zimwimtu
JF-Expert Member
- Mar 7, 2012
- 1,988
- 1,095
Mr horsepower, u are always a great thinker.Kwa Zamani, wanawake walifunzwa vilivyo kupitia unyago namna ya kuishi na wanaume na kuwavumilia. Na ndiyo sababu ndoa nyingi za zamani zilikuwa zinadumu sana ukilinganishi na hizi za sasa. Ila kwa sasa, kutokana na elimu, exposure waliyopewa wanawake pamoja na mfumo wa haki sawa na zile tamaduni za ki-magharibi, suala la Wanawake kunyamaza kimya na kutii waume zao hata kama kosa ni la mume, hilo halipo na kama lipo basi ni kwa wachache sana.
Mfumo mzima wa sasa kaka mtambuzi, wa mahusiano ya wanandoa ni wewe ukimwaga mboga, mke anamwaga ugali, hapo tunaita ngoma droo!
Natamani kama mila na desturi zetu zingerudi na kufanyiwa maboresho kidogo dada zetu wasinyanyaswe but wapewa mafundisho sahihi ya kutunza na kuheshimu ndoa zao, huku na sisi vidume tukipewa yale mambo ya jandoni basi ndoa zingedumu sana.
Samahani kwa kutoa mchango nje kidogo ya mada, I was just tying to think beyond kidogo ya hii mada ...