Herbalist Dr MziziMkavu
JF-Expert Member
- Feb 3, 2009
- 42,346
- 33,183
- Thread starter
- #121
Mke wangu alinifanya niwe Mchawi - 51..........
ILIPOISHIA...
Kama haya ninayokuambia unaona nakudanganya, nenda kwa mganga yeyote unayeamini ni makini utaambiwa wewe ndiye uliyemuua baba yako na mwanao.
SASA ENDELEA...
Waganga wengi tumekuwa tunaangalia tatizo bila kuangalia chanzo chake. Matokea yake tunakimbilia kuua tu. Kama ungekuwa umeonewa kweli, ningekufanyia kazi ambayo hakuna yeyote angeingiza mkono, kila mtu asingekuona. Ningekutengeneza ukawa kiza, watu wangekwenda Mashariki na Magharibi wasingekuona.
Mzee wangu nimekusikiliza vizuri na nimekuelewa, utanisaidia vipi?
Nitakusaidia kuyaondoa maisha ya mama na mkeo katika ndizi kisha nitakupa dawa ya kumtuliza mkeo. Nina imani ukiondoka hapa utatulia na mpenzi wako najua unampenda, basi tatizo litakuwa limekwisha ila jiepushe kupenda kuua, damu ya watu wengine ni nuksi unaweza kuandamwa na matatizo na kila mganga akawa halioni kwa vile aliyetenda ameisha kufa.
Mzee wangu nakuapia kwa Mungu sitarudia tena, nikitoka hapa nakuwa kiumbe kipya.
Wapo waganga wanaosifika kwa kuua lakini, mimi nasifika kwa kutibu matatizo kama yako.
Nashukuru mzee wangu, nimejifunza kitu, naamini nitakuwa mwalimu mwema kwa wengine.
Fanya hivyo ili tupunguze mauaji yasiyo na sababu, kazi ya Mungu tumuachie Mungu, tangu nianze uganga sijawahi kuua na sitaua.
Baada ya makubaliano mganga alituomba tukapumzike nje ili kusubiri muda wa kufanya kazi yangu.
Tulitoka kwenda kukaa sehemu ambayo tuliletewa maziwa na viazi vya kuchemsha.
Kwa vile tulikuwa hatujala tangu asubuhi tulikishambulia chakula chote. Baada ya kula tulioneshwa sehemu ya kupumzika kwa vile muda ulikuwa umekwenda sana. Kutokana na uchovu wa safari tulilala mpaka siku ya pili.
****
Baada ya kupatiwa kifungua kinywa cha uji wa maziwa na viazi, tuliitwa kilingeni na kukaribishwa kukaa kwenye ngozi ya chui, mzee Ngugude alichukua ungo na kuuweka mbele yake ambapo ndani ulikuwa na ndizi saba. Mbili zilikuwa zimeoza, mbili zilikuwa zimeiva sana na kuanza kubadilika rangi na kuingia weusi kwa mbali na mbili zilikuwa zimeanza kuiva na moja ilikuwa mbichi kabisa.
Unaziona hizi ndizi? aliniuliza huku akinisogezea ungo mbele yangu.
Ndiyo mzee wangu, nilijibu huku nikizitumbulia macho.
Umegundua nini?
Sijagundua kitu, nilisema huku nikitikisa kichwa kusisitiza.
Basi hii ndiyo familia yako.
Familia yangu? nilishtuka kidogo, japokuwa sikumwelewa.
Ndiyo.
Una maanisha nini kusema hii ndiyo familia yangu?
Ulipokwenda kwa mganga alikueleza nini kuhusiana na ndizi?
Alisema familia yangu imetegewa uhai wake kwenye ndizi.
Basi ndizi zenyewe ndizo hizi, nimefanya kazi kubwa kuzivuta, kwa kweli kazi hii ilikuwa ngumu sana. Nimekesha kwa kazi hii lakini nimefanikiwa. Kabla ya kufanya kitu chochote nilitaka uone ili niifanye hii kazi.
Kwa hiyo hapa panakuwaje?
Kazi iliyopo ni kutoa sumu katika ndizi ili kuyafanya maisha ya familia yako yaondokane na uchawi uliotegwa kwenye ndizi.
