Mitandao ya Kijasusi

X-PASTER

JF-Expert Member
Feb 12, 2007
11,610
1,810
Dibaji

Yapo maainisho kadhaa tofauti ya neno ujasusi, hata hivyo wataalamu wote wanaafikiana na ainisho jepesi kuwa ni utendaji wa siri chini ya mtandao wa siri uliosukwa kwa namna ya usiri ndani ya taasisi au vitengo maalum vya siri vinavyochunga ulinzi na usalama wa dola, watu, taasisi au biashara kwa njia za siri. Ni shughuli iliyozungukwa na mazingira ya usiri inayogusa maeneo yote ya jamii. Ni mtandao wenye malengo ya kulinda maslahi ya kidola, kibiashara, raia na mali zao dhidi ya mipango na njama za wahalifu au maadui. Ujasusi ni utafutaji wa habari au taarifa muhimu kwa njia za siri juu ya/au dhidi ya shughuli, biashara au maslahi ya kundi, jumuiya, taasisi au kampuni. Kwa ajili hiyo, ujasusi kama fani una mielekeo tofauti ambapo dhana yake kuu ni ulinzi wa kichunguzi.

Uelekeo wa Ujasusi wa upande wa mashariki(ikiongozwa na Urusi) zama za vita baridi, ulikuwa wa kulinda watawala, vyama na itikadi za dola kwa maslahi ya wachache wenye mamlaka. Kutokana na uelekeo huo, lililokuwa shirika la ujasusi la Urusi KGB lilivuma kwa mbinu za kudhibiti njama zote dhidi ya iliyokuwa serikali ya Kikomunisti nchini humo. Ama uelekeo wa ujasusi wa magharibi(ukiongozwa na Marekani) unaelezwa kuwa una shabaha ya kulinda watu na mali zao, nchi na maslahi yake dhidi ya wanaokiuka amani na demokrasia ndani na nje ya mipaka ya dola husika. Kwa ajili hiyo, Marekani ikilitumia shirika lake la CIA imekuwa ikichunguza na kuwahi kuchukua hatua dhidi ya inaowatuhumu kulihujumu Taifa hilo kabla hawajafanya madhara (pre emptive attack).

Mielekeo yote miwili inasisitiza kuwa wajibu wa msingi wa ujasusi unaokusanya ushushushu na ukachero ni kuchungua, kuyachimba, kuyachambua na kuyatathimini mambo kimya kimya, kitaalamu na kiufundi. Shughuli hiyo hufanyika ndani na nje ya mipaka ya dola au biashara fulani hatimaye kushauri hatua kwa ajili ya maslahi ya dola husika na raia wake au biashara husika na wadau wake. Wachambuzi wa mielekeo yote wanazingatia ujasusi wa kiushindani na zimeanzishwa taratibu tofauti kwa ajili ya kuleta ushindani katika shughuli za kijasusi baina ya shirika na shirika au baina ya nchi na nchi (Competitive Intelligence/counter intelligence).

Yapata miaka thelathini tangu uimarishaji ujasusi uanze kinchi, kiserikali, kijumuiya na kibiashara. Chachu ya uimarishaji huo ina mitazamo zaidi ya mmoja ambapo mtazamo mmoja wasemekana unatokana na fikra ya Afisa Usalama chipukizi wa cheo cha chini kwa wakati huo. Kijana huyo alikuwa na mazoea ya kuongea na watu wenye nyadhifa katika shirika moja lililopo jimbo la Midwest nchini Marekani. Wakubwa wa shirika hili walikuwa wakimpa heshima kubwa kijana huyo na hata wakati mwingine walikuwa wakimpa taarifa nyeti za shirika na nchi kwa jumla. Kumbe sababu kubwa ilikuwa ni manufaa ya kumtumia kijana huyu ambaye ndiye kwanza alikuwa anamaliza mafunzo yake, walikuwa wakitimiza vyema matarajio yao. Walikuwa wakipata taarifa na kuzipeleka kwa watoaji wakuu wa maamuzi mjini Washington. Taarifa hizo zilihusu hali na hatua za kiusalama za nchi nyingine pamoja na harakati za mitandao mingine ya kiusalama na mambo mengine yaliyogusa maslahi ya taifa.

Siku moja kijana “huyo” alishangazwa na jambo moja. Alisikia taarifa ambazo “mkuu mmoja” alikuwa nazo wakati mkuu mwingine hakuwa nazo na alikuwa akifanya jitihada za kuzitafuta kupitia vyanzo vyake. Baada ya kufuatilia akagundua kuwa hali hiyo ndiyo iliyokuwepo siku zote pale ofisini. Hapakuwa na chombo au mfumo mmoja mahususi wa ukusanyaji wa taarifa za kuwawezesha kufanya maamuzi sahihi. Taarifa nyingi zilizohusiana na mikakati ya wazi na ya siri zilikuwa zikiwafikia wakuu hao lakini hapakuwepo yeyote aliyezikusanya pamoja na kuzifikisha kwa wengine ambao wangeliweza kuzifanyia kazi.

Zaidi ya hivyo, afisa usalama huyo mchanga aligundua hali ya kutokuwepo kwa utaratibu wa kiufundi na uangalifu katika kudhibiti taarifa muhimu ndani ya taasisi hiyo. Hata makampuni mengine makubwa na madogo ambayo kijana huyu aliyafanyia kazi nayo hayakuwa na utaratibu wa kueleweka katika kukusanya, kuchambua na kusambaza taarifa.

Dosari hii ya kimsingi ilidhihiri pia katika maeneo mengi ya Marekani. Ulikuwa kama utamaduni wa wote. MBA (kama kampuni) katika programu zake ilikuwa inapuuzia jambo hili la msingi ambalo ndilo chachu ya utendaji. Kasoro hii ilikuwa imejitokeza katika kipindi hicho cha mapinduzi kwenye mawasiliano nyeti na muhimu. Baadaye ndipo ilipokuja kubainika kwamba kumbe taratibu na mbinu za kijasusi zilizotumiwa na serikali kwa kutekelezwa kwa siri za namna yake pia zingaliweza kutumiwa kwa uwazi katika shughuli nyingine ndani ya jumuiya, taasisi na mashirika ya kibiashara na zingaliweza kuleta manufaa makubwa.

Kijana mwanamapinduzi wa kijasusi aliyeipenda kazi yake, aliamini kuwa alikuwa akitoa mchango muhimu kwa taifa katika fani hiyo ya siri. Mbegu ya fikra aliyopanda kijana huyo ikaleta mabadiliko ya kitaaluma katika uwanda wa ujasusi. Akiwa pamoja na wenziwe waliokuwa na mtazamo kama wake, akaanzisha kazi ya kujenga na kubadili mfumo wa ujasusi ndani ya shughuli za kijumuiya, kidini na kibiashara.

Katika taifa la Marekani msukumo mkubwa wa ujasusi mpya wa ushindani ulikuja kushika kasi katikati ya miaka ya 1980 wakati Marekani ilipokuwa ikishindwa kutamba mbele ya makampuni ya Kijapani katika soko la biashara la kimataifa. Waziri wa Biashara ya Kimataifa na Viwanda wa Japan alipata kutamka katika mkutano na waandishi wa habari wakati fulani mwaka 1985 kwamba:

“Japan ilishindwa katika Vita Kuu ya Pili ya Dunia kiasi fulani kwa sababu ya mtandao na mkakati madhubuti uliopangwa na serikali ya Marekani, sasa kwa nini wafanyabiashara wa Marekani wanashindwa kuendelea kuwa na mbinu bora za kijasusi kama zile zilizotumika wakati wa vita ili kuishinda Japan kibiashara? Wajapan wengi wameshindwa kuielewa siri hii kwa nini Marekani inashindwa katika vita hi

Ili kujizatiti kupambana na Japan kibiashara wafanyabishara wa Marekani wakaanza kukusanya nguvu ya ujasusi, waliitwa mabingwa wa ujasusi kutoka serikalini ili wawasaidie katika shughuli za kibishara ambao wangefuma taratibu madhubuti za upataji wa taarifa za kibishara zilizohusiana na Japan. Mmoja wa majasusi wa serikali aliyeshiriki mpango huu alikuwa Robert Galvin, Mkurugenzi Mtendaji wa zamani wa Motorola aliyepata kuwa Mwenyekiti wa Bodi Kuu ya Motorola. Huyu alikuwa mtendaji wa shughuli za serikali wakati huo akishiriki katika vikao vya usukaji wa mfumo mpya wa ujasusi ndani ya jumuiya, mashirika na makampuni ya kibiashara.

Galvin, mbali ya kuwajibika kiserikali, mwanzoni mwa miaka ya 1980 alifanywa kuwa mshauri wa Rais katika Bodi ya Ujasusi wa nje (PFIAB). Bodi hii iliyoanzishwa mwaka 1956 na Rais Eisenhower, ilikuwa ikitoa ushauri kwa Rais juu ya uimarishaji na ufanisi wa kukusanya, kuchambua, kutathmini na kuzifanyia kazi taarifa za siri.

Fani ya Competitive Intelligence (CI) ni mpya katika mawanda ya kibiashara lakini yenye kukua kwa kasi kubwa. Makampuni mengi ya biashara hivi leo yanatilia maanani shughuli hii. Kampuni ya Future Group (TFG), mojawapo ya vitengo vya CI yenyewe hufanya tafiti kila baada ya muda fulani kuonesha mafanikio katika makampuni. Utafiti wa mwaka 1997 ulibaini kuwa asilimia sitini (60%) ya makampuni yalikuwa na mfumo madhubuti wa ujasusi. Hili ni ongezeko la asilimia mbili tokea ulipofanyika utafiti wa awali miaka miwili ya nyuma. Miongoni mwa makampuni yaliyofanyiwa utafiti ni ya utengenezaji ndege, bidhaa za walaji, huduma za fedha, bidhaa za habari, huduma na madawa ya utabibu.

Theluthi mbili ya makampuni hayo yalikuwa na mapato yaliyovuka dola bilioni moja na asilimia 28 yalikuwa na mapato yaliyovuka dola bilioni 10. Yale makampuni yenye mfumo bora wa ujasusi yalifikia kiwango kamili cha ukusanyaji wa taarifa za siri. Cha kuhamasisha ni kwamba makampuni ya bidhaa tumivu (consumer products), yalitia fora kwa kuvuka lengo, yaliweza kufikia kiwango cha asilimia 6.4 cha harakati zao za kijasusi, yakivuka kile cha kawaida cha asilimia 6.1. Makampuni ambayo yalipata kiwango cha chini kabisa yalikuwa ni ya uundaji wa ndege (aerospace) ambayo hayakufikia asilimia 5.6 chini ya kiwango cha kawaida cha upimaji wa shughuli za kijasusi. Kiwango hiki cha chini kilitokana na sababu kadhaa. Makampuni ya uundaji wa ndege yana asilimia kubwa ya maafisa wa zamani wa jeshi katika nafasi zao za uongozi. Wengi miongoni mwao ni weledi wa ujasusi wa kijeshi kwa hiyo walijiamini kuwa wangaliweza kufanya ujasusi inavyotakikana.

Aidha kumekuwa na mtindo wa baadhi ya maafisa wa zamani kuziendesha shughuli za biashara kwa misingi ya kijeshi au kutumia mbinu na taratibu kutoka kada za jeshi hadi kwenye ulimwengu wa biashara. Katika utafiti wa mwaka hadi mwaka, makampuni ya Microsoft na Motorola yalionekana kuwa na programu bora zaidi za kijasusi. Hiyo ndiyo sababu ya msingi, katika “vita vya biashara”, iliyopelekea makampuni hayo kuitwa “tai”. Asilimia 17 ya makampuni yakaitwa “mbuni”, haya ni yale makampuni ambayo hayakudhani kama makampuni mengine yalikuwa yakifanya ujasusi dhidi yao. Na kumithilishwa huko kwa makampuni hayo na “mbuni” ni kwa kule tabia ya mbuni ya kuficha kichwa mchangani ilhali mwili mzima uko nje!

Lakini jambo lililoshangaza ni kuwa makampuni manane kati ya kumi yalionesha kuwa machapisho waliyoyasoma kama vile magazeti, vyombo vya habari za biashara na majarida ya makampuni ndiyo hasa yaliyokuwa vyanzo vya awali vya taarifa walizokuwa wakizipata. Waajiriwa wa makampuni, wauzaji wa bidhaa na wateja wao ndio hasa walionekana kutoa taarifa muhimu kwa asilimiya 82 ya makampuni. Asilimia 80 ya makampuni yalionesha kupata taarifa zake kupitia mikutano iliyofanywa ndani ya makampuni yenyewe. Asilimia 79 ya makampuni yakaonesha kupata taarifa za siri kutoka kwa wataalamu wa viwanda. Na asilimya 70 ya makampuni yalipata taarifa kutokana na takwimu za kibiashara.

Walipoulizwa (wahusika) ni kipi hasa chanzo muhimu cha taarifa, asilimia 37 ya makampuni yakasema ni wauza bidhaa na wateja, asilima 35 yakasema machapisho waliyoyasoma. Miongoni mwa yale makampuni yenye programu rasmi za kijasusi, asilimia 45 yakaonesha kuwa machapisho waliyoyasoma ndiyo hasa yalikuwa chanzo muhimu cha taarifa. Asilimia 26 ya makampuni yakasema kuwa waajiriwa wa makampuni ndiyo chanzo muhimu cha taarifa. Asilimia 25 yakasema wataalamu wa viwanda ndio chanzo muhimu cha taarifa. Asilimia 24 yakasema mtandao wa Internet ndio chanzo muhimu cha taarifa. Asilimia 18 tu ya makampuni yakasema chanzo muhimu cha taarifa ni mikutano ya makampuni na asilimia 16 tu yakasema takwimu za kibiashara ndiyo chanzo muhimu cha taarifa. Tafiti hizi zinaonesha kuwa japo ‘Competitive Intelligence’ ndani ya makampuni imejitanua vyema kwa kipindi cha muongo mmoja lakini bado nyenzo, taratibu na mbinu wanazotumia katika harakati zake si za kisasa. Mbinu ya kutumia wafanyakazi na mikutano kupata taarifa muhimu za siri ni ushahidi wa wazi wa kukosekana kwa nyenzo bora na za kisasa za kufanyia kazi. Kuongeza vyanzo vya habari na kudhibiti uvujaji wa taarifa ni kanuni muhimu katika ushindani na mapambano ya kijasusi, iwe katika uwanja wa vita, katika biashara, katika uchumi wa soko na kadhalika.

Uwezo wa kampuni au shirika, jumuiya, taasisi, asasi au kundi la harakati katika mapambano hayo utategemea jinsi linavyoweza kunusa, kukusanya, kuchambua, kusambaza, kudhibiti na kutunza taarifa zake. Mashirika mengi hupanga na kuratibu shughuli za vyombo vya ujasusi na vile vya usalama kwa namna tofauti. Kila kimoja hutekeleza wajibu wake mahususi na kila kimoja hakiwezi kufanikisha kazi zake binafsi bila ya kingine. Ujasusi ni jambo muhimu linalohitajika katika maisha ya mtu binafsi, jumuiya, chama cha siasa, Serikali, vikundi vya harakati na kadhalika. Ni muhimu kuwa na mtandao wa kijasusi wa mtu binafsi, jumuiya, chama, serikali na kadhalika. Hivyo basi ni jambo lisilobudi kujifunza mbinu mbali mbali za kijasusi ima kwa sababu za kiusalama (kujihami), au kwa ajili ya kutafuta mafanikio katika harakati mbali mbali ikiwa ni pamoja na vita, biashara, kampeni za uchaguzi na mengineyo. Hivyo kwa kusoma kitabu hiki utaweza kupata maarifa ya kijasusi, utaelewa misingi ya ujasusi na umuhimu wake na unaweza kujitimizia shughuli zake mbali mbali.

Ujasusi wa ushindani “CI”, ambao zaidi hutumika katika ulimwengu wa biashara na harakati waweza kuainishwa kama ni “utaratibu wa kiufundi wa kupata habari nyeti za biashara na kiharakati kuhusu malengo, wateja, washindani, maadui, teknolojia na mazingira ya jumla ya harakati na biashara. Habari hizi zaweza kutoka kwa yeyote yule au vyanzo vyovyote. Ujasusi unatajwa kama ni taaluma ya pili kongwe duniani; ulikuwepo tangu ulimwengu ulipopambazuka. Mashujaa katika vita vya kale wanasema kuwa ujasusi ulikuwa sehemu muhimu ya mkakati wa vita. Kinachomuwezesha kamanda hodari kushambulia, kuteka na kufanya mambo yasiyo ya kawaida yaliyo nje ya uwezo wa kawaida ni ule ujuzi anaokuwa nao kabla. Na ujuzi huo anaokuwa nao kabla, hautokani na uzoefu au uhodari wa kufanya mahesabu, bali unatokana na taarifa za siri za adui ambazo hupatikana kutoka kwa watu wengine.

Aidha Ujasusi umekuwa sehemu muhimu ya taasisi za kijeshi na kibishara. Ulikuwa, na hadi leo umekuwa bado ni chachu ya harakati za kanisa Katoliki. Punde taarifa zinapopatikana, husambazwa kwa usahihi na kwa wakati kwa watoaji maamuzi wa ngazi zote. “CI” ni kifupisho cha Competitive Intelligence ambao ni ujasusi unaoshughulika zaidi na harakati za kibiashara ambao unatofautiana kidogo na ule wa kiserikali. CI inafuata taratibu na maadili ya biashara ambayo hayafuatwi na taasisi za ujasusi unaohami serikali. CI haufanywi chini ya kinga ya kidiplomasia bali una lengo zaidi la kuimarisha uhusiano wa kibiashara, kuboresha huduma na kukabili mikiki ya ulimwengu kwa ajili ya kujipatia faida na ufanisi wa shughuli husika. CI kadhalika inatofautiana na ukachero wa kiserikali ambao huweza kukiuka au kupuuza sheria na taratibu za wengine. Hii ni kusema shughuli hii, mara nyingi haitazamwi kwa wema, inaonekana kama isiyo na uhalali wa kimaadili.

Kwa ajili hiyo, udondozi wa kitabu hiki unatoa changamoto kwa wajuzi wa taaluma hiyo, washiriki wake na watu wa kawaida kuonesha iwapo fani ya ujasusi itafanywa kitaalamu inavyoweza kuwa ya muhimu kwa kurejea mifano ya wakongwe hasa Wazayuni walivyoweza kutawala uwanja huo hivyo kudhibiti kila nyanja kwa ajili ya kulinda na kuendeleza maslahi yao sehemu mbali mbali duniani.


Inaendelea Insha'Allah...
 
Neno La Mwanzo

Wataalamu wa ujasusi wa baada ya vita kuu ya pili, wametoa maainisho mengi wanayoyanasibisha na neno ujasusi. Hata hivyo, ainisho ambalo pengine laweza kukubalika na wote ni, shughuli za uchunguzaji wa mambo mbali mbali kwa njia za uficho; mienendo na harakati za siri za usakaji wa habari muhimu na za hakika kuhusu watu na matendo yao, yaliyo ya dhahiri na ya uficho, yanayoyafanywa dhidi ya watu wengine, serikali, jumuiya, taasisi, nchi, Taifa, kabila, biashara au maslahi ya wengine. Aidha ujasusi kitaaluma, ni ufundi wa kunasa taarifa au uwezo wa kupata taarifa nyingi kutoka vyanzo tofauti zenye kulenga kuhami au kushambulia kwa ufanisi zaidi, ni shughuli za kimya kimya (covert) zenye malengo mazuri au mabaya kwa maslahi ya mtu, kundi, jumuiya, taasisi au Serikali. Kwa tafsiri ya kiutendaji, ni ukusanyaji na uchambuzi wa ‘data’ na taarifa zinazotoka katika chanzo chochote kile, iwe kwa mtu au chombo; taarifa zenye mtazamo wa mbali na zinazotoa taswira ya dhamira, nguvu, harakati na athari au matokeo yanayoelekea kutokea.

Shughuli za kijasusi ni muhimu katika maisha ya kila siku ya ulimwengu huu wenye malimwengu mengi. Zhuge Liang katika kitabu ‘Njia ya Jenerali’(The Way of the General) ameandika, kimaumbile, si kawaida kwa mjinga kuweza kumpiku mwerevu, bali ni mwerevu mwenye fursa ya kumzidi mjinga kwa uwerevu wake. Lakini, ili mwerevu aweze kumshinda mwerevu mwenziwe hanabudi kutumia vizuri mianya na fursa muhimu. Walioitazama taaluma hiyo kwa kuihusisha na historia ya Mwanaadamu wamejaribu kuonesha jinsi ilivyo kongwe ingawa wanakiri kuwa awali haikuwa rasmi kama ilivyo sasa. Kwa mujibu wa vitabu vitakatifu, mmoja wa manabii aliyekuwa pia “kiongozi wa dola ya ajabu”, Suleiman Mwana wa Daudi ametajwa kutumia ujasusi kupata taarifa juu ya nchi jirani kwa kutumia ndege, maarufu kwa jina la Hudi Hudi. Nabii huyo aliyekuwa na uwezo wa kufahamu lugha mbali mbali za wanadaamu, majini, wadudu na wanyama, alipewa taarifa na ndege Hudi Hudi kutoka nchi ya Sabaa (ambayo sasa ni Yemen). Katika sura ya 27 aya ya 20 mpaka 22, Mwenyezi Mungu Anatufahamisha juu ya habari hiyo ya kijasusi kama ifuatavyo:

“Imekuwaje mbona simuoni Hudi Hudi au amekuwa miongoni mwa wasiokuwa hapa”. Kwa yakini nitamuadhibu adhabu kali au nitamchinja au aje na habari muhimu. Basi hakukaa sana (Sulaymaan) mara (Hudi Hudi akafika) akasema nimegunduwa usilogunduwa, na ninakujia hivi kutoka nchi ya Sabaa na habari yenye yakini…” (27:20-22).

Jasusi Sun Tzu na wengineo wameandika kwamba, ujasusi ndiyo mbinu kuu iliyotumiwa na inayoendelea kutumiwa na makamanda katika medani za vita. Kitabu matumizi ya ushushushu (The Use of Spies) kimeandika juu ya anavyoweza kamanda kushambulia, kuteka na kufikia malengo kwa namna isiyotazamiwa, ni umahiri wa ujasusi katika medani ya vita ambapo taarifa alizokusanya kutokaupande wa adui humuwezesha kujua vilivyo, mahali alipo adui na uwezo wake. Taarifa za aina hiyo hupatikana kupitia vyanzo mbali mbali vya wazi na vya siri kutoka kwa watu muhimu, mawakala, ndugu, jamaa, marafiki au adui wa adui huyo.

Steven M. Shaker Afisa wa kesi wa CIA (CIA Case Officer) na Mark P. Gembick (aliyejiunga na shirika la Uwakala wa usalama wa Taifa(National Security Agence) la Marekani akiwa na umri wa miaka 17 tu, ambao ni mabingwa wa fani hiyo na washauri wa ujasusi wa Marekani, wakichambua uwanja huo hasa unaohusisha ushindani kati ya weledi wa fani hiyo, katika kitabu The War Room Guide to Competitive Intelligence wameandika ya kwamba:

“Ujasusi ukijumuisha ukachero na ushushushu ni uzamiaji, ukusanyaji na uchambuzi wa data na habari zinazoweza kupatikana kutoka vyanzo vyovyote vile iwe watu na harakati zao zote za maisha au vyombo vya nguvu vya kitaaluma, ambavyo kwa pamoja husaidia kutoa picha ya malengo, uwezo au shughuli za maadui pamoja na ukadiriaji wa matokeo kwa mnasaba wa ishara ya matendo au harakati hizo. Ni mtandao uliopangika vyema uliokusudiwa kupachikwa katika shughuli mbali mbali za kijamii unaolenga kuwajua na kuwadhibiti mapema wadau, wateja, washindani, washauri, watumishi, teknolojia na kwa ujumla mazingira ya shughuli adui”.
Aidha wakielezea umuhimu wa fani hiyo kiuendeshaji hata katika shughuli za kibiashara au kidini majasusi hao wameandika:

“Fani hii ni muhimu sana katika shughuli za kibiashara kwa taasisi zisizo za kijeshi pia ni muhimu katika uendeshaji wa shughuli mbali mbali za kidini. Kanisa Katoliki limekuwa likitumia ujasusi kujiimarisha.”
Washauri hao wa ujasusi katika kitengo cha utafiti wa operesheni za kijeshi ambao pia ni maafisa waandamizi wa shirika la CIA wanasema, “siri ya mafanikio ya harakati mbali mbali ni kuwepo kwa mitandao adhimu na adimu upatikanaji habari; harakati zisizo na mitandao ya aina hiyo katika mfumo wa habari huwa vigumu kufanikiwa”. Shaker aliye na zaidi ya miaka 18 katika duru za ujasusi na Gembick aliye na zaidi ya miaka 16 katika uwanja huo, kwa pamoja wanasisitiza kuwa “Japan ilishindwa katika Vita Kuu ya Pili kutokana na umahiri wa mtandao wa kijasusi na stratejia pevu za kijeshi za serikali ya Marekani”. Kwa ajili hiyo majasusi hao wanahoji kwa nini wafanyabiashara wa Kimarekani hivi leo wasitumie tajriba hiyo na kuimarisha mfumo wa ukachero wa biashara utakaoshindana na Japan ya leo ili kuweza kuishinda kibiashara kama ilivyokuwa wakati ule? Wajapan wengi hawafahamu kwa nini Wamarekani hawashindi vita hiyo ya kibiashara.

