X-PASTER
JF-Expert Member
- Feb 12, 2007
- 11,610
- 1,810
Dibaji
Yapo maainisho kadhaa tofauti ya neno ujasusi, hata hivyo wataalamu wote wanaafikiana na ainisho jepesi kuwa ni utendaji wa siri chini ya mtandao wa siri uliosukwa kwa namna ya usiri ndani ya taasisi au vitengo maalum vya siri vinavyochunga ulinzi na usalama wa dola, watu, taasisi au biashara kwa njia za siri. Ni shughuli iliyozungukwa na mazingira ya usiri inayogusa maeneo yote ya jamii. Ni mtandao wenye malengo ya kulinda maslahi ya kidola, kibiashara, raia na mali zao dhidi ya mipango na njama za wahalifu au maadui. Ujasusi ni utafutaji wa habari au taarifa muhimu kwa njia za siri juu ya/au dhidi ya shughuli, biashara au maslahi ya kundi, jumuiya, taasisi au kampuni. Kwa ajili hiyo, ujasusi kama fani una mielekeo tofauti ambapo dhana yake kuu ni ulinzi wa kichunguzi.
Uelekeo wa Ujasusi wa upande wa mashariki(ikiongozwa na Urusi) zama za vita baridi, ulikuwa wa kulinda watawala, vyama na itikadi za dola kwa maslahi ya wachache wenye mamlaka. Kutokana na uelekeo huo, lililokuwa shirika la ujasusi la Urusi KGB lilivuma kwa mbinu za kudhibiti njama zote dhidi ya iliyokuwa serikali ya Kikomunisti nchini humo. Ama uelekeo wa ujasusi wa magharibi(ukiongozwa na Marekani) unaelezwa kuwa una shabaha ya kulinda watu na mali zao, nchi na maslahi yake dhidi ya wanaokiuka amani na demokrasia ndani na nje ya mipaka ya dola husika. Kwa ajili hiyo, Marekani ikilitumia shirika lake la CIA imekuwa ikichunguza na kuwahi kuchukua hatua dhidi ya inaowatuhumu kulihujumu Taifa hilo kabla hawajafanya madhara (pre emptive attack).
Mielekeo yote miwili inasisitiza kuwa wajibu wa msingi wa ujasusi unaokusanya ushushushu na ukachero ni kuchungua, kuyachimba, kuyachambua na kuyatathimini mambo kimya kimya, kitaalamu na kiufundi. Shughuli hiyo hufanyika ndani na nje ya mipaka ya dola au biashara fulani hatimaye kushauri hatua kwa ajili ya maslahi ya dola husika na raia wake au biashara husika na wadau wake. Wachambuzi wa mielekeo yote wanazingatia ujasusi wa kiushindani na zimeanzishwa taratibu tofauti kwa ajili ya kuleta ushindani katika shughuli za kijasusi baina ya shirika na shirika au baina ya nchi na nchi (Competitive Intelligence/counter intelligence).
Yapata miaka thelathini tangu uimarishaji ujasusi uanze kinchi, kiserikali, kijumuiya na kibiashara. Chachu ya uimarishaji huo ina mitazamo zaidi ya mmoja ambapo mtazamo mmoja wasemekana unatokana na fikra ya Afisa Usalama chipukizi wa cheo cha chini kwa wakati huo. Kijana huyo alikuwa na mazoea ya kuongea na watu wenye nyadhifa katika shirika moja lililopo jimbo la Midwest nchini Marekani. Wakubwa wa shirika hili walikuwa wakimpa heshima kubwa kijana huyo na hata wakati mwingine walikuwa wakimpa taarifa nyeti za shirika na nchi kwa jumla. Kumbe sababu kubwa ilikuwa ni manufaa ya kumtumia kijana huyu ambaye ndiye kwanza alikuwa anamaliza mafunzo yake, walikuwa wakitimiza vyema matarajio yao. Walikuwa wakipata taarifa na kuzipeleka kwa watoaji wakuu wa maamuzi mjini Washington. Taarifa hizo zilihusu hali na hatua za kiusalama za nchi nyingine pamoja na harakati za mitandao mingine ya kiusalama na mambo mengine yaliyogusa maslahi ya taifa.
Siku moja kijana huyo alishangazwa na jambo moja. Alisikia taarifa ambazo mkuu mmoja alikuwa nazo wakati mkuu mwingine hakuwa nazo na alikuwa akifanya jitihada za kuzitafuta kupitia vyanzo vyake. Baada ya kufuatilia akagundua kuwa hali hiyo ndiyo iliyokuwepo siku zote pale ofisini. Hapakuwa na chombo au mfumo mmoja mahususi wa ukusanyaji wa taarifa za kuwawezesha kufanya maamuzi sahihi. Taarifa nyingi zilizohusiana na mikakati ya wazi na ya siri zilikuwa zikiwafikia wakuu hao lakini hapakuwepo yeyote aliyezikusanya pamoja na kuzifikisha kwa wengine ambao wangeliweza kuzifanyia kazi.
