Jaguar
JF-Expert Member
- Mar 6, 2011
- 3,438
- 1,026
Sitasahau siku moja nilikuwa nakatiza mitaa ya sahare Tanga.Nilikuwa nimeboreka tu kukaa school wikiendi nikaamua kuranda randa mitaa hiyo japokuwa nilikuwa siijui vizuri.Basi katika tembea tembea,nikafuata njia moja pana tu japokuwa sikujua inaelekea wapi.Njiani nilikutana na akina dada watatu wanasukana.Sijui kwa nini niliamue vile,ila niliamua kutowasalimu,nikapita makavu full kuwachunia.Wale akina dada wakaacha kusukana huku wakiniangalia kwa mshangao.Duh!nilipofika mbele nilikutana na bonge la ukuta yaani njia ndo imeishia hapo halafu hakuna njia mbadala ya kuchepuka.No way out,ilibidi nirudi nilikotoka kwa njia ile ile.Nilipowafikia wale akina dada walikuwa hoi kwa kicheko,'hehehee!,haloo!watu bwana,naona hajamkuta mwenyeji wake.Toka siku hiyo nimeshika adabu,salamu muhimu kwa kila ninayemkuta.vipi wewe,umewahi umbuka kwa chochote kile au kushuhudia mtu akiumbuka?,jiachie utupe story yako!