Kwa upande mwingine mtandao mmoja wa kijasusi unapoingiliwa na mwingine ni ishara ya kushindwa kwa mipango na mikakati ya shirika lililoingiliwa. Akifafanua hilo aliyekuwa Mkurugenzi wa Usalama wa ndani ya Uingereza (MI5) miaka ya 1950 jasusi na kachero, Peter Wright, ameandika katika kitabu chake maarufu cha ‘Mnasa kachero’ (Spycatcher)2 kwamba, mwaka 1951 alipokea simu ya ghafla kutoka kwa aliyekuwa Mkuu wa Idara ya Ufundi ambaye alikuwa wakala wa MI5 mahali hapo, Tylor, ambaye alizungumza kwa sauti ya hofu na wasi wasi mkubwa akichelea kuwa tayari mipango ya Uingereza ilielekea kushindwa kwa sababu ya uvujaji wa taarifa kama hivi:

“Tumepigwa katika hili, Taylor alimwambia Peter, ambaye moyoni aliingiwa wasi wasi kuwa mambo yameshaharibika kutokana na kuvuja au kuingiliwa kwa taarifa za idara yake na mitandao mingine ya kijasusi, kwa ajili hiyo haraka aliomba wakutane kujadili pigo hilo.”
Jasusi Peter, anaeleza kuwa walikutana mchana wa siku hiyo katika eneo moja lililojitenga mkabala na iliyokuwa ofisi ya Wizara ya Mambo ya nje. Katika mjadala huo wa faragha Taylor alisema ya kuwa, mwambata wa mambo ya anga katika ubalozi wa Uingereza mjini Moscow alikuwa ameshindwa kazi kwa kuwa mazungumzo na taarifa zake zote zilikuwa zikinaswa na kusikilizwa kupitia transimita iliyopachikwa katika mkono wa simu aliyokuwa akiitumia kufuatilia nyendo za Idara ya Usalama ya jeshi la anga la kirusi.Kwa mujibu wa Taylor aliyekuwa wakala wa MI5 katika kitengo maalumu cha uchunguzi hilo ndilo pigo dhidi ya Uingereza.

Kitabu cha KGB kikielezea umuhimu wa ujasusi wakati wa Vita Baridi kati ya Magharibi iliyoongozwa na Marekani na Mashariki iliyoongozwa na Urusi, kimeandika kwamba, idara za usalama za magharibi zilifanikiwa kupata siri za ndani za shirika la kijasusi la KGB kutoka chuo kimoja cha juu cha mambo ya ujasusi cha mjini Moscow.

“Kitabu cha kiada cha siri za KGB kiliibwa na Idara za kijasusi za nchi za magharibi kutoka chuo kimoja cha juu cha ujasusi mjini Moscow. Kijitabu hicho kiliitwa ‘uzoefu wa kuajiri Waamerika nchini Amerika na katika Nchi zote za ulimwengu wa Tatu’ 8591 (The Practice of Recruiting Americans in the USA and Third World Countries”). Shirika hilo lililokuwa maarufu kwa ujasusi duniani ilikichukulia kitabu hicho kwa unyeti uliolifanya lichapishe nakala mia moja tu”.

Kwa mujibu wa andiko maarufu la ‘kazi ya siri ya Wakala wa Urusi’ (The Secret Work of the Soviet Secret Agents), kitabu kilichokusudiwa kisomwe na kikundi kidogo tu cha maafisa teule”, imeandikwa kuwa kusambaratika kwa Taifa la Urusi na shirika la KGB, kunaelezwa ni moja ya mipango ya muda mrefu ya mataifa ya magharibi kupitia mashirika yao ya kijasusi.

Katika jumla ya mafanikio makubwa ya mashirika hayo dhidi ya uliokuwa Umoja wa Kisoviet ni pamoja na kunasa taarifa na nyaraka muhimu za kambi ya Mashariki zilizoeleza mipango ya kujipenyeza kwa KGB katika serikali na asasi nyingine za kijamii nchini Marekani kuanzia White House hadi ngazi za chini kabisa katika uongozi na utendaji wa shughuli za kila siku za kiserikali. Moja ya nyaraka hizo zilikuwa na mipango ya kutaka kujipenyeza katika Baraza la Mawaziri na Baraza la Usalama; Idara za Dola, zikijumuisha wawakilishi wake jijini New York, ujumbe wa Marekani Umoja wa Mataifa na kitengo cha pasi za kusafiria. Maeneo mengine ni Idara ya Ulinzi ya nchi hiyo, Pentagon, Idara ya Ujasusi ya jeshi na vitengo vyake na katika kundi la kudumu la jeshi la NATO chini ya Marekani. Kadhalika ndani ya CIA yenyewe na FBI, katika kamati zinazosimamia makampuni na viwanda pamoja na mabenki yenye kusimamiwa moja kwa moja na White House.

Aidha mpango huo wa Urusi ulilenga kujitoma na/au kujiingiza kisawasawa kwenye vituo muhimu vya utafiti wa kisayansi na maabara; vitengo vya utawala katika vyama vikubwa nchini Marekani na katika jumuiya nyingine zenye ushawishi kitaifa, jumuiya za vijana na klabu za waandishi. Kadhalika ndani ya makundi ya wanadiplomasia na wafanyabiashara wa mataifa ya nje walioko Marekani, vile vile katika Sekretariati ya Umoja wa Mataifa na katika uwakilishi wa nje katika umoja wa mataifa.

jasusi kwa upande mwingine ndiyo siri ya mafanikio ya Israil yenye mtandao makini wa shughuli hiyo uliyoiwezesha kuwapiku Waarabu kwa ujumla wao. Malengo makuu ya ujasusi wa Israil chini ya idara zao za ujasusi yanaelezwa kuwa kwa miongo mitano iliyopita ilikuwa ni pamoja na kuzichunguza nchi za kiarabu, uwezo wao na dhamira zao dhidi ya Israil, uelekeo na uhusiano wao na iliyokuwa USSR na dola nyingine kuu, vifaa na uwakilishi wao ulimwenguni kote, viongozi ndani ya nchi zao na katika maingiliano yao ya kisiasa, hamasa yao, na kujitayarisha kwao dhidi ya Israil na ufuatiliaji wa karibu wa harakati dhidi ya Uzayuni ulimwenguni kote.

Ujasusi ndiyo siri pekee na ya muhimu ya mafanikio ya Israil katika vita vyake dhidi ya Waarabu. Kwa kushirikiana na CIA, mashirika ya ujasusi ya Israil yameweza kupanga na kufanikisha operesheni zote dhidi ya nchi za kiarabu na zile zilizofikiriwa ni kiislamu. Komandi kuu ya ujasusi miaka ya 1950 iliitwa Vaadat. ambayo shughuli zake za msingi zilikuwa ni pamoja na kuunganisha shughuli zote za kijasusi na uangalizi wa usalama ndani na nje ya Israil. Vaadat inawajumuisha Mkurugenzi wa shirika la ujasusi wa nje, Mossad, Mkurugenzi wa Idara ya Ujasusi Jeshini, Mkurugenzi wa Idara ya Ndani ya Usalama, ShinBeth, IGP na Mkurugenzi Mkuu wa Kituo cha Utafiti na Mipango kilicho chini ya Wizara ya Mambo ya nje. Aidha Mkuu wa Divisheni Maalumu katika Idara ya Upelelezi ya Polisi hujumuishwa katika kamati hii ya usalama ambayo Mwenyekiti wake ni Mkurugenzi wa Mossad anayewajibika moja kwa moja kwa Waziri Mkuu wa nchi hiyo. Huo ndiyo mfumo wa juu wa ujasusi ulioijenga Israil mara tu baada ya kuundwa Taifa la Israil baada ya vita kuu ya pili.

Vaadat iliugawanya ujasusi wa Israil katika mashirika makuu mawili, shirika la nje lililojulikana kama Mossad na la ndani linalojulikana kama ShinBeth, yote yakilenga kuwaandama Waarabu, Wapalestina na kuudhibiti ulimwengu kwa ujumla. Katika mada Israil Foreing Intelligence and Security Service, kitabu hicho kinaainisha kazi za Mossad kwa kuandika kwamba, pamoja na shughuli nyingine, ilihusika zaidi na ukusanyaji wa taarifa za kijasusi kutoka nje pamoja na kuandaa programu za kijasusi nje ya Israil hususan katika nchi zenye Waislamu na hasa wale wa makundi yanayoonekana kuhatarisha usalama wa Israil. ShinBeth ilihusika na usalama wa Waziri Mkuu na maafisa wengine wa juu wa serikali ya Israil.

Wakufunzi wa mafundisho ya Menejimenti ya kiusalama (‘Security Management’) wanaeleza kuwa, kuweza kutatua tatizo lazima kuendane na upataji habari muhimu na za hakika kupitia mbinu mbali mbali ikiwemo ya sura zaidi ya moja ambayo husaidia kuwakinga maafisa au maajenti wahusika kuwa na utambulisho rasmi kimavazi, jina, kabila, utaifa, kazi, taaluma, au mahali anapoishi. Afisa au wakala huyo huweza kujichomeka au kuwepo mahali akitumia utambulisho wa uongo (living under false identities) ama wa kiitikadi akiwa mweledi mzuri wa itikadi hiyo, mahiri wa lugha ya mahali fulani, mila na tamaduni za watu wa sehemu anayoifanyia ujasusi akiwa jasusi mshiriki (spy as a spy and participant) kama alivyofanya jasusi maarufu la Kiingereza Bwana Humphrey katika Hijaz (sasa Saud Arabia) au jasusi mwangalizi (spy as a complete spy) ili kupata taarifa muhimu kwa muda mrefu (deep cover spy) kama alivyofanya Bwana Lawrence. Wakati wa iliyokuwa KGB ujasusi wa kada hii ulikuwa chini ya kurugenzi isiyo rasmi (The Illegals Directorate) iliyokuwa kurugenzi maalumu ndogo kuu ya kurugenzi kuu ya kwanza (The First Chief Directorate). Pamoja na kurugenzi hiyo pia zilikuwepo idara maalum zilizohusika na ujasusi wa habari na uzuiaji wa mitandao mingine ya kijasusi (Information and Counter Intelligence) chini ya vitengo vya upotoshaji na hatua za kiutendaji (dis information and excutive action).

Katika andiko la kijasusi liitwalo Mbinu za kijasusi za ukusanyaji wa taarifa (Intelligence Gathering Devices) imeandikwa ya kwamba, mashirika ya kijasusi ya Israil yamekuwa na mbinu za hali ya juu kupata taarifa muhimu, mipango na mikakati, ikitumia zana bora zaidi. Kwa mujibu wa andiko hilo, hivi leo, Israil inaongoza kwa utumizi wa kamera ndogo sana (micro-cameras) katika uchukuaji wa picha za matukio, taswira za watu na maeneo yanayolengwa bila ya wahusika kubaini. Kutokana na utaalamu huo wa hali ya juu wa utumizi wa vifaa vya elektroniki makala moja ya kijasusi iliyokuwa na anuani Privacy Lost to Electronic Spies iliyochapishwa na Sunday Nation Aprili 16, 2005 inaeleza kupiga hatua kubwa kwa fani ya ujasusi ikiongozwa na wataalamu wa Israil ambako kumesababisha ulimwengu wa siri zaidi ya mtu mmoja usiwepo hivi sasa.

Katika mada iliyopewa kichwa, “Uingiliaji wa faragha za Watu ni jambo la lazima kwa ajili ya usalama wa taifa (intrussions into the privacy of individuals are necessary in the interests of national security), imeelezwa ya kwamba katika mawanda ya kidunia, Uingereza na Marekani na kwa hakika Wazayuni wakiwa nyuma yao, wamekuwa na ushirika wa ki-elektroniki katika kufuatilia kwa karibu zaidi mambo mbali mbali (Eectronic Surveillance Operations). Ushirika huo wa usakaji habari unaojitambulisha kwa jina la kijasusi (code name) ‘Echelon’ ambao ni mtandao wa mawasiliano ya satellite na kompyuta unaonasa taarifa, ujumbe, mazungumzo na habari za ulimwengu mzima zinazopita kwenye vifaa vya elektroniki.

Kwa kuwa ili mtu awe afisa wa idara ya usalama (Intelligence officer) kwamtaka awe mwenye akili iliyotulizana (Intelligent) basi wachapishaji wanakiwasilisha Makala hii kwa wasomaji na weledi wa fani hii kama changamoto na kuonesha umuhimu na/au madhara yake kwa maisha ya wanaadamu. Kutokana na changamoto hiyo, taaluma hiyo itumike kuleta ustawi katika jamii badala ya kudhuru. Aidha Makala yanakusudiwa kutoa mwanga wa jinsi taaluma hiyo inavyopasa kuendeshwa, kwa kuonesha uhalisia wa utendaji wake kinyume na ilivyo kwa baadhi ya mashirika ambapo imefikia jasusi, kachero au afisa usalama kutangaza hadharani kuwa yeye ni muhusika wa shughuli hiyo ili kuwatisha watu kwa maslahi binafsi. Kadhalika makala hii inayapa fununu baadhi ya mataifa ya ulimwengu wa tatu juu ya ujasusi wa kimataifa unaofanywa na Israil katika harakati zake za kutaka kuutawala ulimwengu wa Mashariki ya Kati na dunia kwa ujumla.

Israil, imekuwa ikiziendesha serikali kubwa na taasisi za kidunia zilizo chini ya Umoja wa Mataifa kutokea mafichoni. Hali hiyo ndiyo iliyosababisha taasisi au serikali hizo kushindwa kuendesha mambo kiadilifu kwa ajili ya ustawi wa dunia na wakazi wake.



Ujasusi wa Kimataifa
Dola zote zinafanya ujasusi kuwajua maadui wa ndani na nje ya mipaka, wahalifu na wavunja kanuni. Polisi na majeshi ya vita yanakusanya taarifa na kuchukua hatua, hata hivyo taasisi hizo si maalum kwa shughuli za ujasusi. Neno ujasusi linahusishwa zaidi na shughuli maalum zinazohusika na idara au mashirika maalum yenye utaalamu makhsusi juu ya ukusanyaji wa habari na taarifa za siri. Idara au mashirika ya ujasusi ya dola, huendesha shughuli za ujasusi kwa siri na uficho mkubwa kwa niaba ya serikali. Kadhalika vitengo na idara za ujasusi katika makampuni ya kibishara huendesha ujasusi kwa siri ili kuyaletea tija makampuni husika na kuhifadhi usalama wake.

Nchini Uingereza yapo mashirika makuu mawili ya ujasusi; shirika la siri la ujasusi nje ya Uingereza (Secret Intelligence Services) linalofahamika kama MI6 na shirika la siri la ujasusi wa ndani ya nchi hiyo linalojulikana kama MI5. Idara na mashirika haya hufanya kazi pamoja katika kukusanya, kuchambua na kutathmini habari za kijasusi na za udhibiti wa ujasusi (counter intelligence) katika kuilinda nchi hiyo. Udhibiti wa ujasusi hapa, una maana ya kwamba kiutendaji yapo pia mashirika ya nje ambayo huendesha ujasusi kupata taarifa juu ya Uingereza, ina nini na inakusudia lipi.

Uliokuwa Umoja wa kisovieti, ulikuwa na shirika maarufu la KGB lililovuma sana ndani na nje ya Urusi wakati wa vita baridi baina ya mashariki ya kikomunisti na magharibi ya kibepari. Marekani nayo ina FBI linaloshughulika na upelelezi wa uhalifu na jinai zote dhidi ya mtu na mtu, taasisi, jumuiya au shirika lolote dhidi ya serikali au maslahi ya Taifa ndani ya nchi. Aidha lipo shirika la CIA linaloendesha shughuli za ujasusi nje ya Marekani, duniani kote ili kulinda maslahi ya Taifa hilo. CIA ina maafisa, maajenti na wapasha habari walio Wamarekani na wasio Wamarekani watu wa kawaida, watendaji katika balozi, mashirika ya kiserikali na yasiyo ya kiserikali, taasisi na idara mbali mbali pamoja na watendaji na viongozi wa mashirika na wakuu wa serikali za nchi nyingine. Mashirika mengine ya ujasusi yaliyo mashuhuri ni pamoja na DGSE (Direction Generate de la security Externeur) la Ufaransa.

Hata hivyo, nguvu kubwa na ya hatari katika duru za ujasusi na siasa za ulimwengu wa leo ni Uzayuni yaani Israil yenye mashirika ya Mossad na Shin Beth. Mizizi ya ujasusi wa Uzayuni imetambaa mbali mno kinyume na vile mtu anavyoweza kukadiria. Kama ilivyotangulia kuelezwa kuwa mara baada ya vita kuu ya pili, dunia iligawanyika katika kambi mbili zilizohasimiana:

Kambi ya Ukomunisti iliyoongozwa na Urusi na kambi ya kibepari au ile inayoitwa ya nchi za kidemokrasia ambayo iko chini ya uongozi wa Marekani. Lakini ukweli ni kuwa serikali za Urusi na Marekani zote zimo mikononi mwa nguvu ya hatari na ya siri, nayo ni nguvu ya “Taifa la Wazayuni”, linalojiita “taifa teule”. Israil ina sheria ambayo mantiki yake ni kuunda na kulijenga Taifa la Wazayuni, inayowakandamiza Waislamu na Wakristo kwa manufaa ya Uyahudi. Uingereza, Ufaransa na hususan Marekani zote zipo chini ya ushawishi wa Wazayuni. Lakini ni watu wachache wanaoelewa kuwa Urusi nayo ilikuwa zao halisi la fikra na mipango ya Wazayuni. Hayo yana ushahidi wa matendo na maneno ya waandishi wa habari wa kiyahudi, waandishi wa kawaida na viongozi wa nchi, ambayo yanaelezea wazi wazi kuwa mapinduzi ya Urusi nayo pia yalitokana na mipango ya Wazayuni. Hapa chini ni baadhi ya matukio yanayotupa ushahidi juu ya ujasusi wa kizayuni ulivyofanikisha mapinduzi hayo:

1. Wanafikra wakuu wa harakati za Ukomunisti wote walikuwa Wayahudi. Karl Marx alikuwa Myahudi kwa Baba na kwa Mama. Jina Marx limefupishwa kutoka jina la Mordechai baadaye likabadilishwa kuwa Markus. Baba yake Karl, Heinrich Marx alizaliwa mwaka 1782 akiwa mtoto wa tatu wa Meier Halevi Marx ambaye alibatizwa kuingia Ukristo wa Uprotestant mwaka mmoja kabla ya Marx hajazaliwa.

Meier Halevi Marx alikuwa kiongozi na mwanasheria wa kiyahudi. Karl Marx ananasibihiana na Marabi wengi wa karne ya 16. Mama yake Marx bibi Henrietta ni Myahudi. Bintiye wa mwisho, Eleanor alipata kujinasibu hadharani katika kikao cha wafanyakazi kuwa yeye ni Myahudi. Trosky na Lenin nao walikuwa na asili ya Kiyahudi. Mama zao na wake zao kina Lenin na Starlin wote walikuwa Wayahudi.

2. Muda mfupi kabla ya mapinduzi ya Urusi, Wazayuni walikuwa na pilika pilika nyingi. Baada ya Vita ya Kwanza ya Dunia, Lenin na makomredi wenziwe mia mbili walitiwa kisirisiri ndani ya Treni iliyokuwa imezibwa kotekote kule Ujerumani na kupelekwa kwenye mipaka ya Urusi. Majina ya Makomredi wenzie wasiopunguwa 165 yanajulikana, na kati yao 128 walikuwa Wazayuni. Mara baada ya Lenin kuingia Urusi, Trotsky naye pia akatuwa nchini humo na kundi la Wazayuni 300 kutoka Amerika. Kwa pamoja, Mayahudi hao wakapanga na kutekeleza mpango wa mapinduzi.

3. Baada ya Mapinduzi ya Bolshevik, Wazayuni wakakamata madaraka ya serikali. Kati ya nyadhifa kuu 556 katika serikali mpya, 457 zilishikwa na Wazayuni.

4. Katika kitabu chao kinachozungumzia Mapinduzi ya Urusi, waandishi wa Kiyahudi wameumwagia sifa utawala huu jambo linaloonesha wazi wazi kuwa mapinduzi hayo yalikuwa na mkono wa nje.



Itifaki (Protokoli) Za Wazayuni Na Mipango Yao Ya Ujasusi

Kama ilivyokwishaelezwa, Wazayuni, tangu muda mrefu sana wamekuwa wakipanga kuuweka ulimwengu mzima mikononi mwao. Katika kutimiza lengo lao la kuitawala dunia nzima wanafikra wa Kiyahudi walifanya mikutano kadhaa ya siri kuanzia mwaka 1897 hadi 1905 na wakaweka misingi na programu kwa ajili ya kuleta mapinduzi duniani kote ili kutimiza maslahi ya Uzayuni na kuwatia utumwani wasio Wazayuni. Maelezo ya sera, mkakati na mbinu walizopanga kutumia yote yaliandikwa katika kitabu “Itifaki ya Wanazuoni Wakongwe wa Kizayuni” (The Protocols of the Learned Elders of Zion). Usambazaji wa andiko hilo ulikusudiwa kuishia kwa Wazayuni wachache tu wenye hadhi ya juu. Lakini kwa kiasi fulani nyaraka hizo hazikuhifadhika na kuishia kwa uongozi wa kiyahudi pekee. Nakala za andiko hilo zilivuja katika nyakati mbali mbali na zikaangukia mikononi mwa watu wasiokuwa Wazayuni ambao walizichapisha mwanzoni mwa karne iliyopita. Andiko hilo linajumuisha ule mpango mzima wa Mapinduzi ya Urusi. Matukio yaliyofuatia baada ya mapinduzi hayo yanauthibitisha zaidi ukweli huu. Onyo limetolewa kuwa, “yeyote anayemiliki kitabu hiki anapaswa kuuawa”. Sababu ya hilo ipo wazi kabisa. Andiko hili lingeruhusiwa kusambaa lingefichua Uzayuni na Ukomunisti sawia, lingefichua chanzo cha Mapinduzi ya Kikomunisti na mipango na njama za muda mrefu za Uzayuni.

Mapitio kadhaa ya vitabu vilivyoandikwa kwa lugha ya kiarabu juu ya “itifaki” hizo yana ushahidi wa kutosha juu yake. Upembuzi wa kitabu cha pitio la “itifaki” hizo Namba 83 kwa lugha ya Kiingereza inatoa taswira ileile mahsusi juu yake na muendelezo wake sawia. Ajabu ya kitabu hiki ni kwamba punde tu toleo jipya linapochapishwa, kitabu kinaadimika madukani. Pamoja na kuchapwa tena na tena lakini bado kitabu hicho ni adimu madukani. Kitabu hiki kilikuwepo kwenye jumba la makumbusho la Uingereza mwaka 1905 na kilivutia wengi baada ya Mapinduzi ya Bulshevik. Andiko hili likawa gumzo la kila siku kwani lilielezea mipango na program zote za mapinduzi ya Urusi na mapinduzi na mageuzi mengi mengineyo. Kitabu hicho hicho kinafichua mpango wa kukomesha Ukhalifa katika dini ya Uislamu nchini Uturuki na Programu ya kusimamisha Dola ya Israel.