Zaidi ya hivyo, afisa usalama huyo mchanga aligundua hali ya kutokuwepo kwa utaratibu wa kiufundi na uangalifu katika kudhibiti taarifa muhimu ndani ya taasisi hiyo. Hata makampuni mengine makubwa na madogo ambayo kijana huyu aliyafanyia kazi nayo hayakuwa na utaratibu wa kueleweka katika kukusanya, kuchambua na kusambaza taarifa.
Dosari hii ya kimsingi ilidhihiri pia katika maeneo mengi ya Marekani. Ulikuwa kama utamaduni wa wote. MBA (kama kampuni) katika programu zake ilikuwa inapuuzia jambo hili la msingi ambalo ndilo chachu ya utendaji. Kasoro hii ilikuwa imejitokeza katika kipindi hicho cha mapinduzi kwenye mawasiliano nyeti na muhimu. Baadaye ndipo ilipokuja kubainika kwamba kumbe taratibu na mbinu za kijasusi zilizotumiwa na serikali kwa kutekelezwa kwa siri za namna yake pia zingaliweza kutumiwa kwa uwazi katika shughuli nyingine ndani ya jumuiya, taasisi na mashirika ya kibiashara na zingaliweza kuleta manufaa makubwa.
Kijana mwanamapinduzi wa kijasusi aliyeipenda kazi yake, aliamini kuwa alikuwa akitoa mchango muhimu kwa taifa katika fani hiyo ya siri. Mbegu ya fikra aliyopanda kijana huyo ikaleta mabadiliko ya kitaaluma katika uwanda wa ujasusi. Akiwa pamoja na wenziwe waliokuwa na mtazamo kama wake, akaanzisha kazi ya kujenga na kubadili mfumo wa ujasusi ndani ya shughuli za kijumuiya, kidini na kibiashara.
Katika taifa la Marekani msukumo mkubwa wa ujasusi mpya wa ushindani ulikuja kushika kasi katikati ya miaka ya 1980 wakati Marekani ilipokuwa ikishindwa kutamba mbele ya makampuni ya Kijapani katika soko la biashara la kimataifa. Waziri wa Biashara ya Kimataifa na Viwanda wa Japan alipata kutamka katika mkutano na waandishi wa habari wakati fulani mwaka 1985 kwamba:
Japan ilishindwa katika Vita Kuu ya Pili ya Dunia kiasi fulani kwa sababu ya mtandao na mkakati madhubuti uliopangwa na serikali ya Marekani, sasa kwa nini wafanyabiashara wa Marekani wanashindwa kuendelea kuwa na mbinu bora za kijasusi kama zile zilizotumika wakati wa vita ili kuishinda Japan kibiashara? Wajapan wengi wameshindwa kuielewa siri hii kwa nini Marekani inashindwa katika vita hii
Ili kujizatiti kupambana na Japan kibiashara wafanyabishara wa Marekani wakaanza kukusanya nguvu ya ujasusi, waliitwa mabingwa wa ujasusi kutoka serikalini ili wawasaidie katika shughuli za kibishara ambao wangefuma taratibu madhubuti za upataji wa taarifa za kibishara zilizohusiana na Japan. Mmoja wa majasusi wa serikali aliyeshiriki mpango huu alikuwa Robert Galvin, Mkurugenzi Mtendaji wa zamani wa Motorola aliyepata kuwa Mwenyekiti wa Bodi Kuu ya Motorola. Huyu alikuwa mtendaji wa shughuli za serikali wakati huo akishiriki katika vikao vya usukaji wa mfumo mpya wa ujasusi ndani ya jumuiya, mashirika na makampuni ya kibiashara.
Galvin, mbali ya kuwajibika kiserikali, mwanzoni mwa miaka ya 1980 alifanywa kuwa mshauri wa Rais katika Bodi ya Ujasusi wa nje (PFIAB). Bodi hii iliyoanzishwa mwaka 1956 na Rais Eisenhower, ilikuwa ikitoa ushauri kwa Rais juu ya uimarishaji na ufanisi wa kukusanya, kuchambua, kutathmini na kuzifanyia kazi taarifa za siri.
