Mkapa: Kuna mtu kanizomea?

Tanzanians ooohhh my fellow Tanzanians.
Full of empty words, kwa kuongea tu but when it comes to actions nothing.

Sometimes I see no use of this forum, just full of empty words nasikitika sana.

There is an election at the end of this year lets do something about it. Encourage people to vote you can choose your direction or just encourage people to vote for the right person. Educate people on their rights if you think you know enough instead of filling these pages with EMPTY WORDS!!!!

Lets move forward people!!! or we will never get there.
 
Tizama masikini ya Mungu, wananchi ambao Mkapa aliwahutubia huko Iringa ni wale wale 70%, halafu tizama jinsi standards za uongozi wetu zinavyoshushwa kila siku na hawa maviongozi magoi goi, eti sasa kipimo cha uongozi uliotukuka ni kuzomewa au kutozomewa, halafu kuna mliowahi kutuambia kwamba huyu Mkapa ni Intellectual yaani how low can it get na uongozi wetu?



- Hawa wananchi kwanza wamepewa pilau halafu wakapewa na soda, Mkapa hawezi kwenda mahali na kuanza kudai kwa nini hajazomewa ina maana moja tu kwa wale tunaojua vizuri siasa, ni kwamba kuna mchezo ulifanyika mapema kuhakikisha kwamba hatazomewa, halafu inasikitisha sana Rais mzima wa taifa unajipima uwezo wako wa uongozi kwa kuzomewa au kutozomewa, that is low na ni vyema wananchi wa taifa hili tukaamuka na kuanza kuyazomea like never before, maana sio siri si huyu amesema mwenyewe jinsi anavyoogpa kuzomewa, zomea tu haya tena mwagia hata na michanga ikibidi I mean whatever we have in our disposal

- Hawa kumbe wanaelewa lugha ya kuzomewa tu! Jamani JF tukazane maana sio mchezo kuwaamsha hawa wananchi kama hao juu, A luta Continue mapambano Zomeaa tu!

Respect.


FMEs!
 
Jamani nimesoma maoni yote ya watu humu, kwa kusema kweli na pia tuache unafiki, Mkapa alifanya kazi kubwa sana ambayo huwezi kulinganisha. Mimi namkubali sana jamaa, ukianzia kuinua mapato ya serekali, hazina ya fedha za kigeni BOT, ubinafsishaji ambao umeongeza ajira, barabara, Uwanja mkuu wa Taifa, Daraja kubwa la Rufiji, utendaji kazi masaa mengi ofisini na safari chache za nje, alipambana na mfumuko wa bei (mkate haba Dar ulikua TShs 150,sasa zaidi ya 700, Unga wa sembe ulikua Tshs 250, sasa 900, Daladala ilikua 150 kwa 50 kwa muda mrefu. Amepunguza madeni ya nje
Tumwache apumzike jamaa alifanya kazi kubwa Sana, ila hamna mtu ambaye ni Mungu au Malaika asiye na makosa. Kama swala ni kufanya biashara je ni wangapi wanafanya kwa kupitia migongo ya ndugu zao? Si afadhali huyu alifanya mwenyewe? Mimi nakwambia Tanzania ni kubwa sana, kwa hiyo alifanya mambo mazuri sana jamaa.

Unajua performance ya mtu inabidi uipime kwa kulinganisha na tulikotoka, Mkapa alipokea nchi ikiwa katika hali mbaya sana, vijana walikua hawataki shule, serekali ilikua haina hela, shule ilikua haithaminiki, hospitali dawa kulikua hamna, yeye alipambana kufa na kupona. Vyote tunavyojivunia sasa vimetoka kwenye uongozi wake.
Swala hapa ni kuchambua kwa upeo wa mpana wa kiuchumi na sio kuleta siasa, unayesema mkapa hakufanya kitu je ni nani aliyefanya? Hamna aliyemsafi 100%