Mipango Zaidi Ya Ujasusi Wa Wazayuni

Mwaka 1897, wakati “Wakuu” wa Wazayuni walipokutana kwa siri, kusuka programu ya kuvuruga maadili ya ulimwenguni, mpango wa kwanza ulikuwa kufanya kile kilichokuja kutokea Urusi mwaka 1917, mapinduzi ya Kikomunisti. Baada ya kuupindua Ukhalifa, kilichofuatia ni kufuta alama ya umoja na mshikamano wa Waislamu. Ikiwa ni sehemu ya mkakati huo, walimkabidhi Sultani Abdul-Hamiyd hati ya kumtaka awakabidhi eneo fulani la ardhi ya Palestina ambalo wao walikuwa tayari kulipa gharama yoyote ambayo ingetakiwa. Sultani hakuwa tayari kwa hilo, alilikataa ombi lao. Baada ya kushindwa hapo, Wazayuni wakaanzisha kampeni ya kumpaka matope Sultani huyo ndani na nje ya nchi, wakilenga kuusambaratisha Ukhalifa katika nchi za Waislamu. Propaganda yenye sumu kali iliyoambatana na mipango ya utekelezaji ya Wazayuni kwa kushirikiana na wakuu wa Ulaya, hatimaye ilifanikiwa kusambaratisha mamlaka kuu ya ummah wa Waislamu. Vijana wa Kituruki, kwa kulishwa propaganda za kila wakati sambamba na kupumbazwa na kauli mbiu, walishawishika kuanzisha jumuiya kwa ajili ya kazi mahususi. Baada ya hapo, kidogo kidogo wakajitokeza Waislamu wenye mawazo ya Utaifa. Hili lilikuwa kundi dogo tu lakini lenye nguvu kwani fikra na tabia za watu wake zilisukwa kwa uficho na mfumo tata wa propaganda za Wazayuni. Maskani za Frimasonri (Umasoni) zikatumika kama ngome ya harakati zote ambako walifanya mikutano yao na shughuli zao nyinginezo. Kwa kupiga kauli mbiu, kupandikiza hisia, kuvuruga ukweli wa mambo na kurudia rudia uongo, Wazayuni walifaulu kukoroga bongo za vijana wa Kituruki kupitia maafisa wake mapandikizi (Agent Provocateurs) ikalipua chuki kwa Waturuki dhidi ya Uislamu, Waturuki wakaanza kuwa na hisia za chuki dhidi ya Waarabu, na ikafikia hatua ambapo chuki hii ililipuka kama volkano. Mwishowe ukafika ule wakati ambapo taasisi ya Ukhalifa ilitupiliwa mbali kwa mikono ya jumuiya hii ya vijana na kwa kuchagizwa, kupangiwa mambo na kusaidiwa na mtandao wa uyahudi wa kimataifa wakaanzisha vurugu. Kutokea hapo machafuko katika nchi za waislamu yakawa hayaishi, na jitihada zote za kuwaweka meza moja kushindikana.



Inaendelea Insha'Allah...
 
Umoja Wa Mataifa Na Uzayuni​

Kutokana na utafiti wa kina uliofanywa na mwandishi wa kitabu kiitwacho Jewish Conspiracy, Umoja wa Mataifa, kwa kiasi kikubwa, unaendeshwa na Wazayuni. Hilo linadhihirishwa na ukweli kuwa katika mashirika na matawi yake kumi, si chini ya Wazayuni sabini na watatu wanashika nafasi za juu. Aidha Idara na Vitengo 22 muhimu vya Sekretarieti ya Umoja wa Mataifa vinaongozwa na Wazayuni. Sekretarieti ndiyo sehemu nyeti mno na pengine ndiyo moyo wa taasisi hii ya Ulimwengu ambapo kazi za siri za kubuni sera na programu hufanyika. Endapo utafanyika utafiti makini zaidi juu ya vyombo na mipango ya Wazayuni katika Umoja wa Mataifa basi itabainika kuwa Wazayuni wanautumia Umoja wa Mataifa dhidi ya Mataifa fulani hususani ya Kiislamu. Idara tisa muhimu za UNESCO (Taasisi ya Elimu, Sayansi na Utamaduni ya Umoja wa Mataifa) zinaongozwa na Wazayuni. Takriban Matawi matatu ya ILO (Shirika la kazi duniani) yako mikononi mwa Maofisa wa Kiyahudi. Vile vile kuna Wazayuni wapatao kumi na mmoja ambao wanashika nyadhifa za juu katika Idara muhimu za FAO (Shirika la chakula duniani). Benki ya dunia WB na Shirika la fedha duniani (IMF) zina wakuu wa Idara kumi na tano ambao ni Wazayuni. Sita wako upande wa Benki ya Dunia na tisa wako kwenye fuko la Fedha la Dunia (IMF).

Nafasi zote hizo zinazoshikwa na Wazayuni ndizo nafasi muhimu mno ambazo zina nguvu za ushawishi. Mbali na hao pia kuna Wazayuni wengi katika nafasi za chini katika uendeshaji wa shughuli za Umoja wa Mataifa ambao ni umoja wa nchi malumu na nchi zote. Hebu mtu achekeche bongo na kujiuliza kuwa iwapo Wazayuni wote hawa wanafanya kazi kwa lengo moja na kwa mujibu wa mpango uliosukwa barabara kwa kufuata maelekezo ya makao makuu, ni kwa kiasi gani wanaweza kudhibiti na kuendesha mambo kwa manufaa yao? Na hivi ndivyo ambavyo wamekuwa wakifanya miaka yote tangu pale ulipoanzishwa Umoja wa Mataifa, mwaka 1945. Pengine itawadhihirikia watu wengi kuwa, mashirika ya siri ya Wazayuni yanafanya kazi takriban katika nchi zote ulimwenguni. Katika nchi nyingi, Wazayuni hawana haja ya kuweka taasisi za muundo mwingine bali wanapenyeza watu wao au kuwa na maajenti katika mashirika ya nchi husika na huwa na mamlaka ya kuendesha mambo watakavyo. Kwa mfano, CIA iko mikononi mwa Wazayuni ikipokea malekezo na mikakati toka Israel. Isiajabishe kusikiya kuwa Umoja wa Mataifa ni miongoni mwa vyombo ambavyo kupitia kwavyo Wazayuni wanatimiza malengo yao ya kijasusi kimataifa.

Mwanasiasa, kiongozi au mwanataaluma yeyote anayekwenda kinyume na watakavyo majasusi wa dunia huhatarisha maisha yake, mfano mmojawapo ni wa hapa Tanzania. Aliyekuwa waziri wa elimu, baadaye mipango, kisha fedha marehemu Profesa Kighoma Malima aliondolewa uwaziri wa mipango kwa kuwa hakuwa tayari kupokea sera za kinyonyaji kutoka kwa majasusi wa dunia katika kile kilichoitwa kufufua uchumi wa mataifa hasa ya ulimwengu wa tatu. Ili kumuua kisiasa na kitaaluma, majasusi wa kimataifa waliwatumia maajenti wao hapa nchini. Kazi iliyofanywa na maajenti hao ilikuwa kumpiga vita kupitia magazeti ndani na nje ya nchi. Maajenti hao wakati huo huo walitumia fursa hiyo kufanikisha mipango yao dhidi ya mwanataaluma huyo ambaye kwa wakatoliki alitazamwa kama kikwazo cha masilahi ya kanisa lao wakati huo. Silaha walizotumia zilikuwa udini na uendeshaji vibaya uchumi wa nchi akiwa kama Waziri wa elimu, wa mipango na baadaye wa fedha.

Mwaka wa 1995 iliandikwa makala katika jarida moja kuwa Prof. Malima alikuwa mshiriki katika njama za kuingiza silaha nchini zitumike na “waislamu wenye siasa kali” ili kuvuruga Uchaguzi Mkuu. Wakati ikiandikwa makala hiyo Askofu Polycarp Pengo wa Kanisa Katoliki alisema kuwa Prof. Malima alikuwa mtu hatari ambae ni lazima ashughulikiwe.

Karibu mashirika yote ya Umoja wa Mataifa ni nyenzo ya kutimizia maslahi ya majasusi wa kizayuni duniani kote na Wazayuni wanauona Umoja wa Mataifa na mashirika yake kama ndivyo vyombo muafaka kabisa vya kutimiza malengo yao. Mwanasheria mashuhuri wa Kiyahudi wa Mjini New York, Henry Klein, alielezea mambo haya haya katika kitabu chake kilicho wazi kabisa, Mazayuni wanaotawala dunia (Zions Rule the World, New York, 1948) ameandika:


Umoja wa Mataifa ni Uzayuni. Ni serikali kuu iliyotajwa mara nyingi katika protokali za wanazuoni wakongwe wa Kiyahudi zilizotangazwa rasmi kati ya mwaka 1897 na 1905. Bila kuangalia mawanda ya dunia, mabavu (nguvu za ziada) yanayofanya kazi ulimwenguni pamoja na kuangalia ukubwa wa tatizo, basi hakuna tiba itakayopatikana na hivyo ufumbuzi utabaki kuwa mgumu. Wakati zielezwapo nguvu na hila za Wazayuni dhidi ya ulimwengu wa Waislamu, haina maana kuwa hili ndilo tatizo pekee linalowakabili Waislamu hivi leo. Ila tu hakuna namna ya kuukanusha ukweli kuwa kazi inayofanywa na Wazayuni ndiyo hatari kubwa kwa jamii ya Waislamu popote pale walipo. Matatizo mengineyo ni matokeo tu ya sera zinazotekelezwa na (mtandao wa) Uyahudi wa kimataifa. Wasusi wa mipango ya Wazayuni ni mahodari kweli kweli wa kutekeleza programu yao Duniani kote ikiwa ni pamoja na nchi za Waislamu, ambapo wao hushughulika na kazi ya “kuzalisha” migogoro kwa mpangilio uliotafakariwa barabara. Kwa kweli mbinu yao hii huwa na athari za chinichini mno na ule upeo wa malengo ni wa jumla, kiasi kwamba ni watu werevu na makini tu ndio wanaoweza kuuona mzizi.

******


Uzayuni Na Harakati Za Kuweka Serikali Moja Ya Kidunia

Watu wengi wameuliwa, kuteswa na kutiwa vilema huku ulimwengu wa magharibi (Ulaya) na Marekani ikitoa msaada wa kisiasa na kiuchumi pamoja silaha na zana zinazohitajika kwa wauwaji. Raia wasio na hatia wa Palestina, Afghanistani, Iraq na Lebanon Kusini wameshambuliwa kwa zana nzito za maangamizi, mabomu ya petroli na mabomu ya mtandazo yatolewayo kwa hisani ya taifa linalofuata utamaduni mseto wa Kiyahudi na Kirumi, yaani, Marekani.

Amerika ikiendeshwa na sera za Kizayuni, haijaacha kuwapa wahalifu silaha yoyote iliyo katika bohari yake kuwawezesha kushinda hata kama robo tatu ya watu wamesimama dhidi yao. Mamilioni ya Waislamu katika nchi za Ufilipino, Ethiopia, Eritrea, Somalia, Thailand, Burma, India, Afghanistan, Iraq, Yemen, Misri na kwingineko wanalazimika kupoteza makazi au wanauliwa na kutiwa vilema ama kutokana na mipango na njama za Wazayuni wakiitumia Marekani kama kinga. Huku na kule Waislamu wachache wanaodhaniwa kuwa na misimamo mikali wanapambana kunusurika na tawala kandamizi zinazotaka kuwafutilia mbali. Katika matukio yote haya ya maangamizi, hazijasikika kelele za wito wa kupinga ukiukaji huo wa haki za binaadamu. Hakuna msaada kwa Wahanga, kura ya turufu(veto) imekuwa ikitumika kufunika shutuma za baadhi ya Walimwengu katika umoja wa Mataifa, na kwa hakika Umoja wa Mataifa wenyewe ni mojawapo ya vyombo vinavyotumika kufanikisha njama na mipango ya Wazayuni dhidi ya Waislamu ambao kwa namna itikadi yao ilivyo, wamekuwa wakishukiwa huenda wakawa kikwazo kwa mipango ya kidunia. Mipango ya kusimamisha Serikali moja ya dunia ambayo mabwana wakubwa wake huiita “The New World Order” ni ya tangu siku za uvamizi wa kikoloni duniani, Raisi akiwa Papa na polisi Marekani na Wazayuni wenzao.

Iwapo mtu hafahamu siasa za ulimwengu basi inaweza kumuia vigumu kusadiki kuwepo kwa mpango huo. Hata hivyo utafiti kabambe unaonesha kuwa dunia inasukumwa kibabe, kimila na kiitikadi, kiuchumi, kisiasa na kiteknolojia kuelekea serikali moja ya dunia chini ya wazayuni. Nguvu na hila mbali mbali, zina tamaa kubwa ya kuukamilisha mpango huu baada ya miaka fulani. Taarifa za kijasusi zilizofichuliwa na washiriki wa uundwaji huo wa serikali hiyo ya dunia, zimelitaja shirika la siri la World Constitution and Parliament Association (WCPA), linalomilikiwa na Wazayuni kuwa ndilo lenye kazi hiyo ambalo mipango na nyaraka zake zinathibitisha hayo. Nyaraka hizo zinaweka bayana kuwa mpango wa kuundwa serikali moja ya dunia ni wa kweli kabisa. Ni watu wachache sana wanaoielewa WCPA hivi sasa, lakini uelekeo wa shirika hili umekuwa ukibadilika badilika kulingana na muda na mazingira. WCPA imekuwa haituami na programu za aina moja kwa muda mrefu, programu, utalaamu (wa kitaasisi), mbinu, mipango, mikakati na vitendea kazi vimekuwa vikibadilika mara kwa mara. Japokuwa viongozi wakuu wa mpango huu wamekuwa wakizungumzia “The New World Order” wazi wazi, hakuna hata mmoja anayeweza kuthubutu kufafanua maana halisi ya maneno haya. Ni makundi ya kiislamu yanayoonekana kuwa na mlengo wa siasa kali za kidini ndiyo yanayoonekana kuubaini mpango huo. Huenda hii ndiyo siri kubwa ya kuandamwa Usama Bin Laden na wafuasi wa kundi la Al’qaida. Makundi hayo yamekuwa mawindo ya wauaji wanaojitambulisha kwa ulimwengu kama watetezi wa haki za binaadamu, wapenda demokrasia na wahisani wa misaada ya kibinaadamu. Kati ya hao wamo wanaojiita wanaharakati wa uasilia wa mwanaadamu wakikanusha imani na itikadi za dini zinazoamini Mungu Mmoja, yamo pia makundi ya wanaataluma ambao hushambulia kupitia nyuga za kielimu na yapo makundi fisadi yenye kufisidi kizazi cha mwanaadamu kupitia sanaa, mila na tamaduni. Watu hao wamefanikiwa kuwacheza shere wanwake wote duniani kwa kuwapa urais, uwziri mkuu lakini wakiwavua nguo kwenye magazeti, sinema na michezo ya kisanii. Wanataaluma hufikishwa wakawa maprofesa na kuitwa “great scholars” kwa kukanusha ukweli.

Katika nchi nyingi ulimwenguni, Wazayuni kupitia mawakala wao ambao ni makundi yenye kujitokeza kwa sura ya uhisani (au dini na mila), ndiyo wanaohodhi magazeti makubwa, vituo vya televisheni na redio, mashirika ya habari na vyombo vingine vya mawasiliano ya umma. Wanasuka mambo na matukio ambayo huzidisha matatizo na hali ngumu katika nyanja zote za maisha ya jamii, siasa na uchumi sawia. Wazayuni huamua jambo fulani kuhusu nchi hii au ile; kundi hili au lile; kisha vyombo vya habari hulisuka na kulipa uzito wa juu na baadaye hatuwa kabambe za utekelezaji wa jambo hilo huchukuliwa na hatimaye jambo hilo hutekelezwa. Wanaanzisha harakati fulani za kisiasa, kijamii au kiutamaduni na kutumia ‘kaulimbiu’ kisha vyombo vya habari hutumika kusambaza habari kwa ufundi usiong’amulika ambapo maneno ya hadaa muda si mrefu hutumika ili kuandaa mazingira ya kutimizwa. Hapa watu wanaweza kutafakari juu ya mashindano ya ulimbwende (yanayoitwa Mashindano ya urembo), ndoa za jinsia moja (ulawiti na usagaji), vita dhidi ya kile kinachoitwa ugaidi (hususan kwa watu wenye asili na itikadi ya Uislamu) ambavyo vyote havitenganishwi na mipango ya uyahudi wa kimataifa. Kwa kutumia lugha zao tata, watu hao wanatumai kuupeleka mbali zaidi mpango huo pasipo upinzani au kwa upinzani hafifu kiasi kwamba hautaweza kuwafanya wausitishe.

The New World Order inapiga hodi kama si tayari kufika katika jamii zetu ambapo kadiri muda unavyokwenda inatuwia vigumu kuitathmini mikakati isiyokwisha inayobuniwa na “wakubwa wa ulimwengu” ili kuwaweka watu wote chini ya utawala, mila na utamaduni mmoja wa kufru. Tayari mataifa machanga ni wahanga wa mfumo huu. Raia wa mataifa haya ndiyo waathirika wakubwa, wamekuwa wakiiga na kuthamini kila kiletwacho. Kwa vile itikadi “kuu” ya Wazayuni ni kuhakikisha kwamba ulimwengu unafuata mila yao, kama ilivyobainishwa katika “Ufunuo Mtakatifu wa Karne ya 7” uliyoteremshwa kwa Mtume Muhammad (SAW).


******

Ujasusi Wa Kizayuni Na Mifumo Ya Kijasusi​

Mwaka 1948, serikali ya Kiingereza ilikoma kutawala eneo la Mashariki ya Kati, hata hivyo ikaanzisha “taifa jipya” la Israil ambalo hapakuwa na budi ila kulilinda kwa njia zote kwa kuwa lilizungukwa na wale walioitwa na wanaoendelea kuitwa “maadui” pande zote. Kwa ajili hiyo, usaidizi wa serikali za London na Washington ulihitajika ambapo kiutekelezaji vilihitajika vitengo vya ulinzi wa wazi na siri ndani ya Israil na nje ya mipaka yake isiyo rasmi. Kabla ya hapo mpango wa kulijenga na kuliimarisha Taifa hilo ulisukwa. Makundi kwa makundi ya Wazayuni kutoka ulaya magharibi na Marekani walihamia Israil. Zikabuniwa propaganda kuwa Wazayuni walikuwa katika mateso makali chini ya utawala wa Hitler.

Miongoni mwa vitengo vilivyoundwa kuilinda Israil kilikuwa cha ulinzi na ujasusi, maarufu kikijulikana kama Shay ambacho wakati wa utawala wa Waingereza, wanachama wake walikuwa mkono muhimu wa harakati za chini chini za Mazayuni dhidi ya maeneo ya wenyeji wa asili ya Palestina. Wakazi asilia wa maeneo hayo ni wafilistin na Wayahudi asilia wazawa wa maeneo hayo. Kitengo hiki kilikuwa kikipata msaada mkubwa kutoka kwa ajenti mkubwa wa mazayuni ‘Zionist Congress’, idara iliyoanzishwa mjini Zurich mwaka 1929.

Mara baada ya kuundwa taifa la Israil, wahamiaji kutoka Ulaya na Marekani (Wazayuni) wakiongozwa na Shay walisuka mipango na operesheni za kijasusi sehemu mbali mbali ulimwenguni. Kabla ya hapo, kutokea mwaka 1923 hadi ilipofanikisha mpango wake 1948, Shay ililenga kuanzisha taifa huru la Kizayuni katika maeneo ya Waarabu, kwa hiyo mbinu iliyotumika wakati ule ilikuwa kupandikiza watawala wa Kizayuni kimya kimya ambao kwa sura ya nje, walionekana kama watumishi wa utawala wa Kiingereza, ambao hata hivyo, walitumia fursa ya utawala kuandaa programu na kupanga mikakati dhidi ya Waarabu hasa wakazi wa maeneo hayo. Kwa ajili hiyo, taarifa za kijasusi zilikusanywa ili kutumika katika propaganda na mipango ya utekaji nyara maeneo hayo. Shay ilianza kupandikiza majasusi wake katika makundi pinzani ya Waarabu waliokuwa dhidi ya harakati za uzayuni ndani na pembezoni mwa Palestina. Kazi kubwa ya majasusi hao ilikuwa kuchunguza na kuangalia mienendo ya wanaharakati walioonekana kuwa na misimamo mikali zaidi, hiyo ilikuwa siyo tu katika makundi ya Kiarabu bali pia katika jumuiya za Wazayuni wapinga Uzayuni. Pamoja na kazi hiyo, Shay ilikita ujasusi wake katika kuangalia uuzwaji na uingizaji wa silaha kwa njia za magendo na kuangalia siasa za kinazi ili kuwahakikishia usalama wahamiaji wa kiyahudi waliokuwa wakitoroka kutoka Ulaya kabla na wakati wa vita vya pili vya dunia. Shay iliundwa ikiwa na vitengo vitano vilivyojihusisha pamoja na mambo mengine, ujasusi wa kisiasa (Machlakit Medinit), udhibiti wa mashirika mengine ya kijasusi na usalama wa ndani (Sherut Bitachon Klalt), ujasusi ndani ya jeshi (Sherut Modiin), na polisi maalum ndani ya kitengo cha ujasusi jeshini (Sherut Modiin Shel Mate Arizi).


******

Kuimarishwa Kwa Mfumo Wa Ujasusi Wa Kizayuni

Mwezi Aprili mwaka 1951, aliyekuwa Waziri Mkuu wakati huo, akizungumza katika kikao cha baraza la mawaziri, alitahadharisha kuhusu hali ya kutoelewana iliyosababisha migongano iliyojitokeza ndani ya mfumo wa ujasusi uliokuwepo, hivyo akapendekeza ufanyiwe marekebisho. Kufuatia changamoto hiyo, Baraza likamteua Reuven ShiloahAgaf Modiin). Idara ya ujasusi wa kisiasa ikafanywa ijitegemee ikiwa chini ya wizara ya mambo ya nchi za nje na ikafanywa kuwa idara maalumu ya ujasusi wa nje, Mossad (Mossad Letafkidim Meyouchadim). Kitengo cha ShinBeth kikafanywa kuwa cha usalama wa ndani ya Israil wakati huo huo kikisaidiana na Mossad, kiliwajibika pia kupeleleza harakati dhidi ya Israil nje ya mipaka hasa katika Mataifa ya Waarabu. Idara maalumu iliyokuwa chini ya jeshi la polisi ikawa sehemu ya idara ya usalama kama kitengo maalumu cha ushushushu wa masuala ya ndani kikiwajibika pia chini ya ShinBeth. Mabadiliko yaliyoratibiwa vyema na Shiloah katika mfumo wa ujasusi wa Israil na kuungwa mkono na Mataifa ya Ulaya na Marekani, ndiyo siri ya mafanikio ya Israil kudhibiti mataifa ya Kiarabu yaliyoizunguka pande zote. Mfumo huu mpya ndiyo uliyoongoza vita vya Israil dhidi ya Mataifa ya Kiarabu vilivyoanza mwezi Oktoba na kumalizika mwezi Novemba 1956, na vile vya siku sita vya mwezi juni 1967 na pia mapambano ya mipakani ya mwaka 1963.

Mwezi Julai 1963, kamati ya mabadiliko ya ujasusi iliwasilisha taarifa yake kwa aliyekuwa Waziri Mkuu mpya wa wakati ule, hayati Levi Eskol. Taarifa hiyo ilieleza ya kwamba japo hapakuwa na ulazima utendaji wa Waziri Mkuu na wizara ya ulinzi uwe chini ya mtu mmoja, hata hivyo hapakuwa na budi Waziri Mkuu kuwa na taarifa zote za shughuli za usalama wa Taifa na zile za kijasusi. Waziri Mkuu pia ilitakiwa apewe tathimini huru yenye mitazamo tofauti iliyotokana na vyanzo tofauti juu ya mafanikio na matatizo ya utendaji na watendaji wa idara hizo nyeti kwa maslahi ya Taifa hilo. Kuweza kuyaendea yote hayo, kamati ilipendekeza kitengo cha utafiti kilichokuwa chini ya wizara ya ulinzi kiimarishwe zaidi ili kiweze kujitegemea kiutendaji ambapo kingeyafanyia uchambuzi masuala yote ya kisiasa yenye maslahi kwa Taifa. Ili kukiimarisha kitengo hicho, kamati iliamini kuwa kuundwa kwa kitengo kingine maalumu kwa ajili ya ushushushu na ufanyaji wa tathimini ya taarifa za kijasusi, ilikuwa muhimu zaidi ili kuipunguzia majukumu idara ya usalama jeshini, kwa sababu mpaka wakati ule kazi hiyo kwa kiyasi kikubwa ilikuwa ikifanywa chini ya idara hiyo. Kamati hiyo pia ilioneleya kuwepo kwa Mossad ambayo ingekusanya na kudhibiti taarifa nyeti ambazo zingekusanywa kutoka mataifa ya nje na kuziwasilisha kwenye idara za usalama wa ndani, ShinBeth. Kwa kiasi kikubwa kuwepo kwa utendaji wa aina hiyo kungehimiza mahitajio ya kuundwa kwa kitengo kingine huru cha kutathimini shughuli zote za ujasusi. Kamati hiyo pia iliona ingelikuwa muhimu sana kuwepo mshauri maalumu wa kumsaidia Waziri Mkuu ambaye, akiwa chini ya ofisi ya Waziri Mkuu, angekuwa mwajibikaji wa ngazi ya juu kabisa katika uendeshaji wa shughuli za usalama wa Taifa na Ujasusi. Hata hivyo, utekelezaji wa mapendekezo hayo haukuanza mpaka pale shughuli zote za usalama na ujasusi wa ndani zilipohamishiwa idara maalumu ya ShinBeth ambayo usimamizi wake ulihamishiwa moja kwa moja ofisi ya Waziri Mkuu kutoka ofisi ya Waziri wa Ulinzi. Mwezi julai 1966, aliyekuwa Mwenyekiti wa kamati ya ulinzi na Mkurugenzi wa Mossad, Isser Harel akateuliwa kuwa mshauri maalumu wa Waziri Mkuu katika masuala ya usalama wa Taifa. Hata hivyo, tathmini iliyokuja kufanyika baadaye ilionesha kwamba Harel hakuwa akiwajibika vema, hivyo alilazimishwa kujiuzulu.