Fani ya Competitive Intelligence (CI) ni mpya katika mawanda ya kibiashara lakini yenye kukua kwa kasi kubwa. Makampuni mengi ya biashara hivi leo yanatilia maanani shughuli hii. Kampuni ya Future Group (TFG), mojawapo ya vitengo vya CI yenyewe hufanya tafiti kila baada ya muda fulani kuonesha mafanikio katika makampuni. Utafiti wa mwaka 1997 ulibaini kuwa asilimia sitini (60%) ya makampuni yalikuwa na mfumo madhubuti wa ujasusi. Hili ni ongezeko la asilimia mbili tokea ulipofanyika utafiti wa awali miaka miwili ya nyuma. Miongoni mwa makampuni yaliyofanyiwa utafiti ni ya utengenezaji ndege, bidhaa za walaji, huduma za fedha, bidhaa za habari, huduma na madawa ya utabibu.
Theluthi mbili ya makampuni hayo yalikuwa na mapato yaliyovuka dola bilioni moja na asilimia 28 yalikuwa na mapato yaliyovuka dola bilioni 10. Yale makampuni yenye mfumo bora wa ujasusi yalifikia kiwango kamili cha ukusanyaji wa taarifa za siri. Cha kuhamasisha ni kwamba makampuni ya bidhaa tumivu (consumer products), yalitia fora kwa kuvuka lengo, yaliweza kufikia kiwango cha asilimia 6.4 cha harakati zao za kijasusi, yakivuka kile cha kawaida cha asilimia 6.1. Makampuni ambayo yalipata kiwango cha chini kabisa yalikuwa ni ya uundaji wa ndege (aerospace) ambayo hayakufikia asilimia 5.6 chini ya kiwango cha kawaida cha upimaji wa shughuli za kijasusi. Kiwango hiki cha chini kilitokana na sababu kadhaa. Makampuni ya uundaji wa ndege yana asilimia kubwa ya maafisa wa zamani wa jeshi katika nafasi zao za uongozi. Wengi miongoni mwao ni weledi wa ujasusi wa kijeshi kwa hiyo walijiamini kuwa wangaliweza kufanya ujasusi inavyotakikana.
Aidha kumekuwa na mtindo wa baadhi ya maafisa wa zamani kuziendesha shughuli za biashara kwa misingi ya kijeshi au kutumia mbinu na taratibu kutoka kada za jeshi hadi kwenye ulimwengu wa biashara. Katika utafiti wa mwaka hadi mwaka, makampuni ya Microsoft na Motorola yalionekana kuwa na programu bora zaidi za kijasusi. Hiyo ndiyo sababu ya msingi, katika vita vya biashara, iliyopelekea makampuni hayo kuitwa tai. Asilimia 17 ya makampuni yakaitwa mbuni, haya ni yale makampuni ambayo hayakudhani kama makampuni mengine yalikuwa yakifanya ujasusi dhidi yao. Na kumithilishwa huko kwa makampuni hayo na mbuni ni kwa kule tabia ya mbuni ya kuficha kichwa mchangani ilhali mwili mzima uko nje!
Lakini jambo lililoshangaza ni kuwa makampuni manane kati ya kumi yalionesha kuwa machapisho waliyoyasoma kama vile magazeti, vyombo vya habari za biashara na majarida ya makampuni ndiyo hasa yaliyokuwa vyanzo vya awali vya taarifa walizokuwa wakizipata. Waajiriwa wa makampuni, wauzaji wa bidhaa na wateja wao ndio hasa walionekana kutoa taarifa muhimu kwa asilimiya 82 ya makampuni. Asilimia 80 ya makampuni yalionesha kupata taarifa zake kupitia mikutano iliyofanywa ndani ya makampuni yenyewe. Asilimia 79 ya makampuni yakaonesha kupata taarifa za siri kutoka kwa wataalamu wa viwanda. Na asilimya 70 ya makampuni yalipata taarifa kutokana na takwimu za kibiashara.
Walipoulizwa (wahusika) ni kipi hasa chanzo muhimu cha taarifa, asilimia 37 ya makampuni yakasema ni wauza bidhaa na wateja, asilima 35 yakasema machapisho waliyoyasoma. Miongoni mwa yale makampuni yenye programu rasmi za kijasusi, asilimia 45 yakaonesha kuwa machapisho waliyoyasoma ndiyo hasa yalikuwa chanzo muhimu cha taarifa. Asilimia 26 ya makampuni yakasema kuwa waajiriwa wa makampuni ndiyo chanzo muhimu cha taarifa. Asilimia 25 yakasema wataalamu wa viwanda ndio chanzo muhimu cha taarifa. Asilimia 24 yakasema mtandao wa Internet ndio chanzo muhimu cha taarifa. Asilimia 18 tu ya makampuni yakasema chanzo muhimu cha taarifa ni mikutano ya makampuni na asilimia 16 tu yakasema takwimu za kibiashara ndiyo chanzo muhimu cha taarifa. Tafiti hizi zinaonesha kuwa japo Competitive Intelligence ndani ya makampuni imejitanua vyema kwa kipindi cha muongo mmoja lakini bado nyenzo, taratibu na mbinu wanazotumia katika harakati zake si za kisasa. Mbinu ya kutumia wafanyakazi na mikutano kupata taarifa muhimu za siri ni ushahidi wa wazi wa kukosekana kwa nyenzo bora na za kisasa za kufanyia kazi. Kuongeza vyanzo vya habari na kudhibiti uvujaji wa taarifa ni kanuni muhimu katika ushindani na mapambano ya kijasusi, iwe katika uwanja wa vita, katika biashara, katika uchumi wa soko na kadhalika.