Wanaoamini biblia, Yesu aliletewa mwanamke moja mzinzi na watu wengi. Ila kwa sheria ya kiyahudi ilimpasa kupigwa mawe hadi kufa. Yesu akawaambia makutano, kwa yeyote anayejiona hana dhambi yeyote awe wa kwanza kumpiga jiwe, Yesu akainama chini akawa anachora kwa kidole chini, hapo alikua anandika amri za Mungu. Aliponyanyua kichwa hakumkuta mtu hata mmoja, na akamwamuru yule mama aende zake na asirudie tena dhambi. Kwa mfano huu, anayejiona hana dhami yeyote awe wa kwanza kumyooshea mkapa kidole.
Amefanya makubwa sana, tumwache apumzike

alichaguliwa ili asimamie sheria na aliapa kulinda sheria, hayo makubwa unayosema amefanya ndio alistahili ayafanye kwa sababu urais aliomba mwenyewe hakulazimishwa, moja ya majukumu tuliompa ni kuleta maendelea na kupambana na umaskini, ujinga, na maradhi na sio kuiba na kulinda mafisadi.Ni vema sheria ichukue mkono wake na sio kubagua nadhani angekuwa hakimu wa mahakama ya mwanzo amefanya hayo naamini sasa hivi angekuwa keshafungwa siku nyingi. hapo hakuna cha kuoneana huruma na kulindana
 
icon1.gif
Re: Mkapa: Kuna mtu kanizomea?
- Yale yale hawa wanafundishana unakumbuka "..mimi sio mwizi bwana mbona kamati ya Mwakyembe haikuniita kunihoji ninaonewa tu ndio maana ninajiuzulu" remember this?

Respect.


FMEs!
 
Mkapa aliomba urais akapiga kampeni kwamba atafanya abcd.. ikiwa tutampa kura akifanya hatuna haja ya kumshukuru kwasababu ni wajibu wake na sisi wananchi tumemlipa (bila mkopo) above all tumempa pension hadi kifo chake what more did he wants...pamoja na hayo yote ...

Ametuingiza kwenye mikataba mibovu, kuuza nyumba za serikali, kuiba ikulu si kwamba hajaambiwa au ilikuwa bahati mbaya ni kwa jeuri, kiburi na dharau naona bado anaendeleza libenenge la dharau damn!

Nafikiri tuondelee kumzomea kumbe anaumia...maana njia zingine zimegonga mwamba..lol
 
If not in 10 months, then in 2 years; tusishangae itakapogeuka kuwa: "...kuna mtu kanitupia jiwe au yai viza?"
 
Mkapa aliomba urais akapiga kampeni kwamba atafanya abcd.. ikiwa tutampa kura akifanya hatuna haja ya kumshukuru kwasababu ni wajibu wake na sisi wananchi tumemlipa (bila mkopo) above all tumempa pension hadi kifo chake what more did he wants...pamoja na hayo yote ...

Ametuingiza kwenye mikataba mibovu, kuuza nyumba za serikali, kuiba ikulu si kwamba hajaambiwa au ilikuwa bahati mbaya ni kwa jeuri, kiburi na dharau naona bado anaendeleza libenenge la dharau damn!

Nafikiri tuondelee kumzomea kumbe anaumia...maana njia zingine zimegonga mwamba..lol

Hebu linganisha alichoandika Tumaini hapo juu kuhusu Mkapa na hiki alichoandika hapa chini kuhusu Kikwete:

Tumain said:
Ulitaka akulipie ada za shule wanao? ukiwa mchoyo usiwe mroho pia! agh

Shule za msingi na sekondari zimejengwa chini usimamizi na utawala wake

Vyuo vya elimu na vyuo vikuu vimejengwa chini ya usimamizi na utawala wake

Barabara za mikoa, Maji mikoa na DSM zimejengwa chini ya usimamizi wake

Mafisadi wamepelekwa mahakamani chini ya usimamizi na utawala wake

Uhuru wa vyombo vvya habari, uwazi katika shuighuli za serikali (ndio maana malalamiko mengi kwakuwa mmepewa habari enzio hizo ilikuwa sirikali)

Peace, Foreign Direct Invesment increase, employment ..list goes on and on!