Kufuatia kilichoonekana kushindwa kwa shughuli za ujasusi chini ya Harel, serikali ya Israil ikaunda Tume maalumu mnamo mwezi Novemba 1973 kuchunguza masuala mbali mbali katika idara na vitengo vya usalama na ujasusi. Tume hiyo ilipewa jukumu la kupeleleza idara na vitengo vyote vya ujasusi kisha kuwasilisha tathimini na mapendekezo yake serikalini. Tume hiyo ilikamilisha ujasusi ndani ya idara za ujasusi kisha ikawasilisha Taarifa yake mwezi Aprili 1974 ikipendekeza pamoja na mambo mengine kuwa, nafasi ya mshauri maalumu wa Waziri Mkuu katika masuala ya usalama na ujasusi iimarishwe zaidi. Aidha Tume Maalumu ilipendekeza idara za usalama na ujasusi zifanyiwe mabadiliko mengine kwa kuanzishwa kitengo kingine cha utafiti na tathmini ndani ya idara ya ujasusi wa nje (Mossad) ambayo ingewajibika chini ya Wizara ya Mambo ya nje. Lengo la mabadiliko hayo lilikuwa kuepusha masuala ya usalama na ujasusi kuhusika moja kwa moja na utendaji wa jeshi ingawa watendaji wake walipaswa kuwa na mafunzo kamili ya jeshi. Kiutekelezaji, Tume ilisisitiza uwepo uratibu madhubuti hasa katika ukusanyaji wa “bidhaa” za kijasusi, hata hivyo kiusalama ikatahadharisha kuwa maamuzi ya mwisho yafanywe na kamati maalumu ndani ya mfumo wa usalama.

Mwaka 1974 hadi 1976, mapendekezo ya taarifa huru ya tume ya Agranat yalianza kutekelezwa ambapo aliyekuwa Waziri Mkuu alimteuwa Jenerali Rehavam Zeevi kuwa mshauri wake katika mambo ya usalama na ujasusi. Vile vile Zeevi akawa mshauri wa Waziri Mkuu katika masuala ya vita dhidi ya ugaidi ndani na nje ya Israil na akawa pia mwambata wa mkurugenzi wa usalama jeshini na vile vile akawa afisa maalumu wa kumtaarifu Waziri Mkuu juu ya tofauti za kimawazo zilizokuwa zikijitokeza katika idara na vitengo vya usalama na ujasusi. Hata hivyo, mnamo mwezi Oktoba 1976 Jenerali Zeevi alijiuzulu na nafasi yake ikashikwa na Brigedia Yehoshafat Harkabi aliyekuwa mkurugenzi wa usalama Jeshini. Pendekezo la kuwepo kwa kituo cha utafiti na mipango chini ya wizara ya mambo ya nje, lilianza kutekelezwa mwezi Januari mwaka 1975, kutokea hapo yakafanyika mabadiliko makubwa katika mfumo wa ujasusi. Kitengo kipya cha utafiti na tathmini kikaanzishwa chini ya Mossad ambacho kilipewa kazi ya kupitia taarifa mbali mbali za kijasusi. Walioteuliwa kuwa watendaji, waliwakilisha tanzu zote za mfumo wa ujasusi nchini Israil.

Mwezi Juni 1977, serikali ya Israil ilianzisha kamati maalumu iliyopewa wajibu wa kusimamia na kushauri masuala ya usalama na ujasusi. Shabaha kuu ya kamati hiyo ilikuwa kuyafuatilia mataifa ya Kiarabu na kiislamu kujuwa uwezo na makusudio yao dhidi ya Israil, silaha na mikakati yao ya kijeshi, misimamo ya viongozi wao, siasa za ndani na nje, ari na matayarisho yao kijeshi. Israil pia ilikuwa ikikusanya taarifa zilizoisaidia kutunga sera na utoaji wa maamuzi yenye ushawishi kwa siasa za Marekani. Pamoja na hilo imekuwa ikipenyeza na kupandikiza maajenti wake katika uendeshaji wa serikali ya Marekani. Aidha imekuwa ikikusanya taarifa za kisayansi kwa malengo ya kijasusi kwa ajili ya Marekani na mataifa mengine yaliyoendeleya, vivyo hivyo imekuwa ikifuatilia kwa karibu harakati zote dhidi ya Uzayuni katika mataifa mbali mbali duniani. Komandi kuu ya ujasusi wa Israil imekuwa ikikusanya taarifa zenye malengo ya kisiasa na kiuchumi kutoka maeneo mbali mbali duniani kupitia mawakala wake katika balozi zake na zile za Marekani. Malengo makuu ni kudhibiti maeneo yote yenye masilahi kwa Israil barani Afrika, nchi za Kiislamu, Ulaya na Marekani.

Kwa upande mwingine, Israili imekuwa ikifanya jitihada kubwa kujibu propaganda za mataifa ya Kiarabu na kuzima matendo dhidi ya uzayuni. Hili limekuwa likienda pamoja na mashambulizi dhidi ya makundi ya kiislamu na Kiarabu yanayohusishwa na matendo ya kigaidi. Shughuli za kijasusi ndani na nje ya Israili wakati ule zilikuwa zikifanywa chini ya kifungu namba 29 cha sheria za Israili ambacho kinahalalisha shughuli zote za ujasusi kufanyika bila ya kujali mipaka ya kanuni. kuandaa mpango wa mabadiliko ya mfumo wa ujasusi wa Israili, ambaye katika taarifa yake alipendekeza pawepo na mgawanyo wa kazi na utendaji, kwa ajili hiyo akapendekeza pia pawepo na kitengo cha uratibu wa shughuli zote za ujasusi. Mapendekezo mengine ya Reuven ambaye alipewa uenyekiti wa kamati ya wakuu wa usalama, yalikuwa ni kuunganisha pamoja shughuli za ujasusi za Nava, usalama wa Taifa na ulinzi wa anga. Shughuli zote hizo zilitakiwa kuwajibika chini ya idara ya ujasusi jeshini

“Kwa niaba ya dola na kwa mujibu wa sheria, serikali inaidhinishwa kufanya jambo lolote la kijasusi hata lile linalokiuka sheria kiutekelezaji”.
Kifungu hicho kilikuwa na maana ya kuipa mamlaka serikali kuu kuendesha shughuli za kijasusi na masuala ya usalama kwa kuwa hapakuwa na mamlaka nyingine yoyote ambayo ilipewa uwezo wa kisheriya kufanya shughuli hizo za siri nje ya serikali. Hata hivyo sheria ya usalama wa ndani ya Israili kwa upande mwingine iliainisha bayana kuwepo kwa kanuni za hali za dharura ambazo ziliwekwa mwaka 1945, sheria ya kijeshi namba 21 iliyopitishwa mwezi juni 1955 na kifungu cha sheria ya usalama wa taifa (State Security Act) namba 31 iliyopitishwa mwezi julai mwaka 1957. Sheria ya hali hatari ya mwaka 1945, ilikuwa ikilipa uwezo jeshi kumkamata mtu yeyote, kudhibiti wakorofi na kuvamia au kushambulia maeneo yote yanayotuhumiwa kuwa na hatari dhidi ya Israil. Hiyo ililenga kuvamia makundi ya Wapalestina na kushambulia vituo vya kijeshi vya mataifa ya Kiarabu yalioonekana kuhatarisha usalama wa Israil. Ili kuweza kuwajibika vyema, vitengo vya usalama wa ndani ya Israil viliajiri watendaji rasmi na wale ambao hawakuwa rasmi ambao walikuwa wakiwajibika chini ya idara ya polisi tangu mwaka 1966, mwaka mmoja kabla ya vita na Waarabu mwaka 1967. Sheria ya Israil iliweka adhabu kali ya ama kifo au kifungo cha maisha kwa mtu yeyote aliyepatikana na makosa ya kula njama dhidi ya serikali au kuwasaidia maadui. Vile vile kifungo kisichopungua miaka 15 kwa wale waliokutikana na makosa ya kuipeleleza Israili kwa ajili ya mataifa mengine.

Pamoja na hilo, mtumishi yeyote wa serikali aliyepatikana na kosa la kuvujisha siri za serikali kwa maajenti wa nje, kusaidia au kutenda uhalifu dhidi ya serikali, alikabiliwa na adhabu hizo kali.


(¯`·._.•inaendelea Insha'Allah™•._.·´¯)
 
Last edited by a moderator:
Kamati Maalumu Ya Va’adat

Wakati ukiasisiwa, mfumo wa ujasusi wa Israil ulikuwa chini ya kamati maalumu iliyoitwa Va’adat. Moja ya kazi za kamati hiyo ilikuwa kuunganisha shughuli zote za ujasusi na usalama wa Taifa ndani na nje ya Israil. Va’adat iliundwa na wakuu wa kurugenzi zote. mkurugenzi wa Mossad, mkurugenzi wa kitengo cha ujasusi jeshini, mkurugenzi wa ShinBeth, mkuu wa jeshi la polisi, mkurugenzi mkuu aliyekuwa chini ya wizara ya mambo ya nje, mkurugenzi wa kituo cha utafiti na mipango kilichokuwa chini ya wizara ya mambo ya nje na mshauri wa waziri mkuu katika masuala ya ujasusi wa kisiasa, jeshi na masuala ya ugaidi. Mkuu wa kitengo maalumu katika idara ya upelelezi ya polisi pia alipaswa kuhudhuria baadhi ya vikao vya Komandi hiyo ambaye wakati mwingine alikuwa akimwakilisha mkuu wa Jeshi la Polisi. Komandi hiyo ilifanya vikao vyake vya tathmini kila baada ya wiki mbili, hata hivyo idadi ya vikao iliongezeka kulingana na taarifa za kiusalama. Katika vikao vyote kila mkurugenzi alipaswa kuwasilisha taarifa fupi juu ya mambo muhimu yaliyojitokeza kwenye kurugenzi yake katika muda wa wiki mbili kabla ya kikao. Mwenyekiti wa vikao hivyo alikuwa Mkurugenzi wa Mossad ambaye kwa wadhifa huo alipaswa kuwajibika moja kwa moja kwa Mkuu wa Ujasusi, waziri mkuu wa Israil ambaye anapaswa kuwa na cheo cha Jenerali. Hata hivyo, hiyo haikuwa na maana kuwa mkurugenzi wa Mossad alikuwa na wadhifa zaidi kuliko wengine katika Va’adat. Wajumbe wote wa Va’adat walikuwa na wadhifa sawa ambapo kiutendaji wakati mwingine, ukurugenzi wa ujasusi jeshini alionekana kumzidi mkurugenzi wa Mossad. Hili lilijitokeza zaidi kwa kuwa Israil ililipa jeshi kipaumbele katika siasa zake za kujilinda dhidi ya maadui waliyoizunguka. Wakati ambapo Mossad iliwajibika zaidi na ukusanyaji wa taarifa za kijasusi na kuendesha programu za siri nje ya Israil, ShinBeth iliwajibika na usalama wa ndani ya Israil na udhibiti wa matendo ya kijasusi ya mashirika mengine pamoja (counter intelligence).

ShinBeth ilikuwa ikifanya kazi kama ‘idara nyeti’ ya serikali katika masuala ya Usalama wa Taifa, vile vile iliwajibika kumlinda Waziri Mkuu na maafisa wengine wa ngazi za juu serikalini. ShinBeth pia ilihusika na ulinzi wa siri pamoja na usimamizi mkuu wa ulinzi wa maghala, viwanja vya ndege na maeneo yote nyeti wakati huo huo ikiandaa operesheni maalumu nje ya Israil hasa katika mataifa ya Kiislamu na Kiarabu. Hata hivyo, ShinBeth haikuwa na wajibu wa kukamata watu, dhima hiyo ilikabidhiwa kitengo maalumu cha idara ya upelelezi iliyokuwa chini ya jeshi la polisi ambayo hata hivyo ilishirikiyana kwa karibu na ShinBeth. Katika baadhi ya maeneo maalumu ya mipakani ambayo yaliwekewa ulinzi mkali wa kijeshi, ShinBeth hutumika kuwasaka na kuwakamata maadui. Idara ya usalama ya jeshi, mbali ya kazi zake za kistratejia, huandaa makadiriyo na kufanya tathmini juu ya taarifa zote zihusuzo harakati za makundi ya Kiarabu na Kiislamu eneo lote la mashariki ya kati. Kazi nyingine ilikuwa ni kubuni na kuunda alama maalumu za utambulisho (code numbers) katika mawasiliano ya watendaji wake. Kituo cha utafiti na mipango ya kisiasa ambacho awali ilikuwa kitengo cha utafiti cha wizara ya mambo ya nje, kikapewa kazi ya kuchambua taarifa za awali kutoka vyanzo mbali mbali kwa ajili ya utunzi na uwekaji wa sera. Taasisi nyingine za serikali zilizohusika moja kwa moja na masuala ya usalama na ujasusi zilikuwa ni pamoja na wizara ya fedha na utalii, idara ya mambo ya anga, El Al, na idara ya uchukuzi na upakiaji wa mizigo. Jumuiya zisizo rasmi za mazayuni zinazomilikiwa au kudhaminiwa na jamii za kiyahudi duniani kote nazo zinalazimika kutoa misaada ya kijasusi pale zinapohitajika.

Awali, wakati wa kuanzishwa kwake, ‘idara nyeti’ ya usalama na ujasusi ilikuwa na watumishi waliokadiriwa kufikia 11,600, idadi hii ni mbali ya watumishi 12,000 wa jeshi la polisi na 6000 walinzi wa mipakani. Kimchanganuo, Mossad ilikuwa na watendaji 3500 kati yao 500 walikuwa maafisa. ShinBeth ilikuwa na zaidi ya watumishi 1000 kati yao 550 walikuwa maafisa wa ngazi za juu. Idara ya usalama jeshini ilikuwa na watendaji wasiopunguwa 7000 kati yao 450 walikuwa maafisa wa jeshi wa vyeo mbali mbali, wengine walikuwa wafanyakazi za kiraia wakiwemo makarani wa masjala na wale wa uhasibu. Idadi ya watendaji wa kituo cha utafiti na mipango ya kisiasa kilichokuwa chini ya wizara ya mambo ya nje ilikuwa kati ya 75 hadi 100. Kwa kuwa upatikanaji wa fedha za uendeshaji wa shughuli za ujasusi lilifanywa kuwa jambo la siri kubwa, ilikuwa vigumu kwa mtu au chombo chochote kupata taarifa sahihi juu ya fedha zinazotengwa kwa ajili ya shughuli za ujasusi wa Israili ndani na nje hasa zile za kudhibiti harakati za Mataifa ya Kiarabu na ulimwengu wa Waislamu. Pesa zilizokuwa zikitengwa kwa ajili ya mipango ya kimataifa kupitia taasisi mbali mbali za kimataifa zilizo chini ya Umoja wa Mataifa pia hazikuwa zikifahamika.

Israili ndiyo inayoziendesha serikali mbali mbali duniani kwa siri, yakiwemo mataifa yenye nguvu za kijeshi, kisiasa na kiuchumi. Katika moja ya mikakati yake ya kijeshi, Israil inasema yenyewe haina jeshi kubwa lakini ina uwezo wa kuyatumia majeshi ya nchi kubwa kutimiza malengo yake, kwa ajili hiyo bajeti ya matumizi ya shughuli za ujasusi na usalama wa Taifa zimekuwa zikiunganishwa katika wizara ya ulinzi zikifahamika na watu maalumu; waziri mkuu, waziri wa ulinzi na wasaidizi wao, waziri wa fedha, mdhibiti mkuu maalumu wa masuala ya ulinzi na usalama katika fedha, ambaye hufanya kazi pamoja na wakurugenzi wa Va’adat. Wakurugenzi wote hao, kama dasturi, hupaswa kuwasilisha bajeti zao mwezi Aprili kila mwaka. Kwa ajili hiyo, watendaji wote hao ilikuwa lazima wawe ‘wanachama’ wa Va’adat. Makadirio ya mkurugenzi anayeheshimika zaidi kwa uaminifu na uadilifu, kwa kawaida, ndiyo hukubaliwa mwanzo ikiwa ni hatua ya awali ya maafikiano katika upitishaji wa bajeti. Akiwa mtendaji muhimu katika masuala ya fedha za ulinzi na usalama wa Taifa, mdhibiti na mkaguzi Mkuu wa hesabu za serikali kazi zake ni pamoja na kuandaa mikutano na wakurugenzi wa idara za ujasusi pamoja na watendaji wao wakuu. Mikutano hiyo ni ya upitiaji kwa undani programu na mipango iliyokadiriwa fedha. Hii ilikuwa ikifanyika kabla ya Bajeti na kuendelea hadi mwezi Mei kwa lengo la kuhakiki gharama zilizoainishwa. Mpaka kufikia mwezi Oktoba, upitizi wa kichambuzi wa programu zote hukamilika tayari kuwasilishwa wizara husika ambayo watendaji wake maalumu wa masuala ya bajeti huipitia tena kabla ya kuidhinishwa. Ili kuzifanya kwa usiri, shughuli nyingi za kiutawala katika masuala ya ulinzi, usalama na ujasusi, huendeshwa na wizara ya ulinzi. Kwa hivyo basi, yenyewe ndiyo komandi kuu ya operesheni zote za masuala ya umbo la pembe-tatu, yaani, ulinzi, usalama na ujasusi. Kwa ujumla, idara ya usalama na ile ya ujasusi ndizo zenye umuhimu zaidi serikalini kuliko idara zote, afisa usalama huwa na mamlaka huru kuingia popote serikalini na uraiani kama sehemu za shughuli zake. Shughuli za ujasusi huunganishwa na kila eneo la utendaji ndani ya serikali na vyombo vyake mpaka uraiani, zikisimamiwa na wizara ya mambo ya nje. Watendaji waandamizi wa wizara hiyo ni maafisa usalama wastaafu hivyo ni watu wenye ufahamu mkubwa wa masuala ya ujasusi, wenye kuufahamu nje, ndani, mfumo wa usalama, malengo makuu na matatizo yake. Zaidi ya hilo, karibu kila mwanadisplomasia wa Israil aliyeko nje ya nchi ni jasusi mwanataaluma na mweledi mzuri wa lugha za kigeni ambazo humuwezesha kuhusiana kishughuli na wenyeji wa nchi au eneo alilopo.



Idara Ya Ujasusi Ya Shinbeth

Katika miaka ya mwanzo ya kuundwa kwa Israil, mfumo wa usalama wa Israil uligawanyika sehemu mbili; usalama ndani ya serikali (Government Intelligence and Security) na usalama uraiani (public security). Kwa hiyo, ujasusi chini ya mfumo wa kizayuni umedhibiti kila idara, ofisi, kampuni au shirika serikalini na karibu katika sekta zote binafsi za maisha ya kila siku ya jamii. Karibu kila sehemu ya uraiyani iko chini ya uangalizi wa kijasusi mbali ya vyombo kama polisi na idara zake za wazi na siri zinazohusika na udhibiti wa uhalifu na jinai nyinginezo. Takribani wakurugenzi na mameneja wote wa idara, viwanda, jumuiya na mashirika ya kiserikali na yasiyokuwa ya kiserikali zikiwemo jumuiya za kidini, ni waajiriwa wa idara ya usalama wa ndani, ShinBeth, ambao huhusika ama moja kwa moja au kupitia kwa, na idara hiyo.

Afisa yeyote wa ShinBeth aliyeajiriwa ama katika jumuiya, idara au kitengo chochote cha kijamii, hupaswa kuwajibika sehemu mbili; kama afisa wa idara, ambaye pamoja na “ajira” yake hulazimika kuwasilisha taarifa za kijasusi “idarani”; vile vile hupaswa kuwajibika kiadilifu kama mwajiriwa wa kampuni, jumuiya, ofisi au shirika lililomwajiri. Kwa ajili hiyo, watu waliokuwa na taaluma ya ujasusi mara nyingi ndiyo walioteuliwa kushika nafasi au kufanya kazi muhimu serikalini. Ilifanywa hivyo ili ShinBeth iwe na taarifa kamili za ofisi, wizara, idara na jumuiya zote za kiserikali na zisizo za kiserikali, za umma na za binafsi, kutokana uwezo waliokuwa nao waandamizi waliokuwa pia maafisa usalama wa ufanyaji kazi mbili kwa wakati mmoja; kutekeleza wajibu wao kama waajiriwa sambamba kuwajibika kama maajenti wa idara ya usalama. Maafisa hao hutakiwa kuwa wachapakazi hodari na waaminifu kama kinga ya uajenti wao wa kijasusi. Kwa kawaida, afisa yeyote hakuruhusiwa kujiunga na chama chochote cha siasa bila ya kuwa na shughuli maalumu au kupata rukhsa maalumu kutoka ngazi ya juu ya kurugenzi anayoiwajibikia.

Kwa upande mwingine, kazi ya kujadili masuala nyeti ya nchi ni la Kamati ya Ulinzi na Mambo ya nje ambayo hupitia na kuyatafutiya ufumbuzi masuala mazito yanayohusu maslahi ya nchi. Wakurugenzi wa Mossad na ShinBeth pia ni wajumbe wa vikao vya kamati hiyo hususan katika mijadala, tathmini na upitiaji wa masuala yanayohusisha uwajibikaji wa kurugenzi zao. Katika baadhi ya nyakati, maafisa usalama wa Israil walilazimika kusimama mahakamani kutetea utaratibu wa utendajikazi wa idara za kijasusi hasa katika matukio ya utekaji nyara kama mbinu ya kijasusi iliyokuwa ikitumiwa na mashirika ya kijasusi ya Israil miaka ya sitini dhidi ya makundi ya wapinzani wa mfumo wa kizayuni.

Siri ya mafanikio ya harakati za kizayuni dhidi ya mataifa ya Kiarabu na yale ya Kiislamu ni mtandao wao imara wa ujasusi. Kujiamini kwa Israil katika masuala ya ujasusi kuliimarika zaidi kufuatia ushindi wa vita vya siku sita kati ya Israil na Mataifa ya Kiarabu mwaka 1967. Vikitaarifa ushindi huo kwa shangwe kubwa, vyombo vya habari vya Israil vilisifu mchango mkubwa uliotolewa na duru za usalama na ujasusi. Kitengo cha usalama jeshini, idara ya usalama ya ndani, ShinBeth, idara ya ujasusi nje ya nchi, Mossad na kitengo cha usalama ndani ya Jeshi la Polisi, ndivyo vilivyofanikisha ushindi wa Israil dhidi ya mataifa ya Kiarabu. Kamati ya usalama ya Israil inataarifawa kuwa iliweza kuyatumia mashirika ya CIA ya Marekani na KGB ya iliyokuwa Urusi (USSR) kukusanya taarifa za kijasusi kutoka ndani ya mataifa ya Kiarabu, na miongoni mwa taarifa hizo ndizo zilizofanikisha kulipuliwa kwa ndege za kivita za Misri zilizotengezwa Urusi (USSR) zilizokuwa zikijiandaa kuruka kutoka uwanja wa ndege za kijeshi kwenda kuishambulia Israil.

Uimara wa mtandao wa ujasusi wa Israil unajitokeza pia katika tukio la uwokozi wa mateka wa Israil kwenye uwanja wa ndege wa Entebe, Uganda mwaka 1976. Operesheni hiyo ya aina yake katika ulimwengu wa ujasusi ilipangwa na kuratibiwa vyema chini ya Kamati ya usalama na ujasusi ikishirikisha mawakala waliokuwa wanadiplomasia katika ubalozi wa nchi hiyo Nairobi nchini Kenya wakishirikiana na majasusi wenzao waliokuwa wafanyakazi za kidiplomasia katika baadhi ya balozi za nchi za Ulaya nchini Uganda. Wakati wa utawala wa Jenerali Idd Amin, Israil haikuwa na ubalozi nchini Uganda. Mafanikio hayo yaliifanya Israil izidi kujiamini katika uwanja wa ujasusi ikijilinganisha na mataifa mengine duniani.

Katika mfumo wa ujasusi wa kizayuni, wakurugenzi na maafisa waandamizi wa idara za kijasusi ndio wanaotakiwa kuandaliwa vyema zaidi kitaaluma kuliko watendaji wengine. Waandamizi hao, kila mmoja, hutakiwa kuwa na mtandao wake, vyanzo na utaratibu wa ukusanyaji wa taarifa zinazotakiwa kuwasilishwa ngazi baada ya ngazi kwa ajili ya uchambuzi kabla ya kufikishwa makao makuu. Vilikuwepo viwango maalumu vya elimu vilivyowekwa ambavyo mtu alitakiwa kufikia ili kupata uafisa kamili wa idara la ujasusi na ile ya usalama. Palihitajika kufanya hivyo kwa kuwa mfumo wa ujasusi nchini Israil umegubikwa mwavuli wa usiri mkubwa usiotakiwa kujulikana uhalisia wake na yeyote nje ya jumuiya hiyo. Ni kikundi kidogo sana cha watu wa wadhifa wa juu serikalini wenye kupaswa kuwa na taarifa “nyeti” zihusianazo na masuala “nyeti” yanayohusu utumishi, mipango ya bajeti na uhasibu ndani ya ulimwengu wa ujasusi wa Kizayuni.