Uwezo wa kampuni au shirika, jumuiya, taasisi, asasi au kundi la harakati katika mapambano hayo utategemea jinsi linavyoweza kunusa, kukusanya, kuchambua, kusambaza, kudhibiti na kutunza taarifa zake. Mashirika mengi hupanga na kuratibu shughuli za vyombo vya ujasusi na vile vya usalama kwa namna tofauti. Kila kimoja hutekeleza wajibu wake mahususi na kila kimoja hakiwezi kufanikisha kazi zake binafsi bila ya kingine. Ujasusi ni jambo muhimu linalohitajika katika maisha ya mtu binafsi, jumuiya, chama cha siasa, Serikali, vikundi vya harakati na kadhalika. Ni muhimu kuwa na mtandao wa kijasusi wa mtu binafsi, jumuiya, chama, serikali na kadhalika. Hivyo basi ni jambo lisilobudi kujifunza mbinu mbali mbali za kijasusi ima kwa sababu za kiusalama (kujihami), au kwa ajili ya kutafuta mafanikio katika harakati mbali mbali ikiwa ni pamoja na vita, biashara, kampeni za uchaguzi na mengineyo. Hivyo kwa kusoma kitabu hiki utaweza kupata maarifa ya kijasusi, utaelewa misingi ya ujasusi na umuhimu wake na unaweza kujitimizia shughuli zake mbali mbali.
Ujasusi wa ushindani CI, ambao zaidi hutumika katika ulimwengu wa biashara na harakati waweza kuainishwa kama ni utaratibu wa kiufundi wa kupata habari nyeti za biashara na kiharakati kuhusu malengo, wateja, washindani, maadui, teknolojia na mazingira ya jumla ya harakati na biashara. Habari hizi zaweza kutoka kwa yeyote yule au vyanzo vyovyote. Ujasusi unatajwa kama ni taaluma ya pili kongwe duniani; ulikuwepo tangu ulimwengu ulipopambazuka. Mashujaa katika vita vya kale wanasema kuwa ujasusi ulikuwa sehemu muhimu ya mkakati wa vita. Kinachomuwezesha kamanda hodari kushambulia, kuteka na kufanya mambo yasiyo ya kawaida yaliyo nje ya uwezo wa kawaida ni ule ujuzi anaokuwa nao kabla. Na ujuzi huo anaokuwa nao kabla, hautokani na uzoefu au uhodari wa kufanya mahesabu, bali unatokana na taarifa za siri za adui ambazo hupatikana kutoka kwa watu wengine.
Aidha Ujasusi umekuwa sehemu muhimu ya taasisi za kijeshi na kibishara. Ulikuwa, na hadi leo umekuwa bado ni chachu ya harakati za kanisa Katoliki. Punde taarifa zinapopatikana, husambazwa kwa usahihi na kwa wakati kwa watoaji maamuzi wa ngazi zote. CI ni kifupisho cha Competitive Intelligence ambao ni ujasusi unaoshughulika zaidi na harakati za kibiashara ambao unatofautiana kidogo na ule wa kiserikali. CI inafuata taratibu na maadili ya biashara ambayo hayafuatwi na taasisi za ujasusi unaohami serikali. CI haufanywi chini ya kinga ya kidiplomasia bali una lengo zaidi la kuimarisha uhusiano wa kibiashara, kuboresha huduma na kukabili mikiki ya ulimwengu kwa ajili ya kujipatia faida na ufanisi wa shughuli husika. CI kadhalika inatofautiana na ukachero wa kiserikali ambao huweza kukiuka au kupuuza sheria na taratibu za wengine. Hii ni kusema shughuli hii, mara nyingi haitazamwi kwa wema, inaonekana kama isiyo na uhalali wa kimaadili.
Kwa ajili hiyo, udondozi wa kitabu hiki unatoa changamoto kwa wajuzi wa taaluma hiyo, washiriki wake na watu wa kawaida kuonesha iwapo fani ya ujasusi itafanywa kitaalamu inavyoweza kuwa ya muhimu kwa kurejea mifano ya wakongwe hasa Wazayuni walivyoweza kutawala uwanja huo hivyo kudhibiti kila nyanja kwa ajili ya kulinda na kuendeleza maslahi yao sehemu mbali mbali duniani.