Ongea kuhusu double standards
 
Usiombe kutupiwa yai visa! lina harufu mbaya sana!...watu wtaaanza kutupa viatu kama alivyofanyiwa Bush
..iweje sasa, si huku ndiko wanakukaribisha huku? angalia tu mavazi ya waliohudhuria huo mkutano... ni watu wa kutoa sauti za kuzomea hao, au??
 
..iweje sasa, si huku ndiko wanakukaribisha huku? angalia tu mavazi ya waliohudhuria huo mkutano... ni watu wa kutoa sauti za kuzomea hao, au??


Kwani kuna picha?...mbona siioni?...actual watu wa kijijini kwa kweli ukishawapa tuu shiling 50 wameridhika wala hawana tatizo hawakuzomei bali wata kupigia makofi kwa sanaa wanakuona kama mungu....(si umeona ile movie ya god must be crazy??).....
 
Kwani kuna picha?...mbona siioni?...actual watu wa kijijini kwa kweli ukishawapa tuu shiling 50 wameridhika wala hawana tatizo hawakuzomei bali wata kupigia makofi kwa sanaa wanakuona kama mungu....(si umeona ile movie ya god must be crazy??).....

Check hapo juu kwenye bandiko la Mzee ES..
 
We nnkaapa nyamaza babu usitake kuzomewa watz ni wavivu wa kufikiri but nec yenu imekuokoa mazee. Az wais leo speed an stand. Ungelia nawe.usingepata nafasi ya kubwabwaja ovyo ka unavyosema time hii. Waache wenye wivu wa kike na ujinga wao. But its com a day watakuja waso na wivu wa kike watauliza imekuwaje we ntwara wapi na wapi lushoto may be utaelewana nao.sie wavivu wa kufikiri twakaa kimya ka maiti.sitaki kuamini kuwa mtaendelea kuwa shwari hapo baadaye dunia itakapochukuliwa na hao muwaitao wavuta banga japo mlipaswa kujiuliza ni nani aliyewafikisha hapo kama sio nie vin'ganganizi wa utamu wa madaraka.WAJAPANI WALIIKADIDHI JAPAN KWA HAO MUWAITAO WAVUTA BANGI. Japani i wapi leo. Ni suala la muda tu japo usiwepo hata kaburi lako na wenzio yatajafukuliwa.
 