Mtandao wa usalama na ujasusi wa Israil ni miongoni mwa mitandao bora ya ujasusi, ushushushu na ukachero duniani. Utaalamu mkubwa na mbinu zake za hali ya juu zimeweza kufanikisha mambo mbali mbali yenye masilahi kwa taifa hilo hasa dhidi ya ulimwengu wa Waarabu, Waislamu na Wakristo. Ulimwengu wa Waislamu na ule wa waarabu hivi leo unalizwa na ‘mrejesho’ hali kadhalika ‘mlisho’ wa harakati za kijasusi za Kizayuni. Mfumo huo wa ujasusi ulioundwa na kuendeshwa kwa ustadi mkubwa umewezesha kukusanywa, kuratibiwa, kuchujwa na kutathiminiwa kwa taarifa zote kutoka kwa mawakala, jumuiya za kiyahudi, ofisi za ubalozi, mashirika ya kimataifa yasiyo ya kiserikali, mashirika ya haki za binaadamu na vyanzo vingine vya taarifa ulimwenguni kote, kisha kuandaa operesheni mbali mbali zenye masilahi kwa Israil. Ujasusi umeiwezesha Israil kuziendesha serikali na mataifa makubwa duniani, kuyadhibiti mataifa ya Kiarabu, kupambana na Waislamu, wakristo, kupenyeza mawakala katika mashirika ya Umoja wa Utaifa, makao makuu ya umoja huo, na katika serikali za mataifa makubwa ya Ulaya na Marekani. Kwa mtandao huo, imeweza kuathiri maamuzi, kuweka watawala vibaraka na kuendesha serikali mbali mbali duniani kupitia mawakala wake.


Idara Ya Ujasusi Ya Mossad

Mossad ndilo shirika linalohusika na ujasusi nje ya Israil likikusanya taarifa, kuratibu na kutengeneza matendo au matukio ya kisiasa nje ya Israil na kudhibiti upinzani dhidi ya Israil chini ya kitengo cha ugaidi. Katika kutekeleza kazi zake za kukusanya taarifa sahihi za kijasusi, Mossad imekuwa ikiweka maajenti katika nchi za Kiarabu na imekuwa ikihakikisha kuwa wawakilishi wa nchi hizo sehemu mbali mbali duniani wanakuwa mawakala wake. Wengi wa maafisa wa serikali na wanadiplomasia wa nchi za Kiarabu katika nchi za kigeni hasa katika nchi za Ulaya na Marekani ni mawakala wa Mossad.

Mossad inakusanya taarifa zinazohusu nyadhifa za watendaji, ari, zana za kijeshi na idadi ya vifaa vinginevyo vinavyohusika na jeshi pamoja na kuyachunguza kwa makini majeshi ya nchi za Kiarabu. Mossad pia hukusanya taarifa zote zenye kutoa mwanga juu ya siasa za ndani za nchi za Kiarabu na uhusiano miongoni mwa viongozi mashuhuri katika nchi hizo na harakati zote za kidiplomasia katika nchi zote hizo. Aidha, Mossad imekuwa ikipeleleza shughuli zote za kibiashara za mataifa ya Kiarabu hasa katika ununuzi wa zana za kijeshi kutoka nchi za magharibi na kwa ajili hiyo huingilia kati kuzifanya nchi za Kiarabu zisiweze kujitayarisha vyema kijeshi kwa kuzuiliwa zisiwe na wataalamu wake katika uchumi na siasa. Uingiliaji kati wa Israil mara nyingi ni ule wa kupenyeza mawakala wake katika maeneo hayo au kufanya operesheni za kijeshi. Israil ililipua kiwanda cha zana za kinuklia kilichokuwa kikijengwa Iraq wakati wa Saddam Hussein. Israil kupitia mawakala wake walio watendaji katika serikali ya Marekani iliwalipuwa makomandoo 70 wa Misri waliokuwa wakirejea kutoka Marekani ambako walikwenda kwa ajili ya kile kilichoitwa kufanya mazoezi ya pamoja ya kijeshi baina ya wataalamu wa Marekani na wale wa Misri. Mpango wa kuwalipua maafisa hao wazito ulisukwa na mtandao wa Mossad.

Aidha Mossad imekuwa ikipanga operesheni maalumu za kuchochea migogoro ili kuvuruga uhusiano miongoni mwa nchi za Kiarabu wakati huo huo kujaribu kuhamisha mazingatio ya nchi za Magharibi kwa mataifa hayo na huchunguza mienendo, propaganda na matendo ambayo huyafasiri kama ni ya kigaidi dhidi ya Israil. Nchi ya Lebanon imekuwa uwanja mzuri kwa Mossad kutokana na mchanganyiko wake wa Wakristo, Wadruze na Waislamu, hali ambayo imeiwezesha Mossad kuendesha shughuli za kijasusi kwa mafanikio makubwa. Ilikuwa ikiunda makundi ya wanamgambo wa Kidruze kushambulia maeneo ya Wapalestina, vile vile ilikuwa ikitoa msaada mkubwa kwa Wakristo wa mlengo wa kulia waliokuwa wakichochea migogoro kati ya Waislamu na Wakristo iliyosababisha vita vya wenyewe kwa wenyewe vilivyodumu muda mrefu miaka ya sabini.

Mbali ya kuendesha operesheni dhidi ya mataifa ya Kiarabu na Kiislamu, Mossad imekuwa ikikusanya kijasusi taarifa za kisayansi, kiuchumi na kisiasa kutoka nchi zilizokuwa za kambi ya mashariki na zile za magharibi kwa ajili ya kujilinda yenyewe, kutekeleza sera zake za kizayuni kwa manufaa ya uyahudi. Aidha shughuli za kijasusi za Mossad zilitoa kipaumbele kwa uliokuwa Muungano wa Soviet (USSR) na inaendelea kufanya hivyo kwa Marekani kwa kuwa sera na maamuzi yanayotolewa serikali hizo huwa na athari kubwa kwa Israil na harakati za Uzayuni. Malengo ya shughuli za kijasusi za Mossad kwa uliokuwa Muungano wa Soviet (USSR) na nchi za mashariki kwa ujumla, yalijumuisha, pamoja na mambo mengine, kuhakikisha sera za mataifa hayo, zilizoilenga Israil na tatizo la uliokuwa uhamiaji wa Wazayuni katika maeneo ya wapalestina, kuwa zinaendana na matakwa ya Israil. Hiyo ilikuwa ni pamoja na kupandikiza warasimu kistratejia iliowapata kupitia njia kuu mbili; kuwahonga au kuwashawishi ili kufanya kazi ya kijasusi katika mataifa hayo kwa masilahi ya Uzayuni na kupitia teuzi mbali mbali za watendaji wa serikali hizo. Kwa mfano wakati wa serikali ya Bill Clinton asilimia 80 ya watendaji wake walikuwa Wazayuni kwa utashi wa Jewish Lobby la Marekani12.

Vivyo hivyo, malengo ya Mossad katika mataifa ya Magharibi yalikuwa yale yale ya kutazama maslahi ya Uyahudi. Mossad imekuwa ikikusanya taarifa za kijasusi zinazohusu mipango na sera za Magharibi na Vatican, kupitia mawakala wake walio watendaji wa ngazi za kimaamuzi. Mossad pia imekuwa ikipenyeza kwa siri katika Umoja wa Mataifa sera za kuinufaisha Israil, vile vile imekuwa ikijikusanya taarifa-ghafi muhimu kupitia Umoja huo zinazoisaidia kudhibiti hatua zozote za nchi za magharibi zinazoashiria kuwa dhidi ya malengo ya Israil. Miaka ya mwanzo baada ya taifa la Israil kuundwa, Mossad ilikuwa na kurugenzi nane: Kurugenzi ya Mipango, Uratibu na Operesheni; Idara ya Ukusanyaji wa Taarifa; Kurugenzi ya Siasa na Uambata katika nchi za kigeni; Kurugenzi Kuu ya Utumishi na Utendaji; Fedha; Ugawaji wa Vifaa (logistics); Ubunifu wa mbinu za kijasusi, mafunzo na utafiti, operesheni za kiufundi; na ile iliyohusika na teknolojia.

Kurugenzi ya mipango, uratibu na Operesheni ilihusika na mambo ya utawala na uendeshaji wa shughuli zote za Mossad pia ilikuwa kiungo cha Kurugenzi zote za operesheni ikisimamia kazi zote za utawala ndani ya shirika hilo na ikiunganisha shughuli zote za kijasusi ndani ya Israil. Kurugenzi hiyo pia ilikuwa ikishughulika na yote yaliyohusika na ukusanyaji wa taarifa na upangaji wa mipango. Kurugenzi ya Siasa na Uambata wa Kijasusi katika nchi za kigeni ilihusika na matendo na hali za kisiasa pamoja na uhusiano wa kirafiki na mashirika ya kijasusi ya nje kwa manufaa ya Israil. Kurugenzi hii pia ilihusika na kudumisha mawasiliano na nchi au makundi ambayo Israil haikuwa na uhusiano nayo wa kawaida wa kidiplomasia kama vile nchi za Afrika, Lebanon na Indonesia. Aidha kulikuwa na Kurugenzi ya utengenezaji na udhibiti wa Saikolojia ya Umma hasa katika maeneo ya siasa zilizohusu udhibiti wa matendo yaliyoonekana kuwa ya kigaidi dhidi ya mataifa ya Kiarabu, chama cha Nazi, vitendo vya hujuma na makundi ya Wanamgambo. Sambamba ikijihusisha na kuwauwa kwa propaganda wale wote walioonekana kuleta upinzani dhidi ya sera za Israil. Kurugenzi ya mipango, uratibu na Operesheni ni nyeti sana kiasi kwamba mkurugenzi ndiye mkuu wa opersheni zote na aliaminika pia kukaimu ukurugenzi mkuu wa Mossad kwa miaka kadhaa. Iliyoikaribia kwa unyeti, ilikuwa kurugenzi ya ukusanyaji wa taarifa ambapo mkurugenzi wake aliweza kukaimu ukurugenzi wa kurugenzi hiyo. Makao makuu ya Mossad yanahusika na uunganishaji na uendeshaji wa shughuli zote za kijasusi zilizo chini yake ambapo waliokuwa wakurugenzi wa kurugenzi zote huhusika na usimamizi wa shughuli zote za utawala na ndiyo wasimamizi wakuu wa mafungu ya fedha.
 
Last edited by a moderator:
Majasusi Wa Uzayuni Walivyoishika Marekani

Hivi karibuni wakuu wa kiyahudi nchini Marekani walitoa hotuba kali katika masinagogi yajulikanayo kama Adath Yisrail yaliyopo eneo la Cleveland Park mjini Washington. Wakuu hao walielekeza hutuba zao za Sabato kwa viongozi wa kituo chao cha utamaduni na siasa nchini humo. Kwa mara ya kwanza katika historia ya Marekani, wakuu hao walisema;

“Hatuna haja tena ya kujiona tu ugenini. Marekani kwetu, si serikali tena ya Magoyim, bali ni utawala ambao Wazayuni wanashiriki kikamilifu katika maamuzi ya kila Nyanja.” Umefika wakati sasa kipengele cha dini ya Kiyahudi kinachofafanua neno “Serikali ya Magoyim” kitazamwe upya, kwani kwa hivi sasa kinaelekea kupitwa na wakati kwa jinsi mazingira yetu yalivyo nchini Marekani”

Rais Bill Clinton ndiye anayetajwa kuwa alitoa mchango mkubwa kwa Wazayuni kuimiliki Marekani hivi sasa. Bill Clinton alihitimisha mpango wa kukita utawala wa Kiyahudi nchini Marekani ulioanzwa na Rais Ronald Reagan na waziri wake wa mambo ya nje, Schultz. Katika kipindi cha miongo kadhaa iliyopita, Wazayuni wamejitokeza kuwa na sauti zaidi katika siasa za Marekani kama ilivyoonekana katika harakati za aliyekuwa waziri wa mambo ya nje wa Marekani miaka ya sabini Bwana Henry Kissinger. Waziri huyo wa zamani wa mambo ya nje wa Marekani aliaminiwa sana na aliyekuwa Rais wa nchi hiyo Richard Nixon. Na kama ilivyojitokeza katika serikali ya Jimmy Carter ambayo mawaziri wake kadhaa walikuwa Mayahudi.

Tofauti iliyopo baina ya sasa na miongo kadhaa iliyopita ni kwamba, wakati ule Uyahudi lilikuwa suala la uficho ambapo uteuzi wa kisiasa ulikuwa nadra kumteua Myahudi, “Mtu wa dini”, kushiriki siasa hasa zilizohusiana na Mashariki ya Kati. Hali ya kisiasa ya Marekani hivi sasa imebadilika kabisa kuhusiana na Mashariki ya Kati. Kwa mfano, kila siku saa 12 asubuhi magari kadhaa ya maafisa waandamizi wa idara za kijasusi hutokea makao makuu ya CIA kwenda White House. Msafara huo ni wa uwasilishaji wa taarifa kwa Rais na wasaidizi wake wakuu wanne walio washauri wa mambo ya kiusalama (PDB) - President’s Daily Briefing – neno linalotumiwa katika taarifa nyeti zaidi katika duru za usalama nchini Marekani. Mara nyingi taarifa hizo huandamana na picha za siri sana zilizopigwa na Pentagon kupitia sattelite.

Taarifa zote zinazowasilishwa hupitiwa usiku na afisa maalumu mwandamizi wa kitengo cha usalama aliyebobea katika masula ya ujasusi. Afisa huyu (maalum) ni Myahudi. Afisa huyo pia huchambua telegramu na taarifa zilizofikishwa kutoka katika mtandao wa mawakala wa CIA ulimwenguni kote. Telegramu na taarifa hizo huwa na habari nyeti kulingana na maendeleo ya mambo mbali mbali duniani kote. Kinachofanya nyaraka za usalama zinazowasilishwa White House kuwa za aina yake kulinganisha na za vitengo vingine vya usalama na ujasusi nchini Marekani ni kwamba, zenyewe zimeegamia ukweli ambao mara zote huthibitishwa na vyanzo vya uhakika ambavyo ama huwa nyaraka zilizoibwa na maspai, maajenti au picha na taarifa za sattelite.

Rais wa Marekani anapokuwa mjini Washington huongoza mjadala mfupi juu ya yale yaliyomo kwenye nyaraka hizo ambayo wahusika wake wengine ni pamoja na makamu wa Rais, mshauri wa masuala ya usalama, mnadhimu mkuu, Naibu mshauri wa masuala ya usalama na mshauri wa usalama wa Taifa wa makamu wa Rais. Wakati wa serikali ya Bill Clinton washiriki wa kikao hicho nyeti kabisa walikuwa makamu wa Rais Al Gore, mshauri wa usalama wa taifa, Anthony Lake, mnadhimu mkuu katika ofisi ya Rais’ Leon Penta, naibu mshauri wa usalama wa Taifa Samuel ‘Sandy’ Berger, na mshauri wa usalama wa taifa wa makamu wa rais, Leon Perth. Katika washiriki hawa, wawili Berger na Perth, ni Wazayuni asilia. Wazayuni hao waliwekwa hapo maalumu kuchunga na kuelekeza sera nyeti za Marekani. Nafasi hizo zingali zikiendelea kuhodhiwa na Wazayuni hata katika serikali zilizofuatia. Katika baraza la usalama wa taifa la Marekani, wajumbe 7 wa juu kati ya 11 ni Wazayuni. Ni wakati wa Rais Bill Clinton wajumbe hao saba wenye asili ya kiyahudi walipopenyezwa katika duru hiyo nyeti na ya juu kabisa katika mambo ya usalama na ujasusi ya Marekani ambayo ndiyo inayohusika kupanga mieleko ya siasa na sera za nje za Marekani. Sandy Berger alikuwa makamu mwenyekiti wa baraza hilo wakati mjumbe mwingine mwenye asili ya Kiyahudi Martin Indyk, alikuwa mkurugenzi mwandamizi anayesimamia masuala ya Mashariki ya Kati na Asia. Wakati huo huo mjumbe mwingine Myahudi Dan Schifter, ambaye alikuwa mkurugenzi Mwandamizi na Mshauri wa Rais, aliwekwa katika kitengo kilichohusika na masuala ya Ulaya; Myahudi Don Steinberg, mkurugenzi mwandamizi na Mshauri wa Rais alikuwa msimamizi wa masuala ya Afrika; Myahudi Richard Feinberg, alikuwa mkurugenzi mwandamizi na Mshauri wa Rais wa masuala ya Latin Amerika, na Myahudi Stanley Ross, alikuwa Mkurugenzi na Mshauri wa Rais juu ya masuala ya Asia.

Mbali ya Baraza la Usalama, hali ni hiyo hiyo katika ofisi ya Rais ambapo Wazayuni wanaonekana kukamata nafasi zote muhimu. Aliyekuwa Mwanasheria Mkuu, Abner Mikve ni Myahudi, Mkuu wa Programu zote katika ofisi ya Rais, Ricky Seidman ni Myahudi; na Naibu mnadhimu mkuu, Phil Leida ni Myahudi. Wengine ni mshauri wa masuala ya uchumi, Robert Rubin ni Myahudi; Mkurugenzi wa Habari, David Heiser ni Myahudi; Mkuu wa Utumishi, Alice Rubin ni Myahudi; Ely Segall, aliyekuwa Msimamizi wa Mashirika ya Kujitolea ni Myahudi; Ira Mezina, Mkuu wa Programu za Afya ni Myahudi. Mawaziri wawili wa kazi Robert Reich na Micky Cantor walikuwa wakuu wa mikataba ya kimataifa ya kibiyashara, ni Wazayuni. Hao wote wanaingia katika orodha ndefu ya watendaji waandamizi wa kiyahudi waliyopo katika idara zote za serikali ambao kwa pamoja wako chini ya mkuu wa Timu ya Amani ya Mashariki ya Kati, Dennis Ross, wakifuatiwa na Wazayuni kadhaa waliokuwa manaibu waziri na maafisa waandamizi waliokuwa watendaji katika wizara mbali mbali.

Kwa mtazamo wa kiyahudi mtu muhimu sana ambaye hakuwa akitajwa sana alikuwa Rehm Emmanuel, mshauri wa rais na msimamizi wa uratibu wa miradi maalumu ya Ikulu ya Marekani. Ofisi ya Rehm Emmanuel ilikuwa jirani na Oval Office. Rehm aliyekuwa muhusika wa Baraza la Congress, anaelezwa kuifanya kazi hiyo kwa mafanikio makubwa. Orodha kamili ya Wazayuni waliokuwa katika serikali ya Bill Clinton ni kama ifuatavyo:

MadeleineAlbright
Waziri wa Mambo ya nje

Robert Rubin
Waziri wa Fedha

William Cohen
Waziri wa Ulinzi

Dan Glickman
Waziri wa Kilimo

George Tenet
Mkurugenzi wa CIA

Samuel Berger
Mkuu wa Baraza la Usalama wa Taifa

Evelyn Lieberman
Naibu Mnadhimu Mkuu

Stuart Eizenstat
Naibu Waziri wa Mambo ya nje

Charlene Barshefsky
Mwakilishi wa Masuala ya Biashara

Susan Thomases
Msaidizi wa Mke wa Rais

Joel Klein
Mwanasheria Mkuu

Gene Sperling
Mkuu wa Baraza linalosimamia masuala ya uchumi

Ira Magaziner
Msimamizi wa Masuala ya Afya

Peter Tarnoff
Naibu Waziri wa Mambo ya nje

Alice Rivlin
Mshauri wa Kichumi

Janet Yellen
Mwenyekiti wa Baraza la Uchumi la Taifa

Rahm Emanuel
Mshauri wa Sera

Doug Sosnik
Mshauri wa Rais

Jim Steinberg
Naibu Mkuu wa Usalama wa Taifa

Jay Footlik
Mwakilishi Maalumu wa Jamii ya Kiyahudi

(Hakuna jamii nyingine yenye uwakilishi kama huu katika serikali ya Marekani)


Robert Nash
Mkuu wa Utumishi

Jane Sherburne
Mwanasheria wa Rais

Mark Penn
Mtaalamu wa Masuala ya Asia

Sandy Kristoff
Mkuu wa Idara

Robert Boorstin
Mawasiliano

Keith Boykin
Mawasiliano

Jeff Eller
Msaidizi Maalumu wa Rais

Tom Epstein
Mshauri wa Masuala ya Afya

Judith Feder
Mjumbe wa Baraza la Usalama

RichardFeinberg
Waziri Msaidizi wa Masuala ya Uchumi

Hershel Gober
Chakula na Madawa

Steve Kessler
Mshauri wa Ikulu

Ron Klein
Waziri Elimu Msaidizi

Madeleine Kunin
Mawasiliano

David Kusnet
Mkuu wa Idara inayohusika na Programu za VVU/UKIMWI

Margaret Hamburg
Mkuu wa Usimamizi wa Uandaaji wa Mikutano na Vyombo vya Habari

Many Grunwald
Mwakilishi wa Viongozi wa Wazayuni

Karen Adler
Mkuu wa Idara ya Sera

Samuel Lewis
Mjumbe wa Baraza la Usalama

Stanley Ross
Mjumbe wa Baraza la Usalama

Dan Schifter
Mkurugenzi wa Masuala ya Amani

Eli Segal
Naibu Mnadhimu Mkuu

Alan Greenspan
Mwenyekiti wa Federal Reserve Bank

Robert Weiner
Mratibu wa Sera za Udhibiti wa Madawa

Jack Lew
Naibu Mkurugenzi Utawala na Bajeti

James P. Rubin
Afisa Mwandamizi, ofisi ya Waziri wa Mambo ya nje

David Lipton
Mwandamizi katika Wizara ya Fedha

Lanny P. Breuer
Mshauri Maalumu wa Rais

Richard Holbrooke
Mwakilishi Maalumu katika Umoja wa NATO

Kenneth Apfel
Mkuu wa Hifadhi ya Jamii

Joel Klein
Naibu Mshauri katika ofisi ya Rais, White House

Sidney Blumenthal
Mshauri Maalumu wa Mke wa Rais

David Kessler
Chief of Food & Drug Adiministration

Dennis Ross
Mwakilishi
Maalumu Masuala ya Mashariki ya Kati

Howard Shapiro
Mshauri Mkuu wa FBI

Lanny Davis
Mshauri Maalumu wa Ikulu

Sally Katzen
Waziri wa Utawala na Bajeti

Kathleen Koch
Mkuu wa FBI anayehusika na fursa sawa kwa wote

John Podesta
Naibu Mnadhimu Mkuu

Alan Blinder
Makamu Mwenyekiti wa Federal Reserve

Janet Yellen
Mkuu wa Baraza la Masuala ya Uchumi

Ron Klain
Mnadhimu Mkuu katika ofisi ya Makamu wa Rais


Wazayuni Walio Mabalozi Wa Marekani Nchi Kadhaa Duniani

Ubalozi ni nafasi muhimu sana kwa Wazayuni katika serikali ya Marekani. Kupitia nafasi hizo, wameweza kuwepo karibu nchi zote duniani wakiangalia maslahi ya Wazayuni na Uyahudi. Wazayuni watakaotajwa katika kitabu hiki ni wale wanaoiwakilisha Marekani kama mabalozi katika balozi za nchi hiyo duniani.

Kwa mujibu wa uteuzi huo, Wazayuni hawapewi nafasi hizo kutokana na uasili wao tu bali pia mitazamo yao ya kiitikadi na mielekeo yao kisiasa hasa kuhusiana na hali ya baadaye ya mashariki ya kati.

Orodha hii inathibitisha harakati za Wazayuni katika kuikamata Marekani kiutawala na kimaamuzi, hatua ambayo imesababisha harakati za kuweka ile inayoitwa demokrasia ya kweli nchini Marekani igonge mwamba kwa upande mmoja na kuhatarisha amani mashariki ya kati na duniani kwa upande mwingine.

“Huo ni uchambuzi wa kisiasa uliofanywa na wafuatiliaji wa siasa za kimataifa yakiwemo magazeti ya Israil”, imeandika makala yenye anuani The Jewish Laundry of Drug Money and the Jews Who Run Clinton’s Court.

Harakati za Wazayuni nchini Marekani zimefanikiwa kwa kiasi kikubwa sana kiasi kwamba wale waliopata fursa kuingiya katika utawala huo kama watendaji ni wanachama wa jumuiya zenye nguvu za kiyahudi. Wanachama hao ni waungaji mkono wa harakati na sera za Israil Mashariki ya Kati na katika kuishika Marekani na kwa hivyo Ulimwengu mzima. Kwa mitazamo ya hawa, haikubaliki kwao kutanguliza maslahi ya Marekani mbele ya yale ya Kizayuni. Ifuatayo ni orodha kamili ya mabalozi wa Marekani walio Wazayuni katika nchi mbali mbali duniani:

Balozi wa Marekani Ujerumani: John C. Kornblum, Myahudi: Kufuatia uadui wa muda mrefu wa Ujarumani dhidi ya Wazayuni, kazi ya Balozi huyu ni kuishinikiza nchi hiyo kukomesha uadui huo.

