Mkemia Mkuu kitanzini, ahojiwa siku mbili mfululizo na Mamlaka ya Kupambana na Dawa za Kulevya

Ghazwat

JF-Expert Member
Oct 4, 2015
23,718
66,262
5dedb11606e206ab925503beb2468fbe.jpg
Mkemia Mkuu wa Serikali, Profesa Samuel Manyele amehojiwa na Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya(DCEA) kwa siku mbili mfululizo kuanzia juzi kuhusu utoaji kiholela wa vibali vya kuingizia nchini kemikali bashirifu.

Uingizaji na usambazaji wa kemikali bashirifu hufanyika chini ya udhibiti wa hali ya juu wa mamlaka za kitaifa na kimataifa kuzuia uwezekano wa kuchepushiwa katika utengenezaji wa dawa za kulevya aina ya heroin na cocaine.

Taarifa zinasema Profesa Manyele, ambaye juzi alihojiwa kwa siku nzima, alichukuliwa tena jana mchana kwa mahojiano zaidi yaliyofanyika makao makuu ya DCEA, Upanga jijini Dar es salaam.

Hadi tunakwenda mitamboni Profesa Manyele alikuwa bado mikononi mwa DCEA, kwa mujibu wa taarifa ambazo Mwananchi ilizipata, na kuna taarifa zaidi kuwa huenda akaendelea kushikiliwa hadi leo.

Kuhojiwa kwake kwa siku mbili kumetokea sambamba na uamuzi wa Rais Magufuli kumuondoa Mihayo Msikhela kutoka katika nafasi yake ya kamishna wa operesheni wa DCEA, na kumteua Luteni Kanali Frederick Milanzi kushika wadhifa huo.

Juzi, Rais John Magufuli alifanya mazungumzo Ikulu jijini Dar es salaam na Kamishna Mkuu wa DCEA, Rodgers Siyanga aliyemhakikishia kuwa mapambano dhidi ya biashara na matumizi ya dawa za kulevya nchini yanapata mafanikio makubwa.
 
Utawala huu bwana, mpaka leo watu waliochota pesa ya escrow wanapeta mitaani na hawajachukuliwa hatua zozote, mtu katumia taaluma yake wao wanataka kulazimisha lazima iwe hivyo wanavyotaka wao, ila kwa hili nililijua tu, haya sasa wakabadilishe matokeo,
 
Utawala huu bwana, mpaka leo watu waliochota pesa ya escrow wanapeta mitaani na hawajachukuliwa hatua zozote, mtu katumia taaluma yake wao wanataka kulazimisha lazima iwe hivyo wanavyotaka wao, ila kwa hili nililijua tu, haya sasa wakabadilishe matokeo,
Kwa hiyo biashara ya madawa ya kulevya iachwe kwa sababu tu escrow imeachwa
 
wala sijaamaanisha hivyo, ina maana na wao wakamatwe, kwanini mpaka sasa wanatizamwa tu
Kwani Rugemalira na singh waliibia TBC mkuu?
Halafu hujui kinachofanyika nyuma ya pazia,waliochotewa wote kwanza wametemeshwa,na sasa kazi ni kuzisaka zilizofichwa nje ya nchi zirudishwe
 
Kemikali bashirifu na cocaine na heroine wapi na wapi?,au mimi ndo sijui.Navyoelewa zile hutumika kwenye kutengenezea Meth na madawa ya kulevya mengine ya kisasa.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mwandishi asituchanganyie madesa, isijekuwa ameitwa kukomaza timu mpya kwa kuiongezea ma ujuzi harafu mwandishi anaripoti shari, prof Manyele ni taasis

5dedb11606e206ab925503beb2468fbe.jpg
Mkemia Mkuu wa Serikali, Profesa Samuel Manyele amehojiwa na Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya(DCEA) kwa siku mbili mfululizo kuanzia juzi kuhusu utoaji kiholela wa vibali vya kuingizia nchini kemikali bashirifu.

Uingizaji na usambazaji wa kemikali bashirifu hufanyika chini ya udhibiti wa hali ya juu wa mamlaka za kitaifa na kimataifa kuzuia uwezekano wa kuchepushiwa katika utengenezaji wa dawa za kulevya aina ya heroin na cocaine.

Taarifa zinasema Profesa Manyele, ambaye juzi alihojiwa kwa siku nzima, alichukuliwa tena jana mchana kwa mahojiano zaidi yaliyofanyika makao makuu ya DCEA, Upanga jijini Dar es salaam.

Hadi tunakwenda mitamboni Profesa Manyele alikuwa bado mikononi mwa DCEA, kwa mujibu wa taarifa ambazo Mwananchi ilizipata, na kuna taarifa zaidi kuwa huenda akaendelea kushikiliwa hadi leo.

Kuhojiwa kwake kwa siku mbili kumetokea sambamba na uamuzi wa Rais Magufuli kumuondoa Mihayo Msikhela kutoka katika nafasi yake ya kamishna wa operesheni wa DCEA, na kumteua Luteni Kanali Frederick Milanzi kushika wadhifa huo.

Juzi, Rais John Magufuli alifanya mazungumzo Ikulu jijini Dar es salaam na Kamishna Mkuu wa DCEA, Rodgers Siyanga aliyemhakikishia kuwa mapambano dhidi ya biashara na matumizi ya dawa za kulevya nchini yanapata mafanikio makubwa.
imani yangu ni kuwa Mkemia al
 
Back
Top Bottom