Sawa mzee.
Unaona ndizi hizi mbili zilizooza?
Ndiyo.
Basi hizi ndiyo baba yako na mwanao waliofariki, unaziona hizi zilizoiva sana?
Ndiyo naziona.
Hizi ndiyo mkeo na mama yako, si unaona zilikuwa zikiendelea kuiva.
Ndiyo.
Basi zingeoza lazima ungepoteza watu wawili kwa mpigo japo ingechukua muda kutokana na kinga uliyopewa mwisho, unaziona hizi zilizoanza kuiva?
Ndiyo naziona.
Hizi ni za wanao waliobakia, nao walikuwa wakiiva taratibu japo wasingedondoka, lakini wangeoza na kufa kwa mpigo.
Mungu wangu! nilishika kichwa.
Usishike kichwa hapa nakuonesha ubaya wa kisasi, ungeweza kufanikiwa kuongeza idadi ya vifo vya watu, lakini matokeo yake yalikuwa haya, ungeipoteza familia yako na wewe kuwa chizi.
Na hii ndizi mbichi?
Hii ndiyo wewe, ukweli walikushindwa na kukubali wameshindwa. Unaiona hii ndizi pembeni?
Ndiyo.
Unaona nini?
Kuna mistari myeusi kama chale.
Basi haya ni makombora yaliyotumwa kukuozesha. Lakini mwili wako umekuwa imara, kinga uliyofanyiwa chini ya mti mkuu ndiyo iliyokulinda. Kinga yako ingekuwa ya kawaida ya kuchanjwa tu ungebakia jina.
Sasa mzee wangu utanisaidiaje?
Nitahamisha sumu kutoka kwenye miili ya familia yako huku ukishuhudia kwa macho yako.
Alizichukua ndizi mbichi nne na kuziweka kwenye ungo mwingine kisha alichukua dawa ya unga mweupe na kuzimwagia zile ndizi taratibu huku akinuiza maneno anayoyajua. Baada ya muda aliuweka ungo wenye ndizi mbichi pembeni ya ungo wenye ndizi alizosema ndiyo familia yangu.
Unauona ungo huu?
Ndiyo.
Una nini?
Una ndizi mbichi.
Ngapi?
Nne.
Vizuri, alisema huku akichukua ndizi zilizooza na kuzitupa pembeni na ndizi mbichi akaziweka kwenye kikapu.
Sasa nataka hizi ndizi ziwe kama hizi na hizi ziwe kama hizi.
Sawa mzee wangu.
Aliuchukua ungo wenye ndizi mbichi na kuuweka pembeni ya ungo wenye ndizi zilizoiva na kutulia.
Naomba macho yako yasicheze mbali usijesema nimebadilisha ndizi.
Nilitumbulia macho kwenye ungo wenye ndizi mbichi, kila dakika nilishindwa kuelewa, ghafla nilijikuta nikichanganyikiwa baada ya kuona ndizi zimebadilika na kuhamia ungo mwingine.
Umeona nini? mzee Ngugude aliniuliza.
Sielewi.
Huelewi nini?
Naona kama ndizi zimehamia huku.
Hapana hazijahama bali sumu nimeitoa na sasa ndizi zilizokuwa kwenye ungo huu zimerudi katika hali ya ubichi.
Kwa hiyo.
Ubichi huo ni uhai, sasa hivi vifo katika familia yako vitatokea kwa amri ya Mungu na si mkono wa mtu.
Baada ya kusema vile, alichukua unga mweupe na kunyunyizia, alipomaliza alinieleza niende kuoga maji yaliyokuwa na dawa ili kuondoa mikosi ili nijiandae kwa safari.
Nilifanya kama alivyonielekeza baada ya kumaliza zoezi lile, alinipa unga mweupe akaniambia niubwiye kidogo na mwingine niupulize kama kusafisha njia. Nilifanya kama alivyonielekeza kwa kubwiya unga kidogo, unga ulikuwa na ladha kama ya unga wa ngano. Nilipomaliza tulipewa ruksa ya kurudi nyumbani Tanzania.