Balozi wa Marekani Ufaransa: Felix Rohatyn, Myahudi. Ni Mwanachama katika Benki la Rasilimali la Uyahudi. Mwezi Septemba mwaka 1998 kampuni ya mafuta ya Ufaransa, “Total”, liliwekeza dola biIioni 2 katika uzalishaji wa mafuta nchini Iran. Balozi Rohatyn akapiga kura ya turufu kupinga mradi huo kutokana na uadui wa Israil dhidi ya Iran. Katika kutetea msimamo wake, Rohatyn alisema: “Utandawazi usikuze vitisho bali ubebe nidhamu

Balozi wa Marekani Poland: Daniel Fried Chester Grabowski, Myahudi. Pia ni mhariri wa jarida la “Polish Post Eagle”. Kabla ya balozi huyu, hapakuwahi kuwepo Balozi wa Marekani ambaye ni Myahudi kutokana na uadui waliojenga Wazayuni dhidi ya Wapoli, mwenyewe alizowea kusema, “Ninachotaka sasa ni kujisafisha kwa lugha yao”.

Balozi wa Marekani Denmark: Edward E. Elson, Myahudi Dkt. Fields alipata kuhudhuria mahafali ya shule moja ya Kiyahudi mjini Atlanta akiandamana na ndugu wa Balozi Elson. Anasema aligunduwa kuwa jamaa hao walikuwa washabiki wakubwa wa chama cha Demokratiki.

Balozi wa Marekani Hungary: Donald M. Blinken, Myahudi: Nchi hii kwa muda mrefu imekuwa ikituhumiwa kuwa ilikuwa dhidi ya wahamiaji”. Jiji la Budapest lina idadi kubwa ya Wazayuni katika nchi za Ulaya, zaidi ya Wazayuni 125,000 wanaishi katika jiji hilo likitanguliwa na jiji la Paris. Kwa hiyo kazi ya Balozi Blinken ni kulinda maslahi ya kipesa ya Wazayuni.

Balozi wa Marekani Romania: Alfred H. Moses, Myahudi. Kwa wakati fulani Romania ilitawaliwa na chama cha Kikomunisti cha Kiyahudi kilichoongozwa na Anna Pauka. Romania ni mshirika wa karibu wa Israil. Maseneta sita, kati yao watatu mapadri, walipinga kuteuliwa kwa balozi huyo kwa maelezo kwamba alikuwa mshirika wa aliyekuwa mtawala wa Romania Dikteta Ceausescu.

Balozi wa Marekani Ubelgiji: Alan J. Blinken, Myahudi. Jiji la Antwerp nchini Ubelgiji ni la pili kwa uuzaji wa almasi duniani baada ya Tel Aviv. Biashara ya almasi duniani inamilikiwa na Wazayuni. Kwa hiyo, Balozi Blinken amepewa nafasi hiyo kulinda maslahi ya biashara ya almasi ya Wazayuni katika nchi hiyo.

Balozi wa Marekani Belarus: Kenneth S. Yalowitz, Myahudi. Belarus iko kati ya Poland na Urusi. Wakati fulani ilikuwa na idadi kubwa ya wakazi wenye asili ya Kiyahudi. Wazayuni bado wangali na maslahi katika nchi hiyo, hivyo balozi huyo ameteuliwa maalumu kwa ajili hiyo.

Balozi wa Marekani Afrika Kusini: James A. Joseph, Myahudi. Ni Wazayuni wanaomiliki migodi yote katika nchi hiyo yenye utajiri wa madini duniani. Wazayuni ndio waliokuwa wameasisi chama cha Kikomunisti Afrika Kusini kwa malengo ya kuishika serikali ya nchi hiyo. Vile vile ilikuwa karibu na serikali ya makaburu, ikiwa mshauri wa karibu wa idara ya ujasusi ya makaburu, BOSS. Chama kinachotawala sasa, ANC, kimeonesha utii mkubwa kwa Wazayuni na kinachunga maslahi yao yanayotokana na madini ya dhahabu na almasi.

Balozi wa Marekani India
: Frank G. Wisner, Myahudi. India ni nchi kubwa inayokuwa kiuchumi kwa haraka ambayo imekuwa ikiwaunga mkono Waarabu dhidi ya Israil. Kwa mujibu wa protokali za Kiyahudi, India inahitaji udhibiti mkubwa wa Wazayuni. Balozi Frank G. Wisner ameteuliwa kwa ajili ya kufanikisha wajibu huo wa Kizayuni.

Balozi wa Marekani Uturuki: Marc Grossman, Myahudi.Uturuki ni moja ya nchi zenye uhusiano wa kijeshi na Israil katika nchi zinazopakana na eneo la Mashariki ya Kati. Muasisi wa Uturuki “mpya” alikuwa Mustafa Kemal Ataturk aliyekuwa wakala wa ujasusi wa Kiyahudi katika nchi hiyo. Ni sababu hii inayoelezea ushirika uliokuwepo kati ya utawala wa kijeshi wa Ataturk na dola Israel. Hiyo pia inabainisha ule ukweli wa upinzani wa Kermal Atartuki dhidi wa mwamko wa kiislamu miyongoni mwa Waislamu wa Uturuki wakati wa utawala wake hata baadaye kutokana na sera alizopanda yeye (Ataturk) kuligeuza taifa la kiislam kuwa la kikanisa kwa kutumia kiini macho cha usekula.

Balozi wa Marekani New Zealand: Josiah H. Beeman, Myahudi.

Balozi wa Marekani Misri: Daniel C. Kurtzer, Myahudi. Misri ni nchi ya pili duniani inayopokea kiasi kikubwa cha msaada kutoka Marekani. Kwa maana iliyo pana na ya kina zaidi, Misri imenunuliwa kwa misaada ya ki-Marekani. Kununuliwa huku kumeondoa uwezekano wa Misri kuwa tishio kwa Israil kwa sababu jaribio lolote dhidi ya Israil litakuwa limehatarisha msaada huo.

Balozi wa Marekani Sweden: Thomas L. Siebert, Myahudi

Balozi wa Marekani Morocco
: Marc C. Ginsberg, Myahudi

Balozi wa Marekani Singapore: Timothy A. Chorba, Myahudi. Nchi ndogo tajiri katika nchi za Mashariki ya Mbali na China. Mwaka 1994 Singapore ilinunua ndege kubwa za kisasa 80 (Boeing) kwa fedha taslimu. Balozi Timothy A. Chorba yuko huko kuchunga maslahi ya Wazayuni katika kisiwa hicho tajiri.

Balozi wa Marekani Zambia: Arlene Render, Myahudi

Balozi wa Marekani Brazil: Melvyn Levitsky, Myahudi. Brazil ni nchi inayokuwa kwa haraka kiuchumi katika Marekani ya Kusini. Wazayuni wana maslahi makubwa katika nchi hiyo.

Balozi wa Marekani Bolivia: Curt W. Kamman, Myahudi. Ni nchi yenye utajiri mkubwa wa madini hasa shaba na zebaki. Curt W. Kamman yuko kama mwakilishi wa Marekani lakini mwenye kulinda maslahi ya Wazayuni.

Balozi wa Marekani Mexico: Jeffrey Davidow, Myahudi. Davidow awali alikuwa Msaidizi wa Waziri wa Mambo ya nje wa Marekani kwa nchi za Marekani ya Kusini wakati wa Albright. Mexico ndiyo nchi yenye wahamaji wengi wanaoingia Marekani, na inayofanya biashara kubwa na Marekani kuliko taifa jingine.

Balozi wa Marekani Canada: Gordon Giffin, Myahudi.

Balozi wa Marekani Cuba: Michael G. Kozak, Myahudi.

Huyu ndiye Mkuu wa waangalizi wa maslahi ya Marekani duniani. Yuko katika nafasi hiyo akiwa na kazi nyingine ya kuchunga maslahi ya Wazayuni.

Balozi wa Marekani Norway
: David B. Hermelin, Myahudi. Hermelin ni milionea mkazi wa Michigan na Rais wa Umoja wa Wazayuni Ulimwenguni (ORT Union). Anamiliki jumba la michezo na ukumbi wa starehe, “Jumba” la Auburn Hills na ukumbi mkubwa, “Pine Knob Music Theater”.

Balozi wa Marekani Uswisi: Madeleine M. Kunin, Myahudi. Kunin awali alikuwa gavana wa chama cha Demokratiki katika jimbo la Vermont.
 
duuuuu!!!!!!!!!! kuna vitu vingine hata ukijitahidi kuvielewa ni shida kimoja waponihiki. mambomengi haya hayataki schedule wala computer ya jirani.hii inabidi mtu tu asome halafu anisimulie kwa ufupi. kwa mimi nawahi mavuvini maji yatakupwa.
 
Nimekufuatilia kwa kina nadhani ukimaliza kutudodolea kuna vi maswali vya kuuliza kama alivyosema Kizamkazi mambo mengine mpaka ufafanuzi. Ila heshima mbele mkuu imetulia.
 
Uzayuni Na Harakati Dhidi Ya Makundi Ya Waislamu​

Shambulio la kwanza zito la Uzayuni dhidi ya Uislamu ni kutwaa ardhi za Waislamu. Mafanikio waliyoyapata yakiwatia hamasa zaidi na kuanza kupiga hatua nyingine ambapo ndani ya kipindi cha miaka 26 tu waliweza kutwaa ardhi ya Palestina. Kwa kweli ‘Israel’ haikusimama bila upinzani kutokea upande wa Waislamu. Waislamu walipambana vikali kweli kweli kwa hali na fasili walizojaaliwa kwa wakati na mazingira yao. Katika mstari wa mbele wa mapambano hayo, walikuwepo wana-ikhwaan (Muslim Brother hood). Wazayuni wakagundua kuwa adui yao mkubwa ni Ikhwaan. Yale maadili yao yaliyoepukana na ubinafsi na ile ari ya kujitoa mhanga waliyokuwa nayo wana-ikhwaan katika mapambano iliwafanya Wazayuni watanabahi wapi ilipo nguvu kubwa dhidi yao. Kumbukumbu ya machungu na hasara waliyoipata Wazayuni mikononi mwa Ikhwaan haikuweza kufutika kirahisi walipatwa na kihoro kikubwa juu ya hii nguvu kubwa ya Uislamu iliyokuwa ikichomoza. Uzayuni ukaiona hatari ya Ikhwaan na kutanabahi kuwa kama hatari hiyo isingaliondoshwa, basi wasingaliweza kujiimarisha kule Palestina seuze kuunasa na kuutia utumwani ulimwengu mzima wa kiislamu kama ilivyopangwa na wakuu wao.Wazayuni walibaini kuwa tishio kubwa kwa Israel ni nguvu hizi mbili;

(1) Umoja wa ulimwengu wa Waislamu na Uislamu hasa muungano wowote wa Waarabu wanaoizunguka Israel na,

(2) harakati za Ikhwaan Muslimiyn. Hivyo, mara moja wakaanza kutekeleza mipango yao ya kuondosha vitisho hivi katika mustakabali wao wa kisiasa Mashariki ya Kati. Kinachoelezwa hapa ni kuwa Wazayuni na Kanisa katoliki wamefikia mkataba wa maelewano na sasa nguvu hizi mbili zimeunda nguvu moja dhidi ya Uislamu. Na sasa pande zote mbili zinashirikiana kuushinda ulimwengu wa Waislamu. Nchi za kiarabu zilizo jirani na Wakristo na Wazayuni zikawa shabaha yao ya kwanza ambapo nguvu za pamoja za Ukristo na Uzayuni zinataka kutoa pigo kubwa kwa Waislamu na kwa umoja wao. Licha ya kushindwa kwake, Mfalme Faaruuq alizitetea jitihada za kuleta umoja wa nchi za Kiarabu na alisimamia umoja na uhuru wa Misri na Sudan.

Waingereza walitumia kila njia kumshawishi, kumchochea na hata kumtishia lakini hakusalimu amri na mwishowe mikataba yote ya Kiingereza katika suala hili ikavunjika kabisa. Hii ilikuwa katikati ya mwaka 1951. Nguvu za kuupiga vita Uislamu zikapanga kumuondoa Mfalme Faaruuq madarakani haraka iwezekanavyo. Pilika pilika za kumtafuta mtu ‘anayefaa’ zikaanza. Walitaka kuua ndege wawili kwa jiwe moja. Kumpata mtu ambaye angeweza kuzuia Umoja baina ya Sudan na Misri na kuisambaratisha Ikhwaan. Jamal ‘Abdun-Naaswir akachaguliwa kufanya kazi hiyo na njia ikafagiliwa ili aibu ife. Idara za usalama za Uingereza MI5 na MI6, za Marekani FBI, CIA pamoja na iliyokuwa KGB zikashirikiana kwa karibu zaidi na kamati ya kijasusi ya Israil ya Vaadat.

Hatimaye mwaka 1952 Faaruuq akang’olewa na Jamal ‘Abdun-Naaswir akawekwa madarakani. Mara moja akaanza kutimiza kazi aliyopewa kama mtawala kibaraka. Alifanya kila alivyoweza kuzitenganisha Misri na Sudan. Na katika kutimiza kazi ya pili, aliwafunga jela wana-ikhwaan elfu hamsini na kuwanyonga wengine ambao, kwa kweli Misri ilifanya kazi kubwa kuwaandaa kwa miaka mingi. Hivyo Jamal ‘Abdun-Naaswir alileta pigo ambalo majeraha yake ni vigumu kupona. Hapana shaka kabisa kuwa ‘Abdun-Naaswir alikuwa kibaraka wa Uzayuni wa pande zote ndani ya Misri.

*************

Wazayuni Walitumia CIA Kumpandikiza Jamal ‘Abdun-Naaswir

Katika kitabu chake mashuhuri, CIA Crest Book, 1963, uk 84 –89, Andrew Tully anaeleza kuwa, nchini Misri, shirika la ujasusi la Marekani – CIA lilisaidia kumng’owa Mfalme Faaruuq. Kisha, Jamal ‘Abdun-Naaswir akasaidiwa na shirika hilo kukalia kiti cha uongozi katika ulimwengu wa kiarabu. CIA ilimfahamu vizuri ‘Abdun-Naaswir wakati ule akishirikiana kwa karibu na baadhi ya wanaikhwaan huku akiwa na mipango yake ya siri. Mwanzoni shirika hili lilipata shukrani kutoka sehemu nyingi za ulimwengu wa Waarabu waliokuwa wanataka kuondokana na utawala wa Faaruuq. Ikhwaan pia ilishiriki kikamilifu katika mapambano ya kumng’oa Mfalme Faaruuq kwa kuwa katika utawala wake aliamuru muasisi wa kundi hilo, Shahiid Hassan al Banna aliuawa kwa kupigwa risasi mwaka 1949. Hasira za ulimwengu wa Magharibi zilimlipukia mfalme huyo mwezi Oktoba mwaka 1951 pale serikali yake ilipoukataa mkataba wa mwaka 1936 na Uingereza na kuchukuwa hatuwa ya kuwafurusha Waingereza kutoka ukanda wa Mfereji wa Suez.


Ni katika kipindi hiki ambapo Marekani na Uingereza zilikata hukumu kuwa Faaruuq ang’olewe madarakani. Hii ikiwa na maana kuwa mashirika ya Ujasusi ya nchi hizi mbili; CIA kwa upande wa Marekani na lile la Uingereza yalianza kushirikiana kumsaka mtu wa kushika madaraka. CIA ikapeleka nguvu nyingi za kiufundi jijini Cairo kuudhoofisha utawala wa Faaruuq. Walipelekwa huko maafisa usalama wastaafu wa jeshi ambao, kwa kipindi kirefu cha utumishi wao, walifanya kazi Mashariki ya Kati na ambao Jamal ‘Abdun-Naaswir alikuwa karibu nao wakati huo huo ‘Abdun-Naaswir mwenyewe akiwa karibu na chama cha Ikhwaan Muslimiin. CIA ikatoa taarifa yake mwishoni mwa mwezi Julai mwaka 1952, na kisha kikosi cha maofisa wa ‘Abdun-Naaswir kikaingia kazini wakaigeukia Ikhwaan wakashirikiana kuisambaratisha.

Ni jambo la hakika kuwa, kimsingi, mikakati ilipangwa na Wazayuni. Na ‘Abdun-Naaswir, kama ajenti wao, akatimiza malengo ya Wazayuni hao. Kosa kubwa la utawala wa ‘Abdun-Naaswir kwa upande wa Palestina lilikuwa ni lile la kukubali kiwekwe kituo cha majeshi ya dharura ya kimataifa katika Ukanda wa Ghaza. Kwa kufanya hivyo ulimwengu wa Waarabu ukafungua mlango katika eneo hilo kuruhusu harakati za Wazayuni. Ukanda wa Ghaza (Ghaza Strip) ndio eneo rahisi ambalo wapiganaji wa kujitoleya wangeweza kujipenyeza ndani ya Israel kuendesha vita vya chini kwa chini au mitaani. Kuanzia hapo majeshi ya kimataifa yakawa hayaruhusu Waarabu kuingia katika eneo hilo. Israel ikalitumia eneo hilo kutimiza malengo yake ya kiuchumi na kistratejia. Vile vile Ghuba ya ‘‘Aqabahh wakapewa Wazayuni tena katika kisahani cha fedha kupitia mpango wa udhibiti wa kimataifa wa ghuba hilo.

Kabla ya udhibiti huo wa kimataifa, Wazayuni hawakuthubutu kuingia katika Ghuba ya ‘‘Aqabahh. Hapo ndipo Israel ilipojenga Bandari yake ya Eilath katika ghuba hiyo na meli zake zikaanza kupasua kwa madaha kutoka huko na kuelekea kwenye maeneo nyeti ya Afrika kueneza ushawishi wao. Kuifungulia milango Israel katika Ghuba hiyo kukaondosha kizuizi ambacho, hapo kabla, kiliifanya Israel ibakie kuota ndoto za “alinacha” za maendeleo ya kiuchumi kwani kiliwaumiza sana kwa vile uchumi wake ulikabiliwa na hali ngumu sana.

Kwa kuondoshwa kizuizi kilichokuwa kikiwakwaza, Wazayuni wakajiimarishia masoko katika sehemu za kistratejia ndani ya Afrika. Na kutokana na nguvu zao za kiuchumi Waarabu na Waislamu wakaanza kukabiliwa na hatari kubwa. Yote hayo ni kwa sababu Misri, chini ya Naser ilikubali kuikabidhi ghuba hiyo kwa Wazayuni. Kwa kweli sababu ya msingi ya shambulio lililofanywa na Israel katika eneo la Sinai ilikuwa ni kuimarisha udhibiti wa ghuba hiyo. Huku Waarabu na Waislamu wakibutwaika, Israel ikafikia malengo yake ya kistratejia na ikazidi kuchemka kujiimarisha kwa nguvu katika maslahi yake juu ya kutamalaki eneo lililokusudiwa.

Hatua iliyofuata ilikuwa ni ya kumiliki mfereji wa Suez kutoka Bandari ya Eilath katika Ghuba ya ‘Aqabah hadi Ashdodi pwani ya Bahari ya Mediterania, na hivyo kufungua njia nyingine ya baharini. Mipango ya matengenezo ya njia hiyo iliandaliwa na mhandisi wa kiyahudi aliyezaliwa Moscow, Urusi. Gharama za matengenezo ya mfereji huo wa umbali wa maili 178, zilikuwa ni dola bilioni tatu. Jambo la kuhuzunisha juu ya hali hiyo ni kwamba Redio ya Misri na vyombo vingine vya habari vya serikali vilivurumisha propaganda za kuwashawishi Wamisri waamini kuwa hapakuwa na mradi kama huo. Wamisri, baadhi yao wakikoromea mikononi mwa Polisi wa Serikali, wakawa watu wa kusikia tu kile ambacho serikali ilitaka watu waamini. Huenda itashangaza kusikia kuwa uamuzi juu ya mustakabali wa Ghuba la ‘Aqabah ulikwishafanywa kwa siri katikati ya utawala wa Wazayuni na rais Truman wa Marekani. Bwana Alfred Lilienthal katika kitabu chake (uk.70-71) anafichua jambo hili;

“Juma moja kabla ya kura ya Umoja wa Mataifa kupigwa, Weizmann (Kiongozi wa Wazayuni) alimtembelea Rais Truman kushadidia msimamo wa Wazayuni ili kuhakikisha kwamba Ghuba ya ‘Aqabah, njia ya kuelekea Bahari ya Hindi haitengwi mbali na “dola” ya Israel. Mawasiliano ya karibu yalidumishwa wakati wote baina ya White House na Wazayuni kupitia kwa David Niles na Edward Jacobson wote wakiwa Wazayuni. Kule Umoja wa Mataifa, wakati Balozi Herschel Johnson na Meja Jenerali H. Hilldring walipokuwa wakitoa taarifa za kusikitisha kwa wawakilisha wa shirika moja la Wazayuni kuhusiana na Ghuba ya ‘Aqabah, punde simu ikaita. Alikuwa ni Rais, akitoa maagizo kuwa Ghuba hiyo likabidhiwe kama vile alivyotaka Weizmann (Tazama Weizmann, Trial and Error, uk 459).

‘Abdun-Naaswir hakuishia hapo tu, bali alikuwa akiingilia mambo ya nchi nyingine za Waislamu. Kwa mfano kupitia mashirika ya kijasusi alijaribu kufanya mapinduzi Iran na Uturuki. Yeye ndiye alikuwa msukaji mkuu wa mipango. George Haddad ametaarifa kuwa ghasia za mwaka 1963 ambazo ziliirusha roho Iran pamoja na jaribio la mapinduzi nchini Uturuki mwezi Mei, mwaka 1962, ni matukio yaliyoanzishwa na kudhaminiwa na makachero wa Rais ‘Abdun-Naaswir wa Misri. Jenerali Hassan Pakranan, Mkuu wa Polisi na Usalama wa taifa alitaja jina la kachero mmoja wa ‘Abdun-Naaswir na akadai kuwa kachero huyo alikiri kuwa yeye alikuwa akisafirisha pesa yenye thamani ya paundi milioni mbili za Kilebanon na kuvipelekea vikundi vya Wairan waliokuwa wakimpinga Shah. Kwa ushahidi zaidi wa hili soma gazeti la New York Times la Juni 6, 1963. Itakumbukwa kuwa mhariri wa Al Hayat aliuawa na ushahidi ukaonesha kuwa waliomuua ni makachero wa ‘Abdun-Naaswir. Kulikuwa na nguvu isiyoonekana ambayo ilimshabikia “Fir’aun” huyu kwamba eti alikuwa mkombozi. Hivyo ndivyo ilivyokuwa Uturuki pale mzayuni Kamal Atartuk aliposhabikiwa kuwa eti alikuwa mkombozi japo alifanya kila jitihada kuangamiza uislamu na kufutilia mbali alama yoyote ya utamaduni wa kiisalmu na hata chembe chembe za fikra za kiislamu. Kamal aliua takriban Waislamu 25,000 WachaMungu, wakiwemo wanazuoni na wanaharakati mashuhuri. Bado, pamoja na yote hayo ya kinyama na kishenzi, muuwaji huyo akaitwa mkombozi. Waandishi wa Kiyahudi wamemmwagia sifa nyingi Kamal Atartuk. Na hata mwandishi asiye Myahudi ambaye ameonesha hisia za kuuchukia Uislamu basi alipewa heshima kubwa na Wazayuni hata kuzidi thamani ya kazi yake. Hii ni moja ya mbinu za Wazayuni ambapo huangalia nani anaandika nini kupitia macho ya majasusi wao katika vyuo vikuu na vyuo vingine vya elimu vya ulaya na Amerika na kote duniani na hasa Afrika ambapo watu hupewa Uprofesa kwa kutukana dini nyingine na hasa Uislamu na waislamu, hata kukana ramani na historia na utamaduni mzima wa watu na jamii yao kwa kuwa tu, kwa mfano, Jumuiya ya Waswahili, kusemwa hawapo na wizara inaruhusu vitabu kama hivyo kufundishwa shuleni na vyuoni. Watu hao wanafanya kazi zao kwa mtazamo wao basi hujaziwa sifa kwa propaganda hadi kuwafanya mashuhuri. Wanatunza rekodi za wasomi wa mambo ya utafiti na miradi. Huwapatia misaada kupitia mashirika yao mbali mbali, na hivyo kuzitumia kazi zao kwa maslahi yao bila wenyewe kujua.

*************


Wazayuni Walimtumia Ghulam Husayn Kuanzisha Bahai


Wazayuni katika kuhakiki mwendo wa jamii ya dunia wamejizatiti katika uwanja wa kuwekeza katika “misheni” za kidini. Moja ya stratejia wanayotumia ni ile ya kuingia katika dini nyingine na kupanda mbegu ya kuvuruga akida, akili, upembuzi na stahamala ya mwendo wake.

