Nguruvi3
Platinum Member
- Jun 21, 2010
- 15,426
- 31,474
Baada ya 'kiza' cha siku kadhaa katika mtandao, tutakuwa na mabandiko yakiangalia uchaguzi uliomalizika
Kwa kutambua hatma ya taifa letu ni yetu sote. Mtazamo wetu upo wazi kujadiliwa kwa maono na maoni mbali mbali
Njia nzuri kama taifa ni kujadiliana, na taifa lenye mijadala lina 'afya' kuliko lile linalotenda kizani
Kwamba, eti kuzungumzia mustakabali wa taifa ni makosa , uhalali ni kupiga makofi na kumeza bila kutafuna
Hatuwezi kuwa jamii iliyokamilika kama tutaendelea na utamaduni wa kufanya mambo gizani, kubinya uhuru wa kujieleza, kunyima fursa ya wananchi kujadiliana kwa amani na viongozi kusikia wananchi wanajadiliana nini
UTANGULIZI
Tumewahi kuzungumzia maana ya uchaguzi. Kwa uchache, ni hatua za kuchagua au kuchaguliwa kushika madaraka ya uongozi iwe katika serikali, taasisi ,jamii n.k.
Tumefanya uchaguzi wa serikali kuu na za mitaa kwa pamoja mwaka huu
Tumechagua wanasiasa watakaounda serikali au uwakilishi bungeni
Matokeo yametangazwa na tume ya uchaguzi na mshindi kupatikana
Jambo moja la kukumbuka, uchaguzi ni mtiririko wa hatua na wala si kupiga kura tu
Kura ni hatua ya kileleni kabla ya kukamilisha uchaguzi kwa hatua ya mwisho ya kutangaza matokeo
Kuanzia kuitishwa uchaguzi, kampeni hadi kupiga kura na kutangaza matokeo, vyote hivyo hufanya uchaguzi ukamilike
Na ili uchaguzi ukamilike ni lazima uwe huru na wa haki (Free and fair) katika hatua zote
Lakini pia,uchaguzi kuwa wa huru na haki (free and fair) haimaanisha uchaguzi huo umetoa mshindi halali
Ili uchaguzi uwe huru na haki, inapaswa kuwepo vionjo (elements), baadhi vikiwa vifuatavyo
1. Integrity ikimaanisha ubora wa kuaminika uliojengwa katika misingi ya maadili ya kiwango cha juu
2. Credible - Unaoweza kuaminika na wenye nguvu ya kushawishi kwamba ulifanyika kama ilivyo namba 1 hapo juu
3 Legitimate- Kwamba upo katika misingi ya kisheria au kanuni kwavile umepata integrity na ni credible
Siku zote wanasiasa wamekimbilia kauli rahisi ya 'uchaguzi ulikuwa huru na haki' je, uchaguzi huo ulikuwa na integrity, ni credible au legitimate? Haya hutayasikia hasa kwa viongozi wa nchi masikini kama zetu
Hivyo, tunatakiwa tujiulize, baada ya miaka 50 ya kujitawala, je uchaguzi 2015 ulikuwa free and fair, ulikuwa na integrity, credibility au legitimacy?
Tutaanza na sehemu ya 1 kati ya V.
Wakati ukifika tutajadiiliana, tunaomba subra kidogo
Inaendelea.......sehemu ya I
Kwa kutambua hatma ya taifa letu ni yetu sote. Mtazamo wetu upo wazi kujadiliwa kwa maono na maoni mbali mbali
Njia nzuri kama taifa ni kujadiliana, na taifa lenye mijadala lina 'afya' kuliko lile linalotenda kizani
Kwamba, eti kuzungumzia mustakabali wa taifa ni makosa , uhalali ni kupiga makofi na kumeza bila kutafuna
Hatuwezi kuwa jamii iliyokamilika kama tutaendelea na utamaduni wa kufanya mambo gizani, kubinya uhuru wa kujieleza, kunyima fursa ya wananchi kujadiliana kwa amani na viongozi kusikia wananchi wanajadiliana nini
UTANGULIZI
Tumewahi kuzungumzia maana ya uchaguzi. Kwa uchache, ni hatua za kuchagua au kuchaguliwa kushika madaraka ya uongozi iwe katika serikali, taasisi ,jamii n.k.
Tumefanya uchaguzi wa serikali kuu na za mitaa kwa pamoja mwaka huu
Tumechagua wanasiasa watakaounda serikali au uwakilishi bungeni
Matokeo yametangazwa na tume ya uchaguzi na mshindi kupatikana
Jambo moja la kukumbuka, uchaguzi ni mtiririko wa hatua na wala si kupiga kura tu
Kura ni hatua ya kileleni kabla ya kukamilisha uchaguzi kwa hatua ya mwisho ya kutangaza matokeo
Kuanzia kuitishwa uchaguzi, kampeni hadi kupiga kura na kutangaza matokeo, vyote hivyo hufanya uchaguzi ukamilike
Na ili uchaguzi ukamilike ni lazima uwe huru na wa haki (Free and fair) katika hatua zote
Lakini pia,uchaguzi kuwa wa huru na haki (free and fair) haimaanisha uchaguzi huo umetoa mshindi halali
Ili uchaguzi uwe huru na haki, inapaswa kuwepo vionjo (elements), baadhi vikiwa vifuatavyo
1. Integrity ikimaanisha ubora wa kuaminika uliojengwa katika misingi ya maadili ya kiwango cha juu
2. Credible - Unaoweza kuaminika na wenye nguvu ya kushawishi kwamba ulifanyika kama ilivyo namba 1 hapo juu
3 Legitimate- Kwamba upo katika misingi ya kisheria au kanuni kwavile umepata integrity na ni credible
Siku zote wanasiasa wamekimbilia kauli rahisi ya 'uchaguzi ulikuwa huru na haki' je, uchaguzi huo ulikuwa na integrity, ni credible au legitimate? Haya hutayasikia hasa kwa viongozi wa nchi masikini kama zetu
Hivyo, tunatakiwa tujiulize, baada ya miaka 50 ya kujitawala, je uchaguzi 2015 ulikuwa free and fair, ulikuwa na integrity, credibility au legitimacy?
Tutaanza na sehemu ya 1 kati ya V.
Wakati ukifika tutajadiiliana, tunaomba subra kidogo
Inaendelea.......sehemu ya I