Inaendelea Insha'Allah...
Yapo maainisho kadhaa tofauti ya neno ujasusi, hata hivyo wataalamu wote wanaafikiana na ainisho jepesi kuwa ni utendaji wa siri chini ya mtandao wa siri uliosukwa kwa namna ya usiri ndani ya taasisi au vitengo maalum vya siri vinavyochunga ulinzi na usalama wa dola, watu, taasisi au biashara kwa njia za siri. Ni shughuli iliyozungukwa na mazingira ya usiri inayogusa maeneo yote ya jamii. Ni mtandao wenye malengo ya kulinda maslahi ya kidola, kibiashara, raia na mali zao dhidi ya mipango na njama za wahalifu au maadui. Ujasusi ni utafutaji wa habari au taarifa muhimu kwa njia za siri juu ya/au dhidi ya shughuli, biashara au maslahi ya kundi, jumuiya, taasisi au kampuni. Kwa ajili hiyo, ujasusi kama fani una mielekeo tofauti ambapo dhana yake kuu ni ulinzi wa kichunguzi.
Uelekeo wa Ujasusi wa upande wa mashariki(ikiongozwa na Urusi) zama za vita baridi, ulikuwa wa kulinda watawala, vyama na itikadi za dola kwa maslahi ya wachache wenye mamlaka. Kutokana na uelekeo huo, lililokuwa shirika la ujasusi la Urusi KGB lilivuma kwa mbinu za kudhibiti njama zote dhidi ya iliyokuwa serikali ya Kikomunisti nchini humo. Ama uelekeo wa ujasusi wa magharibi(ukiongozwa na Marekani) unaelezwa kuwa una shabaha ya kulinda watu na mali zao, nchi na maslahi yake dhidi ya wanaokiuka amani na demokrasia ndani na nje ya mipaka ya dola husika. Kwa ajili hiyo, Marekani ikilitumia shirika lake la CIA imekuwa ikichunguza na kuwahi kuchukua hatua dhidi ya inaowatuhumu kulihujumu Taifa hilo kabla hawajafanya madhara (pre emptive attack).
Mielekeo yote miwili inasisitiza kuwa wajibu wa msingi wa ujasusi unaokusanya ushushushu na ukachero ni kuchungua, kuyachimba, kuyachambua na kuyatathimini mambo kimya kimya, kitaalamu na kiufundi. Shughuli hiyo hufanyika ndani na nje ya mipaka ya dola au biashara fulani hatimaye kushauri hatua kwa ajili ya maslahi ya dola husika na raia wake au biashara husika na wadau wake. Wachambuzi wa mielekeo yote wanazingatia ujasusi wa kiushindani na zimeanzishwa taratibu tofauti kwa ajili ya kuleta ushindani katika shughuli za kijasusi baina ya shirika na shirika au baina ya nchi na nchi (Competitive Intelligence/counter intelligence).
Yapata miaka thelathini tangu uimarishaji ujasusi uanze kinchi, kiserikali, kijumuiya na kibiashara. Chachu ya uimarishaji huo ina mitazamo zaidi ya mmoja ambapo mtazamo mmoja wasemekana unatokana na fikra ya Afisa Usalama chipukizi wa cheo cha chini kwa wakati huo. Kijana huyo alikuwa na mazoea ya kuongea na watu wenye nyadhifa katika shirika moja lililopo jimbo la Midwest nchini Marekani. Wakubwa wa shirika hili walikuwa wakimpa heshima kubwa kijana huyo na hata wakati mwingine walikuwa wakimpa taarifa nyeti za shirika na nchi kwa jumla. Kumbe sababu kubwa ilikuwa ni manufaa ya kumtumia kijana huyu ambaye ndiye kwanza alikuwa anamaliza mafunzo yake, walikuwa wakitimiza vyema matarajio yao. Walikuwa wakipata taarifa na kuzipeleka kwa watoaji wakuu wa maamuzi mjini Washington. Taarifa hizo zilihusu hali na hatua za kiusalama za nchi nyingine pamoja na harakati za mitandao mingine ya kiusalama na mambo mengine yaliyogusa maslahi ya taifa.
Siku moja kijana huyo alishangazwa na jambo moja. Alisikia taarifa ambazo mkuu mmoja alikuwa nazo wakati mkuu mwingine hakuwa nazo na alikuwa akifanya jitihada za kuzitafuta kupitia vyanzo vyake. Baada ya kufuatilia akagundua kuwa hali hiyo ndiyo iliyokuwepo siku zote pale ofisini. Hapakuwa na chombo au mfumo mmoja mahususi wa ukusanyaji wa taarifa za kuwawezesha kufanya maamuzi sahihi. Taarifa nyingi zilizohusiana na mikakati ya wazi na ya siri zilikuwa zikiwafikia wakuu hao lakini hapakuwepo yeyote aliyezikusanya pamoja na kuzifikisha kwa wengine ambao wangeliweza kuzifanyia kazi.