Halisi,
Naifungua makala ya salehe, ili iwe rahisi kutambua ninachosema.
Salehe anamalizia kuwa Muungwana hujibu yale anayotuhumiwa (Angalau).
Salehe UUNGWANA si kuvaa suti na tai, Waswahili husema "Ada ya mja Muungwana ni VITENDO" ukichanganya hicho cha kukaa kimnya na vingine vingi huyo Mtu si Muungwana bali kinyume chake, neno sitaliandika nina hakika wote tunalifahamu, kwa hiyo wakati wa kuliita Chepe kwa jina lake umefika tuache kuliita Koleo.
KATIKATI ya wiki hii kulikuwapo taarifa za kukamatwa kwa vijana wa Wilaya ya Kinondoni, hasa eneo la Kawe, kwa madai ya kumzomea Rais mstaafu wa Awamu ya Tatu, Benjamin Mkapa, kwa kumuita fisadi.
Vijana hao waliona njia sahihi ya kufikisha ujumbe wao kwa Rais mstaafu huyo ni kwa kumzomea na kumwita fisadi, kwa sababu wasingeweza kupata nafasi ya kwenda Seaview kuzungumza naye.
Wangeweza vipi kuipata nafasi hiyo wakati hata vyombo vya habari ambavyo vina ukaribu na mwanasiasa huyo kila kukicha vimekuwa vikitafuta nafasi hiyo bila mafanikio, hivyo kuendelea kuandika matendo ya kifisadi aliyoyafanya kiongozi mstaafu huyo bila upande wa pili kujibu mapigo hayo.
Hivi sasa ni rahisi zaidi kupanga miadi ya Rais Jakaya Kikwete, na kuzungumza naye kuliko kuweka miadi hiyo na Mkapa, ambaye moja kati ya taaluma alizonazo ni uandishi wa habari, ambao unaeleza wazi kuwa mtu maarufu siku zote ni habari.
Habari yoyote iliyojificha ndiyo wananchi wana kiu nayo zaidi kuliko zile za kupikwa au kuandaliwa kwa lengo la kujisafisha au kuficha ukweli fulani ama kwa makusudi au bahati mbaya.
Vijana waliomzomea Mkapa walikuwa sahihi kwani hawaoni kama serikali yao ina juhudi za dhati za kumuwajibisha kiongozi huyo na wenzake waliotumia madaraka yao vibaya kwa kujineemesha.
Mkapa, aitwe nani kwa kuingia mikataba mibovu ya madini, kubariki uuzwaji wa nyumba za serikali, kuongeza mkataba wa TICTS kinyume na taratibu, kutowawajibisha watendaji wake walioelekea kulega lega katika kazi.
Tanesco kila siku hutoa sh milioni 146 kuilipa Kampuni ya Tanpower Resources Limited ambayo inaaminika kuwa inamilikiwa na Mkapa na Daniel Yona, ambao waliingia mkataba wa kinyonyaji wenye lengo la kujinufaisha zaidi.
Watanzania ambao wanaishi vijijini na hawapati huduma ya umeme kutokana na Tanesco kutokuwa na uwezo huo kwa sababu ya kulipa madeni mengi kwa kampuni zilizoingia mikataba mibovu wanamwonaje na watamwitaje Mkapa?
Si yeye na Mramba ndio walioidhinisha ununuaji wa rada ya kijeshi mwaka 2002, ambayo Tanzania ililanguliwa mara mbili ya bei halisi, yote hiyo ikiwa na lengo la kuchukua teni pasenti yao. Bila shaka vijana wale hawakukosea kumwita Mkapa fisadi, si tunaona hata Marekani, Rais George Bush, anaitwa gaidi kutokana na sera ya kuzivamia nchi nyingine kwa kisingizio cha kupingana na ugaidi.
Mbona polisi hawakumkamata Dk. Slaa, Mrema, Mbowe, Mbatia, Kimaro na wengineo wengi wenye nafasi zao katika siasa ya nchi hii walioweka wazi na kutaja majina ya viongozi akiwemo Rais Kikwete wanaotuhumiwa kwa ufisadi.
Je, wanasiasa waliotaja listi ya viongozi mafisadi wapo juu ya sheria na hawaguswi, isipokuwa wale vijana wasio na mbele wala nyuma ndio wapo chini ya sheria na wanagusika kirahisi?
Kama utaratibu huu wa kuanza kuwakamata watu kwa kuwaita majina fulani wenzao umeidhinishwa, basi ni vema ukaanzia kwa viongozi wenyewe, kwani wao ndio vinara wa kuyakuza majina hayo. Kwa mtindo huu kila mtu atakamatwa, maana hakuna hata mtu mmoja asiyetamka neno ufisadi katika nchi hii kwa hivi sasa.
Ingawa taarifa za kukamatwa kwa vijana hao kwa kutenda kosa hilo zimekanushwa na Mkuu wa Polisi wa Mkoa wa Kinondoni, Jamal Rwambow, aliyebainisha kwamba, si kweli kuwa waliwakamata vijana hao kwa kosa hilo, bali inawezekana walifanya kosa jingine.
Alisema ni kawaida jeshi lake hufanya operesheni mbalimbali katika wilaya hiyo kwa lengo la kupunguza vitendo vya kihalifu, hivyo kuna uwezekano vijana hao walikutwa na makosa mengine na watu wakaamua kuyakuza mambo kwa kudai wamekamatwa kwa kosa la kumwita Mkapa fisadi.
Pamoja na majibu hayo, lakini bado kuna taarifa kuwa baada ya kuona jamii itakuja juu endapo itabainika wamekamatwa kwa kosa hilo, Polisi wameamua kubadilisha kibao kuwa waliokamatwa walikutwa na bangi.
Kama taarifa hizo ni za kweli, Polisi wamekosea na dhamira zao zitakuja kuwasuta au kuwashitaki siku za usoni, kwa kufanya uonevu kwa watu walio sahihi kuwaita majina wanayostahili watu fulani.
Mkapa analazimika kuitwa hivyo, kwani hakuna kumbukumbu zinazoonyesha alishawahi kutoa ufafanuzi juu ya tuhuma zinazomkabili ili jamii ijue mbivu na mbichi, bali amekuwa kimya kwa kile kinachotafsiriwa kuwa watu wanaopiga kelele hawamkoseshi usingizi.
Ni kweli hizi ni kelele za chura hazimzuii ng’ombe kunywa maji, lakini kwa muungwana ni lazima angalau angepaza sauti yake juu ya kile kinachosemwa juu yake.
Kulindana na kuoneana aibu kwa watendaji wa serikali hasa wanaofanya vibaya, ndiko kunakowasababisha wananchi kuanza kuwaita viongozi wetu majina ya aibu na ya kudhalilisha.
Serikali isipobadilika kuna kila dalili wananchi siku za usoni wakachukua hatua kali zaidi ya hizo na hata ikiwezekana kuwapiga mawe viongozi wa aina hiyo.
Waswahili walishaweka bayana kuwa usipoziba ufa utajenga kuta.
 
