Mke wangu hanisikii

kaka pole saaaaana, enenda ktk njia iliyonyoofu ukimshukuru mungu kwa kila jambo linalotokea, sababu yeye tu ndiye ajuaye ni kipi kakuepusha nacho na njia ipi atakufungulia uione dunia ktk mwanga maridhawa. piga moyo konde tafuta mke na si mwanamke sababu si wote wanawake uwaonao waweza pewa hadhi ya mke. narudia tena pole sana ndugu yangu.
 
Pole sana,hongera yataka moyo kuoa mwanamke aliyeisha achika kwa mumewe kwanza.......

Nakushauri tulia na jipange vizuri kukabiliana naye.....huo ni mwanzo tu,kama alimuacha wa kwanza akakupata wewe then anajua aweza mpata/kama si anaye mwingine.......

Muombe Mungu akulinde na aondoke salama,huna mke,una mwanamke unayeishi nae chini ya dari moja.......let her go....forgive....move on!!!!

Na kama yuko kwa dada yake na dada yake haoni tatizo,then hata ndugu zake hawana busara au labda hawakutaki......kama unampenda sana mpe muda uone,mshirikishe Mungu na wazazi na ndugu zako pia,watakushauri.


Michele,

Umezungumza kwa busara sana mno mno mno. Huu ndio ushauri huyu ndugu yetu alikua anautafuta.
 
tatizo you did do a background check on her kabla hujamwoa. na kwako anataka talaka huyo mpe awe huru. And learn your lesson.
 
ila siriazz kama ni kweli una uhakika aliitoa mimba yako......then that should be a warning sign,haoni future na wewe!..tunatoa mimba za maboyfriend tu sio waume zetu...mnh????:twitch::twitch::twitch::sick:

MmmmmmmmmMmmmmmmmmMmmmmmmmmmmMmmmmmmmmMmmmmmmMmmmhh.
Hivi mimba za maboyfriend ni watoto??

Anyway mmmmmmmh, tuko tofauti kweli!!!!
 
Huyo amepata Mwingine,apo una jinsi achana nae,na ata ikitokea one day anataka rudi kwako KIMBIZA ni kimeo cha Nguvu.Najua unaweza kuwa UNAMPENDA but piga Moyo Konde usiangalie Nyuma(nnajua ipo siku atakutafuta) wewe mpotezeee mlupo huyo.MALAYA NI MALAYA AFAI KUWA MKE


Daaaaa, mheshimiwa Chipukizi, Onyaneni kwa upole na upendo. Bwana kama wewe ungehesabu maovu yetu ni nani angesimama? Lakini kwako Mungu kuna msamaha ili wewe uogopwe.........., She is not right to this man but she can be right to another man!! No matter what?? Mungu ni wa rehema sana.
 
Mleta tatizo upo wapi kuna maswali members wanataka ufafanuzi ili wakushauri vizuri. Ila avatar yako ni kama vile hua nasikia sikia naye tatizo kama lako vile!
 
nimeoa mwanamke aliyeisha olewa zamani na akaachika, maelewano na masikilizano ndani ya nyumba mwanzo yalikuwa mazuri, ukorofi ukaanza ghafla, akashika mimba akaenda itoa kisha akadai imetoka yenyewe, safari za kwenda kwao zikawa haziishi , na vitu vyake alivyokuja navyo kwangu akawa anahamisha kidogo kidogo kila nnapokuwa sipo.

Nilipomuuliza akadai yeye kuna mtu amemuazima pesa na ili akasome ndio kaamua na yeye amuazime vitu vyake kisha akimaliza kusoma ataenda kuvigomboa, nikamuuliza mbona mimi hukunishirikisha ktk hilo japo vitu ni vyako, basi kuanzia hapo ni makeke tu na hivi niongeapo yuko kwa dada yake yapata wiki na zaidi hakuna ugomvi zaidi ya hilo suala, jana ananiambia uko kimya hali ya kuwa unajua nahitaji kwenda kusoma huku sina hela nikueleweje, NIMEMWAMBIA KAMA UNAJUA MIMI NI MUMEO NAWAJIBIKA KWA HILO NI VIPI UKAE KWA DADA YAKO ...?

NIMEKATA MAWASILIANO NA YEYE KAKAA KIMYA ..........

km jina lako ama kweli HUNA FUNGU.
POLE.
ndo maana aliachika.
na we utamuacha siku si nying
yeye ANAITWA SI RIDHIKI NA WEWE WAITWA SINAFUNGU SO..

SI RIDHIKI +SINA FUNGU=?
 
Ulipomuoa ulichunguza vizuri sababu ya kuachika kwake kwa mume wa kwanza?
Inaelekea ungewezachukua tahadhari mapema shemeji.

Pole sana.
 
naogopa ku mwambia umwache yasije nitokea yaliyonikuta huko nyuma. mwaka juzi mdogo wangu alioa mke kutoka mikoani, sasa alipomuowa yule mke akawa na vitimbi vya ajabu ajabu na mara anadai huyo mme siyo chaguo lake, ndani pakawa hapakaliki na mimi mwenyewe nikaona kweli ndani hakuna maelewano. siku moja mdogo wangu akawapigia wazazi wa yule mke wake akawaelezea kila kitu. wale wazazi walipompigia mtoto wao (mke wa dogo), mwanao akawajibu hivi...kwani baba we ndio umeolewa huku? msinilazimishe kuishi na mtu ambaye mm simtaki. hapo na mm nilikuwa naskia na naona hiyo movie...hapohapo nikachukua uamuzi wa kumshauri dogo amuache. sikujua kuwa dogo alikuwa anaomba ushauri wa kumfukuza mke wake ili hali bado anampenda, wakienda kitandani wanabembelezana. baade dogo kanambia..aah, nimeamua nimsamehe amesema atajirekebisha, ngoja tuone itakuwaje hapo baadae.
then wakaanza kuishi wote na mimi niliyetoa ushauri wa kuachana nikaanza kuona aibu. pamoja na kuwa wanaishi lakini wanaishi maisha ya bora liende..mwanamke ni mchungu kama pilipili, namuonea sana huruma dogo maana ile siyo ndoa ni ndoano.
ndio maana nasema msimshauri amwache huenda anampenda sana na nyie atawashangaa kwa ushauri wenu maamuzi ya mwisho anayo yeye...maana ndiye anayefinywa...
 
Baradhuli mkubwa we. Subiri akutie na vidole ndio utajua.

Mmmm ndo nini hivi jamani.
Upole wenu na ujulikane na kila mtu,

Linda kinywa chako kuliko vyote ulindavyo, maana katika kinywa hutoka laana na baraka.
Kwa kinywa hicho twamuabudu Mungu, na kwa kinywa hiki hiki, twatukana??

Naomba msamaha kwa ajili yake kama amekukosea au kama una bifu nae, msamehe tu,
Maisha yaendelee. God loves you.
 
Second hand unategemea nini??

Not really.................some other second hands are the best mydia................ It all depend on tabia ya mtu. Anawezakuwa wa kwanza kwa maana ya kwamba ni first husband wake na bado ikawa worse.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom