Mke wangu mjamzito ila analalamika sana kuumwa na tumbo

TAI DUME

JF-Expert Member
Feb 20, 2014
8,859
23,119
Wakuu habari zenu,

Shemeji au wifi yenu ni mjamzito karibu anafunga mwezi wa tatu. Mimba bado ni changa.

Kuanzia mimba ilipotimiza miezi miwili amekuwa akilalamika sana tumbo kumuuma kwenye kinena. Maumivu yalianza taratibu lakini sasa imefikia hatua mpaka anashindwa kuamka. Wakati mwingine anakuwa anaishiwa nguvu hawezi hata kuamka.

Hospitali tumeenda mara nyingi sana. Anaishia kupimwa ultra sound na kupewa dawa za kutuliza maumivu. Madaktari wanasema mimba ipo salama ila aache kufanya kazi ngumu. Tumekuwa tukijitahidi sana asifanye kazi ngumu hata kunyanyua ndoo ndogo ya maji anajizuia. Lakn haipiti siku tumbo likaacha kumuuma.

Hii itakuwa ni nini? Kama kuna mtu anauzoefu na changamoto kama hiyo tunaomba uzoefu pengine utasaidia.

Muwe na jioni njema.

NB: Hii ni mimba ya mtoto wetu wa pili, ya kwanza haikumsumbua, ya pili iliharibika ilipokuwa na miezi sita. Yaani navurugwa sana.
 
Badilisha hospital Master. Madaktari wanazidiana uwezo, lakini pia hospital Nazo zinazodiana technolojia
 
Badilisha hospital Master. Madaktari wanazidiana uwezo, lakini pia hospital Nazo zinazodiana technolojia
Tumebadilisha kama nne. Last time kuna mtu alituconnect na mtaalam wa magonjwa ya wanawake mwenye jina kubwa tu dr tikaya lakini nae anatoa majibu hayo hayo kwamba aache kufanya kazi ngumu kitu ambacho tumezingatia sana
 
Kaka miezi 3 ya mwanzo ni migumu sana na inataka uangalifu mkubwa maana mimba inaweza kutoka kama hatopata muda wa kupumzika, achukue bed rest mpaka miezi 3 ya mwanzo iishe
 
Tumebadilisha kama nne. Last time kuna mtu alituconnect na mtaalam wa magonjwa ya wanawake mwenye jina kubwa tu dr tikaya lakini nae anatoa majibu hayo hayo kwamba aache kufanya kazi ngumu kitu ambacho tumezingatia sana
Kuna kipindi nilikuwa nasumbuliwa na maumivu ya kwenye korodani. Nilipiga x rays 2 times. Nikafanya Ultra sound like 3 or 4 times, nikakutana na doctors kadhaa,ambao wote walifanana kwenye baadhi ya maelezo na dawa walizopendekeza. Sometime nikawa nawaambia dawa Fulani na fulani nimeshatumia sana ila hakuna changes.

Wanachofanya ni kurecommend aina nyingine ya dawa. Na hizo x ray na Ultra sound zote zilikuwa zinaonesha nipo nomo. Mwisho wa siku nikaamua kumpotezea.

Kuna siku nilienda zahanati Fulani kijijini kwa tatizo jingine tofauti na ilo. Pale nilihudumiwa na clinical officer (sio doctor), after matibabu na kuniandikia dawa za nilichokuwa naumwa wakati huo, story za hapa na pale, wakati tunaagana, akaniuliza "Hauna shida nyingine ya kiafya?" Nikasema Niko vizuri, basi akaniambia nakutakia siku njema.

Ila wakati nataka kutoka ndio nikakumbuka kuhusu Yale maumivu, nikataka kupotezea, maana ukikaangalia kale kazahanati japo local, alaf yule bibi ni C/O sio doctor. Alivyoona nimesita, ndio akaniuliza "Vipi kuna tatizo?". Ikabidi nimuelezee. Akanisikiliza wee, then akaomba anifanyie physical inspection. Mwisho wa siku akaniambia, anahisi utakuwa ugonjwa fulani, ila hospital hawatakiwi kwenda nahisia, hivyo akashauri nikirudi town nikafanyiwe kipimo cha aina fulani maana zahanati yao Haina hicho kipimo. So, aliniandikia kwenye kikaratasi hicho kipimo.

Nilivyorudi town, nikaamua kwenda hospital kuchek. Kufika nikamuelekezea daktari situation yangu yote, lakini pia nikamwambia na recommendation za kipimo alichosema c/o. Daktari nae akanifanyia physical check-up, alaf akasema sawa, kulingana na historia yako, ngoja Tuanze na kipimo cha c/o, japo alihisi ultra sound za mwanzo palikuwa na makosa. Tukaanza na kile kipimo. Huwezi amini, yule c/o alikuwa sahihi.

So, mkuu usichoke kuzunguka. Madokta wanazidiana ujuzi na uzoefu
 
Back
Top Bottom