Hapa kuna mambo matatu kuhusu kauli ya huyu mheshimiwa,
1.Kuna uwezokano mkubwa kwamba ameanza kudata.

2.Ameamua kutoa kauli ya kisiasa kama aliyotoa ile siku aliyoulizwa kama anadhani anasifa za uongozi bora.

3.Anaendeleza majaribio yake ya kuona Kama Watanzania bado wanakumbuka maovu aliyoyafanya na reaction zetu.

Kwa ujumla itakuwa ngumu sana kwa Watanzania kusahau aliyoyafanya,Huyu Bwana ameingia kwenye orodha ya Marais wa nchi maskini duniani walioshinikiza kununuliwa Rada na Ndege ya raisi kwa bei ya juu kabisa wakati watu wake wakifa na njaa vijijini,kibaya zaidi pamoja na kupewa onyo na wanasiasa wenye utu kama Clere Shot na Gordon Brown kwa wakati ule bado rada ilinunuliwa kwa dili,imagine mpaka jamaa wameamua kuturudishia chenji...
 
sisi wapiga kura ambao hatuna elimu, njaa, tunajua hujazomewa hata kidogo mheshimiwa Rais Mstaafu, ila tulisikiwa huko Da es salaam vijana pale Kawe walikushangilia saaaaaana ulipokuwa unapita, eti ni kweli Mzee??Tumefarijika sana kwa kutuletea chenji walau kidogo ya keki yetu ya taifa ambayo mligawana na Anna, Yona, Mramba,Balali, Mgonja, Tafadhali mzee naomba uwaambie na wao wasisahau kutuletea hapo walau hata makapi kwani sisi na SISIM ni damu damu
 
Hebu linganisha alichoandika Tumaini hapo juu kuhusu Mkapa na hiki alichoandika hapa chini kuhusu Kikwete:



Ongea kuhusu double standards

Wewe ndi kibaraka kweli, mkapa kafanya mambo list kubwa tu lakini kaiba lazima ajibu hizo tuhuma za uwizi...lol

JK kafanya mambo yake nimeweka kwenye lists nilikuwa najibu hoja za mtu anayesema hajafanya chochote, huo ni uwongo..akiiba atatakiwa kujibu tuhuma zake lol...