Zaidi ya hivyo, afisa usalama huyo mchanga aligundua hali ya kutokuwepo kwa utaratibu wa kiufundi na uangalifu katika kudhibiti taarifa muhimu ndani ya taasisi hiyo. Hata makampuni mengine makubwa na madogo ambayo kijana huyu aliyafanyia kazi nayo hayakuwa na utaratibu wa kueleweka katika kukusanya, kuchambua na kusambaza taarifa.
Dosari hii ya kimsingi ilidhihiri pia katika maeneo mengi ya Marekani. Ulikuwa kama utamaduni wa wote. MBA (kama kampuni) katika programu zake ilikuwa inapuuzia jambo hili la msingi ambalo ndilo chachu ya utendaji. Kasoro hii ilikuwa imejitokeza katika kipindi hicho cha mapinduzi kwenye mawasiliano nyeti na muhimu. Baadaye ndipo ilipokuja kubainika kwamba kumbe taratibu na mbinu za kijasusi zilizotumiwa na serikali kwa kutekelezwa kwa siri za namna yake pia zingaliweza kutumiwa kwa uwazi katika shughuli nyingine ndani ya jumuiya, taasisi na mashirika ya kibiashara na zingaliweza kuleta manufaa makubwa.
Kijana mwanamapinduzi wa kijasusi aliyeipenda kazi yake, aliamini kuwa alikuwa akitoa mchango muhimu kwa taifa katika fani hiyo ya siri. Mbegu ya fikra aliyopanda kijana huyo ikaleta mabadiliko ya kitaaluma katika uwanda wa ujasusi. Akiwa pamoja na wenziwe waliokuwa na mtazamo kama wake, akaanzisha kazi ya kujenga na kubadili mfumo wa ujasusi ndani ya shughuli za kijumuiya, kidini na kibiashara.
Katika taifa la Marekani msukumo mkubwa wa ujasusi mpya wa ushindani ulikuja kushika kasi katikati ya miaka ya 1980 wakati Marekani ilipokuwa ikishindwa kutamba mbele ya makampuni ya Kijapani katika soko la biashara la kimataifa. Waziri wa Biashara ya Kimataifa na Viwanda wa Japan alipata kutamka katika mkutano na waandishi wa habari wakati fulani mwaka 1985 kwamba:
Japan ilishindwa katika Vita Kuu ya Pili ya Dunia kiasi fulani kwa sababu ya mtandao na mkakati madhubuti uliopangwa na serikali ya Marekani, sasa kwa nini wafanyabiashara wa Marekani wanashindwa kuendelea kuwa na mbinu bora za kijasusi kama zile zilizotumika wakati wa vita ili kuishinda Japan kibiashara? Wajapan wengi wameshindwa kuielewa siri hii kwa nini Marekani inashindwa katika vita hii
Ili kujizatiti kupambana na Japan kibiashara wafanyabishara wa Marekani wakaanza kukusanya nguvu ya ujasusi, waliitwa mabingwa wa ujasusi kutoka serikalini ili wawasaidie katika shughuli za kibishara ambao wangefuma taratibu madhubuti za upataji wa taarifa za kibishara zilizohusiana na Japan. Mmoja wa majasusi wa serikali aliyeshiriki mpango huu alikuwa Robert Galvin, Mkurugenzi Mtendaji wa zamani wa Motorola aliyepata kuwa Mwenyekiti wa Bodi Kuu ya Motorola. Huyu alikuwa mtendaji wa shughuli za serikali wakati huo akishiriki katika vikao vya usukaji wa mfumo mpya wa ujasusi ndani ya jumuiya, mashirika na makampuni ya kibiashara.
Galvin, mbali ya kuwajibika kiserikali, mwanzoni mwa miaka ya 1980 alifanywa kuwa mshauri wa Rais katika Bodi ya Ujasusi wa nje (PFIAB). Bodi hii iliyoanzishwa mwaka 1956 na Rais Eisenhower, ilikuwa ikitoa ushauri kwa Rais juu ya uimarishaji na ufanisi wa kukusanya, kuchambua, kutathmini na kuzifanyia kazi taarifa za siri.
