona wanasimamia misingi bora ya kazi na haki na wanaoutakia mema mfuko.
Amekuwa mtu wa kujikomba kwa wakubwa ili aendelee kubaki hapo. Ameufanya mfuko huo kuwa kama mali yake na kusahau kuwa ni mali ya umma. Unatuumiza siye wanachama masikini na umeshachuma vya kutosha sasa utuhurumie na utuachie mfuko wetu watanzania. Tanzania hii inabidi ibadilike kama tunataka maendeleo hasa kwenye sekta hii ya afya.
Mungu msimamia haki anilinde na kunisaidia kwa sina sababu ya kuamini kuwa nimemsingizia mtu. Nawakilisha.
Pia kama mnakumbuka kuna post iliwahi kutolewa humu kipindi cha nyuma kidogo ikimtuhumu Mkurugenzi mkuu wa mfuko huo wa wakati huo ambaye ndiye bado yuko mpaka sasa kwa mambo mbalimbali ikiwemo ufujaji wa fedha, ubabe, kuhamisha wafanyakazi hovyo hovyo, upendeleo usio na tija na mengineyo. Kama malalamko haya yote yasingechukuliwa kwa masihara na wahusika basi pengine fedha hizi na hata nyingine ambazo hatuzijui, na ni zetu sisi wanachama zisingepotea.
Leo hii wanachama tunaendelea kulalamikia kiwango kidogo tunachowekewa kama limit ya kiwango cha matibabu huku baadhi ya watendaji wakiongozwa na Mkurugenzi mkuu huyo asiye na maadili na mwonevu wakifuja fedha zetu kujinufaisha.
Ni wakati sasa kwa wahusika kuchukua hatua sahihi ili pesa zetu wanachama zitunufaishe wengi na si wachache. Mkurugenzi mkuu wa mfuko huo ameshatuhumiwa pia kwa kujichukulia maamuzi yake binafsi bila kufuata ushauri sahihi wa watendaji walio chini yake.
Atafanya anachokiona yeye ni sahihi na chenye manufaa kwake binafsi. Hufikia hatua ya kuwatishia, kuwahamisha, kuwapa onyo na kuwachukia sana wale wote anawaona wanasimamia misingi bora ya kazi na haki na wanaoutakia mema mfuko.
Amekuwa mtu wa kujikomba kwa wakubwa ili aendelee kubaki hapo. Ameufanya mfuko huo kuwa kama mali yake na kusahau kuwa ni mali ya umma. Unatuumiza siye wanachama masikini na umeshachuma vya kutosha sasa utuhurumie na utuachie mfuko wetu watanzania. Tanzania hii inabidi ibadilike kama tunataka maendeleo hasa kwenye sekta hii ya afya.
Mungu msimamia haki anilinde na kunisaidia kwa sina sababu ya kuamini kuwa nimemsingizia mtu. Nawakilisha.