Hakuna cha double standards huo upuuzi mimi sijui.. unaujua wewe kwasababu ndiyo kazi yako..
 
Kila awamu ilikuwa na mazuri yake na mabaya ukianzia kwa Mwl Nyerere hadi kwa Kikwete. Hayo madudu yaliyofanywa kwenye miaka ya mwisho ya Ben na wasaidizi wake yasiwe nongwa. Kina Mkono, Bhoke na wengine walifaidika na utawala wa awamu ya kwanza.
Linga nisha yaliyofanyika katika awamu ya nne kwa miaka hii mitatu na halafu jaribu kufikiria hali itakuwaje mpaka tunapofika 2015.


Wewe muibie au mhujumu muajiri wako uangalie kama atakusamehe??? waliomchagua wameibiwa sasa wasilalamike? wasidai haki yao? hatukumtuma kuiba, kulinda mafisadi; kufanya biashara kwenye ile nyumba takatifu aka IKULU,

kama wewe ni muumini nenda kanisani au msikitini then toa sadaka baadae rudi kinyemela ujaribu kuiiba uangalie kama waumini watakusamehe, watu wengine sijui mkoje kinachodaiwa hapa ni haki ambazo hatukutendewa,pesa ziolizotafunwa zingejenga shule ngapi? zingeokoa maisha ya akina mama na watoto wangapi jiulize kwanza hayo then ndo utoe utetezi wako
 
Cha msingi tusihukumu, mimi nimeangalia pamoja na mabaya aliyotenda lakini ametenda azuri mengi sana. Wengi waliopo madarakani hawawezi kuwa perfect 100%. Wewe mwenyewe jiangalie je uko perfect 100%? Mimi nawaeleza mkapa alifanya kazi yake vizuri sana. Kuzomewa sio tatizo hata malaika wanazomewaga na shetani. Sure I'm tell you guys, historia itahukumu, jamaa alichapa mzigo kweli kweli. Sasa tumezongumzia mabaya tu mbona mazuri hatuyasemi? Au dhamira yetu inatusuta? Unajua watu tusizungumze kwa kusikia vyombo vya habari tu, tuzungumzie pia vinavyoweza kuonekana kwa nacho pia. Tusidanganayane Mkapa alipiga mzigo sana, alikua hataki utani na kazi hata kidogo.
Mkombozi,
Hakuna mwenye nguvu ya kuhukumu kati yetu hapa JF, tungekuwa nayo Mkapa angepotelea Gerezani zamani. Na ili iwe Fundisho kwa wengine tungeandika atumikie kifungo chake Taslim hata msamaha wa Rais usimuhusu. Kwa hiyo ikiwa swala la kuhukumiana lipo na hakuna aliye juu ya sheria Chombo cha kazi hiyo tunacho, wanaohusika wafanye kazi zao wamkabidhi Mkapa kwa Mahakama na ikiwa hana Hatia bila shaka itadhihirika.
 
Mkombozi,
Hakuna mwenye nguvu ya kuhukumu kati yetu hapa JF, tungekuwa nayo Mkapa angepotelea Gerezani zamani. Na ili iwe Fundisho kwa wengine tungeandika atumikie kifungo chake Taslim hata msamaha wa Rais usimuhusu. Kwa hiyo ikiwa swala la kuhukumiana lipo na hakuna aliye juu ya sheria Chombo cha kazi hiyo tunacho, wanaohusika wafanye kazi zao wamkabidhi Mkapa kwa Mahakama na ikiwa hana Hatia bila shaka itadhihirika.

Ndugu wanaogopa

Hukumsikia Lowasa, miongoni mwao hakuna msafi hata moja, kikubwa nani atadhubutu kuanza kumfunga paka kengele????? ukianza kuwapeka mahakamani hutawamaliza, naamini wanaambiana wewe bwana ukingia nilinde mie nilimlinda aliyenitangulia, Hatujawa na huo uthubutu hata kidogo ndugu yangu
 
Back
Top Bottom