Fani ya Competitive Intelligence (CI) ni mpya katika mawanda ya kibiashara lakini yenye kukua kwa kasi kubwa. Makampuni mengi ya biashara hivi leo yanatilia maanani shughuli hii. Kampuni ya Future Group (TFG), mojawapo ya vitengo vya CI yenyewe hufanya tafiti kila baada ya muda fulani kuonesha mafanikio katika makampuni. Utafiti wa mwaka 1997 ulibaini kuwa asilimia sitini (60%) ya makampuni yalikuwa na mfumo madhubuti wa ujasusi. Hili ni ongezeko la asilimia mbili tokea ulipofanyika utafiti wa awali miaka miwili ya nyuma. Miongoni mwa makampuni yaliyofanyiwa utafiti ni ya utengenezaji ndege, bidhaa za walaji, huduma za fedha, bidhaa za habari, huduma na madawa ya utabibu.
Theluthi mbili ya makampuni hayo yalikuwa na mapato yaliyovuka dola bilioni moja na asilimia 28 yalikuwa na mapato yaliyovuka dola bilioni 10. Yale makampuni yenye mfumo bora wa ujasusi yalifikia kiwango kamili cha ukusanyaji wa taarifa za siri. Cha kuhamasisha ni kwamba makampuni ya bidhaa tumivu (consumer products), yalitia fora kwa kuvuka lengo, yaliweza kufikia kiwango cha asilimia 6.4 cha harakati zao za kijasusi, yakivuka kile cha kawaida cha asilimia 6.1. Makampuni ambayo yalipata kiwango cha chini kabisa yalikuwa ni ya uundaji wa ndege (aerospace) ambayo hayakufikia asilimia 5.6 chini ya kiwango cha kawaida cha upimaji wa shughuli za kijasusi. Kiwango hiki cha chini kilitokana na sababu kadhaa. Makampuni ya uundaji wa ndege yana asilimia kubwa ya maafisa wa zamani wa jeshi katika nafasi zao za uongozi. Wengi miongoni mwao ni weledi wa ujasusi wa kijeshi kwa hiyo walijiamini kuwa wangaliweza kufanya ujasusi inavyotakikana.
Aidha kumekuwa na mtindo wa baadhi ya maafisa wa zamani kuziendesha shughuli za biashara kwa misingi ya kijeshi au kutumia mbinu na taratibu kutoka kada za jeshi hadi kwenye ulimwengu wa biashara. Katika utafiti wa mwaka hadi mwaka, makampuni ya Microsoft na Motorola yalionekana kuwa na programu bora zaidi za kijasusi. Hiyo ndiyo sababu ya msingi, katika vita vya biashara, iliyopelekea makampuni hayo kuitwa tai. Asilimia 17 ya makampuni yakaitwa mbuni, haya ni yale makampuni ambayo hayakudhani kama makampuni mengine yalikuwa yakifanya ujasusi dhidi yao. Na kumithilishwa huko kwa makampuni hayo na mbuni ni kwa kule tabia ya mbuni ya kuficha kichwa mchangani ilhali mwili mzima uko nje!
Lakini jambo lililoshangaza ni kuwa makampuni manane kati ya kumi yalionesha kuwa machapisho waliyoyasoma kama vile magazeti, vyombo vya habari za biashara na majarida ya makampuni ndiyo hasa yaliyokuwa vyanzo vya awali vya taarifa walizokuwa wakizipata. Waajiriwa wa makampuni, wauzaji wa bidhaa na wateja wao ndio hasa walionekana kutoa taarifa muhimu kwa asilimiya 82 ya makampuni. Asilimia 80 ya makampuni yalionesha kupata taarifa zake kupitia mikutano iliyofanywa ndani ya makampuni yenyewe. Asilimia 79 ya makampuni yakaonesha kupata taarifa za siri kutoka kwa wataalamu wa viwanda. Na asilimya 70 ya makampuni yalipata taarifa kutokana na takwimu za kibiashara.
Walipoulizwa (wahusika) ni kipi hasa chanzo muhimu cha taarifa, asilimia 37 ya makampuni yakasema ni wauza bidhaa na wateja, asilima 35 yakasema machapisho waliyoyasoma. Miongoni mwa yale makampuni yenye programu rasmi za kijasusi, asilimia 45 yakaonesha kuwa machapisho waliyoyasoma ndiyo hasa yalikuwa chanzo muhimu cha taarifa. Asilimia 26 ya makampuni yakasema kuwa waajiriwa wa makampuni ndiyo chanzo muhimu cha taarifa. Asilimia 25 yakasema wataalamu wa viwanda ndio chanzo muhimu cha taarifa. Asilimia 24 yakasema mtandao wa Internet ndio chanzo muhimu cha taarifa. Asilimia 18 tu ya makampuni yakasema chanzo muhimu cha taarifa ni mikutano ya makampuni na asilimia 16 tu yakasema takwimu za kibiashara ndiyo chanzo muhimu cha taarifa. Tafiti hizi zinaonesha kuwa japo Competitive Intelligence ndani ya makampuni imejitanua vyema kwa kipindi cha muongo mmoja lakini bado nyenzo, taratibu na mbinu wanazotumia katika harakati zake si za kisasa. Mbinu ya kutumia wafanyakazi na mikutano kupata taarifa muhimu za siri ni ushahidi wa wazi wa kukosekana kwa nyenzo bora na za kisasa za kufanyia kazi. Kuongeza vyanzo vya habari na kudhibiti uvujaji wa taarifa ni kanuni muhimu katika ushindani na mapambano ya kijasusi, iwe katika uwanja wa vita, katika biashara, katika uchumi wa soko na kadhalika.