Dini ya Bahai ilianzia Iran mwaka 1843. Mwanzilishi wa dini ya Bahai Mirza Ghulam Husayn, alikamatwa na utawala wa Uthmaniyya na kuwekwa gerezani ili upotovu wake usiendelee. Hata hivyo kutokana na upana wa mitandao ya kijasusi ya Kiyahudi ya wakati huo aliweza kuhamishwa kutoka gereza moja hadi lingine huku akiandika vitabu ambavyo leo vinatumika na wafuasi wa Bahai duniani. Huku taasisi za Bahai zikienea dunia yote, makao makuu ya Bahai yameendelea kuwa Haifa ndani ya Israel. Ina maana kwamba, dini ya Bahai inaendeshwa kwa nguvu ya Uzayuni kiuchumi, kijamii na kisiasa.

Dini ya Bahai inapinga kwa ndani wafuasi wake kujihusisha na siasa ilhali taasisi zake zmekuwa ni vituo vya ukusanyaji wa taarifa za kijasusi dhidi ya mataifa, watu, jamii na tamaduni zao. Malengo ya taasisi hizi za Bahai ni kueneza fikra juu ya kuchanganya dini tofauti kwa muelekeo wa kuleta “Dini Mseto”13. Chimbuko halisi la “dini Mseto”, linatokana na harakati za dini ya Bahai. Dini ya Bahai ni mpango mahsusi wenye lengo mahsusi juu ya kuharibu jamii, siasa na hatimaye kutawala dunia isiyo na maadili.


*************


Jamal Abdul ‘Abdun-Naaswir Alikuwa Ajenti Wa ujasusi

Huwa panazuka ubishi kama kweli Jamal ‘Abdun-Naaswir alikuwa ajenti wa Wazayuni. Iwapo ni kweli basi ‘Israel’, Uingereza, na Ufaransa, zisingemshambulia na Urusi nayo isingetishia kuingiza majeshi yake nchini mwake kupambana na wachokozi. Kwa kweli watu wengi sana wanajidanganya hivyo. Wasomaji wanaweza kukumbuka mfano wa karibu zaidi pale Saddam Husayn al’Tikrit (aliyekuwa rais mtawala wa Iraqi) alipokuwa rafiki mkubwa wa Ulaya na Marekani na baadaye marafiki hao hao kumgeuka na kuanzisha vita vilivyosababisha kuanguka kwake na kuendelea kwa vita hivyo hadi sasa. Kadhalika watu wanaweza kushangazwa iwapo watasikia kuwa waliokuwa wakipigana vita baina ya Iran na Iraq walikuwa ni FBI na CIA, mashirika ya ujasusi ya Marekani yaliyo chini ya udhibiti wa mazayuni. Katika vita ile, kwa upande mmoja majasusi wa FBI walikuwa wakimpelekea silaha Sadamu Husayn kwa ajili ya kuzifanyia majaribio, kwa upande mwingine CIA ndiyo iliyokuwa ikiiuzia Iran silaha, hata hivyo zilikuwa za zamani. Ili kuhamisha mazingatio ya watu, baada ya vita, ikaibuliwa kesi dhidi ya rais Regan katika kile kilichodaiwa kashfa ya uuzaji wa silaha nchini Iran!

Hata hivyo, kadri kunavyopambazuka, taratibu, upande uliofunika siri hii unatoweka. Jambo la msingi la kukumbuka, kwa mnasaba wa suala hili ni kuwa lengo halisi lililofichikana katika ule ugomvi wa Mfereji wa Suez, lilikuwa ni kutowa fursa na njia kwa Israel kujitanua kiutawala, na kujiimarishia nguvu na maendeleo kwa njia zisizokuwa za moja kwa moja na za kutatanisha. Kwa sababu zilizo wazi kabisa, Israel ilikuwa inataka kutekeleza mipango yake kwa awamu, kidogokidogo. Suala la mfereji wa wa Suez haliwezi kueleweka barabra bila kuyatupia macho mazingira husika na yale mafanikio waliyoyapata Wazayuni baadaye. Madola yote matatu yaliyoishambulia Misri yaliungwa mkono kikamilifu na Marekani, lakini ilirudi nyuma (kama vile imejitenga). Kwa nini Marekani ilifanya hivyo? Hili linasimuliwa kwa kina na Waziri Mkuu wa Uingereza wa wakati huo, Anthony Eden, katika kumbukumbu zake. Kwa kweli madola yote haya mane yalikuwa na hakika kabisa ya ushindi, lakini kujitenga kwa Marekani kulibadilisha muelekeo mzima wa matukio.

Marekani ilijua si kwa sababu za kibinaadamu au za kimaadili bali kwa sababu za kidiplomasia. Marekani ilitaka kuitoa Uingereza katika siasa za Mashariki ya Kati na kujiongezea nafasi ya ushawishi katika eneo hilo. Kuhusiana na dai kuwa mbona Dikteta wa Misri mara nyingi alikuwa akitangaza hadharani msimamo wa kuipinga Marekani, na hivyo angewezaje kuhesabiwa kuwa ni kibaraka wa Wazayuni. Hii si lolote bali ni jitihada tu alizokuwa akizifanya Jamal ‘Abdun-Naaswir katika kujaribu kuwapumbaza wananchi wa Misri. Shutuma za ‘Abdun-Naaswir dhidi ya Marekani zilikusudiwa kuizuga jamii ya watu wa Misri. Mbinu za namna hii, kwa vyovyote vile, ilibidi zitumike kuwatuliza Waarabu. Ilikuwa ni hadaa ya hali ya juu ya Jamal ‘Abdun-Naaswir kujiimarisha madarakani. Kama kuna mtu anayesadiki kinyume na hivi, basi hebu alitafakari suali hili jepesi tu. Kama Marekani na Misri zingalikuwa nchi maadui, mbona basi taifa hilo kubwa lilikuwa tayari kutoa msaada wake wote kwa ‘Abdun-Naaswir? Miongoni mwa nchi zote ulimwenguni, Misri ilikuwa inapata msaada mkubwa mno kutoka Marekani, kwa nini basi ilikuwa hivyo?

Bila shaka Marekani haiwezi kuzembea kiasi cha kupoteza bure mali zake kwa ajili ya nchi adui, au isiyo tayari kutekeleza mipango na malengo yake, kwa nini basi itoe msaada mkubwa namna hiyo? Ukweli wa mambo ni kwamba kupitia kwa Waamerika, Wazayuni waliweza kupata yote waliyoyataka kutoka kwa Jamal ‘Abdun-Naaswir kwa minajili ya kuimarisha mamlaka yao. Kwa kweli ‘Abdun-Naaswir kwa kule kuwa kwake mshirika wa karibu wa Wazayuni, ndio maana aliweza kupata misaada yote hiyo ya hali na mali ya Wamarekani. Hapana shaka kabisa kuwa ‘Abdun-Naaswir alidhihirika wazi kuwa alikuwa mshirika mkuu na muaminifu wa sera za Marekani, inayomilikiwa na Wazayuni juu ya ulimwengu wa Waislamu. Upo ushahidi wa kina, mpana na madhubuti juu ya jambo hili. Hatua ya awali ya uimarishaji wa usalama na upanuzi zaidi wa “Israel” ilichukuliwa kwa njia ya kusambaratisha harakati mashuhuri za Mashariki ya Kati, ambazo kuwepo kwake kusingeiwezesha serikali yoyote ya Misri kuonesha imani au unyonge kwa Wazayuni. Si jambo ambalo lingeweza kuingia akilini kwa mtawala yeyote kuonesha hata kiasi kidogo cha mapenzi kwa Wazayuni, au hata kukubali kuitambua iwe kwa njia ya moja kwa moja au kwa njia nyingine. Lakini Kanali Jamal ‘Abdun-Naaswir alifanya hivyo! Na lazima awajibike kwa kumtoa mbwa mwitu sandukuni.

Pale Wanaharakati wa Misri walipoandamwa 1954-1955, na viongozi wake wakuu kunyongwa, huku maelfu ya wanachama wake wakifungwa jela, Kanali ‘Abdun-Naaswir katika mahojiano na mwandishi wa gazeti la The New York Times la Oktoba 15, mwaka 1955, aliwahakikishia Wazayuni wa mashariki ya kati na washirika wake kuwa hakukuwa na Mwarabu yeyote aliyetaka kuing’oa “Israel”. “…Bali kitu pekee walichotaka Waarabu ni haki ya kuishi ya Wapalestina waliotimuliwa, na mali zao zirejeshwe kama ilivyotakiwa na Azimio la Umoja wa Mataifa miaka saba nyuma”.

*************


Nguvu Ya Pamoja Dhidi Ya Wanadini

Kwa upande mmoja Jamal ‘Abdun-Naaswir alimwaga damu za Waislamu wasiokuwa na hatia na kusababisha fujo na machafuko katika ulimwengu wa Waarabu, na kwa upande mwingine alishirikiana mkono kwa mkono na kila nchi iliyofuata sera iliyopinga Uislamu. Kwa mfano:

Jamal ‘Abdun-Naaswir alikuwa mshirika wa India kwa sababu utamaduni wa Kiislamu ulikuwa ukipigwa vita na kufutwa huko. Damu ya Waislamu ni rahisi kuimwaga kuliko maji na heshima, hadhi yao imekuwa jambo la zamani. Wagiriki wa Cyprus walikuwa washirika wake, wao hawakuona ubaya kumwaga damu za Waislamu. Haile Selasie wa Ethiopia alikuwa rafiki wa ‘Abdun-Naaswir kwa sababu aliyafanya maisha ya Waislamu nchini mwake kuwa ya huzuni na aliwatweza katika nafasi watwana na watumwa na alitaka kuwashurutisha kuwa Wakristo. ‘Abdun-Naaswir hakuhisi uchungu wakati Haile Selasie alipokuwa akitumia kila njia kuwasagasaga na kuwafuta Waislamu kwa kosa la kufuata Uislamu. ‘Abdun-Naaswir alikuwa rafiki kipenzi wa Rais wa Tanzania Mwalimu Julius Kambarage Nyerere ambaye historia inamshuhudia alivyowakandamiza Waislamu walioendesha harakati za kuikomboa Tanganyika kisha kumteua yeye (Nyerere) kuwa Rais katika kile kilichokuwa kikiitwa Umoja wa kitaifa usiyozingatia dini. Wakati “Israel” ilipokuwa ikiwashambulia Wapalestina, ‘Abdun-Naaswir aliamua kukaa kimya kabisa kana kwamba mateso ya Wapalestina hayakuhitaji msaada. Ikhwaan ingaliweza kutoa pigo kali dhidi ya ndoto za Israil lakini hamsini elfu kati yao (wakiwemo wanawake 800) walitiwa jela na ‘Abdun-Naaswir. Wakapata mateso yasiyosemekana na kudhalilishwa. Hii ndiyo kazi iliyofanywa na mtetezi Mkuu wa Utaifa wa Waarabu. Wahanga wa kwanza wa dhana ya Umoja wa Warabu ni Waarabu wenyewe, tena basi, mikononi mwa mtu ambaye kila kukicha alikuwa akipiga kelele juu ya haja ya kuwepo Umoja wa Waarabu. Mwenyezi Mungu anajua ‘Abdun-Naaswir alikuwa anafanya kazi ya nani na anajua msukumo aliokuwa akiupata na anawajua waajiri wake waliompa kazi ya kuchimba kaburi la Waarabu na Waislamu.

Hebu tuitazame sehemu ya ulimwengu wa Waislamu ambayo Nchi za Magharibi imeiita Mashariki ya Kati. Picha ni ya kuhuzunisha kwa kweli. Hali ya mambo huko ni ya kutatanisha na ni ya hatari. Eneo muhimu zaidi, Palestina, ndio hilo lililomo mikononi mwa Wazayuni. Serikali ya Misri, inayodhibitiwa na Marekani kupitia shirika lake la kijasusi la CIA linalodhibitiwa na Wazayuni, inamiliki nchi yenye rutuba zaidi miongoni mwa ulimwengu wa Waislamu. Kwa mujibu wa Katiba ya Lebanon, licha ya Waislamu kuwa wengi, ni mkiristo tu ambaye anaweza kuwa kiongozi wa dola. Nguvu zote hizi zinajua kuwa Waislamu wana utambulisho uliopandikizwa ndani kabisa ya nyoyo zao, na wana hisia nzito za umma. Hivyo iwapo wangepata fursa ya kuishi kwa mujibu wa Uislamu wao, basi watafanya kila waliwezalo kuunganisha Ulimwengu wa Waislamu. Na kutokana na nguvu na msukumo wa Ujumbe wa Uislamu, Waislamu wangeujenga umma wao na kuupa nguvu ya kudumu. Ndio sababu, madikteta na madhalimu, katika jitihada za kuwavunja ari na dhamira Waislamu, wanaimba nyimbo za demokrasia, uhuru wa binadamu nakadhalika. Watatumia nguvu zote kuwatia watu utumwani kwa kutumia dhana hizi. Sanjari na sera hii, wanajitahidi kwa kila hali kuchafua mazingira ya jamii kimaadili, wanavuruga murua wa maadili ya kiislamu kupitia mfumo wa elimu, fasihi, filamu na zile zinazoitwa shughuli za kiutamaduni. Lengo ni kughafilisha umma wa kiislamu usikumbuke mafundisho na maisha yajayo, na hivyo kuwafanya wasijali kabisa vigezo vya maadili ya Uislamu kiasi kwamba pale mkondo wa demokrasia unapowasomba kwa nguvu na watu kupata fursa ya kutawala watakavyo basi tena na wao huutupilia mbali Uislamu na hata kuubeza.

Kiulimwengu, Wazayuni ndio wanaohodhi magazeti makubwa, mashirika ya habari na vyombo vingine vya mawasiliano ya umma. Vyombo hivyo vya habari vinasuka mambo na matukio ambayo huzidisha matatizo na hali ngumu. Kwanza wahusika huamua jambo fulani kuhusu nchi hii au ile ya Waislamu kisha vyombo vyao vya habari hulisuka na kulipa uzito wa juu na baadaye hatua kamambe za utekelezaji wa jambo hilo huchukuliwa na hatimaye jambo hilo hutekelezwa kinyama. Wanaanzisha harakati fulani na kutumia kaulimbiu kisha vyombo vyao hutumika kusambaza habari zao kwa ufundi usiong’amulika ambapo kaulimbiu na maneno ya hadaa muda si muda huandaa mazingira ya kisiasa ya kutimizia mipango yao. Yote haya hufanywa kwa mbinu makini kiasi kwamba umma wa Waislamu wakiwemo wasomi hulewa sumu ya propaganda. Haya hufanywa kwa watu mmoja mmoja, kikundi, asasi, taasisi, wilaya, nchi nakadhalika alimradi Waislamu wagombane.


*************


Mambo Yahitaji Kutafakariwa

Dawa ni ipi basi? Hali ya mambo yahitaji kutafakariwa kwa kina kizito na wasomi wa ngazi zote. Hapana budi kutafakari kipi cha kufanya ili kuweza kuutoa umma katika wigo wa shetani na kupanga mikakati madhubuti. Kwanza inapendekezwa kuwa kwa muhtasari watu, hususan Waislamu, waelewe ni Uzayuni wakitumia majasusi wa frimasonri ambao wametoa mchango mkubwa mno katika ile hila ya kuitenga Ulaya mbali kabisa na dini na badala yake kujenga mfumo mpya wa maisha kwa misingi ya falsafa za Religion of Humanity, ‘Positivism’,‘materialism’ na ‘secular humanism’, yaani itikadi zinazomkana Mwenyezi Mungu Muumba. Vilevile frimasonri ikiwa pazia la Wazayuni imeshiriki, kwa kiasi kikubwa, katika harakati za kupandikiza itikadi hizi katika jamii nyingine mbali na zile za Magharibi. Mitalaa ya elimu ya juu duniani kote hivi leo inawalazimisha wasomi wawajue na kuwaheshimu wanafalsafa waliojenga msingi wa falsafa za Ulaya kuanzia Socrates, Plato, Aristotle, na waliofuata mkondo wao. Mawazo ya kisiasa, kiuchumi na kijamii ya wanafalasafa hao yanakana ufunuo wa Muumba hivyo humuandaa msomi amkane Muumba wake na abaki kuenzi na kunyenyekea mawazo ya wanafalsafa hao katika kuendesha maisha yake ya kila siku.

Kuuelewa undani wa frimasonri na kukosoa falsafa yake, hapana budi kuyatafakari kwa upeo mpana mambo mengi ya dunia kuanzia, shule, vyuo vya kawaida na vyuo vya falsafa, sera za uchumi, mielekeo ya magazeti, televisheni, internet (mtandao wa kompyuta zilizounganishwa na zinazowasiliana), muziki na itikadi za siasa na kuelewa vyema maana, malengo na hila zilizofichikana nyuma ya mambo haya. Hapa pia zingependekezwa hatua kadha wa kadha za kuchukuliwa ambazo tunaamini zitakuwa na tija fulani katika utatuzi wa tatizo kubwa linaloukabili ulimwengu wa wanadini yaani Waislamu na Wakristo. Kwa maoni yetu kuna haja kubwa ya wanadini huku wakizingatia ibada zao maalum na miiko ya kidini na kiimani, kuunda mitandao maalumu itakayoratibu na kuendesha shughuli zote za kijamii za Wanadini. Aidha kila dini iunde chombo makhsusi cha kukusanya, kutathimini na kuchuja taarifa mbali mbali. Kwa madhumuni hayo, chini ya mtandao huu, jumuiya na mashirika ya kidini yaanzishwe katika maeneo yote ya wanadini kitaifa na kimataifa, washirikishwe wasomi, watu wenye vipawa ambao watafanya utafiti wa nguvu za kijamii, kisiasa, kiuchumi na kiutamaduni kukomesha uvurugaji wa makusudi wa maadili. Katika harakati hizo, vile vile wawemo watu wa kawaida ambao kila mmoja atawajibika kulingana na uwezo wake. Dhima zao ziwe kupata taarifa na kugundua nguvu zote zinazopinga ufunuo wa Muumba. Kung’amua mipango, programu na mbinu zao, jumuiya hizi zifuatilie kwa karibu kila kinachochapishwa na mashirika ajenti wa Wazayuni na wasio Wazayuni na kubaini hila na malengo yanayaofichwa. Mashirika haya yapate taarifa zote za machapisho, majarida na vipeperushi katika lugha mbali mbali na kuitangaza haraka habari yoyote ile yenye umuhimu wowote ule kwa Ulimwengu wana dini. Mashirika haya binafsi hayanabudi kuzitupia macho harakati za za majasusi wanaotumia ukristo kufanya shuguhuli zao mbali mbali za kijasusi na kubaini mbinu, njia na nyenzo wanazotumia.

Mbali na uchambuzi wa taarifa ghafi, mashirika haya pia yafanye utafiti wa matatizo yanayozikabili nchi za ulimwengu wa tatu. Kwa kufanya hivyo, zile taarifa ghafi zilizokusanywa zitakuwa na manufaa makubwa. Utafiti ufanyike kihalisia na taarifa ghafi zikusanywazo zitumike kama msingi wa upangaji wa mipango ya taifa. Kutokana na tafiti hizi kila sehemu yaweza kuwa na taarifa kuhusu matatizo ya sehemu nyingine na ufahamu huu utafungua njia mpya ya ushirikiano na kusaidia kusafisha njia ya umoja miongoni mwao. Kwa hivi sasa tuna uelewa hafifu kuhusu nchi nyingine na tunatafuta ufumbuzi wa matatizo kwa kutegemea makisio yasiyo na uhakika. Ndio sababu mara nyingi tunapapasa gizani bila kuyapata matatizo na kuyapatia ufumbuzi wa kudumu. Haja kubwa kwa hivi sasa ni kufanya kazi katika maeneo yote ambayo kwayo twahitaji watu wenye vipaji na taaluma mbali mbali. Kuna kazi kubwa inayotakiwa kufanywa katika maeneo mbali mbali na hiyo ni lazima kwa mashirika kwa ajili ya kufikia shabaha na malengo yaliyowekwa. Kwa kweli tunahitaji mashirika na vikundi vya watu wenye ari ya kujitolea kwa ajili ya Allaah (Subhaanahu wa Ta’ala) ili kupata saada hapa duniani na kesho akhera.


*************


Kujinusuru Na Kitanzi Cha Ujasusi Wa Kizayuni

Wanadini hawana budi kutafuta njia, stratejia na mbinu za kuzuia mlipuko wa utamaduni wa kimagharibi wa kuamsha matamanio ambao mataifa ya mabara yote yametumbikizwa kwao hivi leo na ambao unashambulia misingi ya maisha ya wanaadamu kama jamii za kiitikadi. Hapanabudi kuchukua hatua madhubuti na tahadhari makini kuzuia athari zake ili kuwakomboa Walimwengu wa kila hali kutoka katika taathira zake mbaya. Utamaduni wa kiitikadi unaofunzwa na dini zote yaani Uislamu na Ukristo ni utamaduni uliotofautiana kabisa na utamaduni wa kuamsha matamanio wa Ulimwengu wa magharibi usio na itikadi sahihi ya maisha yenye kuungwa mkono na matendo ya ibada za kiroho. Kwa kweli nguvu za utamaduni wa Ulaya na Marekani ni kubwa mno kiasi kwamba kama Wanadini hawatagutuka juu ya hatari hii inayowakabili, imani na msingi wa maisha yao ya kimaadili na kiitikadi vyote vitakuwa hatarini. Kukosekana kwa hamasa ya kidini na kutokuwa na hisia za kupenda mafunzo ya kidini na kupuuzia misingi ya imani miongoni mwa vijana, fikra za uzushi, kumomonyoka kwa maadili, kutopea katika misemo ya kimaskhara, kuishi maisha ya kizembezembe, na kupenda mambo ya kipuuzi yote haya na mengine mengi ni ishara ya kufuata kiupofu utamaduni wa Ulaya na Marekani. Kwa jinsi mambo yalivyosukwa kijasusi, vijana wanatumbukia kichwakichwa kwenye mfumo mwingine wa utamaduni na kuondolewa kabisa utambulisho wao na dhima yao ya kufikisha ujumbe wa kidini na imani ya Muumba kwa wanadamu wote. Bila kujitambua mielekeo ya utamaduni inadhoofisha misingi ya mfumo wao wa jamii na maadili na hali hii itaendelea iwapo hapatachukuliwa hatua madhubuti za haraka kuwazindua kutoka kwenye usingizi fofofo waliolazwa kiufundi na Ulimwengu wa Magharibi.

Tatizo kubwa wengi wa wanajamii hawatambui kuwa uvumbuzi wa kihalisia na muundo wa jamii na utamaduni ambamo yamo maendeleo hayo ya kisasa ni vitu viwili tofauti. Havitegemeani kwa namna yoyote ile. Jamii yoyote ile inaweza kunufaika na maendeleo ya sanaa, sayansi na teknolojia yaliyofikiwa na jamii nyingine lakini si lazima maendeleo hayo yaigwe pamoja na mifumo ya jamii na utamaduni wa nchi za kigeni au mfumo wa maisha ya jamii hiyo yenye mandeleo nao pia uigwe. Tunaweza kupiga hatua za maendeleo ya sanaa, sayansi na teknolojia huku tukifuata kikamilifu maadili ya jamii yetu, utamaduni wa dini yetu na utaratibu wetu mzima wa maisha. Mfumo pofu wa elimu ndio hasa unaozalisha dhana hii pofu. Dhana hii imejikita kwenye vichwa vya watu wengi kwamba ili wapate maendeleo ya sanaa, sayansi na teknolojia lazima wajenge mazingira yatakayokaribisha tamaduni za nchi za Magharibi. Mathalani, kama taaluma ya tiba au uhandisi wa Marekani uko katika kiwango cha juu lakini utamaduni wa nchi hiyo unajumuisha ulevi, uvaaji nusu uchi wa wanawake, ushoga na michanganyiko ya kijinsia, kwa nini mandeleo hayo yaigwe pamoja na tamaduni hizo? Kwa hili watu wa dunia ya tatu wanaweza kuiga ufanisi wa kitaaluma katika sanaa, sayansi na teknolojia ambavyo havina uvundo na taathira mbaya na kuacha ushenzi uliofumwa kifundi na majasusi wa kizayuni kupitia mataifa yenye teknolojia kubwa kwenye mila na dasturi!
 
Hii mbona imekaa kidini dini na ki-anti semitism?

Mie nimeisha wahi kuisikia zaidi ya mara tatu nne hivi japo kwa ufupi sana, na woote niliowasikia ni watu wenye kuweka dini yao mbele kila wakati bila hata kufikiri sana.
Anachotakiwa mheshimiwa ni kuifupisha hiyo habari kwani anaonekana kama anaielewa vema, aitie angalau kwenye page moja hivi.
 
KUNA DINI MOJA KUBWA IMETAWALIWA NA chuki, ubinafsi, visasi, ubaguzi na yote yanayofanana na hayo....!
na katika posti hii yamejidhirisha...!
 
KUNA DINI MOJA KUBWA IMETAWALIWA NA chuki, ubinafsi, visasi, ubaguzi na yote yanayofanana na hayo....!
na katika posti hii yamejidhirisha...!
 