Je, Kazala kakubaliana na mganga Ngugude? Ili kuyajua yote tukutane baadae
ILIPOISHIA...
Kama haya ninayokuambia unaona nakudanganya, nenda kwa mganga yeyote unayeamini ni makini utaambiwa wewe ndiye uliyemuua baba yako na mwanao.
SASA ENDELEA...
Waganga wengi tumekuwa tunaangalia tatizo bila kuangalia chanzo chake. Matokea yake tunakimbilia kuua tu. Kama ungekuwa umeonewa kweli, ningekufanyia kazi ambayo hakuna yeyote angeingiza mkono, kila mtu asingekuona. Ningekutengeneza ukawa kiza, watu wangekwenda Mashariki na Magharibi wasingekuona.
Mzee wangu nimekusikiliza vizuri na nimekuelewa, utanisaidia vipi?
Nitakusaidia kuyaondoa maisha ya mama na mkeo katika ndizi kisha nitakupa dawa ya kumtuliza mkeo. Nina imani ukiondoka hapa utatulia na mpenzi wako najua unampenda, basi tatizo litakuwa limekwisha ila jiepushe kupenda kuua, damu ya watu wengine ni nuksi unaweza kuandamwa na matatizo na kila mganga akawa halioni kwa vile aliyetenda ameisha kufa.
Mzee wangu nakuapia kwa Mungu sitarudia tena, nikitoka hapa nakuwa kiumbe kipya.
Wapo waganga wanaosifika kwa kuua lakini, mimi nasifika kwa kutibu matatizo kama yako.
Nashukuru mzee wangu, nimejifunza kitu, naamini nitakuwa mwalimu mwema kwa wengine.
Fanya hivyo ili tupunguze mauaji yasiyo na sababu, kazi ya Mungu tumuachie Mungu, tangu nianze uganga sijawahi kuua na sitaua.
Baada ya makubaliano mganga alituomba tukapumzike nje ili kusubiri muda wa kufanya kazi yangu.
Tulitoka kwenda kukaa sehemu ambayo tuliletewa maziwa na viazi vya kuchemsha.
Kwa vile tulikuwa hatujala tangu asubuhi tulikishambulia chakula chote. Baada ya kula tulioneshwa sehemu ya kupumzika kwa vile muda ulikuwa umekwenda sana. Kutokana na uchovu wa safari tulilala mpaka siku ya pili.
****
Baada ya kupatiwa kifungua kinywa cha uji wa maziwa na viazi, tuliitwa kilingeni na kukaribishwa kukaa kwenye ngozi ya chui, mzee Ngugude alichukua ungo na kuuweka mbele yake ambapo ndani ulikuwa na ndizi saba. Mbili zilikuwa zimeoza, mbili zilikuwa zimeiva sana na kuanza kubadilika rangi na kuingia weusi kwa mbali na mbili zilikuwa zimeanza kuiva na moja ilikuwa mbichi kabisa.
Unaziona hizi ndizi? aliniuliza huku akinisogezea ungo mbele yangu.
Ndiyo mzee wangu, nilijibu huku nikizitumbulia macho.
Umegundua nini?
Sijagundua kitu, nilisema huku nikitikisa kichwa kusisitiza.
Basi hii ndiyo familia yako.
Familia yangu? nilishtuka kidogo, japokuwa sikumwelewa.
Ndiyo.
Una maanisha nini kusema hii ndiyo familia yangu?
Ulipokwenda kwa mganga alikueleza nini kuhusiana na ndizi?
Alisema familia yangu imetegewa uhai wake kwenye ndizi.
Basi ndizi zenyewe ndizo hizi, nimefanya kazi kubwa kuzivuta, kwa kweli kazi hii ilikuwa ngumu sana. Nimekesha kwa kazi hii lakini nimefanikiwa. Kabla ya kufanya kitu chochote nilitaka uone ili niifanye hii kazi.
Kwa hiyo hapa panakuwaje?
Kazi iliyopo ni kutoa sumu katika ndizi ili kuyafanya maisha ya familia yako yaondokane na uchawi uliotegwa kwenye ndizi.
Sawa mzee.