Uwezo wa kampuni au shirika, jumuiya, taasisi, asasi au kundi la harakati katika mapambano hayo utategemea jinsi linavyoweza kunusa, kukusanya, kuchambua, kusambaza, kudhibiti na kutunza taarifa zake. Mashirika mengi hupanga na kuratibu shughuli za vyombo vya ujasusi na vile vya usalama kwa namna tofauti. Kila kimoja hutekeleza wajibu wake mahususi na kila kimoja hakiwezi kufanikisha kazi zake binafsi bila ya kingine. Ujasusi ni jambo muhimu linalohitajika katika maisha ya mtu binafsi, jumuiya, chama cha siasa, Serikali, vikundi vya harakati na kadhalika. Ni muhimu kuwa na mtandao wa kijasusi wa mtu binafsi, jumuiya, chama, serikali na kadhalika. Hivyo basi ni jambo lisilobudi kujifunza mbinu mbali mbali za kijasusi ima kwa sababu za kiusalama (kujihami), au kwa ajili ya kutafuta mafanikio katika harakati mbali mbali ikiwa ni pamoja na vita, biashara, kampeni za uchaguzi na mengineyo. Hivyo kwa kusoma kitabu hiki utaweza kupata maarifa ya kijasusi, utaelewa misingi ya ujasusi na umuhimu wake na unaweza kujitimizia shughuli zake mbali mbali.
Ujasusi wa ushindani CI, ambao zaidi hutumika katika ulimwengu wa biashara na harakati waweza kuainishwa kama ni utaratibu wa kiufundi wa kupata habari nyeti za biashara na kiharakati kuhusu malengo, wateja, washindani, maadui, teknolojia na mazingira ya jumla ya harakati na biashara. Habari hizi zaweza kutoka kwa yeyote yule au vyanzo vyovyote. Ujasusi unatajwa kama ni taaluma ya pili kongwe duniani; ulikuwepo tangu ulimwengu ulipopambazuka. Mashujaa katika vita vya kale wanasema kuwa ujasusi ulikuwa sehemu muhimu ya mkakati wa vita. Kinachomuwezesha kamanda hodari kushambulia, kuteka na kufanya mambo yasiyo ya kawaida yaliyo nje ya uwezo wa kawaida ni ule ujuzi anaokuwa nao kabla. Na ujuzi huo anaokuwa nao kabla, hautokani na uzoefu au uhodari wa kufanya mahesabu, bali unatokana na taarifa za siri za adui ambazo hupatikana kutoka kwa watu wengine.
Aidha Ujasusi umekuwa sehemu muhimu ya taasisi za kijeshi na kibishara. Ulikuwa, na hadi leo umekuwa bado ni chachu ya harakati za kanisa Katoliki. Punde taarifa zinapopatikana, husambazwa kwa usahihi na kwa wakati kwa watoaji maamuzi wa ngazi zote. CI ni kifupisho cha Competitive Intelligence ambao ni ujasusi unaoshughulika zaidi na harakati za kibiashara ambao unatofautiana kidogo na ule wa kiserikali. CI inafuata taratibu na maadili ya biashara ambayo hayafuatwi na taasisi za ujasusi unaohami serikali. CI haufanywi chini ya kinga ya kidiplomasia bali una lengo zaidi la kuimarisha uhusiano wa kibiashara, kuboresha huduma na kukabili mikiki ya ulimwengu kwa ajili ya kujipatia faida na ufanisi wa shughuli husika. CI kadhalika inatofautiana na ukachero wa kiserikali ambao huweza kukiuka au kupuuza sheria na taratibu za wengine. Hii ni kusema shughuli hii, mara nyingi haitazamwi kwa wema, inaonekana kama isiyo na uhalali wa kimaadili.
Kwa ajili hiyo, udondozi wa kitabu hiki unatoa changamoto kwa wajuzi wa taaluma hiyo, washiriki wake na watu wa kawaida kuonesha iwapo fani ya ujasusi itafanywa kitaalamu inavyoweza kuwa ya muhimu kwa kurejea mifano ya wakongwe hasa Wazayuni walivyoweza kutawala uwanja huo hivyo kudhibiti kila nyanja kwa ajili ya kulinda na kuendeleza maslahi yao sehemu mbali mbali duniani.
Inaendelea Insha'Allah...