Hizo ni propaganda xpaster hiyo makala umetafsiri toka mtandao fulani sasa angalia vizuri sana ndugu yangu katika mtandao ule umesoma vision na mission yao ni nini haswa ??
 
There was a time when national security, for the most part, meant military projections. And so it was that within the tenets of the traditional paradigm of security, the purpose of national security was to safeguard national values which centered on survival, self preservation and self-perpetuation and the pursuit of objectives that contributed to the growth and preeminence of the nation.



During the Cold War, the national security goal of both spheres was to expel external aggression and contain internal upheavals. Today, there is more to it and with several components, i.e. economic and ecological concerns, terrorism and weapons proliferation, international health concerns, migration, shifting demographics, and more. While most of the world has come to grips with these concerns, Tanzania continues to stick to an archaic model of national security.



To be specific, national security is undergoing a metamorphosis. The world now speaks of human security -- a more encompassing and human-centered paradigm -- as opposed to national security which is state-centered and revolves around military projection. Even so, one area of our national security we seldom discuss is the intelligence agencies. For most of us, the intelligence community is a shadowy no-go area, a forbidden topic. For most people, spies are like mystical and mythical creatures.



But when we think or talk about it, it is generally in the context of a spy agency -- an agency that operates in foreign land. The truth is that members of this community operate both inside and outside of Tanzania . The Tanzania government website did not list its intelligence agencies .



In addition, the Tanzanian Diplomatic service also has its intelligence service - as does all the diplomatic services of all the nations of the world. The British, French, Chinese, the American, German, and the Italian embassies for instance abound with intelligence officers with or without diplomatic covers. Some pose as entrepreneurs while others pose as expatriates working for foreign companies, or as researchers and university professors.


It should be noted that just as these countries play the spy game, so does Tanzania against these countries and against other African countries. South Africa, China, France, and Japan for instance, are masters at economic espionage -- an area Tanzania has not particularly wise up to. Intelligence, in its proper form, is still in its infancy in Tanzania.



No matter the nature and structure of the intelligence community, its primary purpose is to assist governments in the policy and decision making process. In other words: the intelligence agencies exist to do one thing and one thing only: assist the government in the furtherance of its domestic and foreign policy objectives -- whatever those objectives might be whether or not they fall within the bounds of law and human decency.



During the Apartheid era in South Africa, the intelligence community focused more on covert political and paramilitary operations, and in the process used intelligence as an instrument of intimidation and extra-judicial operations, i.e. the assassination of Blacks and other minority segments of the population who opposed the Apartheid regime.



However, since the collapse of the apartheid regime (and the introduction of popular sovereignty), reforms have been introduced by way of legislations and judicial mandate in order to restructure and reorient the intelligence and other security services. The expectation is that these reforms will have a positive impact on how the intelligence agencies conduct their operations.



The guiding principle of the South African intelligence community is/was well known; however, one wonders what the guiding principles of the Tanzanian intelligence agencies are. I especially wonder why the Tanzanian intelligence community has had so many monumental failures. Why for instance, have these agencies not been able to embed some of their members into the inner circles of those responsible for scandals and conflicts in TARIME or KILOMBERO?



The weakness and or the failure of the Tanzanian Intelligence Community is glaring. For instance, why is it that year after year, politicians and government officials are able to siphon public funds without the intelligence agencies being abreast and ahead of the culprits? Also, they seem not to know who is involved in money laundering, bunkering, arms dealings ( Remember Darwins NightMare ), and other manifestation of low intensity conflict.



Thousands of Tanzanian and foreigners are engaged in illegal deals and in other crimes-- including white-collar crimes; yet, the government have no way of stopping these activities before they happen. What then are the duties and responsibilities of the police and these agencies? What are the duties of these agencies vis-à-vis transnational terrorism, transnational armed robbery, transnational prostitution and cross-border child-trafficking?


Derisively, some have jokingly said that "with little determination, Rwanda or Uganda could catch Tanzania napping," if those countries were bent on invading and annexing Tanzania. What we have in Tanzania is a near monumental failure in intelligence gathering. True, no intelligence agency any where in the world is one hundred effective and competent. As good as the MOSSAD is they have had to struggle with several failures and challenges.


And in spite of the billions and billions of dollars and superior human intelligence and electronic gadgets in the arsenal of the CIA, the FBI and other American agencies, they too have had to suffer some grave failures. The unfortunate events of 9/11 are examples of such failures. In the end though, the US, Israel, France, Germany and others can justify the resources at the disposal of their intelligence agencies because their failures are rare.


Does the Tanzanian intelligence community have the ability to stop foreign intelligence from gathering sensitive information from our policy and decision-makers? In other words: are we capable of preventing opposing security organizations from eavesdropping on our ministers, Mps and RCS -- considering the fact that we have foreign agents posing as business men and women crawling all over hotels in Dar es salaam and Arusha and all over government ministries in Dodoma , Mwanza and elsewhere?



Who, for instance, is keeping an eye on the German Bundesnachrichtendienst, the British M15 and M16, Israel's HaMossad leModi'in v'leTafkidim Meyuhadima, and the Federal Security Service of the Russian Federation? Tanzania has the National Intelligence Agency.


Some of our public servants -- greedily in search of dollars and pounds and travel visa for their relatives and self -- easily sell or exchange state secrets. When the President and other government officials buy Planes, telephones and fax machines, vehicles, computers and other equipments from abroad -- how certain are we that they are not secretly fitted with audio and video devices?



It is impossible to put a stop to hostile intelligence activities. Friends spy on friends. Political allies spy on each others. That is a given -- but worst still are enemies who have grand evil intentions. The Tanzanian intelligence agencies must resolve to do a better job of protecting our vital interests. As things are, our boundaries, airports, seaports and waterways are not well-manned and so are not secured.

YONA FARES MARO
DAR ES SALAAM
TANZANIA
 
There was a time when national security, for the most part, meant military projections. And so it was that within the tenets of the traditional paradigm of security, the purpose of national security was to safeguard national values which centered on survival, self preservation and self-perpetuation and the pursuit of objectives that contributed to the growth and preeminence of the nation.



During the Cold War, the national security goal of both spheres was to expel external aggression and contain internal upheavals. Today, there is more to it and with several components, i.e. economic and ecological concerns, terrorism and weapons proliferation, international health concerns, migration, shifting demographics, and more. While most of the world has come to grips with these concerns, Tanzania continues to stick to an archaic model of national security.



To be specific, national security is undergoing a metamorphosis. The world now speaks of human security -- a more encompassing and human-centered paradigm -- as opposed to national security which is state-centered and revolves around military projection. Even so, one area of our national security we seldom discuss is the intelligence agencies. For most of us, the intelligence community is a shadowy no-go area, a forbidden topic. For most people, spies are like mystical and mythical creatures.



But when we think or talk about it, it is generally in the context of a spy agency -- an agency that operates in foreign land. The truth is that members of this community operate both inside and outside of Tanzania . The Tanzania government website did not list its intelligence agencies .



In addition, the Tanzanian Diplomatic service also has its intelligence service - as does all the diplomatic services of all the nations of the world. The British, French, Chinese, the American, German, and the Italian embassies for instance abound with intelligence officers with or without diplomatic covers. Some pose as entrepreneurs while others pose as expatriates working for foreign companies, or as researchers and university professors.


It should be noted that just as these countries play the spy game, so does Tanzania against these countries and against other African countries. South Africa, China, France, and Japan for instance, are masters at economic espionage -- an area Tanzania has not particularly wise up to. Intelligence, in its proper form, is still in its infancy in Tanzania.



No matter the nature and structure of the intelligence community, its primary purpose is to assist governments in the policy and decision making process. In other words: the intelligence agencies exist to do one thing and one thing only: assist the government in the furtherance of its domestic and foreign policy objectives -- whatever those objectives might be whether or not they fall within the bounds of law and human decency.



During the Apartheid era in South Africa, the intelligence community focused more on covert political and paramilitary operations, and in the process used intelligence as an instrument of intimidation and extra-judicial operations, i.e. the assassination of Blacks and other minority segments of the population who opposed the Apartheid regime.



However, since the collapse of the apartheid regime (and the introduction of popular sovereignty), reforms have been introduced by way of legislations and judicial mandate in order to restructure and reorient the intelligence and other security services. The expectation is that these reforms will have a positive impact on how the intelligence agencies conduct their operations.



The guiding principle of the South African intelligence community is/was well known; however, one wonders what the guiding principles of the Tanzanian intelligence agencies are. I especially wonder why the Tanzanian intelligence community has had so many monumental failures. Why for instance, have these agencies not been able to embed some of their members into the inner circles of those responsible for scandals and conflicts in TARIME or KILOMBERO?



The weakness and or the failure of the Tanzanian Intelligence Community is glaring. For instance, why is it that year after year, politicians and government officials are able to siphon public funds without the intelligence agencies being abreast and ahead of the culprits? Also, they seem not to know who is involved in money laundering, bunkering, arms dealings ( Remember Darwins NightMare ), and other manifestation of low intensity conflict.



Thousands of Tanzanian and foreigners are engaged in illegal deals and in other crimes-- including white-collar crimes; yet, the government have no way of stopping these activities before they happen. What then are the duties and responsibilities of the police and these agencies? What are the duties of these agencies vis-à-vis transnational terrorism, transnational armed robbery, transnational prostitution and cross-border child-trafficking?


Derisively, some have jokingly said that “with little determination, Rwanda or Uganda could catch Tanzania napping,” if those countries were bent on invading and annexing Tanzania. What we have in Tanzania is a near monumental failure in intelligence gathering. True, no intelligence agency any where in the world is one hundred effective and competent. As good as the MOSSAD is they have had to struggle with several failures and challenges.


And in spite of the billions and billions of dollars and superior human intelligence and electronic gadgets in the arsenal of the CIA, the FBI and other American agencies, they too have had to suffer some grave failures. The unfortunate events of 9/11 are examples of such failures. In the end though, the US, Israel, France, Germany and others can justify the resources at the disposal of their intelligence agencies because their failures are rare.


Does the Tanzanian intelligence community have the ability to stop foreign intelligence from gathering sensitive information from our policy and decision-makers? In other words: are we capable of preventing opposing security organizations from eavesdropping on our ministers, Mps and RCS -- considering the fact that we have foreign agents posing as business men and women crawling all over hotels in Dar es salaam and Arusha and all over government ministries in Dodoma , Mwanza and elsewhere?



Who, for instance, is keeping an eye on the German Bundesnachrichtendienst, the British M15 and M16, Israel’s HaMossad leModi’in v’leTafkidim Meyuhadima, and the Federal Security Service of the Russian Federation? Tanzania has the National Intelligence Agency.


Some of our public servants -- greedily in search of dollars and pounds and travel visa for their relatives and self -- easily sell or exchange state secrets. When the President and other government officials buy Planes, telephones and fax machines, vehicles, computers and other equipments from abroad -- how certain are we that they are not secretly fitted with audio and video devices?



It is impossible to put a stop to hostile intelligence activities. Friends spy on friends. Political allies spy on each others. That is a given -- but worst still are enemies who have grand evil intentions. The Tanzanian intelligence agencies must resolve to do a better job of protecting our vital interests. As things are, our boundaries, airports, seaports and waterways are not well-manned and so are not secured.

YONA FARES MARO
DAR ES SALAAM
TANZANIA

Ha ha ha, Shy bwana!
Umeenda kukopi page nzima ukabadili few words instead of Nigeria unaweka Tanzania.... thats funny!
U know it is a crime.. right?
The Nigerian Village Square - Nigeria’s Intelligence Agencies (Spy Network)
 
Nigeria's Intelligence Agencies (Spy Network)
Written by Sabella Ogbobode Abidde
Thursday, 18 September 2008
There was a time when national security, for the most part, meant military projections. And so it was that within the tenets of the traditional paradigm of security, the purpose of national security was to safeguard national values which centered on survival, self preservation and self-perpetuation and the pursuit of objectives that contributed to the growth and preeminence of the nation.



During the Cold War, the national security goal of both spheres was to expel external aggression and contain internal upheavals. Today, there is more to it and with several components, i.e. economic and ecological concerns, terrorism and weapons proliferation, international health concerns, migration, shifting demographics, and more. While most of the world has come to grips with these concerns, Nigeria continues to stick to an archaic model of national security.



To be specific, national security is undergoing a metamorphosis. The world now speaks of human security -- a more encompassing and human-centered paradigm -- as opposed to national security which is state-centered and revolves around military projection. Even so, one area of our national security we seldom discuss is the intelligence agencies. For most of us, the intelligence community is a shadowy no-go area, a forbidden topic. For most people, spies are like mystical and mythical creatures.



But when we think or talk about it, it is generally in the context of a spy agency -- an agency that operates in foreign land. The truth is that members of this community operate both inside and outside of Nigeria. The Nigerian government website did not list its intelligence agencies; however, the Federation of American Scientist has a listing of Nigeria's intelligence agencies that was current as of 1998.



Most Nigerians are familiar with the Defense Intelligence Agency State Security Service and the National Security Organization, but are not conversant with the fact that the Navy, Air force, Police, the National Drug Law Enforcement Agency and the Army all have intelligence wings.



In addition, the Nigerian Diplomatic service also has its intelligence service - as does all the diplomatic services of all the nations of the world. The British, French, Chinese, the American, German, and the Italian embassies for instance abound with intelligence officers with or without diplomatic covers. Some pose as entrepreneurs while others pose as expatriates working for foreign companies, or as researchers and university professors.



It should be noted that just as these countries play the spy game, so does Nigeria against these countries and against other African countries. South Africa, China, France, and Japan for instance, are masters at economic espionage -- an area Nigeria has not particularly wise up to. Intelligence, in its proper form, is still in its infancy in Nigeria.



No matter the nature and structure of the intelligence community, its primary purpose is to assist governments in the policy and decision making process. In other words: the intelligence agencies exist to do one thing and one thing only: assist the government in the furtherance of its domestic and foreign policy objectives -- whatever those objectives might be whether or not they fall within the bounds of law and human decency.



During the Apartheid era in South Africa, the intelligence community focused more on covert political and paramilitary operations, and in the process used intelligence as an instrument of intimidation and extra-judicial operations, i.e. the assassination of Blacks and other minority segments of the population who opposed the Apartheid regime.



However, since the collapse of the apartheid regime (and the introduction of popular sovereignty), reforms have been introduced by way of legislations and judicial mandate in order to restructure and reorient the intelligence and other security services. The expectation is that these reforms will have a positive impact on how the intelligence agencies conduct their operations.



The guiding principle of the South African intelligence community is/was well known; however, one wonders what the guiding principles of the Nigerian intelligence agencies are. I especially wonder why the Nigerian intelligence community has had so many monumental failures. Why for instance, have these agencies not been able to embed some of their members into the inner circles of those responsible for fanning religious and ethnic conflicts?



The weakness and or the failure of the Nigerian Intelligence Community is glaring. For instance, why is it that year after year, politicians and government officials are able to siphon public funds without the intelligence agencies being abreast and ahead of the culprits? Also, they seem not to know who is involved in money laundering, oil bunkering, arms dealings, and other manifestation of low intensity conflict.



Thousands of Nigerians and foreigners are engaged in illegal oil deals and in other crimes-- including white-collar crimes; yet, the government have no way of stopping these activities before they happen. What then are the duties and responsibilities of the police and these agencies? What are the duties of these agencies vis-à-vis transnational terrorism, transnational armed robbery, transnational prostitution and cross-border child-trafficking?



Derisively, some have jokingly said that "with little determination, Togo or Chad could catch Nigeria napping," if those countries were bent on invading and annexing Nigeria. What we have in Nigeria is a near monumental failure in intelligence gathering. True, no intelligence agency any where in the world is one hundred effective and competent. As good as the MOSSAD is they have had to struggle with several failures and challenges.



And in spite of the billions and billions of dollars and superior human intelligence and electronic gadgets in the arsenal of the CIA, the FBI and other American agencies, they too have had to suffer some grave failures. The unfortunate events of 9/11 are examples of such failures. In the end though, the US, Israel, France, Germany and others can justify the resources at the disposal of their intelligence agencies because their failures are rare.



Does the Nigerian intelligence community have the ability to stop foreign intelligence from gathering sensitive information from our policy and decision-makers? In other words: are we capable of preventing opposing security organizations from eavesdropping on our ministers, governors and on Aso Rock -- considering the fact that we have foreign agents posing as business men and women crawling all over hotels in Abuja and Lagos and all over government ministries in Kaduna, Port Harcourt and elsewhere?



Who, for instance, is keeping an eye on the German Bundesnachrichtendienst, the British M15 and M16, Israel's HaMossad leModi'in v'leTafkidim Meyuhadima, and the Federal Security Service of the Russian Federation? Nigeria has the National Intelligence Agency. Past Director Generals have included Albert Horsfall, Haliru Akilu, Zakari Y. Ibrahim, Godfrey B. Preware, Uche O. Okeke, and Emmanuel E. Imohe.



Some of our public servants -- greedily in search of dollars and pounds and travel visa for their relatives and self -- easily sell or exchange state secrets. When the President and other government officials buy planes, telephones and fax machines, vehicles, computers and other equipments from abroad -- how certain are we that they are not secretly fitted with audio and video devices?



It is impossible to put a stop to hostile intelligence activities. Friends spy on friends. Political allies spy on each others. That is a given -- but worst still are enemies who have grand evil intentions. The Nigerian intelligence agencies must resolve to do a better job of protecting our vital interests. As things are, our boundaries, airports, seaports and waterways are not well-manned and so are not secured.

Sabidde@yahoo.com
 
Mifumo Mingine Ya Ujasusi Duniani: CIA, RGU, KGB
Ukusanyaji wa taarifa za kijasusi umekuwa mpevu mno ambapo mashirika, idara na jumuiya za ujasusi, ushushushu na ukachero una zana na mbinu za hali ya juu za namna ya kuzikusanya kiteknolojia au upandikizaji wa watendaji wa mashirika husika kwenye jumuiya za kiserikali, zisizo za kiserikali, makundi, vyama, taasisi za serikali za binafsi ndani na nje ya nchi ili kupata taarifa muhimu, mipango na mikakati (intelligence gathering devices).

Hivi leo, kompyuta yaweza kuunganishwa na nyaya kisha kuwekwa kifaa kidogo mahali popote, iwe ofisini au kwingineko ambacho huweza kufuatilia nyendo za wote wanaopita jirani na mahali hapo. Kifaa hicho kilichounganishwa na Kompyuta huweza kuchukua picha na kuzisafirisha hadi kwenye kompyuta ambapo mtumiaji huzitumia atakavyo iwe kiulinzi au kiukachero. Kamera ndogo sana (micro-cameras) ndizo zitumikazo kuchukua picha za matukio, taswira za maeneo au watu wanaolengwa na mashirika ya kijasusi bila ya wenyewe kubaini. Kutokana na shughuli za ujasusi kupiga hatua kubwa, simu za upepo na kamera ndogo ambazo huko nyuma zilikuwa zikitumiwa na mashirika au jumuiya za kijasusi, hivi sasa rukhsa kutumika maeneo ya uraiani kwa ajili ya huduma za kijamii.

Kamera hizo huweza kufichwa sehemu mbali mbali ambazo huwa vigumu kubainika. Sehemu hizo ni pamoja na tai za mashati, kosi za fulana, taa za mezani, saa, kalamu, mawani, makoti, soketi za umeme za ukutani, vitabu, kofia, radio ndogo za kushika mikononi, wanasesere, simu za mikononi, ashtrei za sigara, milangoni na vyombo vya kugunduwa mioto pamoja na maua ya mapambo ya nyumbani. Kamera hizo huweza kupachikwa kwa baadhi ya wanyama hasa wale wafugwao nyumbani ili kuweza kunasa picha na mienendo ya kila siku ya watu wanaotafutwa bila ya wao wenyewe kufahamu. Kamera zenye ukubwa wa kati ya milimita mbili au sentimita chache hivi, zina uwezo wa kupiga picha kubwa na nzuri zinazolingana na zile zipigwazo na kamera kubwa. Uwezo huo unatokana na betri zake kuwa na nguvu inayowezesha kamera kuchukua picha za aina zote zisizo za rangi (black-and-white) na za rangi (coloured). Baadhi ya kamera hizo huweza hupiga picha mfululizo bila ya kusimama, nyingine huweza kuwekwa maeneo ya matukio kisha kufuatilia kila kitu kwa kasi ndogo sana kisha kujizima pindi tukio au matukio yanapokwisha. Betri za kamera hizo zina uwezo mkubwa wa kuifanya ipige picha kwa muda mrefu.

Aidha baadhi ya kamera hizo (infra-red cameras) zaweza kupiga picha eneo lenye ukubwa wa mita 150 sawa na futi 450 hata kama lina kiza kinene. Zipo ‘bugs’ ambazo ni vifaa nyeti vya kunasia siri ambavyo huwekwa maeneo maalumu hasa kupitia mitambo ya elektroni na kompyuta ili kuzuwia kuingiliwa na mawasiliano mengine au kupitisha taarifa za kijasusi (transmit intelligence) kutoka eneo moja kwenda jingine. Mtu anayenasa taarifa hizo huweza kukaa umbali wa mita 100 na zaidi na bado akaweza kusikia kikamilifu kila kinachozungumzwa kwenye vikao, kumbi au ofisi husika. Utengenezaji wa vifaa hivi nyeti, ununuzi na upandikizaji wake, hugharimu mamilioni ya dola za kimarekani. Kwa sababu hiyo, mara nyingi ni idara za kijasusi tu zenye uwezo wa kumiliki, kuchunguza na kupeleleza uhalifu au njama kupitia simu (bug telephones) kwa kupachikwa maeneo yanayoshukiwa.

Zipo aina nyingine za utegaji na ufuatiliaji wa simu zikiwemo za unasaji wa sauti na kuzibadilisha kwa namna tofauti zinazoweza kutumiwa na mashirika ya kijasusi, idara za usalama na upelelezi (ultrasonic variety) zikiwemo zile za mawimbi ya redio (convert into audio signals) ambayo baadaye hugeuzwa kuwa sauti kamili kuweza kuzisikilizwa vyema na wachambuzi wa taarifa na matukio walioko komandi kuu za usalama na ujasusi (these signals are later converted back into audio).
 
Shirika La CIA

CIA (Central Intelligence Agency) iliundwa Juni 20, 1944 chini ya sheria ya usalama wa taifa iliyowekwa na aliyekuwa Rais wa Marekani Truman. Ili kufikia malengo yake katika uwanja wa ujasusi, CIA hujishughulisha na utafiti, maendeleo na utumiaji wa teknolojia mbali mbali za kisasa kwa madhumuni ya ujasusi.
Likiwa shirika huru la ujasusi, CIA lina vyanzo huru vya utafiti na uchambuzi wa habari za kijasusi na linafanya kazi kwa kushirikiana na taasisi nyingine za kijasusi kuhakikisha kwamba wapokezi wa habari hizo mjini Washington na makamanda katika maeneo ya vita wanapokea habari sahihi na bora kwa kadri iwezekanavyo.
Ili kuweza kwenda na hali mbali mbali za kidunia kwa maslahi ya Marekani, shirika la CIA limekuwa likikabiliwa na changamoto mbali mbali za kubuni vituo maalum vilivyo na utaalamu tofauti, kwa kuyapa kipaumbele masuala yenye maslahi kwa taifa, yakiwemo:

1. Mikataba ya kuzuia ueneaji silaha kali hasa za kinyuklia duniani, Ugaidi dhidi ya ugaidi (Ugaidi pinzani), ujasusi dhidi ya ujasusi (Ujasusi pinzani na pandikizi), Uhalifu wa kupangiliwa kimataifa, na ueneaji wa mihadarati (dawa za kulevya) Ulinzi na uharibifu wa Mazingira, pamoja na ujasusi wa udhibiti silaha.
2. Kubuni na kuongoza ushirikiano wenye nguvu kati ya taasisi kadhaa za kijasusi na vyombo mbalimbali vya uchambuzi wa habari za kijasusi.
3. Kuchukua sehemu muhimu na yenye nguvu katika juhudi za uchambuzi wa taarifa za kishushushu na vyanzo vyake kwenye jumuiya za kijasusi zinazoweza kuathiri usalama wa Taifa.
4. Kuchangia uimarishaji wa mageuzi ya jumla katika jumuiya ya Ujasusi, kwa kusimamia huduma muhimu zinazopewa kipaumbele katika uchambuzi wa taarifa za kijasusi katika matumizi ya tamathali za usemi kwenye mazungumzo, maandishi, sanamu, picha; na hata michoro; na ukusanyaji taarifa katika vyanzo vya wazi, kwa kushiriki katika ushirikiano wa mipango kakatavu na taasisi nyingine za kijasusi, kwenye maeneo ya utafiti, maendeleo, na ukusanyaji wa taarifa za kiufundi.

Kwa kutilia mkazo marekebisho ya ukusanyaji taarifa za kijasusi, the CIA imerekebisha kulingana na malengo uungaji mkono wake, kwa walengwa wake wakuu wa ujasusi kusaidia mahitajio yao, kama walivyokutana na masuala mbalimbali ya kipindi cha baada ya vita baridi ulimwenguni
 
Back
Top Bottom