Unaona ndizi hizi mbili zilizooza?
Ndiyo.
Basi hizi ndiyo baba yako na mwanao waliofariki, unaziona hizi zilizoiva sana?
Ndiyo naziona.
Hizi ndiyo mkeo na mama yako, si unaona zilikuwa zikiendelea kuiva.
Ndiyo.
Basi zingeoza lazima ungepoteza watu wawili kwa mpigo japo ingechukua muda kutokana na kinga uliyopewa mwisho, unaziona hizi zilizoanza kuiva?
Ndiyo naziona.
Hizi ni za wanao waliobakia, nao walikuwa wakiiva taratibu japo wasingedondoka, lakini wangeoza na kufa kwa mpigo.
Mungu wangu! nilishika kichwa.
Usishike kichwa hapa nakuonesha ubaya wa kisasi, ungeweza kufanikiwa kuongeza idadi ya vifo vya watu, lakini matokeo yake yalikuwa haya, ungeipoteza familia yako na wewe kuwa chizi.
Na hii ndizi mbichi?
Hii ndiyo wewe, ukweli walikushindwa na kukubali wameshindwa. Unaiona hii ndizi pembeni?
Ndiyo.
Unaona nini?
Kuna mistari myeusi kama chale.
Basi haya ni makombora yaliyotumwa kukuozesha. Lakini mwili wako umekuwa imara, kinga uliyofanyiwa chini ya mti mkuu ndiyo iliyokulinda. Kinga yako ingekuwa ya kawaida ya kuchanjwa tu ungebakia jina.
Sasa mzee wangu utanisaidiaje?
Nitahamisha sumu kutoka kwenye miili ya familia yako huku ukishuhudia kwa macho yako.
Alizichukua ndizi mbichi nne na kuziweka kwenye ungo mwingine kisha alichukua dawa ya unga mweupe na kuzimwagia zile ndizi taratibu huku akinuiza maneno anayoyajua. Baada ya muda aliuweka ungo wenye ndizi mbichi pembeni ya ungo wenye ndizi alizosema ndiyo familia yangu.
Unauona ungo huu?
Ndiyo.
Una nini?
Una ndizi mbichi.
Ngapi?
Nne.
Vizuri, alisema huku akichukua ndizi zilizooza na kuzitupa pembeni na ndizi mbichi akaziweka kwenye kikapu.
Sasa nataka hizi ndizi ziwe kama hizi na hizi ziwe kama hizi.
Sawa mzee wangu.
Aliuchukua ungo wenye ndizi mbichi na kuuweka pembeni ya ungo wenye ndizi zilizoiva na kutulia.
Naomba macho yako yasicheze mbali usijesema nimebadilisha ndizi.
Nilitumbulia macho kwenye ungo wenye ndizi mbichi, kila dakika nilishindwa kuelewa, ghafla nilijikuta nikichanganyikiwa baada ya kuona ndizi zimebadilika na kuhamia ungo mwingine.
Umeona nini? mzee Ngugude aliniuliza.
Sielewi.
Huelewi nini?
Naona kama ndizi zimehamia huku.
Hapana hazijahama bali sumu nimeitoa na sasa ndizi zilizokuwa kwenye ungo huu zimerudi katika hali ya ubichi.
Kwa hiyo.
Ubichi huo ni uhai, sasa hivi vifo katika familia yako vitatokea kwa amri ya Mungu na si mkono wa mtu.
Baada ya kusema vile, alichukua unga mweupe na kunyunyizia, alipomaliza alinieleza niende kuoga maji yaliyokuwa na dawa ili kuondoa mikosi ili nijiandae kwa safari.
Nilifanya kama alivyonielekeza baada ya kumaliza zoezi lile, alinipa unga mweupe akaniambia niubwiye kidogo na mwingine niupulize kama kusafisha njia. Nilifanya kama alivyonielekeza kwa kubwiya unga kidogo, unga ulikuwa na ladha kama ya unga wa ngano. Nilipomaliza tulipewa ruksa ya kurudi nyumbani Tanzania.
Je, Kazala kakubaliana na mganga Ngugude? Ili kuyajua yote tukutane baadae