NGOSWE.120
JF-Expert Member
- Jul 9, 2011
- 219
- 233
Ndugu zangu wana JF,
Last edited:
Baba, pole na matatizo!
Nashindwa kuamini, ina maana huyo mchaga wa kimara baruti anaitumia na kuisasambua kiasi cha kuchoka ndani ya mwezi mmoja tu?! Ina maana wewe ulikuwaga unabofya tu?
Natamani ungeangalia nafasi yako kwenye kusimamia nyumba yako.
1 humuulizi mkeo hela yake anapeleka wapi. Je, ulishawahi kuwaza anatumia kiasi gani cha kipato chake kidogo cha ualimu kwa nauli na chakula mchana? Je anachoka kiasi gani kutoka umbali mnaoishi na kibaha? Ulishajaribu walau kumsaidia ahamie karibu ama kupangisha nyumba yenu na nyie kuhamia kibaha ama kibamba ili asiwe mbali sana na kazini?
2 pamoja na mkeo kuwa mnunaji, ulishawahi kuvunja ukimya hata kwa hisani yako? Unasema hujapewa unyumba muda mrefu; ulishawahi kujadili na mkeo na kumjulia khali kama yeye anapata wapi unyumba kama nyumbani haupatikani?
3 Funga kazi ni mkeo kukuambia anataka kuhamia karibu na kazini, chumba na kitanda na godoro tayari na wewe kuona ahueni! Na unaacha mkeo na mwanao kuhamia tena kwa basi mahali usipopajua! Kwa hela usizozijua?!
Pole kwa kukupa dawa chungu! Ukijitathmini ulipokosea utajua jinsi ya kushona na kuweka viraka koti lako.
Huo mtihani mkubwa ndugu yangu. Hapo nakushauri umrudishe tu hapo Dar uishi naye akiendelea kuishi peke yake huko Kibaha ataendelea kukusaliti.